Mh. Waziri mwenye dhamana, Wanafunzi wa Mitihani(secondary) na Vyuo warudi vyuoni kuendelea na masomo yao

Akilitime

JF-Expert Member
Dec 27, 2017
581
757
Wasalaam
Ndugu Waziri hongera kwa jitihada zako za kukabiliana na janga la Corona nchini.

Ushauri wangu kwako hawa wanafunzi wa secondary wenye mitihani yao ya mwisho pamoja na wanafunzi wa vyuo ni bora tu waendelee na masomo yao huko huko walipokuwa.

Nchi za wenzetu wamefunga shule lakini bado wanafunzi wao wanaendelea kupata masomo yao kupitia online learning! (Kurudi nyumbani hakuwaathiri)

Pia kulikuwa hakuna ulazima sana wanafunzi wa vyuo kurudishwa nyumbani kwao, kitu pekee kingefanyika vyuoni kwao ni pamoja na kudhibiti mihadhara mikubwa wakati wa ufundishaji, na hili wangeratibu manaopanga ratiba za ufundishaji huko vyuoni.

Shule za secondary za boarding zisizo na michanganyo ya watu kutoka nje, basi hawa wanafunzi wangebakizwa tu huko Shuleni wakiwa chini ya uangalizi wa walimu wao.

Swali je kama kukiendelea kuwepo viashiria vya virusi, inamaana masomo yatasitishwa nchini? Au serikali mmejipangaje juu ya hili?

Jana wataalamu wa afya nchini Marekani wanasema chanjo ya Corona yaweza patikana baada ya miezi 18, you see hili sio tatzo la kuisha saivi (Though God can intervine the spread)

Kuruhusu wanavyuo kurejea kwao na kuanza kuzurura mitaani pasipo kuweka Lockdown, Ni sawa na kuchochochea maambukizi tu.

Serikali liangalie upya watoto warudishwe waendelee na masomo, na Elimu ya kujikinga wapatiwe huko huko.

Pia suala la kusogeza mitihani mbele halitaathiri wanafunzi tu, bali hata Wizara itaathiriwa mno.

Ni ushauri tu, unaruhusiwa kuupinga kwa hoja zako, ili kwa pamoja tuendelee kudhibiti maambukizi ya virusi.

Hapa sio mahali pa kuonesha ujuaji bali Ni sehemu ya kujifunza, hivo toa maoni yako kwa lengo la kutuelimisha , na sio kucrash maoni ya mtu.


Mwisho: Sijapinga maamuzi ya serikali kufunga secondary na vyuo. Ninaunga mkono jitihada za serikali kwa kutoa maoni yangu.

Nawasilisha.
 
nilitegemea uandike hivi,


wasingewaruhusu warudi, ila wangefunga muingiliano wa shule hizi na makazi ya wasio wanafunzi. Wangekuwa salama.
 
Upo sahihi mkuu, lakini watafungaje muingiliano pasipokurudishwa vyuoni?

Upo sahihi 💯

nilitegemea uandike hivi,


wasinhewaruhusu warudi,ila wangefunga muingiliano wa shule hizi na makazi ya wasio wanafunzi.wangekuwa salama.
 
Wewe wafikiri waweza kuwa THINK TANK, zaidi ya hao waliolifanyia hilo maamuzi??

Muingiliano wa wafanyakazi, watoa huduma, walimu na familia zao, nani ataudhibiti??

Mitihani ipo watafanya siku ingine, wakiwa na afya ya roho na mwili...maisha ni zaidi ya NECTA na UE.

Everyday is Saturday..................... :cool:
 
Kwa wanafunzi wasiopenda shule kurudishwa nyumbani kwao imekuwa ni sherehe, Lakini kwa wanafunzi wanaojitambua wanaomba kurudishwa shuleni kuendelea na masomo, [="The Masterpiece, post: 34725876, member: 568039"]
Kwani wanafunzi wenyewe wanasemaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
[/QUOTE]
 
Hebu tuache ujuaji kwenye hii Corona , tatizo bado ni kubwa mnoo.

Kwa taarifa yako taasisi nyingi zimeanza kupunguza wafanyakazi ambapo wengine wameelekezwa kufanyia kazi nyumbani ili kupunguza msongamano kwenye maofisi. Serikali ndiyo inasimamia hili tena kimya-kimya ili kupunguza taharuki.

Video za kina Mwana-FA zisiwafanye mkarelax na kujidanganya,
upungufu wa maambukizi huko China usitufanye tukarelax kwasababu very soon tutajuta.

Corona bado ni tishio especially kwa nchi masikini kama hii Tz mnayoiita "dona kantre"

Kama kuna mwanafunzi au mwanachuo nyumbani kwako msisitize atulie nyumbani hii sio likizo ya kuetembeleana kwenda kupiga selfie.
Tutalia very soon tukiendelea kuchukulia poa hili janga.

#StayHome
 
Akilitime,
Hoja yako ni nzuri lakini hazitekelezeki.
1. Wanafunzi wa shule za bweni wakiruhusiwa kuendelea na masomo, vipi kuhusu wa shule za kutwa katika vidato hivyo hivyo?.

2. Wanachuo wakiruhusiwa kuendelea na masomo, wakati vyuo vina miingiliano mikubwa ya watu, udhibiti wa kuenea kwa Corona ungekuwaje?

3. Kusitisha masomo ni njia nzuri ya kudhibiti kuenea kwa virusi haraka hivyo serikali imetenda vyema, masomo yataanzia hapo hapo yalipokomea.

4. Wazazi, walezi na jamii, wasaidieni wanafunzi kujifunza huko majumbani, Elimu sio shuleni/Chuoni pekee.
Big up Serikali kwa hatua hii muhimu
 
Mkuu ujuaji nivmwingi sana Tanzania na wewe ni miongoni mwa hao wajuaji,OK chukulia wanafunzi kunauwezekano wa kuwabana wasitoke,je mtumishi(mwalimu) kama Mimi ambaye nazunguka huku na kule kutafuta riziki nikiukwaa huo ugonjwa huoni kuwa ni rahisi sana kuwaambukiza watoto? Pia fuatilia Irani wafungwa wanaachiwa huru ,unataka kuniambia wafungwa wako huru kama wanafunzi?

Pili umeongea kwa kuuzaradharau ugonjwa pengine kutokana na kusikia idadi ya waathirika nchi mwetu kuwa ni ndogo,tambua kuwa huu ugonjwa hauna masihara,ukikupata unaondoka na wewe,hebu angalia Uganda hii nchi haijakumbwa na ugonjwa lakini still wamefunga vyuo na mashuleni for 32 days

Tatu sidhani kama wewe unauelewa zaidi kuliko wizara ya elimu na afya zote kwa pamoja kwani huko kunawasomi wamekaa wakachambua na kuona ni heri vyuo na shule zifungwe


Mwisho watanzania tupunguze ujuaji,tuiache serikali ifanye lile inaloamini ni jema kwa masirahi ya afya za watu wake Akilitime,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom