Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,770
- 121,823
Wanabodi,
Kwa mujibu wa katiba yetu, Uchochezi ni kosa la jinai, hivyo chombo chochote cha habari kinacholeta uchochezi wowote hakihitaji kuonewa huruma yoyote bali kifungiliwe mbali mara moja.
Mhe rais wetu ametoa onyo kwa magazeti mawili ama yaache uchochezi, ama atayaadhibu kwa kuyafungia bila huruma!.
Naamini Watanzania wote wenye kulitakia mema taifa letu, wataungana na rais wetu kuyalaani haya magazeti mawili chochezi kwa kutaka yachukuliwe hatua kali za kisheria kwa kufungwa toka jana.
Kwa vile Tanzania ni sehemu ya global Village, inawezekana kabisa huo unaoitwa uchochezi ni uchochezi kwa kijiji kimoja na freedom of expression kwa kijiji kingine.
Mfano gazeti likiibua kashfa fulani kubwa kutokana na data kwenye confidential document, gazeti likichapisha habari hiyo, litakuwa limefanya kosa la kuchapisha siri za serikali hivyo inabidi lifungiwe! .
Lakini kwenye "open government initiatives" media inayoibua madudu ya serikali ndio yenye kupaswa kupongezwa kwa sababu japo kweli ni siri lakini ndio ukweli wenyewe.
Ila katika kumuunga mkono rais wetu, na wakati huo kuilinda nchi yetu tusitengwe na jumuiya ya kimataifa, jee mnaonaje kama turamshauri rais wetu, ayataje tuu hayo magazeti, halafu sisi Watanzania wote katika umoja wetu, tukayasusia kabisa kuyanunua, hivyo badala ya kuyafunga na kusababisha kelele nyingi, yatadodea kwenye meza za magazeti na kujifia natural death! .
Mnaliona hili? .
Paskali
Kwa mujibu wa katiba yetu, Uchochezi ni kosa la jinai, hivyo chombo chochote cha habari kinacholeta uchochezi wowote hakihitaji kuonewa huruma yoyote bali kifungiliwe mbali mara moja.
Mhe rais wetu ametoa onyo kwa magazeti mawili ama yaache uchochezi, ama atayaadhibu kwa kuyafungia bila huruma!.
Naamini Watanzania wote wenye kulitakia mema taifa letu, wataungana na rais wetu kuyalaani haya magazeti mawili chochezi kwa kutaka yachukuliwe hatua kali za kisheria kwa kufungwa toka jana.
Kwa vile Tanzania ni sehemu ya global Village, inawezekana kabisa huo unaoitwa uchochezi ni uchochezi kwa kijiji kimoja na freedom of expression kwa kijiji kingine.
Mfano gazeti likiibua kashfa fulani kubwa kutokana na data kwenye confidential document, gazeti likichapisha habari hiyo, litakuwa limefanya kosa la kuchapisha siri za serikali hivyo inabidi lifungiwe! .
Lakini kwenye "open government initiatives" media inayoibua madudu ya serikali ndio yenye kupaswa kupongezwa kwa sababu japo kweli ni siri lakini ndio ukweli wenyewe.
Ila katika kumuunga mkono rais wetu, na wakati huo kuilinda nchi yetu tusitengwe na jumuiya ya kimataifa, jee mnaonaje kama turamshauri rais wetu, ayataje tuu hayo magazeti, halafu sisi Watanzania wote katika umoja wetu, tukayasusia kabisa kuyanunua, hivyo badala ya kuyafunga na kusababisha kelele nyingi, yatadodea kwenye meza za magazeti na kujifia natural death! .
Mnaliona hili? .
Paskali