Mh. Rais Magufuli; Iongezee uwezo STAMIGOLD

Mh. Rais Magufuli; Iongezee uwezo STAMIGOLD

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,198
Reaction score
7,539
Nimekuwa nikiwaza kwa muda sasa tokea sakata la Makinikia ya ACACIA na Barrick Gold.

Nimewaza ikiwa Makampuni haya yalikuwa na yamekuwa yakitengeneza faida kubwa kiasi ambacho tumeelezwa na yangeweza kulipa kodi ya Matrilioni tuliyoelezwa na bado makampuni hayo yakabaki na faida nzuri baada ya kutoa gharama zauendeshaji, basi Tanzania tuna dhahabu yenye thamani kubwa sana.

Kwa mantiki hiyo, namshauri Rais Magufuli; akiona inafaa, aijenge uwezo wa hali ya juu kampuni ya kizalendo ya STAMIGOLD kwenye eneo la mtaji, vifaa mitambo na rasilimali watu.

Hii itasaidia kwa maana kwamba, faida hiyo kubwa, na ile ambayo ingelipwa kama kodi na ajira za kutosha vyote vitabaki hapa hapa nchini kwa maendeleo ya Watanzania.

Naomba kuwasilisha hoja.
 
sawa ngoja nipeleke hoja yako kwenye meza ya rais mzalendo akalishugulikie swala lako
 
sawa ngoja nipeleke hoja yako kwenye meza ya rais mzalendo akalishugulikie swala lako
Nafikiri kama uwekezaji kwenye dhahabu unalipa kwa kiasi hicho, ipo haja ya kujitahidi kuchimba wenyewe dhahabu yetu. Haimaanishi kuwa kampuni zinazotaka kuchimba zinyimwe vibali, lakini tuwe na kampuni ambayo inaweza kufanya vizuri kama au zaidi ya kampuni binafsi za kigeni.
 
Nafikiri kama uwekezaji kwenye dhahabu unalipa kwa kiasi hicho, ipo haja ya kujitahidi kuchimba wenyewe dhahabu yetu. Haimaanishi kuwa kampuni zinazotaka kuchimba zinyimwe vibali, lakini tuwe na kampuni ambayo inaweza kufanya vizuri kama au zaidi ya kampuni binafsi za kigeni.
nimekuelewa na nimemudokezea hapa alishugulikie hili tupate utajili haraka tuachane na kukopa ili tuanze kukopesha harakahara.
 
Nafikiri kama uwekezaji kwenye dhahabu unalipa kwa kiasi hicho, ipo haja ya kujitahidi kuchimba wenyewe dhahabu yetu. Haimaanishi kuwa kampuni zinazotaka kuchimba zinyimwe vibali, lakini tuwe na kampuni ambayo inaweza kufanya vizuri kama au zaidi ya kampuni binafsi za kigeni.

Ikiwa ni kampuni binafsi ya watanzania hilo litawezekana. Lakini kama ni hizi kampuni za umma itakuwa ngumu maana hata bodi zake utakuta zimejaa makada wastaafu wanaomini kwenye chama chao kubaki tu madarakani. Nasema hivyo kwa uzoefu wa makampuni ya umma yanavyoondeshwa chini ya viwango. Labda kama utahitaji mifano.
 
Haina shida kama akiweka mezani kama Trillioni 1.0 hivi watachimba ndoh tabu.....
 
Makampuni binafsi ya kibongo huwa wanachimba kienyeji ila wanabahatisha kupata ( KUHIRA) dhahabu nyingi zikiwemo VIKOLE lakini badala ya kununua vifaa ili kuchimba kisasa zaidi wanazifanyia fedha hizo vitoko vya ajabu na kesho yake wanaanza kuililia serikali iwape uwezo wakati wamezichezea walizozipata
 
Makampuni binafsi ya kibongo huwa wanachimba kienyeji ila wanabahatisha kupata ( KUHIRA) dhahabu nyingi zikiwemo VIKOLE lakini badala ya kununua vifaa ili kuchimba kisasa zaidi wanazifanyia fedha hizo vitoko vya ajabu na kesho yake wanaanza kuililia serikali iwape uwezo wakati wamezichezea walizozipata
 
