Mh. Mabumba, Mh. Manyanya & Mh. Mwigulu, Msituharibie CCM yetu!

Tangu Mjadala wa bajeti uanze nimebahatika kumuona na kumsikia kijana Nchemba akichangia bajeti, binafsi nimesikitika sana kwa michango yake kama kijana. Nilitegemea kabisa michango yake akiwa kama mchumi kijana itakuwa inalisaidia taifa hili kuondokana matatizo yaliyopo lakini imekuwa kinyume kabisa. Michango aliyotoa mpaka sasa kwenye bajeti sio ya mchumi mwenye elimu ya masters. Kwa mwendo huu wa michango ya aina hii hatuwezi kutoka huku tulipo. Mungu ibariki TZ
Kiazi kweli huyu! Ameshindwa kuitumia Masters yake ya uchumi! Kila anapopata nafasi ya kuchangia yeye anazungumzia upinzani tu, badala ya kuzungumza hoja za kukutoa tulipo yeye anaongea upumbavu tu.
 
hivi Manyanya hawezi kuisaidia polisi? ila hawa jamaa (manyanya, Mabumba, na Mwigulu) waliniboa sana, nakiri waliniharibia siku
 
Naendelea kuprove zile porojo alizokuwa anazisema kwenye Uchaguzi wa Arumeru Mashariki zinaendelea mpaka bunge inasikitisha sana kwa Mtu anayefikirika kuwa ni Msomi kupoteza muda kujadili vitu ambavyo havina Tija kwa Jamii ya Kitanzania.Kinachoenekana ni Mtu kusoma doc akipata sentensi ambayo anaona imekosewa anatumia 30 dakika kupotosha umma.Mwisho wa siku anaishia kupigwa Miongozo na Taarifa.
Hili la walimu wa shule za msingi kufanya biashara katika mazingira ya shule yana ukweli na linajulikana hata Mrisho Mpoto aliimba kwenye nyimbo yake ...Mjomba!
Kuhusu Walimu kufundisha zaidi ya chuo kimoja hilo ndiyo wala usiseme Na katika kudhibitisha hili nakupa Mfano Dr. Mbura wa UDBS anafundisha UDSM,MZUMBE,IFM,CBE,UDOM endelea mwenye...... sasa uongo au udhalilishaji uko wapi hapo?
Mi nilifikiria mngekaa chini mjiulize kwanini hao walimu wa shule na msingi na Waaziri wanafanya hivyo?Baadala ya kukajadili ***** usiokuwa na tija!
 
Inasikitisha kwa hilo, lakini mwana CCM hawezi kusema haya:USHAURI WANGU
1. Tuache kuhusianisha migomo na chadema tutazidi kujizika
2. Raisi arudi tena kuongea na ma dr ni watoto wake huwezi kuwakimbia, hili HALIKIMBILIKI MR RAISI
3. Wanaofanya unyama wakupiga watu wakamatwe haraka.
4. Wabunge woote wajadili mambo ya nchi zaidi na si ushabiki wa vyama.
6. Ikiwezekana waite wapinzani kwa siri wakupe ushauri wao
7. Tufanye juhudi za kutimiza ahadi zetu badala ya kuweka majungu na watoto kama Mnyika na Sugu.

Plz Chama changu yafanyeni haya tunaweza kupona

Nilifurahia rais wangu alipo toa msimamo kuhusu ma daktari walio goma, ambao hawapendi mshahara wanao upata sasa, Ni kweli wamtafute mwajiri mwingine. Jana nikamsikia Katibu wa jumuiya ya Madaktari akisema rais amepotoshwa wao hawakuwa ving'ang'anizi, ametoa kauli kali sana. Niliweza kuungana naye kwa kuwa anajitambua, sababu amejua alilofanya ndio maana akaomba warudi kwenye meza ya mazungumzo. Amejifikiria walio nyuma yake ambao wanamtegemea. Sasa sisi wengine tunapandikiza chuki humu ili ionekana kuna bonge la ishu wakati mwajiri mkuu amesema hawezi kuwalipa mshahara huo.
 
Msemaji umeandika kwa busara kubwa sana.Hao watu ulowataja wanaongea kauli mbaya sana na 2015 watavuna wakipandacho kwa sasa.
 
Tatizo ni watu kuingia kwenye siasa kwa kutaka kuchumia matumbo yao.2015 kama CCM itapona na ghadhabu ya watanzania nitashangaa kwa sababu imebaki kua genge la wahuni kama kina mabumba,manyaya na mtoto wa mkulima bila kumsahau mr dhaifu

Ujinga wa wabunge wa ccm ni kwamba, wanadhani wakiisema vibaya na kuitukana matusi cdm basi wataonekana kwamba wanaipenda sana ccm na kujiongezea credit ya upendeleo kutoka kwa viongozi wa juu wa ccm. Ndio maana siku hizi kila mbunge wa ccm kabla hajasimama anatafuta (kwa juhudi kubwa) nineno gani baya aiseme cdm ili kuwafurahisha wakubwa wake ndio aendelee kuchangia.
 
Ndugu yangu (babykailama), nakuunga mkono kwa kauli zako hapa. Umenena vema; kasoro ni moja tu hao unaowashauri "wana masikio ya kusikilia????
Kwa kuwa umejitambulisha kuwa Mwana CCM nakushauri pamoja na kupitia jukwaa hili jengeni utamaduni wa kuelezana ukweli huu katika vikao vyenu pia. Aidha jengeni utamaduni wa kuonyana na kukemea ikiwezekana kumuadhibu anayekwenda kinyume. Haya mmmeyachangia na kuyalea wenyewe. Alipoanza Job Lusinde kutukana alipigiwa makofi. Kwa kuonesha huu ndio mwendo mliokubaliana katika Chama namna ya kuwawakilisha wananchi Samweli Sitta naye akajiunga upande huo. Sitta akaamua kudhalilisha heshima yake aliyojijengea akiwa Spika wa bunge lililosifiwa sana!. Lusinde alipotukana mbele ya umma kule Arumeru, akatetewa na Katibu wa chama chenu. Kuona hivyo, Mwinchemba naye akaona hii ndio style na haya ndio maisha! Akaamua kuwa mtukanaji kuliko Lusinda. Kudhihirisha hili akachangiwa takribani laki 2 za pongezi mbele ya bunge, machoni pa naibu spika Ndungai na umma wa watanzania ukiona kupitia TV taifa. (Mama yangu pamoja na uzee wake anasema "hawa waliotuletea vyombo vya kuona (akimaanisha Televisheni) wametusaidia sana, zamani kwenye radio na magazeti walikuwa wanatudanganya sana"). Kwa kuona pongezi apatazo Nchemba Komba naye kajunga tera na sasa msomi (kama elimu ni cheti) Stella Manyanya kaingia katika timu ya kebehi na kufurahia maumivu ya wengine.
Alipoanza Makinda kuendesha bunge kibabe (kwa wabunge wa upinzani hasa CHADEMA) na kuwapiga vijembe; hamkuonya. Walio chini yake Ndungai na Mabumba wakaona huu ndio utaratibu mpya wa kuendesha vikao vya bunge. Wakaamua kwa nia moja; kama mbunge wa upinzani akichangia chochote aombwe "uthibitisho", akiongea kinachosemekana ni lugha ya maudhi kama alivyosema Mh.Mnyika kuwa Mh. Rais ni dhaifu akaambiwa kamtukana Rais. Ingawa "dhaifu" (weakness) si tusi wala lugha ya maudhi; anafukuzwa bungeni. Kwa bahati mbaya kwenu ni kuwa madai mengi ya wenzetu hawa wa upinzani huwa wameyafanyia utafiti wa kina na yana uthibitisho; thats why kila mara wakiombwa uthibitisho ni wepesi kukubali, ila mara zote maelezo yao ya uthibitisho na vielelezo huishia katika kabati la spika. Maana yaliyo mengi huwa na ukweli mchungu kuliko waliyoyasema kwa maneno. Rejea hoja ya Mh. Lema kuwa Waziri mkuu Mh. Pinda akadangaya bunge juu ya mauaji ya Arusha. Mh. Makinda pasi na kufikiri uzito wa madai/ kauli ya Lema na kwa kufikiri anawafurahisha mabwana wake; akakimbilia kudai Mh. Lema kwa kusema Mh.Pinda kadanganya kakosea (amemdhalilisha PM kwa kumuita muongo) kwa hiyo athibitishe. Mh. Makinda hakujipa ngaa sekunde 10 kujiuliza hivi kama upo ushahidi itakuwaje? Akashindwa kuirejesha nyuma akili yake juu ya taarifa kupitia vyombo vya habari kuhusu mauaji ya Arusha na chanzo chake/ kilichochochea. HADI anavuliwa ubunge na mahakama LEMA HAKUWAPATA FURSA YA KUTOA UTETEZI WAKE BUNGENI. Mh. mmoja alipouliza Makinda aliishia kusema, "ni kweli nilimtaka mh. Lema athibitishe, lakini si lazima atoe taarifa hiyo hapa. Nimeshawailiana naye ameleta ofisini pangu". KWA NINI LEMA HAKUPEWA FURSA YA KUJITETEA BUNGENI? TAARIFA YA UTHIBITISHO WA KAULI YAKE ILIBEBA NINI KINACHOSTAHILI KUFICHWA? Makinda analo jibu!
Mh. Zitto alipoeleza bungeni kuwa waziri wa madini kasaini mkataba nje ya nchi tena hotelini; alikemewa, alikaripiwa na akaishia kutolewa nje ya bunge. Lakini je, baada ya muda mbona mambo yakawa hadharani? Nashukuru Mungu Zitto hakujivuna wala kuwananga kwa kusema "si niliwaambia mkabisha?" Ila kama mwanamwema wa nchi hii alijua ametimiza jukumu lake.
Mh. Kafulila aliposema "Serikali legelege haikusanyi kodi" alizomewa na kuombewa mwongozo. Mh. Mhagama akamtaka afute kauli (tena kwa kumkaripia) Kafulila akakomaa na kueleza ukweli kutibitisha hilo. Mhagama akaishia kusema "kauli ya baba wa Taifa iheshimiwe".

