Mwananzengoo
Member
- Jun 8, 2014
- 56
- 25
Hizi kauli za watuhumiwa wa escrow, Mhe. Kikwete unajitenga vipi nazo ?
Najaribu sana kuilazimisha akili yangu izione kauli za waheshimiwa watuhumiwa wa uchotaji wa fedha za akaunti ya Tegeta escrow kuwa za kawaida, lakini inashindikana. Hapa zimesemwa kauli nyingi ambazo zinaonyesha kujiamini kunakovuka mipaka kwa watuhumiwa wa escrow. Majibu haya ya kujiamini yameanza tangu kuibuliwa kwa kashifa hii nzito inayotia doa kubwa utawala wa awamu ya nne nje na ndani ya nchi.
Majibu ya AG bungeni yalionyesha kujiamini kana kwamba Kuna mtu mkubwa anahusika na hiyo issue. Hiyo ilisindikizwa na mbunge mmoja kuitwa tumbili. Nasikia kuwa Mhe Rais wakati akijibu ombi la kujiuzulu alimpongeza na kutambua uadililifu wake.
Mhe. waziri Tibaijuka naye katoa kauli inayomtaka rais ajitenge nayo, pale aliposema kuwa akijiuzulu rais atamshangaa. Hii inaonyesha boss anafahamu madudu haya. Kujiamini kwa mama huyu kunaacha maswali mengi zaidi ya majibu.
Watanzania wameshangazwa na waziri Tibaijuka kuandaa mkutano wa waandishi wa habari kwa hela ya serikali ili kuzungumzia tuhuma zake binafsi. Wadau hawakubaliani na hoja kwamba tuhuma hizi ni za mtu binafsi. Nyerere alipata kusema kuwa, " Watanzania wanataka mabadiliko, wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM."
Najaribu sana kuilazimisha akili yangu izione kauli za waheshimiwa watuhumiwa wa uchotaji wa fedha za akaunti ya Tegeta escrow kuwa za kawaida, lakini inashindikana. Hapa zimesemwa kauli nyingi ambazo zinaonyesha kujiamini kunakovuka mipaka kwa watuhumiwa wa escrow. Majibu haya ya kujiamini yameanza tangu kuibuliwa kwa kashifa hii nzito inayotia doa kubwa utawala wa awamu ya nne nje na ndani ya nchi.
Majibu ya AG bungeni yalionyesha kujiamini kana kwamba Kuna mtu mkubwa anahusika na hiyo issue. Hiyo ilisindikizwa na mbunge mmoja kuitwa tumbili. Nasikia kuwa Mhe Rais wakati akijibu ombi la kujiuzulu alimpongeza na kutambua uadililifu wake.
Mhe. waziri Tibaijuka naye katoa kauli inayomtaka rais ajitenge nayo, pale aliposema kuwa akijiuzulu rais atamshangaa. Hii inaonyesha boss anafahamu madudu haya. Kujiamini kwa mama huyu kunaacha maswali mengi zaidi ya majibu.
Watanzania wameshangazwa na waziri Tibaijuka kuandaa mkutano wa waandishi wa habari kwa hela ya serikali ili kuzungumzia tuhuma zake binafsi. Wadau hawakubaliani na hoja kwamba tuhuma hizi ni za mtu binafsi. Nyerere alipata kusema kuwa, " Watanzania wanataka mabadiliko, wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM."