Mhe. Sitta, Kwa heshima kubwa nauliza, kwanini mnataka kukimbiza mambo?

Nov 15, 2010
19
230
Kwa heshima kubwa nauliza, kwanini mnataka kukimbiza mambo? kuna lipi tusilolijua mnalotaka kulitimiza? Mnajua muda hautoshi, kwanini mnalazimisha kila kitu kifanyike kabla ya tarehe 4 Oktoba. Ilhali mnajua tumeshindwa kukubaliana, kujenga muafaka na kufanya maridhiano, Dhambi iko wapi, si tuache wenye busara zaidi yetu waendelee na mchakato 2016. Au unahofu Bunge la 2016 halitakuwa na busara kama yetu na kwamba wao watashindwa kujenga muafaka wa kitaifa, kufanya maridhiano na kuwa na uelewa wa pamoja wa misingi.?

Wengi wenu mnajua hata Rasimu Toleo la Pili hamkuisoma vizuri na wengine hamkuielewa mpaka leo na mmekuwa nayo kwa miezi kadhaa, je Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa iliyotoka kwa Kamati ya Uandishi tarehe 24 Mtakuwa mmeweza kuisoma, kuielewa na kuweza kuifanyia maamuzi kabla ya tarehe 4 Oktoba?


Je Muhimu kwenu ni kupiga kura ili kazi iende au ni kuwa na uelewa, ufahamu na uhakika wa kwamba mnachokifanyia maamuzi ndicho kitatuvusha kutoka sasa hadi miaka zaidi ya 50 ijayo? Je mmejipa muda, siku 10 zinawatosha, please lets be serious to our country Tanzania, Please Please, For once tuahirishe tuendelee 2016.

Nina uhakika Historia itatukumbuka, kila mmoja mmoja wetu kwa kazi aliyofanya kwa Taifa letu leo.
 
Wewe na wajumbe wenzii wa tume ya mabadiliko ya katiba, mtakumbukwa sana kaka @ Polepole. Tunafaham kabisa kua kila mtu ana ubinafc wake kwa namna moja au nyingine, lakini kitendo cha kuuweka pembeni ubinafsi wenu na kusimama kwa maslahi ya Taifa letu, ni zawadi na heshima kubwa kwa watanzania toka kwenu.
Waache walazimishe tu, mwisho wake wanaufaham
 
Mtandao wowote wa urais 2015 utakao kuwa karibu na Sitta utapotea moja kwa moja. Pengine Mungu ameamua kuingilia kati na kumuanika Sitta kupitia hili Bunge la katiba. Neno Dictator halitoshi kumueleza huyu Mzee. Jambo zito na muhimu kama katiba anageuza mradi binafsi?
 
Humphrey Polepole

Nchi yetu inaendeshwa kiajabu sana... Hakuna anayejali, kila mtu anafanya analotaka.. Rais wetu ndiyo kimya kabisa utafikiri huu mchakato haukuuanzisha yeye na yanayoendelea ni kama yanatokea nchi jirani.

Sasa SITTA anataka hata walioko nje wapige kura... Swali la kujiuliza kitabu cha mahudhurio kiliwekwa cha nini? Je, vipi kuhusu posho watalipwa wakiwa hukohuko...? Kama wakipiga kura hata kama mtu akiwa nje ya nchi basi na posho zake zote apewe.. Maana amepigia kura sura na ibara zote.

Uongozi wa Tanzania kwa sasa ni kama familia ya kambare... Kila mtu ana-ndevu, ana-sauti na mamlaka ya kufanya maamuzi anavyotaka.

Lakini hiki kibuli chao kinatusaidia kujua upande wa pili kuna nini.. Ni wakati wa kuiondoa CCM mabadarakani..
 
Last edited by a moderator:
Mimi nauliza wakipiga kura wakiwa nje ya bunge watalipwa posho zao au hawatalipwa?

Nauliza hivyo kwa sababu tumezoea kusikia kuwa asiyekuwepo bungeni posho hapati! hapa itakuwaje????
 
Hakuna cha bunge wala nini hawa ni wezi wakawaida tunawajua nn wanachokitaka ,hawana huruma na nchi hii wao ni watu wa kujali matumbo yao,ipo siku tutachoka ndio watajua kwAmba watz wanaufahamu
 
Humphrey Polepole

Ignoring constitutional conventions does not always result in a crisis.Because of its pivotal role in providing independence and establishing democracy
 
Last edited by a moderator:
Leo wazi wazi nimemsikia akiwatahadharisha wajumbe kuwa sio vyema kuipigia kura ya hapana rasimu itakayopendekezwa kwa kigezo cha gharama. Yaani maono ya katiba kwa muktadha wa maridhiano kwake wala sio jambo la muhimu....yeye anataka kuonesha ubabe kuwa amefanikisha suala hilo ili apate sifa. Siku zotee waliopo nje ya bunge wamekuwa wakiambiwa warudi bungeni kwani huko ndipo maamuzi yatafanyika......sasa inakuwaje hawa watakaokuwa nje leo hii walazimishwe kufanya maamuzi hata wakiwa hija? Kila kitu kinafichwa kwenye kamati bila umma kuona nini kinafanyika huko ndani. Itoshe kusema kuna siri nzito inayofanywa na kiongozi huyu.... historia ni Mwalimu mzuri sana....na tusubiri
 
Rasimu itapita,sherehe za kupongezana zitakuwepo,mafao kwa wingi lakini dhamira itamsuta Samwel Sitta mpaka ndani ya kaburi lake.
Hii haraka y a kufanya mpaka watu waliopo Hijja wapige kura inatoka wapi?
Hii haraka ya kulazimisha Mawaziri wafike Dodoma ili kura zitoshe inatoka wapi wakati katiba hii haitatumika katika uchaguzi?
Samweli Sitta kila la heri lakini historia haifutiki,tutakukumbuka kwa upeo wako mdogo katika mustakabali wa nchi yetu.
 
Humphrey Polepole

kwanza kaka nakukubali sana, nimekuwa nikikusikiliza, una hoja za msingi! pili kwa hili swal a la katiba si kila mtu ana lengo la lililo kusudiwa, wengi wao hapo wako hapo kujipatia kipato, wala hawasikilizi kinacho ongelewa, na kwa uapande wa Sitta yuko hapo kujikomba kwa chama cha Kifisadi akiona kama hii inaweza kuwa ni tiketi ya kupata nafasi ya kugombe nafasi ya urais...
 
Last edited by a moderator:
Sitta katuonesha upande wske wa pili

Na watu walikua wakimpigia chapuo sana hapa,jana nimemsikia Akimkatisha Mjumbe mwakilish wa CWT na baadae mzee Arfi,yaan aloyasema Profesa kabudi kuna watu wameshupaa hawashauriki,n then suala lingine babu 6 hataki kushauriwa hatak critcism,na anawaita wenzie waongo,sababu ya jana kubadil kanun ni kutokana na shutma za watanzania juu ya suala la wajumbe walio nje kupiga kura,Sasa me naliona hili ni Bunge Maalum la Kanuni(BMK) na si la KATIBA
 
MIGNON

'Kuna Mpumbavu na Mjinga,Mpumbavu hushupaa hashauriki,ila mjinga hutaka kujifunza,sisi wajinga wao wapumbavu'-Profesa Paramagamba Kabudi
 
Last edited by a moderator:
Hakuna cha bunge wala nini hawa ni wezi wakawaida tunawajua nn wanachokitaka ,hawana huruma na nchi hii wao ni watu wa kujali matumbo yao,ipo siku tutachoka ndio watajua kwAmba watz wanaufahamu

ambao wanaiba kwa kusaidiwa na sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2013
 
Tatizo wajumbe wengi wa BMK kwa sasa wanachowaza ni maslahi binafsi tu, huenda walichokifanya ukawa kinaonekana kama sio kitendo cha kiungwana kwa baadhi ya watu, lakini kwa hali inavyoendelea, wataonekana heri!
 
Ni shidaaaah
 

Attachments

  • 1411445580858.jpg
    1411445580858.jpg
    30.4 KB · Views: 193
Watanzania tumepokwa fursa adimu ya kutunga KATIBA mpya kweupe tukiwa tunashuhudua.Katiba inayopendekezwa na bunge hili hakika haitapokelewa na wananchi waliowengi kutokana na Rasimu ya Pili kupotezewa.Rasimi ya Pili ndio ilibeba maoni na mapendekezo ya kweli ya Watanzania.
 
Mungu yupo jamani character ya sita imeonekana, je ajekuwa rais huyu sijui ingekuwaje aiseee
 
Back
Top Bottom