Mh.Sitta amekiri Serikali ya sasa ni dhaifu

Mh.Sitta amekiri Serikali ya sasa ni dhaifu

BONGOLALA

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2009
Posts
16,511
Reaction score
11,911
Amesema hayo katika kipindi cha duru za siasa StarTV kwani imeshindwa kabisa kudhibiti biashara ya madawa ya kulevya nchini.Pia anategemea raisi mwaka 2015 ni yule anayepita na kugawa gawa fedha hovyo hovyo wanafiki wanamsupport!Msikose Jumapili saa 4:30 asubuhi kuangali akipindi hicho
 
Hata mimi nimemsikia lakini nikadhani labda nimesikia vibaya
 
huyu mzee hata haeleweki,kwa nini hachui uamuzi kama alioufanya mrema wakati ule alipojiuzulu toka madarakani ndani ya ccm?anafanyaje kazi na watu anaojua kuwa hawana tija kwa taifa?
 
naye kwa kuwa anaendelea kukaa kwenye serikali hii naye ni🙂dhaifu. Hata hivyo kama anataka kupoteza kucha na meno si awataje? yeye ikulu si kama nyumbani si amfuate Mkulu ampe orodha. Unajua mkulu naona aibu kwani hata mawaziri nao wamo; hivyo uenda naye yumooo?
 
Huyo mzee ni kinyonga sana haeleweki anatafuta masalai yake hana jipya mwanzo nilimkubali lakini sasa sitaki ata kumwona na kumsikiliza utakuta anawapiga vijembe wapinzani na kati wale wanatetea wanyonge.
 
huyu mzee hata haeleweki,kwa nini hachui uamuzi kama alioufanya mrema wakati ule alipojiuzulu toka madarakani ndani ya ccm?anafanyaje kazi na watu anaojua kuwa hawana tija kwa taifa?

Jamani mbona mnamlaumu mzee wa watu bure? Ina maana wewe ukiwa mchezaji mzuri katika timu ambayo ina wachezaji wengine dhaifu ni lazima uihame timu yako? Si unasubiri usajiri ujao uone kama mambo yatabadirika?

La sivyo Messi angehama timu yake siku nyingi!
 
Six alishawahikufanya jambo gani kwa maslahi ya taifa unaloweza kulipigia mfano?
 
Ukiona mwanafamilia anaongelea nje ya familia issue ambazo angepaswa kuongea ndani ya familia ujue kachoshwa. Pia inasaidia kuonesha watu kuwa familia ile haiko intact, kuhama ni jambo jingine na kukaa kunatupa picha nzuri ambao tuko nje kujua kuwa pale si shwari. Angehama mara moja Mh Sitta wangesema na kuzusha yale ambayo yangesikilizwa sasa hivi hawana cha kusema.
 
jamani hebu wanapsychology wamkalishe wamwambie hivi unataka nini mzee?
Ana mambo mengi ila naona kama hajayapangilia maana anazungumza hili halijaisha anazungumza na lingine
Hao watakaogawa hela anaowazungumzia ni kutokana na mtandao wao ulivyofanya au kashafika 2015 hofu yake nini
 
Mkwereee ni dhaifu kiasi kwamba hakuna tena collective responsibility serikalini ;kila waziri ana mapembe na ndio maana wakina Mwakyembe wanaingilia kazi za kuendesha mashirika wakati hiyo siyo kazi ya wizara na hakuna wa kuwakalipia!!!
 
Ameishiwa serikali ni nani ?baraza la mawaziri si yumo? Aache kuzeeka vibaya ,kama sisi tunamsapoti mpinzani wake anatuona wanafiki yeye ndo mnafiki namba moja
Amelitia hasara taifa kwa kutudanganya mitambo ya richmond sekelepa tumemkaria kimya ndo mana anadiriki kututukana .

Sent from my BlackBerry 9700 using Jamii Forums
 
Mhhhh blaza yaani umesikia promo tu na umeshaunganisha dot!

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
BONGOLALA na wewe ukaamin kwamba mrema alijiuzulu ndan ya ccm!!!?????? Bhaaaaaaaaaaaa....
 
Last edited by a moderator:
jamani mbona mnamlaumu mzee wa watu bure? Ina maana wewe ukiwa mchezaji mzuri katika timu ambayo ina wachezaji wengine dhaifu ni lazima uihame timu yako? Si unasubiri usajiri ujao uone kama mambo yatabadirika?

La sivyo messi angehama timu yake siku nyingi!

acha ubwege messi angekuwa arsenal angehama sio barca..ka hujui mpira kaa kimya.
 
Huyu ashatuchosha mara CCJ ndo maana wazee wa Tabora wamemtosa Uchifu na kumpa mamvi. Hv wang'oa kucha mko wapi?
 
Huo ni mtizamo wake, na pengne hawezi fanya lolote khs sakata la drugsdealer.

akili za kuambiwa ongeza na za kwako..
 
Tatizo kubwa ni kwamba hatuna uvumilivu wa kupokea mawazo chanya ya wenzetu.Mtu anapotoa mawazo yake ni vyema tukayatafukari kwa kina na siyo kuyabeza pasipo kutoa hoja.Mzee Sitta anakipa Chama chake changamoto na kuonyesha wapi kimepotoka.Asihukumiwe kwa kumbeza.
 
Back
Top Bottom