Mh!..... Nadaiwa karibu naadhirika sasa………..

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,393
Hebu tuchukulie kwamba unadaiwa fedha na wanaokudai au anayekudai amechachamaa. Huenda amefikia hatua ya kutaka kukuadhiri sasa. Anataka kuja kwako kuchukua vifaa vyako au amepania kukupeleka mahakamani. Labda niseme tu kwamba, unadaiwa na anayekudai amekubadilikia na umeingia kwenye hofu.

Hebu niambie, kama ni wewe umeingia kwenye dhahama hiyo ungefanyaje?
 
Ni wewe unayedaiwa au unatoa mfano watu waujadili? Kwasababu heading na content havina uhusiano kabisa.
 
mtambuzi mtata ww.
wel ni iv bora ukope kwingine umlipe yy jaman kuliko kusubiri kudharirishwa.
dawa ya deni kulipa kaka.
 
Naam, Dawa ya deni kulipa. Tumia maarifa yote ulipe deni then angalia next time usikope deni ambalo litakushinda kulipa na kukuletea matatizo.
 
Hebu tuchukulie kwamba unadaiwa fedha na wanaokudai au anayekudai amechachamaa. Huenda amefikia hatua ya kutaka kukuadhiri sasa. Anataka kuja kwako kuchukua vifaa vyako au amepania kukupeleka mahakamani. Labda niseme tu kwamba, unadaiwa na anayekudai amekubadilikia na umeingia kwenye hofu.

Hebu niambie, kama ni wewe umeingia kwenye dhahama hiyo ungefanyaje?

Dawa ya deni ni kulipa na si kulikimbia
 
inabidi akili ya ziada itume ,unatafuta sehemu nyingine inayokuamini unakopa na kwenda kumlipa mhusika ,wakati huo unaanza kujipanga kurudisha pesa nyingine uiyokopa,
Kukopa ni harusi kulipa ni matanda
 
Hapo ni kukopa sehemu nyingine na kulipa, kama ikishindikana ni kukimbia!

Kama watu wengine washakusoma kuwa wewe ni kimeo na hulipi madeni wakagoma kukukopesha utafanyaje?
Na kama una familia ukikimbia hudhani familia ndio itaadhirika. Je ukirudi na mkeo akikwambia alibangaiza akalipa hilo deni utamuamini?
 
inabidi akili ya ziada itume ,unatafuta sehemu nyingine inayokuamini unakopa na kwenda kumlipa mhusika ,wakati huo unaanza kujipanga kurudisha pesa nyingine uiyokopa, Kukopa ni harusi kulipa ni matanda


Yaani unadaiwa, halafu unaendelea kukopa!
 
mtambuzi mtata ww.
wel ni iv bora ukope kwingine umlipe yy jaman kuliko kusubiri kudharirishwa.
dawa ya deni kulipa kaka.

Ha ha ha ha haaaaa...................Kumbe mimi ni mtata!
 
Kuliko kutolewa vyombo nyumbani kwangu bora aende mahakamani kesi inaendelea namimi naendelea kutafuta hela ya kulipa.... lakini usipende kukopa usichoweza kulipa
 
Back
Top Bottom