Ikiwa ni kampuni binafsi ya watanzania hilo litawezekana. Lakini kama ni hizi kampuni za umma itakuwa ngumu maana hata bodi zake utakuta zimejaa makada wastaafu wanaomini kwenye chama chao kubaki tu madarakani. Nasema hivyo kwa uzoefu wa makampuni ya umma yanavyoondeshwa chini ya viwango. Labda kama utahitaji mifano.
Mkuu yanaweza kubadilika, ishu ni mitizamo ya watu kama walibadili mitizamo, wakijifunza kwa nchi nyingine wanavyofanya, wakawa na watu wenye ujuzi na morali, vifaa vya kisasa na teknolojia na wakapatiwa mtaji, pendine wanaweza kufanya vizuri. Kampuni binafsi sawa lakini tatizo mitaji na huwezi ukasema serikali itoe mtaji kwa kampuni binafsi bure bure. Makampuni binafsi yanaweza kukopa benki kama vile TIB n.k
 
Nafikiri ungejaribu kwanza kufanya uchunguzi kule Tulawaka ambapo kampuni yetu mama ya stamigold inachimba dhahabu, hapo ndio ungepata picha kamili kama tunaweza au hatuwezi..

Tukiweza kutenganisha siasa na serikali, siasa na utendaji, siasa na utalaamu tutafanikiwa lakini tofauti na hapo hakuna tutakachofanikiwa..
 
Makampuni binafsi ya kibongo huwa wanachimba kienyeji ila wanabahatisha kupata ( KUHIRA) dhahabu nyingi zikiwemo VIKOLE lakini badala ya kununua vifaa ili kuchimba kisasa zaidi wanazifanyia fedha hizo vitoko vya ajabu na kesho yake wanaanza kuililia serikali iwape uwezo wakati wamezichezea walizozipata
Pia sijaona njia nyingine ambayo serikali inaweza kusaidia kampuni binafsi zaidi ya njia ya mikopo ya benki. Sioni kama kuna njia nyingine inaweza kuwa effective.
 
Nafikiri ungejaribu kwanza kufanya uchunguzi kule Tulawaka ambapo kampuni yetu mama ya stamigold inachimba dhahabu, hapo ndio ungepata picha kamili kama tunaweza au hatuwezi..

Tukiweza kutenganisha siasa na serikali, siasa na utendaji, siasa na utalaamu tutafanikiwa lakini tofauti na hapo hakuna tutakachofanikiwa..
Kutokana na yele tuliojifunza kwenye somo la Acacia, hapo sasa ndio tunatakiwa kuona hata umuhimu wa kuangalia maeneo yeye udhaifu kwenye kampuni za kizalendo na kuyafanyia kazi. Changamoto zipo kila siku lakini kama zikishughulikiwa kikamilifu, mafanikio yanaweza kupatikana.
 
Kuna jamaa yangu anafanya kazi kule anasema wamefunga kule Tulawaka kwa wiki mbili na sababu ni kupungukiwa mafuta na gharama za uendeshaji kwa ujumla,ni kweli kuna umuhimu wa kupeleka nguvu kubwa kwenye cha kwetu na kua na usimamizi wa hali ya juu.hata hii migodi mingine tunapaswa tuchimbe wenyewe na mzungu awepo tu kama mfanyakazi na mkodisha mitambo tumlipe kulingana na tutakachopata.

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Kuna jamaa yangu anafanya kazi kule anasema wamefunga kule Tulawaka kwa wiki mbili na sababu ni kupungukiwa mafuta na gharama za uendeshaji kwa ujumla,ni kweli kuna umuhimu wa kupeleka nguvu kubwa kwenye cha kwetu na kua na usimamizi wa hali ya juu.hata hii migodi mingine tunapaswa tuchimbe wenyewe na mzungu awepo tu kama mfanyakazi namkodisha mitambo tumlipe kulingana na tutakachopata.

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
Kama ikitokea hiyo migodi ya wawekezaji wa kigeni wakalipa sehemu ya kodi wanayodaiwa, ni vyema kiasi ikatumika kuimarisha STAMIGOLD kwa kuwa kazi ya uchimbaji dhahabu huhitaji mtaji mkubwa ili iweze kuwa na ufanisi.
 
