Andiko langu litatofautiana kidogo na wengi. Kwanza nampa pongezi Bakari kwa kurekebisha hesabu zake za kwanza. Ila angekuwa muungwana kwa kukana hesabu zake katika toleo la kwanza. Angalau sasa tunaweza kujadili facts.
Hio figure zako ni stagnant. Kuna vitu vingi hujaviaacount. Naomba nikukumbushe baadhi ya mambo muhim ambayo umeyaacha. Mosi; Wafanyakazi hupanda vyeo. Mf wewe katika sekta uliopo ukiwa unaweza kuwa mhadhiri kamili baadae. Sasa kila sekta watu hupanda vyeo. Pili umesahau kwamba serikali kwa sasa hivi inaajiri saana sekta ya kilimo, afya na elimu. Sijui hesabu za hao watu umeziaccount vipi. Tukiachana na hesabu in real world serikali ikilipa mshahara huo based on yr hesabu ninakuhakikishia ni lazima ifilisike. Kwahiyo ishu iwe ni ukweli kwa kusimamia taaluma na ni vyema pia ukaanisha na madhara kwa uchumi wetu kama mishahara hiyo italipwa.
Hiyo 5 trillion ndiyo makusanyo ya serikali. Sasa hoja yako 5.7 ya GDP, unataka kusema nini? remember si 5.7 ya budget ni GDP!Kikwete amezidi sana Utapeli.. Ikiwa Takwimu zake mwenyewe zinasema serikali ililipa mishahara ya mwaka 2009/10 Trillioni 1.77 ambayo ni asilimia 5.7 tu ya GDP ile hesabu ya makusanyo ya serikali ya Trillion 5. 7 kwa mwaka yalitoka wapi?.. au Mheshimiwa alichanganya asilimia na makusanyo?
Astrolojia sio sayansi, ni upuuzi uliopanguliwa zamani sana! Kwa hiyo napata shida kumtake huyu mtu serious.
NB: Baadhi yetu tuliofurahishwa na sehemu ya kwanza ya ushambulizi wa kihoja na kiakili wa hotuba ya vitisho kwa wafanyakazi ya Rais Kikwete tumempa moyo Mhadhiri Bakari Mohammed wa Chuo Kikuu cha Mzumbe na kupendekeza kwake kwamba japo sehemu ya kwanza ilikuwa imegusa kwa kiasi matatizo ya kifalsafa na kimantiki ya hotuba ya Kikwete Bw. Mohammed angeweza kwenda mbele zaidi. Nashukuru kwamba Bw. Bakari ameenda mbele zaidi katika sehemu hii ya pili ya majibu yake kwa hotuba ya Rais Kikwete. Kinachofurahisha zaidi ni uwezo uliokubuhu wa kuweza kuunganisha hoja zake na sehemu ya historia yetu. Kwa tulio mashabiki wa fikra za Nyerere tumefurahishwa na utetezi wa hoja zake kwa kutumia mojawapo ya hazina kubwa za kifikra yaani hoja za Mwalimu hasa kutoka kijitabu maarufu (ambacho Watanzania wengi nina uhakika hawajawahi kukisoma licha ya kukisikia, yaani "TUJISAHIHISHE". Sehemu hii ya pili ina lengo la kugusa dhamira ya Kikwete na kuamsha dhamira za wananchi kuelewa kuwa mfumo wa utawala wa kifisadi hauwezi kuwa endelevu (the unsustainability of a corrupt political system). Soma kwa furaha!
HOTUBA YA RAIS KIKWETE (2)UPEMBUZI WA KITAKWIMU NA KIASTROLOJIA
§ Takwimu za bajeti zabainisha alivyopotoshwa
§ Vitisho, jazba, na kebehi nini ishara yake?
§ Ilikuwaje Siku ya Jumatatu?
§ Ushauri elekezi
Watanzania, wa hali zote za maisha (masikini, matajiri, wakulima, wafanyakazi, wakwezi, wasomi na wanazuoni) bado tungali wanaitafakari hotuba ya Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliyoitoa siku ya Jumatatu tarehe 3, Mei 2010. Pamoja na jitihada za mtu mmoja mmoja, vikundi vvya watu hata wazee wastaafu (kama Rais wa Awamu ya Pili Mzee Ruksa) wanaitafakari hotuba ile na hatma ya Tanzania kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010 na miaka mitano ijayo! Kwa kuwa (1) takwimu, (2) vitisho, jazba, na kebehi, na (3) Siku ya Jumatatu vilitumika; kwa hivyo basi, makala haya yanajaribu kupembua: (1) vielelezo vya takwimu za bajeti ili kuona uhalali wa shilingi trilioni 6.85293; (2) ishara ya hamaki aliyoionesha Rais wa Nchi; na (3) Upembuzi wa Sayari ya Jumatatu.
