Meitinyiku L. Robinson
JF-Expert Member
- Aug 29, 2011
- 412
- 90
Kila binadamu amejaliwa kuwa na kipaji chake na kipaji halisi hutoka kwa Mwenyezi Mungu ambaye ndiye Muumbaji na mgawaji wa vyote kwa wanadamu ila kuna vipaji vingine ambavyo hutokana na mambo mbali mbali mathalan elimu n.k. Naungana na NOVA aliyejitahidi kuwakilisha hisia zake kwa Ushairi na kuonesha yale yaliyo moyoni mwake.
Binafsi nianze kwa kukupongeza kwa ujasiri, uvumilivu na hatua uliyofikia kuzungumzia yale uliyokuwa nayo ambayo kwayo baadhi ya Watanzania wasio na ushabiki na wenye nia njema kwa Watanzania wenzao wameweza kugundua yaliyokuwa sirini yatosha kusema kuwa japo ulichelewa ila sasa UMESHAFIKA. Mhe. Lowassa yaliyokupata naamini kama ni mwanadamu mwingine asiye na uvumilivu, staha na hata ujasiri basi ungekuta ameshazikwa ila ninacho amini ni kweli kwamba MTETEZI wako yu hai. Natambua una familia na umezungukwa na marafiki ambao wengi wao hawakuwa wakipendezwa kabisa na jinsi ulivyokuwa unashambuliwa kwa kejeli, matusi na dhihaka zisizo kuwa na kikomo yapata miezi saba kama mwenyewe ulivyosema ila sasa naamini wote wamepata japo kwa uchache kujua kuwa mchele ulikuwa upi na chuya vile vile.
Si rahisi sana kuamini kwamba ulijaribu kushawishi kuvunjwa kwa mkataba uliosababisha wewe kufikia hapo ulipo lakini vile vile si rahisi mtu wa kawaida kuamini kuwa uliwajibika kwa maslahi ya Chama na Serikali yako pia, ila tamko lako basi litufungue fikra na mawazo yetu. Na kama kweli "urafiki wenu si wa barabarani Israeli na aseme sasa." Kuna baadhi ya vyombo vya habari vilieleza kuwa wakati ukiwasilisha hoja yako kuna baadhi ya Wajumbe walionekana kutaka kulia ukweli ni kwamba kama hayo uliyoyasema ndivyo ilivyokuwa sintashangaa hata mtu akili na nashawishika sasa kuamini yale maneno yako kwamba "ulionewa sana na ulidhalilishwa sana" huu msalaba, haya mateso na hatimaye udhalilishaji na matusi yote na jina ulilobandikwa la kifisadi hukustali ila naamini umwaminiye alisimama imara katika kuhakikisha hutetereki.
Yatosha kusema unastahili pongezi, na sasa hata mimi binafsi naweza kusimama mbele ya umati wa watu nikasema neno juu yako kwa kuwa nitakuwa na ujasiri si tu wa kuwasilisha mada ila vile vile ya kutetea na kujenga hoja kwa hoja kwa nadharia na ushahidi. Samehe mara Saba Sabini sisi ndio vijana mlio tuzaa na tunajaribu kwa namna moja ama jingine kuhakikisha majina yetu yanajengeka katika mwamba imara japo tunaonekana kukosa hekima, busara, maarifa, uwezo, vigezo na hata staha katika kufanya hayo ndiyo maana tunaishia kukutukaneni tukiamini kuwa kwa kufanya hivyo basi tutakuwa na wakati mzuri na wakati mwingine tunaonekana kutumiwa na pande zisizotutakia mema. Mhe kwa kuwa vijana tumepotoka na utukufu wa Mungu unaelekea kupungua kwetu tusamehe manake naamini si wote walio hivyo kwa hiyo kwa kupitia wale wachache basi na wengine nao wapata msamaha naamini nao pia watakaa na kutafakari na kisha watatubu.