Kutokana na yele tuliojifunza kwenye somo la Acacia, hapo sasa ndio tunatakiwa kuona hata umuhimu wa kuangalia maeneo yeye udhaifu kwenye kampuni za kizalendo na kuyafanyia kazi. Changamoto zipo kila siku lakini kama zikishughulikiwa kikamilifu, mafanikio yanaweza kupatikana.

Mkuu uchimbaji madini kwa njia za kisasa in large scale tunahitaji akili iliyokomaa isiyo na chembe ya ujinga na uzembe. Ukweli ni kwamba hao Wazungu wamewekeza hapa lakini kwa 90% wameajiri watanzania na wanafanikiwa kwa kuwatumia hao watanzania..

Kwa nini hao wageni wanafanikiwa kwa kuwatumia watanzania?? Jibu ni rahisi saana maslahi mazuri na kujali watendaji... Huwezi kuajiri Engineer mzuri mwenye uzoefu na mgodi na anayeweza kufanya kazi kwa kasi ya mgodi ukamlipa hizi tunaita TGS sijui..

Mshahara mnono, matibabu binafsi na kwa familia kwenye hospitali za kisasa kama Aghakhan na South Africa ikibidi, usalama kazini kwa viwango vya kimataifa, kulipa kwa wakati masupplier na wafanyakazi, kutokuwa na urasimu kwenye uendeshaji, usawa katika utoaji wa ajira na kwa wafanyakazi..
 
Mkuu uchimbaji madini kwa njia za kisasa in large scale tunahitaji akili iliyokomaa isiyo na chembe ya ujinga na uzembe. Ukweli ni kwamba hao Wazungu wamewekeza hapa lakini kwa 90% wameajiri watanzania na wanafanikiwa kwa kuwatumia hao watanzania..
Mkuu kwa kiasi kikubwa uko sahihi lakini ili hayo yawezekene, inahitajika utashi wa kisiasa na kuwekeza mtaji mkubwa. Nakubaliana nawe mkuu, na yote haya yanaweza kufanyika tukiamua na viongozi wetu wakiwa na mtizamo wa namna hiyo.
 
Samurai umeeleza ni kwanini hata viwanda vyetu vingi vilikufa sababu ni fedha za uendeshaji. Mfanyakazi yoyote akilipwa vizuri na akasimamiwa vizuri bila upendeleo atawajibika.

Stamigold wengi walikuwa acacia lakini walipotoka kwenda huko wanalialia kwamba mambo si mazuri sababu yale waliyokuwa wakilipwa acacia hayapo tena.
Training and Development pia acacia waliwekeza vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samurai umeeleza ni kwanini hata viwanda vyetu vingi vilikufa sababu ni fedha za uendeshaji. Mfanyakazi yoyote akilipwa vizuri na akasimamiwa vizuri bila upendeleo atawajibika.

Stamigold wengi walikuwa acacia lakini walipotoka kwenda huko wanalialia kwamba mambo si mazuri sababu yale waliyokuwa wakilipwa acacia hayapo tena.
Training and Development pia acacia waliwekeza vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umezungumzia eneo la training and development. Mkuu hili ni eneo muhimu mno ila naona ni kama taasisi za kizalendo hazilitilii manani karibu kwenye kila sekta. Kwa kiasi kikubwa training zinaonekana ni kama kupoteza fedha ila kiuhalisia mafunzo ya mara kwa mara ni muhimu sana kwa maendeleo ya taasisi hasa zile ambazo ni strategic na zinazolenga kutengeneza faida. Nafikiri tunajifunza kutoka kwenye taasisi za kimataifa na siku moja tutalielewa hili na kulifanyia kazi.

usitembee juu ya ardhi kwa majivuno
 
Barrick zamani Acacia kuna dogo mmoja namjua wa undeground mining alipelekwa Australia miaka 3 alikuwa junior geologist, Acha Sierra Leone, Mid level managers wengi walipelekwa Capetown University kufanya Management Courses.

Huwezi kupanda mbigiri ukavuna mchicha hata siku moja. Training an Development ndio ina add value to production

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom