Mzee wa ngano
Senior Member
- May 3, 2012
- 184
- 55
Niliposikia huyu bwana kapewa wizara ya uchukuzi nilijua kuwa sasa kumekucha. Mimi hua siku zote namchukulia huyu muheshimiwa kama mtu wa kazi miongoni mwa watu wachache wa CCM. Nilijua anataka kufufua makampuni ya uchukuzi likiwemo TRL. Nasikitika kuwaambia watanzania kuwa hayo mambo ambayo hadi sasa kayafanya hayana mchango wowote kwa maendeleo ya TRL bali kwa wakazi wa maeneo ambayo reli inapita na zaidi sana yanaididimiza TRL. wana JF Napenda mjue kuwa TRL haiwezi kufaidika kwa ajili ya city train, train ya abiria ya kwenda Mwanza, Kigoma au Mpanda.
Hizi train zinatembea ili kutoa huduma kwa wananchi wa nchi hii. Kwa mantiki hiyo mimi sikuona kama huyu muheshimiwa sana alikuwa na sababu ya kuanza na haya mambo. Ila najua kwavile mambo haya yanagusa watanzania wLio wengi naona kaona bora ayafanye kwanza ili watu wamjue. Kakosea sana. Kama kumjua watu tulishamjua tangu enzi za sakata la richmond na anguko la Lowasa. Akiendelea kutafuta sifa zaidi anguko lake kisiasa litakuwa kubwa kuliko mtu awaye yote aliyewahi kuongoza hiyo wizara. NAWASILISHA.
Hizi train zinatembea ili kutoa huduma kwa wananchi wa nchi hii. Kwa mantiki hiyo mimi sikuona kama huyu muheshimiwa sana alikuwa na sababu ya kuanza na haya mambo. Ila najua kwavile mambo haya yanagusa watanzania wLio wengi naona kaona bora ayafanye kwanza ili watu wamjue. Kakosea sana. Kama kumjua watu tulishamjua tangu enzi za sakata la richmond na anguko la Lowasa. Akiendelea kutafuta sifa zaidi anguko lake kisiasa litakuwa kubwa kuliko mtu awaye yote aliyewahi kuongoza hiyo wizara. NAWASILISHA.