Kosa kubwa linalofanywa na wanabunge hasa wa chama chenu CCM (mimi sina chama chochote) ni kujiona kuwa wana HAKI SANA JUU YA HATIMA YA TAIFA HILI. Wanajiona wao wanajua kila kitu na kuwa WANAWATAWALA WATANZANIA WAPUMBAVU (kwamba hawawezi kuelimika). WANAHISI WATANZANIA WANAISHI KWA KUFUNGIWA KTK CHUPA HIVYO HAWAJUI KINACHOENDELEA! Na mbaya zaidi wanawaona WABUNGE WA UPINZANI (kwa sasa hasa wale wa CHADEMA NA NCCR) kuwa ni MAMLUKI TU, SI RAIA WA HAPA NA HAWANA HAJA YA KUDAI AU KUSHINIKIZA LOLOTE KWA VILE HAWANA HAKI HIYO KAMA RAIA WA NCHI HII. Hebu tujiulize kwa makini, Mbowe, Zitto, Kafulila na wenzao ni akina nani? Si watanzania hawa? Je, wanachopigia kelele kila siku (bungeni na nje ya bunge) ni UZUSHI TU? JE, NI KINYUME NA HALI HALISI YA TANZANIA?
Ndugu tangu asubuhi ya leo nimesafiri na watu toka kijiji cha Ikengeza (Kiko Iringa vijijini jimbo la Ismani kwa Mh. Lukuvi); hawa akina mama wakawa wakizungumzia tatizo la maji lililopo kijijini kwao. Watu wenye punda ndio wanaomudu kwenda umbali wa km 10-15 kuchota maji na wakifikisha wanawauzia. Kulingana na hali ngumu ya kipato na mavuno haba ni ngumu mtu kupata fedha ya kutosha kununua maji ya kutumia kwa kunywa, kukipa, kuoga, kufua, kusafisha vyombo, nk ili kubana matumizi watoto wengi na hata watu wazima huoga mara moja kwa juma. Mama huyu alisema, "tunaoga jumapili tu anapokuja padri, kwa wenye kipato kidogo huoga mara moja kwa siku au kila baada ya siku 2 hadi3". Yaani miaka 50 baada ya uhuru watu wana BAJETI YA KUOGA! Ismani sio kisiwani, hawa watu anasikia namna fedha za umma zinavyoliwa, miradi ya maji inavyohujumiwa wanajua maana hata kwao ipo ilioanza lakini haikukamilika na fedha iliyotengwa aliisha. Wananchi hawa wa Ismani, na kwingineko wakisusia kuchangi miradi ya maendeleo (maana haina tija kwao) TUKIMBILIE KUDAI CHADEMA/ NCCR/ TLP, WAMEWACHOCHEA? Wananchi wa Kigoma vijijini(vijiji vya Songambele, Sunuka, nk) wanatumia kivuko katika mto Malagalasi ambacho hakina usalama (kati ya injini 4 ni moja tu inafanya kazi tena kwa kufanyiwa marekebisho kila asubuhi); hawa wakipiga kelele CCM itadai KAFULILA ANAWACHOCHEA?

Nani hajui hata kabla ya mdaktari kugoma rasmi walishakuwa na mgomo? Kwa nini watu wanakimbilia "vikombe"? Nani hajui hospitali zilizobatizwa jina"hospitali za rufaa" hazina huduma za muhimu?

WAZALENDO WACHACHE MLIOSALIA NDANI YA CCM, JIVIKENI UJASIRI NA KUWAKATAA MAFISADI NA WANAFIKI MLIO NAO. WAKATAENI NA KUWAFUKUZA MIONGONI MWENU HARAKA SANA. BORA MBAKI WACHACHE NA MJIPANGE. KINYUME CHA HAPO "KIAMA YA CCM KIMEFIKA" NA KAMA MKING'ANG'ANI KWA VILE VYOMBO VYA DOLA MNAVIMILIKI SASA, JIANDAENI KUONA VITA KUBWA TZ. VITA YA HAKI DHIDI YA UDHALIMU!


