Mh. Mwakyembe TRL ITAKUSHINDA UKIENDEKEZA KUTAKA SIFA.

Mh. Mwakyembe TRL ITAKUSHINDA UKIENDEKEZA KUTAKA SIFA.

Jamaa kachemsha ilikuwa story tu bar plus moja moto moja baridi asubuh anaamka tu jf ndani ya room.......
 
Hivi lowassa akiwa presidaa mwakyembe atapewa wizara kweli?
 
Niliposikia huyu bwana kapewa wizara ya uchukuzi nilijua kuwa sasa kumekucha. Mimi hua siku zote namchukulia huyu muheshimiwa kama mtu wa kazi miongoni mwa watu wachache wa CCM. Nilijua anataka kufufua makampuni ya uchukuzi likiwemo TRL. Nasikitika kuwaambia watanzania kuwa hayo mambo ambayo hadi sasa kayafanya hayana mchango wowote kwa maendeleo ya TRL bali kwa wakazi wa maeneo ambayo reli inapita na zaidi sana yanaididimiza TRL. wana JF Napenda mjue kuwa TRL haiwezi kufaidika kwa ajili ya city train, train ya abiria ya kwenda Mwanza, Kigoma au Mpanda.

Hizi train zinatembea ili kutoa huduma kwa wananchi wa nchi hii. Kwa mantiki hiyo mimi sikuona kama huyu muheshimiwa sana alikuwa na sababu ya kuanza na haya mambo. Ila najua kwavile mambo haya yanagusa watanzania wLio wengi naona kaona bora ayafanye kwanza ili watu wamjue. Kakosea sana. Kama kumjua watu tulishamjua tangu enzi za sakata la richmond na anguko la Lowasa. Akiendelea kutafuta sifa zaidi anguko lake kisiasa litakuwa kubwa kuliko mtu awaye yote aliyewahi kuongoza hiyo wizara. NAWASILISHA.

Kha umetumwa?
 
Jamani kutumiwa kubaya sana. Huyu katumwa kumchafua Mwakyembe, sasa hata hajui aanzie wapi. Waambie walikutuma wakupe na maneno ya kuandika.
 
Wewe mwenyewe unakiri kuwa huduma zinawagusa wananchi..hapohapo unatarajia anguko la Mwakyembe. Unataka huduma zimguse nani kuzuia anguko la Mwakyembe kisiasa.?
 
Mtoa mada hajaeleweka...ila ndani ya trl kuna mazonge mengi mno ie, wafanyakazi viongozi ni wengi yaani kazi moja inasimamiwa na watu 5, shirika lina idara mingi zisizo na tija..ubunifu ni hakuna bora Mwakyembe na amsha amsha zake.
 
mleta mada anayo hoja lakini ameshindwa kujieleza. mashirika yetu ya reli ambayo ni TRL na TAZARA yako ktk hali mbaya kifedha na ufanisi ni wa chini kabisa. utetezi kwa Mwakyembe kwasasa ni kwamba tukubaliane kwamba ameteuliwa kuongoza wizara wakati bajeti ya 2012/13 tayari imeisha andaliwa. hana fedha za kutekeleza mipango ya maendeleo zaidi ya hiyo aliyopangiwa!

na hiyo pesa aliyobajetiwa kaifanyia kazi walau, lingekuwa li tanzania lingine lingekomba pesa na halafu tungesikia ooo kuna mipango na michakacho kabambe ooo tunasubiri bajeti ooo! blah blah nyiingiii.

safi sana Mwakyembe, kwangu mimi faida ya usafiri ni kuweza kufika haraka na salama ninakokwenda, hizo faida nyingingine kama zipo hata sizifahamu, labda wajuao wanielimishe
 
Mkuu punguza jazba na jenga hoja vizuri!
 
Mleta mada au nawewe umekumbwa na uwajibikaji aw waziri Huyu kwa namna moja AMA nyingine namaanisha umetimuliwa Huko bandari nini?maana hakuna asiyeona kazi ya Harrison labda watu wenye walakini kma wewe

Mkuu hapo umenena hakika nami nahisi huyu jamaa amekumbwa na ile issue ya magari ya Dandho katimuliwa huyu pia hatutakushangaa sana kwakuwa unaonekana ni kambi ya E.l lolote afanyalo kwenu hamuwezi likubali ila tupo tunaweza kuona na kuhisi kuna kitu cha tofauti
 
Niliposikia huyu bwana kapewa wizara ya uchukuzi nilijua kuwa sasa kumekucha. Mimi hua siku zote namchukulia huyu muheshimiwa kama mtu wa kazi miongoni mwa watu wachache wa CCM. Nilijua anataka kufufua makampuni ya uchukuzi likiwemo TRL. Nasikitika kuwaambia watanzania kuwa hayo mambo ambayo hadi sasa kayafanya hayana mchango wowote kwa maendeleo ya TRL bali kwa wakazi wa maeneo ambayo reli inapita na zaidi sana yanaididimiza TRL. wana JF Napenda mjue kuwa TRL haiwezi kufaidika kwa ajili ya city train, train ya abiria ya kwenda Mwanza, Kigoma au Mpanda.

Hizi train zinatembea ili kutoa huduma kwa wananchi wa nchi hii. Kwa mantiki hiyo mimi sikuona kama huyu muheshimiwa sana alikuwa na sababu ya kuanza na haya mambo. Ila najua kwavile mambo haya yanagusa watanzania wLio wengi naona kaona bora ayafanye kwanza ili watu wamjue. Kakosea sana. Kama kumjua watu tulishamjua tangu enzi za sakata la richmond na anguko la Lowasa. Akiendelea kutafuta sifa zaidi anguko lake kisiasa litakuwa kubwa kuliko mtu awaye yote aliyewahi kuongoza hiyo wizara. NAWASILISHA.
We utakua ndio wale miongoni mwa watu Mwakyembe alisema ni wadokozi TRL kama sio basi utakuwa BANDARI wewe
 
Kaka umeandika pumba,umeacha mchele pembeni! Toa ushauri kwa Mwakyembe cio ulete unaa!! Na waliokuwepo kwenye hiyo wizira walifanya nini?, watz tubadilike!jamani penye sifa papewe sifa, penye mapungufu ushauri upewe nafasi! Jf kisiwe kijiwe cha kahawa!!
 
Mbona hueleweki, kipi ulitaka afanye au ww unadhan iwe vp, kwani umeambiwa train ya kigoma na mpanda hazifanyi kazi? Na hujui treni ya mwanza ilokuwa imesimama kwa miaka mitatu imeanza kufanya kazi siku chache baada ya kuanza kwa city train, yawezekana una point ila kwa uliyoyaeleza umekaa kimajungu na hueleweki.
Nadhani akimaanisha kuwa 'huwezi panda mbegu zikaota katika shamba lililojaa magugu!' Mie nashindwa kujua ugumu wa kuunda BODI upo wapi maana haya yangefanywa na bodi tuu.
 
Nadhani akimaanisha kuwa 'huwezi panda mbegu zikaota katika shamba lililojaa magugu!' Mie nashindwa kujua ugumu wa kuunda BODI upo wapi maana haya yangefanywa na bodi tuu.

Bodi siyo soln, ni kuongeza mitz isiyona tija tu humo (ukiritimba)..bodi zimekuwepo miaka nenda rudi ...ni wakati sasa wa uongozi uliopo kuonyesha njia na kuacha porojo.
 
Back
Top Bottom