Mh.spika!

laigwenan

JF-Expert Member
Apr 13, 2012
325
79
Ndugu wa Tz wenzangu habari za muda huu,Hakika tumeshuhudia udhaifu mkubwa wa Spika wetu sababu ya Uchama badala ya uspika,ni maoni yangu kuwa spika atokane na chama tawala na naibu spika atoke upinzani
 
nimeshasema hakuna kutaja kesi iliyoko mahakamani.
jamani mbona mnataka ku...........
wenje we unataka ku............
jamani.......

my take.
rais yupo juu ya sheria kuongelea kesi iliyopo mahakamani na kuitolea maamuzi.
vyombo vya habari viko juu ya sheria kuripoti habari za mahakamani na kuna siku kwa makinda ukitaja tu neno ulimboka utakuwa umevunja kanuni za bunge.
 
Ndugu wa Tz wenzangu habari za muda huu,Hakika tumeshuhudia udhaifu mkubwa wa Spika wetu sababu ya Uchama badala ya uspika,ni maoni yangu kuwa spika atokane na chama tawala na naibu spika atoke upinzani

Mambo yatakua yaleyale, spika atakua hatoki katika kiti mwanzo mwisho.....
 
Maoni yangu spika asiwe mwanachama wa chama chochote cha siasa na asiwe mbunge.
Tunaweza kumpata mtu wa aina hiyo Tanzania? Kwa sababu mimi nadhani tatizo ni chama tawala kutaka kulitawala Bunge. Anayoyafanya Spika hayafanyi kwa matakwa yake, bali matakwa ya chama tawala
 
Hivi ni kweli kwamba mbunge akitaja matukio ya mauaji yanayoonekana ni ya kisiasa yaliyoko mahakamani bila kueleza mwenendo wa kesi hizo unavyokwenda, atakuwa ameingilia uhuru wa mahakama? Au uhuru wa mahakama ni salama unapotajwa na wabunge wa ccm pamoja na baba mwenye nyumba tu ila sio wabunge wa upinzani? Mmhh! kweli ukiona mtu mzima analia ..............................
 
Speaker kwa tanzania alikuwa mzee Samwel Sitta, hao wengine wanalinda masilahi tu na watajutia kumfanyia Sitta hiyana na kumng'oa kwenye kiti cha speaker.....
 
madhara ya kuweka spika bila ridhaa ya wananchi ni makundi na matabaka bungeni.Kwasasa masula yenye kero ya wananachi hayatakiwi bungeni, ili kuilinda serikali na chama chake tawala.Kimsingi ni uvunjanji wa katiba sababu bunge si serikali , ni chombo cha kusimamia serikali na ni chombo cha kitetea serikali.Haya yanatokea kwa dhana ya kudhibiti uozo serikalini na watendaji wake baovu wasifichuliwe.Ni ushahidi wa wazi kuwa bajeti hii ni upotezaji wa muda kijadli sababu kero za wananchi kwa masilahi ya umma, zinadhibitiwa.Spika muhimili wa chama na serikali .Ni aibu sana
 
:alien: NA KWELI HUYO SPIKA ANNA MAKINA a.k.a Bi KIROBOTO AVAE KABISa. Unajua CCM wamechukia SITA kwa sababu he was transparent and not basing on any Political Parties kwa hivyo wakamtua hawa CCM kumweka huyo KIROBOTO ili atete CCM na kunyamazisha Wapinzani. Kwa kweli kuna kazi kwa CCM na awataweza. Ya pili sisi Watanzania tunataka recruitements zote za kila kitu hata kuajiri iwe wazi kama wenzetu WAKENYA wanafanya. sIO MTOTO WA FLANI AU MKUBWA FLANI.

SPIKA ANNA MAKINA AVAE KABISA NA ANA ELIMU YAKUA SPIKA KABISA. NANI ANA CV YAKE APOSTI JAMANI. TUMA MAVIHIYO WENGI CCM AMBAE WANALINDWA NA CCM
.
 
Maana yangu ni kwamba chama tawala chenye Wabunge wengi wana pinda Upinzani wanaofuatia wana Mbowe, chama tawala wana Lukuvi upinzani wana Tundu lissu kwanini isiwe hivyo kwa uspika ili kuleta usawa! Chama tawala chenye wabunge wengi watuletee spika na upinzani watuletee naibu spika?
 
Dawa ni usawa tu! Chama chenye wabunge wengi wamtafute Spika chama kikuu cha upinzani watutafutie Naibu spika kwisha!
 
Siku mheshimiwa Mkosamali alivyokuwa anachangia Bajeti ya Wizara ya fedha, alisema serlkali ya CCM imeshindwa kila idara huku Lukuvi akimtolea macho anatafuta mwongozo.
Wanaona wakiachia bunge liwe huru basi kushindwa kwao katika kila sekta kutaonekana dhahiri!
 
:alien: NA KWELI HUYO SPIKA ANNA MAKINA a.k.a Bi KIROBOTO AVAE KABISa. Unajua CCM wamechukia SITA kwa sababu he was transparent and not basing on any Political Parties kwa hivyo wakamtua hawa CCM kumweka huyo KIROBOTO ili atete CCM na kunyamazisha Wapinzani. Kwa kweli kuna kazi kwa CCM na awataweza. Ya pili sisi Watanzania tunataka recruitements zote za kila kitu hata kuajiri iwe wazi kama wenzetu WAKENYA wanafanya. sIO MTOTO WA FLANI AU MKUBWA FLANI.

SPIKA ANNA MAKINA AVAE KABISA NA ANA ELIMU YAKUA SPIKA KABISA. NANI ANA CV YAKE APOSTI JAMANI. TUMA MAVIHIYO WENGI CCM AMBAE WANALINDWA NA CCM
.
Wengine matatizo tu. Kiswahili taabu kingereza shida. Hebu na ww tupe cv yako
 
Viongozi wengi wa ccm hawana hofu ya Mungu na ndivyo ilivyo kwa Spika wetu, wao wanaabudu sangoma zaidi ukiwaona misikitini au makanisani ni ili tu wananchi wajue ni wenzetu kumbe hakuna kitu.

Kimsingi Sitta alikuwa na hofu ya Mungu japo kwa kiwango flani ndio maana yeye alikuwa uchama pembeni uzalendo mbele katika kujadili mustakabali wa taifa letu.. nakumbuka dk zake 15 wakati wa hotuba ya Kikwete bungeni zilikuwa na nguvu kuliko hotuba ya karibu masaa 2..!
 
kweli demokrasia haipo bungen.sisi tuseme ya mahakamani lakini wao kwanini wazuiwe.hii sasa wana ccm wenzetu mnatufukuza kijanja.mimi ni mjumbe wa ccm ngaz ya mkoa lakini mwenendo tunaokwenda nao sio,
 
Back
Top Bottom