EJL
 
Ni siku nyingine tena, mwenzetu Mh. Mabumba alipokuwa amekalia kiti cha Bunge alijitelezesha na kujiingiza katika tope lililomchafua na baadaye akashindwa kutoka humo hadi watani zetu wakaanza kutucheka na mbaya zaidi wananchi tunaowategemea wanaanza kutuona kuwa sisi hatuna watu makini na kwamba pengine tupo si kwa ajili ya haki na maendeleo yao.

Mh. Mabumba: Hivi ulipomwambia Mh. Mnyika kuwa ‘anawashwa, akae chini’ ulimaanisha nini na ulitumia kanuni ipi kuachilia tusi hilo na kwa faida ya nani. Unafikiri kuwa CCM tunapata sifa kwa kutoa matusi au kujibu kwa matusi Wapinzani wakati umepewa dhamana ya kuongoza kikao cha juu sana katika nchi- cha muhimili wa Taifa? Yaani mwangwi wa sauti yako ya “Kaa chini!!... cheap popularity !!....” imekuexpose kuwa huwezi kuongoza vikao vya namna hiyo wala ku-controll heated debates. A Moderator will never dream to be defamatory.


Mh. Eng. Manyanya: Ulianza vyema kumpa pole Dr. Ulimboka na pia si vibaya ulipoonyesha masikitiko ya Wananchi kukoswa huduma muhimu za Afya tokana na mgomo. Lakini imeshangaza ulimwengu, kwa heshima uliyonayo kama Msomi, Mbunge na Mkuu wa Mkoa kujiingiza katika kauli tata na za mipasho hadharani.
Ni kitu gani kilikupeleka uendelee hadi kufikia kutamka waziwazi ndani ya Bunge hitimisho kuwa CHADEMA wanahusika katika kumteka na kumjeruhi Dr. Ulimboka? Ukasema kwamba wao ndio wenye magandwa kama wale waliomteka Daktari. Aidha ulijisukumiza katika shimo hatari kwa kuanza kumbeza Dr. Ulimboka aliye katika matibabu ya kuokoa maisha yake kwa kumfananisha hadharani na Muuaji Hitler; Eng. what a scrawny analysis, fallacious, insalubrious talk & dodgy statements!

Injinia, je huwezi kufikiri kwa nini hata katika speech ya Rais, aliongelea mgomo usio halali lakini aliwaomba Madaktari warudi kazini na kuhusu Ulimboka alitoa kauli za kuagiza vyombo vya dola kuwatafuta wahusika (wawe ni wa CCM, CHADEMA, CUF au wasio na Chama sisi hatujui) na shauri hilo lifikishe mbele ya haki. Wewe unaanza kumhukumu mtu kama huyo aliyepona kuuawa na kumwita Muuaji katika hali aliyo nayo sasa kwa faida ya nani? Unafikiri kuwa wananchi wataipenda CCM zaidi kwa kuongea hivyo wakati wananchi wote wanalaani kwa namna yeyote mtu kutekwa na kupigwa au kuuwawa hata kama ana makosa maana kwa nini asifikishwe katika vyombo vya dola kama ana kesi ya kujibu?


Mh. Mwigulu:
Ulishashauriwa siku za nyumakuwa kwa level yako kama Mbunge na Kiongozi wa Kitaifa wa CCM (NEC – Uchumi & Fedha), kabla ya kuongea ebu tulia na kufikiri kidogo. Ile statement uliyo quote Bungeni ya Wapinzani wakisema “endeleeni kudai haki zenu sisi tunawaunga mkono”, huwezi kuitumia kuthibitisha kuwa CHADEMA wamehusika na tukio la kumteka Daktari wala kuongoza migomo isiyo halali! Hata mimi na wengi wetu wana CCM tunasema kuwa moja ya majukumu yetu ni kuwaunga mkono Wananchi kudai haki zao. Rejea Lengo namba 5 la CCM;
“Kuona kwamba kila mtu anayo haki ya kupata kutoka katika jamii hifadhi ya masiha yake na mali yake kwa mujibu wa sheria” na “pia namba 7 ;
“Kusimamia haki na maendeleo ya Wakulima, Wafanyakazi na Wananchi wengine wenye shughuli halali za kujitegemea; na hasa kuona kuwamba kila mtu ana haki ya kupata malipo yanayostahili kutokana na kazi yake.

