Mhe Temba alikuwa JWTZ au JKT?

Alimaliza kozi ya jkt (jeshi la kujenga taifa) baadae ajira zilipokuja akajiunga na jwtz akafaulu kwenye usaili, nakumbuka wakati tupo kwenye kozi kipindi cha kubadilisha roho ya raia na kuingiza roho ya kijeshi (six week) nakumbuka tulikuwa kwenye mchakamchaka tupo hoi porini tukapewa tano (mapumziko ya muda mfupi) pembeni kuna bwawa la maji tukawa tunaoga bahati mbaya ndugu Amani Temba alijisahau akavua kombat ya juu mkufunzi akaiona ile tattoo yake akaitwa, basi tangu siku ile hatukumuona tena kikosini mpaka nakuja kusikia jamaa yupo uraiani kawa msanii. Ila jamaa aliwahuzunisha watu wengi sana kutokana na ucheshi wake, baadhi ya maofisa pia walihuzunika maana kuingia kwake jkt mpaka jwtz ulikuwa mpango ili baadae aje kuwa mchezaji wa kikapu kwenye timu ya jeshi ndio maana hata uingiaji wake ulikuwa ni hamasa kutoka kwa walimu wa michezo (wanajeshi) pale jitegemee sekondari.
Mkuu naomba elimu, tattoo INA madhara gani jeshini?
 
Samahani kidogo Mkuu katika majina yote ya nchi zilizopo duniani na hata katika Kitabu takatifu cha Wakristo Biblia hakuna nchi iitwayo ' Islael ' bali kuna nchi inayotambulika hadi Kijiografia kama ' Israeli ' yenye mji mkuu wake Tel Aviv Yafo.
mji mkuu wa Israel ni Jerusalem,
 
Wakuu jana ilikua ni siku ya kizaliwa ya msanii kutoka kundi lililofahamika kama TMK 'Amani Temba' maarufu kama Mh Temba,katika kuufahamisha umma kuhusu siku yake hiyo pendwa alisikika kwenye redio kubwa hapa nchini akisema kwamba "hata nikiwa jeshini nilipenda muziki".

Ningependa kufahamu je alikua JWTZ au JKT, mwenye historia yake kidogo anaweza share nasi wa mikoani.

3441654f33d5f90ff5929920fefdf9d8.jpg
Kwa hiyo hapo pichani huyo Temba ni yupi?
 
Mkuu naomba elimu, tattoo INA madhara gani jeshini?
kwa hapa Tanzania tattoo haziruhusiwi jeshini kwa sababu:-
1. Nidhamu, kwa mazingira ya tz MTU mwenye tattoo huonekana kuwa ni mhuni asiye na nidhamu kinyume na sheria na misingi ya jeshi LA tanzania .

2. Tattoo yaweza kuwa alama ya makundi ya kihalifu, hivyo kutoa mafunzo ya kijeshi kwa kijana mwenye tattoo ni sawa na kuwapa mafunzo magaidi ndani ya jeshi ( japo yawezakuwa sio sahihi) lakini msimamo wa majeshi yetu ndo huo.
 
kwa hapa Tanzania tattoo haziruhusiwi jeshini kwa sababu:-
1. Nidhamu, kwa mazingira ya tz MTU mwenye tattoo huonekana kuwa ni mhuni asiye na nidhamu kinyume na sheria na misingi ya jeshi LA tanzania .

2. Tattoo yaweza kuwa alama ya makundi ya kihalifu, hivyo kutoa mafunzo ya kijeshi kwa kijana mwenye tattoo ni sawa na kuwapa mafunzo magaidi ndani ya jeshi ( japo yawezakuwa sio sahihi) lakini msimamo wa majeshi yetu ndo huo.
OK thanks
 
watu eleweni kuwa JKT ni jeshi kama ilivyo jwtz, ndio maana jkt ni kamandi kamili kwenye muundo wa JWTZ, msifikiri kuwa jkt ni mchezo mchezo waliopita kule ndo wanajua, na ndio kugumu kuliko hata RTS
 
kwa hapa Tanzania tattoo haziruhusiwi jeshini kwa sababu:-
1. Nidhamu, kwa mazingira ya tz MTU mwenye tattoo huonekana kuwa ni mhuni asiye na nidhamu kinyume na sheria na misingi ya jeshi LA tanzania .

2. Tattoo yaweza kuwa alama ya makundi ya kihalifu, hivyo kutoa mafunzo ya kijeshi kwa kijana mwenye tattoo ni sawa na kuwapa mafunzo magaidi ndani ya jeshi ( japo yawezakuwa sio sahihi) lakini msimamo wa majeshi yetu ndo huo.
Umejibu vema kabisa
 
Back
Top Bottom