Nikutatakie heri katika yote na naamini wana Monduli, wana wa Arusha na vitongoji vyake wanakusubiri kwa hamu kwani "Mlifurahi pamoja, Mlihuzunika pamoja na mtasonga mbele pamoja"
Ni mwanzo mwingine wa hatua 1,000 mbele....................... I believe as we goby the game will change now from an enemy of the to a man of the people..............
Binafsi nianze kwa kukupongeza kwa ujasiri, uvumilivu na hatua uliyofikia kuzungumzia yale uliyokuwa nayo ambayo kwayo baadhi ya Watanzania wasio na ushabiki na wenye nia njema kwa Watanzania wenzao wameweza kugundua yaliyokuwa sirini yatosha kusema kuwa japo ulichelewa ila sasa UMESHAFIKA. Mhe. Lowassa yaliyokupata naamini kama ni mwanadamu mwingine asiye na uvumilivu, staha na hata ujasiri basi ungekuta ameshazikwa ila ninacho amini ni kweli kwamba MTETEZI wako yu hai. Natambua una familia na umezungukwa na marafiki ambao wengi wao hawakuwa wakipendezwa kabisa na jinsi ulivyokuwa unashambuliwa kwa kejeli, matusi na dhihaka zisizo kuwa na kikomo yapata miezi saba kama mwenyewe ulivyosema ila sasa naamini wote wamepata japo kwa uchache kujua kuwa mchele ulikuwa upi na chuya vile vile.
Si rahisi sana kuamini kwamba ulijaribu kushawishi kuvunjwa kwa mkataba uliosababisha wewe kufikia hapo ulipo lakini vile vile si rahisi mtu wa kawaida kuamini kuwa uliwajibika kwa maslahi ya Chama na Serikali yako pia, ila tamko lako basi litufungue fikra na mawazo yetu. Na kama kweli "urafiki wenu si wa barabarani Israeli na aseme sasa." Kuna baadhi ya vyombo vya habari vilieleza kuwa wakati ukiwasilisha hoja yako kuna baadhi ya Wajumbe walionekana kutaka kulia ukweli ni kwamba kama hayo uliyoyasema ndivyo ilivyokuwa sintashangaa hata mtu akili na nashawishika sasa kuamini yale maneno yako kwamba "ulionewa sana na ulidhalilishwa sana" huu msalaba, haya mateso na hatimaye udhalilishaji na matusi yote na jina ulilobandikwa la kifisadi hukustali ila naamini umwaminiye alisimama imara katika kuhakikisha hutetereki.
Yatosha kusema unastahili pongezi, na sasa hata mimi binafsi naweza kusimama mbele ya umati wa watu nikasema neno juu yako kwa kuwa nitakuwa na ujasiri si tu wa kuwasilisha mada ila vile vile ya kutetea na kujenga hoja kwa hoja kwa nadharia na ushahidi. Samehe mara Saba Sabini sisi ndio vijana mlio tuzaa na tunajaribu kwa namna moja ama jingine kuhakikisha majina yetu yanajengeka katika mwamba imara japo tunaonekana kukosa hekima, busara, maarifa, uwezo, vigezo na hata staha katika kufanya hayo ndiyo maana tunaishia kukutukaneni tukiamini kuwa kwa kufanya hivyo basi tutakuwa na wakati mzuri na wakati mwingine tunaonekana kutumiwa na pande zisizotutakia mema. Mhe kwa kuwa vijana tumepotoka na utukufu wa Mungu unaelekea kupungua kwetu tusamehe manake naamini si wote walio hivyo kwa hiyo kwa kupitia wale wachache basi na wengine nao wapata msamaha naamini nao pia watakaa na kutafakari na kisha watatubu.
Nikutatakie heri katika yote na naamini wana Monduli, wana wa Arusha na vitongoji vyake wanakusubiri kwa hamu kwani "Mlifurahi pamoja, Mlihuzunika pamoja na mtasonga mbele pamoja"
Ni mwanzo mwingine wa hatua 1,000 mbele....................... I believe as we goby the game will change now from an enemy of the to a man of the people..............