Mh. Mwigulu, kwa utetezi au upingaji wa kauli hiyo tu, Wananchi wataweza kutofautisha kuwa ni nani yuko kwa ajili ya haki zao na ni yupi hayuko nao. Hakika mnasababisha watu kutuchukia na Chama chetu bila kujua maskini! Taarifa yako Bungeni leo tena haikuwa na mashiko. Sikilizeni, Kazi yetu CCM inatakiwa kuwa kusukuma kwa ushawishi Madaktari & Serikali kukutana na kutatua mgogoro uliopo. Pili, ni kuhakikisha kuwa yeyote aliyeshiriki jaribio la kumwondoa uhai Dr. Ulimboka anafikishwa mbele ya haki. Kama tuna madai juu ya Ulimboka tuyafaili afikishwe polisi na mahakamani ayajibu. Na kamwe iwe marufuku yeyote mwana CCM kushabikia dhuluma, vitisho, utekaji wa wananchi na kujichukulia sheria mkononi hata kama ana hatia. Anayebisha basi avuliwe uanachama wa CCM maana yu kinyume na lengo letu la CCM namba 16.

“Kuona kwamba katika nchi yetu hakuna aina yoyote ya dhuluma, vitisho, ubaguzi , rushwa , uonevu na au upendeleo”. Halafu tuelewe kuwa kuwa na nia ya kusikiliza madai ya madakrari ni tofauti na kwamba yametekelezwa.

Nauliza hivi ni Madaktari wangapi leo hii wameshapewa hayo magari au hata kujaza fomu za mikataba hiyo nchini kote, waliokwisha pewa makazi, ambao wameshaanza kupokea hiyo allowance mpya wanazosema na mishahara ya juu wakati tunajua kuwa kuna Madaktari wengi sana kote nchini (hii si issue ya Muhimbili tu) ambao bado wana madai ya arrreas za mishahara yao ya toka mwaka jana!

Kwa nini mnapenda sana kumpa taarifa zisizo kamili Rais wetu eti yote kasoro mawili tu ndiyo yametekelezwa? Wabunge muitishe taarifa za ma- RMO's kama hawana madai ya Madaktari ya siku nyingi tena ya vile viwango vya zamani na hayajalipwa? Ndani ya CCM tupo wengi ambao hatuvumi lakini tupo. Msituharibie CCM yetu- Arhrhghh!!

Jueni kuwa CHADEMA wanapoona tunakubali kuvaa viatu walivyotuazima wanafurahi sana! Watch out our role & strategies are completely different:yawn:!

Good job. Nashauri if possible send this message to mwigulu's personal email!
 
Hongera mwan ccm -wewe unastahilil kuitwa hivyo -siyo kauli za wanaojiita wana ccm kwa sababu ya kujipendekeza na kujinufaisha. Haiingii akilini kwa mtu kama Manyanya kutoa kauli kama zile hadharani kutokana na usomi wako (mimi ni msomi) kana kwamba wengine siyo, ukuu wa mkoa na ubunge (japo wa fadhila) kutoa kauli kama zile (jana jioni) licha ya Mabunda (mwenyekiti wa kikao) kumpa ishara ya kubadilisha mwelekeo lkn sikio la kufa halisikii dawa maskini -akajiingiza bichwa mpaka ndani. Lau serikali au polisi wangekuwa wakweli basi leo hii angekuwa amekwisha andikisha maelezo ya kuisaidia polisi kumpa aliyehusika na utekekaji wa ulimboka na kujeruhiwa kwake, lkn -eh maskini hata hawafikirii hilo.
Hao ndo watekelezaji wa usalama wetu, wanasubiri nini ili wajue kuwa watu wanataarifa za kulisaidia jeshi hili? Akina manyanya, mwigulu, msangi (aliyetajwa kuhusika na ulimboka mwenyewe) maofisa wa ikulu waliompigia simu ya kukutana, nk. lkn mhhhhhh nani amfunge paka kengele?
Ngoja niwahamishe kwa bigula uwenda wakaamuka :director::director::director::director:
 
Wabunge wa CCM cjui wamerogwa na nani! Wanavyoongea utafikiri wanafikiri kwa kutumia masaburi.
Ni siku nyingine tena, mwenzetu Mh. Mabumba alipokuwa amekalia kiti cha Bunge alijitelezesha na kujiingiza katika tope lililomchafua na baadaye akashindwa kutoka humo hadi watani zetu wakaanza kutucheka na mbaya zaidi wananchi tunaowategemea wanaanza kutuona kuwa sisi hatuna watu makini na kwamba pengine tupo si kwa ajili ya haki na maendeleo yao.