Ukiisoma Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2009/2010 iliyosomwa na Waziri wa Fedha na Uchumi Mheshimiwa Mustafa Haidi Mkullo (MB) aliyoisomwa mbele ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) tarehe 11 Juni, 2009 na inayopatikana kwenye www.mof.go.tz/mofdocs/budget na kwenye wavuti wa Bunge la JMT ina mengi ya kelezea juu ya mwelekeo wa gharama za mishahara ya watumishi wa Serikali. Pamoja na mambo mengine na kwa kurahisisha haja ya upembuzi tufanye udondozi, upekuzi na uchambuzi wa taarifa za takwimu juu ya malipo ya mishahara peke yake. Jedwali lifuatalo limenyofolewa (detached) kutoka kwenye Jedwali 2a na Jedwali 2b ya Hotuba ya Bajeti 2009/2010.
Download:
I can challenge you if una uhakika na unachosema na pia kama una facts to back it up.
Tunaweza kujadili hili tukawekana sawa, coz watanzania na waafrika kwa ujumla tunapotoshwa sana,asrtology si uchawi,sasa tujadili ni kivipi siyo science....Ama kwako wewe science ni nini?
Sikubaliani nawe kwenye hoja yako hii. Hotuba za JK ni nzuri pengine ni zile za Mwalimu tu ndizo zinazizidi kati ya Marais tuliowahi kuwa nao. Tatizo zinakosa nguvu ya hoja. Ushahidi ni idadi ya thread zilizoanzishwa humu baada hotuba ile. Tumejikita mno kumjadili yeye kama Kikwete na mapungufu yake tunahama nayo kwenda kila thread itakayomgusa. Tulinganishe tu hoja za Mhadhiri Bakari na hotuba ile ya JK.Kimsingi Rais Kikwete yuko shallow ktk ku-analyse mambo. Mimi huwa sipendi hata kuangalia na kusikiliza hotuba zake kwani anakera sana.
Sikubaliani nawe kwenye hoja yako hii. Hotuba za JK ni nzuri pengine ni zile za Mwalimu tu ndizo zinazizidi kati ya Marais tuliowahi kuwa nao. Tatizo zinakosa nguvu ya hoja. Ushahidi ni idadi ya thread zilizoanzishwa humu baada hotuba ile. Tumejikita mno kumjadili yeye kama Kikwete na mapungufu yake tunahama nayo kwenda kila thread itakayomgusa. Tulinganishe tu hoja za Mhadhiri Bakari na hotuba ile ya JK.
Tumekwisha mchukia basi. Sasa kila atakalolisema litabamizwa ukutani tu. Hotuba ya juzi ilikuwa nzuri ukiondoa "uswahili" mchache alookuwa akiuingiza hapa na pale. Ndio maana bado tunaijadili na wengine wanamjadili yeye badala ya ile hotuba.hotuba za kikwete nthuri..bwa bwa bwa bwa bwa bwaaaa ha!!!.......
si bora kumsikiliza bambo au mzee jangala.....!!
hotuba pekee ya kikwete nzuri ni ile aliyoitoa ya kwanza baada ya kuapishwa bungeni...itafuteni!! kweli tukajuwa nyerere kazaliwa...baada ya hapo ni sarakasi mtindo mmoja!!
Tumekwisha mchukia basi. Sasa kila atakalolisema litabamizwa ukutani tu. Hotuba ya juzi ilikuwa nzuri ukiondoa "uswahili" mchache alookuwa akiuingiza hapa na pale. Ndio maana bado tunaijadili na wengine wanamjadili yeye badala ya ile hotuba.
Mkuu sivyo kabisa, ila imenishangaza tu hizi namba zinavyofanana kwani najua fika kwamba asilimia ya Uzalishaji wa ndani sii sawa na makusanyo ya kodi za serikali. Kisha basi, hakuna mtu anayepinga mfumo mzima wa serikali ktk ukusanyaji wa kodi zake kama mimi kwa sababu najua fika wanaoumia ni wajasiliamali na wafanyakazi kuliko matajiri na viongozi wanaoweza kutumia nguvu ya fedha na vyeo vyao kutolipa kodi stahiki.Hiyo 5 trillion ndiyo makusanyo ya serikali. Sasa hoja yako 5.7 ya GDP, unataka kusema nini? remember si 5.7 ya budget ni GDP!
Andiko langu litatofautiana kidogo na wengi. Kwanza nampa pongezi Bakari kwa kurekebisha hesabu zake za kwanza. Ila angekuwa muungwana kwa kukana hesabu zake katika toleo la kwanza. Angalau sasa tunaweza kujadili facts.
Hizo figure zako ni stagnant? Kuna vitu vingi hujaviaacount. Naomba nikukumbushe baadhi ya mambo muhim ambayo umeyaacha. Mosi; Wafanyakazi hupanda vyeo. Mf wewe katika sekta uliopo unaweza kuwa mhadhiri kamili baadae. Sasa kila sekta watu hupanda vyeo. Pili umesahau kwamba serikali kwa sasa hivi inaajiri saana sekta ya kilimo, afya na elimu. Sijui hesabu za hao watu umeziaccount vipi. Tukiachana na hesabu hizo, in real world serikali ikilipa mshahara huo based on yr hesabu ninakuhakikishia ni lazima ifilisike. Kwahiyo ishu iwe ni ukweli kwa kusimamia taaluma na ni vyema pia ukaanisha na madhara kwa uchumi wetu kama mishahara hiyo italipwa. Pia hoja zako zinasahau kuainisha matumizi mengine muhim ya serikali km miundo mbinu nk.