Mh. Mabumba: Hivi ulipomwambia Mh. Mnyika kuwa ‘anawashwa, akae chini’ ulimaanisha nini na ulitumia kanuni ipi kuachilia tusi hilo na kwa faida ya nani. Unafikiri kuwa CCM tunapata sifa kwa kutoa matusi au kujibu kwa matusi Wapinzani wakati umepewa dhamana ya kuongoza kikao cha juu sana katika nchi- cha muhimili wa Taifa? Yaani mwangwi wa sauti yako ya “Kaa chini!!... cheap popularity !!....” imekuexpose kuwa huwezi kuongoza vikao vya namna hiyo wala ku-controll heated debates. A Moderator will never dream to be defamatory.


Mh. Eng. Manyanya: Ulianza vyema kumpa pole Dr. Ulimboka na pia si vibaya ulipoonyesha masikitiko ya Wananchi kukoswa huduma muhimu za Afya tokana na mgomo. Lakini imeshangaza ulimwengu, kwa heshima uliyonayo kama Msomi, Mbunge na Mkuu wa Mkoa kujiingiza katika kauli tata na za mipasho hadharani.
Ni kitu gani kilikupeleka uendelee hadi kufikia kutamka waziwazi ndani ya Bunge hitimisho kuwa CHADEMA wanahusika katika kumteka na kumjeruhi Dr. Ulimboka? Ukasema kwamba wao ndio wenye magandwa kama wale waliomteka Daktari. Aidha ulijisukumiza katika shimo hatari kwa kuanza kumbeza Dr. Ulimboka aliye katika matibabu ya kuokoa maisha yake kwa kumfananisha hadharani na Muuaji Hitler; Eng. what a scrawny analysis, fallacious, insalubrious talk & dodgy statements!

Injinia, je huwezi kufikiri kwa nini hata katika speech ya Rais, aliongelea mgomo usio halali lakini aliwaomba Madaktari warudi kazini na kuhusu Ulimboka alitoa kauli za kuagiza vyombo vya dola kuwatafuta wahusika (wawe ni wa CCM, CHADEMA, CUF au wasio na Chama sisi hatujui) na shauri hilo lifikishe mbele ya haki. Wewe unaanza kumhukumu mtu kama huyo aliyepona kuuawa na kumwita Muuaji katika hali aliyo nayo sasa kwa faida ya nani? Unafikiri kuwa wananchi wataipenda CCM zaidi kwa kuongea hivyo wakati wananchi wote wanalaani kwa namna yeyote mtu kutekwa na kupigwa au kuuwawa hata kama ana makosa maana kwa nini asifikishwe katika vyombo vya dola kama ana kesi ya kujibu?


Mh. Mwigulu:
Ulishashauriwa siku za nyumakuwa kwa level yako kama Mbunge na Kiongozi wa Kitaifa wa CCM (NEC – Uchumi & Fedha), kabla ya kuongea ebu tulia na kufikiri kidogo. Ile statement uliyo quote Bungeni ya Wapinzani wakisema “endeleeni kudai haki zenu sisi tunawaunga mkono”, huwezi kuitumia kuthibitisha kuwa CHADEMA wamehusika na tukio la kumteka Daktari wala kuongoza migomo isiyo halali! Hata mimi na wengi wetu wana CCM tunasema kuwa moja ya majukumu yetu ni kuwaunga mkono Wananchi kudai haki zao. Rejea Lengo namba 5 la CCM;
“Kuona kwamba kila mtu anayo haki ya kupata kutoka katika jamii hifadhi ya masiha yake na mali yake kwa mujibu wa sheria” na “pia namba 7 ;
“Kusimamia haki na maendeleo ya Wakulima, Wafanyakazi na Wananchi wengine wenye shughuli halali za kujitegemea; na hasa kuona kuwamba kila mtu ana haki ya kupata malipo yanayostahili kutokana na kazi yake.

Mh. Mwigulu, kwa utetezi au upingaji wa kauli hiyo tu, Wananchi wataweza kutofautisha kuwa ni nani yuko kwa ajili ya haki zao na ni yupi hayuko nao. Hakika mnasababisha watu kutuchukia na Chama chetu bila kujua maskini! Taarifa yako Bungeni leo tena haikuwa na mashiko. Sikilizeni, Kazi yetu CCM inatakiwa kuwa kusukuma kwa ushawishi Madaktari & Serikali kukutana na kutatua mgogoro uliopo. Pili, ni kuhakikisha kuwa yeyote aliyeshiriki jaribio la kumwondoa uhai Dr. Ulimboka anafikishwa mbele ya haki. Kama tuna madai juu ya Ulimboka tuyafaili afikishwe polisi na mahakamani ayajibu. Na kamwe iwe marufuku yeyote mwana CCM kushabikia dhuluma, vitisho, utekaji wa wananchi na kujichukulia sheria mkononi hata kama ana hatia. Anayebisha basi avuliwe uanachama wa CCM maana yu kinyume na lengo letu la CCM namba 16.

“Kuona kwamba katika nchi yetu hakuna aina yoyote ya dhuluma, vitisho, ubaguzi , rushwa , uonevu na au upendeleo”. Halafu tuelewe kuwa kuwa na nia ya kusikiliza madai ya madakrari ni tofauti na kwamba yametekelezwa.

Nauliza hivi ni Madaktari wangapi leo hii wameshapewa hayo magari au hata kujaza fomu za mikataba hiyo nchini kote, waliokwisha pewa makazi, ambao wameshaanza kupokea hiyo allowance mpya wanazosema na mishahara ya juu wakati tunajua kuwa kuna Madaktari wengi sana kote nchini (hii si issue ya Muhimbili tu) ambao bado wana madai ya arrreas za mishahara yao ya toka mwaka jana!

Kwa nini mnapenda sana kumpa taarifa zisizo kamili Rais wetu eti yote kasoro mawili tu ndiyo yametekelezwa? Wabunge muitishe taarifa za ma- RMO's kama hawana madai ya Madaktari ya siku nyingi tena ya vile viwango vya zamani na hayajalipwa? Ndani ya CCM tupo wengi ambao hatuvumi lakini tupo. Msituharibie CCM yetu- Arhrhghh!!

Jueni kuwa CHADEMA wanapoona tunakubali kuvaa viatu walivyotuazima wanafurahi sana! Watch out our role & strategies are completely different:yawn:!
 
by babykailama;Ni siku nyingine tena, mwenzetu Mh. Mabumba alipokuwa amekalia kiti cha Bunge alijitelezesha na kujiingiza katika tope lililomchafua na baadaye akashindwa kutoka humo hadi watani zetu wakaanza kutucheka na mbaya zaidi wananchi tunaowategemea wanaanza kutuona kuwa sisi hatuna watu makini na kwamba pengine tupo si kwa ajili ya haki na maendeleo yao.

Mh. Mabumba: Hivi ulipomwambia Mh. Mnyika kuwa ‘anawashwa, akae chini’ ulimaanisha nini na ulitumia kanuni ipi kuachilia tusi hilo na kwa faida ya nani. Unafikiri kuwa CCM tunapata sifa kwa kutoa matusi au kujibu kwa matusi Wapinzani wakati umepewa dhamana ya kuongoza kikao cha juu sana katika nchi- cha muhimili wa Taifa? Yaani mwangwi wa sauti yako ya “Kaa chini!!... cheap popularity !!....” imekuexpose kuwa huwezi kuongoza vikao vya namna hiyo wala ku-controll heated debates. A Moderator will never dream to be defamatory.


Mh. Eng. Manyanya: Ulianza vyema kumpa pole Dr. Ulimboka na pia si vibaya ulipoonyesha masikitiko ya Wananchi kukoswa huduma muhimu za Afya tokana na mgomo. Lakini imeshangaza ulimwengu, kwa heshima uliyonayo kama Msomi, Mbunge na Mkuu wa Mkoa kujiingiza katika kauli tata na za mipasho hadharani.
Ni kitu gani kilikupeleka uendelee hadi kufikia kutamka waziwazi ndani ya Bunge hitimisho kuwa CHADEMA wanahusika katika kumteka na kumjeruhi Dr. Ulimboka? Ukasema kwamba wao ndio wenye magandwa kama wale waliomteka Daktari. Aidha ulijisukumiza katika shimo hatari kwa kuanza kumbeza Dr. Ulimboka aliye katika matibabu ya kuokoa maisha yake kwa kumfananisha hadharani na Muuaji Hitler; Eng. what a scrawny analysis, fallacious, insalubrious talk & dodgy statements!

Injinia, je huwezi kufikiri kwa nini hata katika speech ya Rais, aliongelea mgomo usio halali lakini aliwaomba Madaktari warudi kazini na kuhusu Ulimboka alitoa kauli za kuagiza vyombo vya dola kuwatafuta wahusika (wawe ni wa CCM, CHADEMA, CUF au wasio na Chama sisi hatujui) na shauri hilo lifikishe mbele ya haki. Wewe unaanza kumhukumu mtu kama huyo aliyepona kuuawa na kumwita Muuaji katika hali aliyo nayo sasa kwa faida ya nani? Unafikiri kuwa wananchi wataipenda CCM zaidi kwa kuongea hivyo wakati wananchi wote wanalaani kwa namna yeyote mtu kutekwa na kupigwa au kuuwawa hata kama ana makosa maana kwa nini asifikishwe katika vyombo vya dola kama ana kesi ya kujibu?


Mh. Mwigulu:
Ulishashauriwa siku za nyumakuwa kwa level yako kama Mbunge na Kiongozi wa Kitaifa wa CCM (NEC – Uchumi & Fedha), kabla ya kuongea ebu tulia na kufikiri kidogo. Ile statement uliyo quote Bungeni ya Wapinzani wakisema “endeleeni kudai haki zenu sisi tunawaunga mkono”, huwezi kuitumia kuthibitisha kuwa CHADEMA wamehusika na tukio la kumteka Daktari wala kuongoza migomo isiyo halali! Hata mimi na wengi wetu wana CCM tunasema kuwa moja ya majukumu yetu ni kuwaunga mkono Wananchi kudai haki zao. Rejea Lengo namba 5 la CCM;
“Kuona kwamba kila mtu anayo haki ya kupata kutoka katika jamii hifadhi ya masiha yake na mali yake kwa mujibu wa sheria” na “pia namba 7 ;
“Kusimamia haki na maendeleo ya Wakulima, Wafanyakazi na Wananchi wengine wenye shughuli halali za kujitegemea; na hasa kuona kuwamba kila mtu ana haki ya kupata malipo yanayostahili kutokana na kazi yake.

Mh. Mwigulu, kwa utetezi au upingaji wa kauli hiyo tu, Wananchi wataweza kutofautisha kuwa ni nani yuko kwa ajili ya haki zao na ni yupi hayuko nao. Hakika mnasababisha watu kutuchukia na Chama chetu bila kujua maskini! Taarifa yako Bungeni leo tena haikuwa na mashiko. Sikilizeni, Kazi yetu CCM inatakiwa kuwa kusukuma kwa ushawishi Madaktari & Serikali kukutana na kutatua mgogoro uliopo. Pili, ni kuhakikisha kuwa yeyote aliyeshiriki jaribio la kumwondoa uhai Dr. Ulimboka anafikishwa mbele ya haki. Kama tuna madai juu ya Ulimboka tuyafaili afikishwe polisi na mahakamani ayajibu. Na kamwe iwe marufuku yeyote mwana CCM kushabikia dhuluma, vitisho, utekaji wa wananchi na kujichukulia sheria mkononi hata kama ana hatia. Anayebisha basi avuliwe uanachama wa CCM maana yu kinyume na lengo letu la CCM namba 16.

“Kuona kwamba katika nchi yetu hakuna aina yoyote ya dhuluma, vitisho, ubaguzi , rushwa , uonevu na au upendeleo”. Halafu tuelewe kuwa kuwa na nia ya kusikiliza madai ya madakrari ni tofauti na kwamba yametekelezwa.

Nauliza hivi ni Madaktari wangapi leo hii wameshapewa hayo magari au hata kujaza fomu za mikataba hiyo nchini kote, waliokwisha pewa makazi, ambao wameshaanza kupokea hiyo allowance mpya wanazosema na mishahara ya juu wakati tunajua kuwa kuna Madaktari wengi sana kote nchini (hii si issue ya Muhimbili tu) ambao bado wana madai ya arrreas za mishahara yao ya toka mwaka jana!

Kwa nini mnapenda sana kumpa taarifa zisizo kamili Rais wetu eti yote kasoro mawili tu ndiyo yametekelezwa? Wabunge muitishe taarifa za ma- RMO's kama hawana madai ya Madaktari ya siku nyingi tena ya vile viwango vya zamani na hayajalipwa? Ndani ya CCM tupo wengi ambao hatuvumi lakini tupo. Msituharibie CCM yetu- Arhrhghh!!

Jueni kuwa CHADEMA wanapoona tunakubali kuvaa viatu walivyotuazima wanafurahi sana! Watch out our role &

strategies are completely different:yawn:![/QUOTE]

Babykailama;

Ukichoka chama hama tafuta kwingine
 
TANGAZO;Wabunge waliotajwa hapo juu na wengine watakaojitokeza kuweka ushabiki kwa maswala yasiyo na maslahi kwa taifa wasirudi bungeni 2015.nawasilisha.
 
stella manyanya ni mwanasiasa anayeheshimika sana. kauli yake ya jana kuwa Dk, ulimboka amejiepusha na kuwa hitler ni sahihi au imemvunjia heshima mbele ya jamii?
 
mwenye macho na aone na mwenye masikio askie mwenyewe ccm hakuna mtu wa namna hiyo ni wadhalimu kuliko kaburu alivyokuwa na siku ya ukombozi ikifika ccm mtajichimbia kwenye mahandaki

Hakika umenena vyema... Uzito wa mtu ni akili na jinsi anavyoitumia
 
stella manyanya ni mwanasiasa anayeheshimika sana. kauli yake ya jana kuwa Dk, ulimboka amejiepusha na kuwa hitler ni sahihi au imemvunjia heshima mbele ya jamii?

Huyo Manyanya anaheshimika kwa lipi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom