Mh JK kwa ajili ya tunu ya utulivu nchini unda tume kusikiliza sauti ya CHADEMA!

mgen

JF-Expert Member
Nov 18, 2010
22,631
8,417
CDM Ni SAUTI ya wengi wasiokuwa na SAUTI.

Viongozi wengi walio jifungia Ikulu na kusikia tu sauti nzuri za wapambe na kushindwa kutambua sauti ya wengi niipate vipi, WAMEANGUKA bila ya kujua sababu la anguko, na hawakuinuka tena.

Hivyo basi CDM inawakilisha ule umati ulio andamana, wana haki ya kusikilizwa wanacho dai na kukifanyia kazi.

Ushauri unda tume huru ambayo haitakuwa na wapambe kutambua ULIPO JIKWAA ILI KISIKI KING'OLEWE TUANZE UPYA.

INAWEZEKANA.
 
hamna cha tume wanaichi ni mahakimu na wameshaihukumu hii mutu JK, anajua yote aliyoyatenda na kama hajui basi spika Makinda hajui lilipo jengo la bunge Dodoma.

Namshauri aende radio iman ya kiislam aongee kiarabu nini cha kufanya kwa waislam kwa kuwa sera ya kutugawa inaelekea kushindwa.
 
Hatuijui siku wala saa! Kilicho tokea Mbeya wengi tulikuwa tunakula na kunywa, wenye kuuza na kununua walikuwa bize, wafanyi kazi, wakulima, walianza kazi kky ya kila siku! Na viongozi waliona ni shwari tu! Kumbe......Bado hatukuona Funzo? Raisi nakuomba, Bila kujali wapambe, Unda TUME ya MARIDHIANO ya KITAIFA! ili kudumisha UTULIVU.
 
tume zimekuwanyingi wanatumia pesa nyingi kuanda ripoti then inawekwa kwenye mashelf.ni kamati gani ambayo matokeo na ushauri wao umefanyiwa kazi?hizi tume zimekuwa zikitumika kuaadaa wananchi kuwaonyesha kuwa serikali hi sikivu kumbe wapi.
 
tume zimekuwanyingi wanatumia pesa nyingi kuanda ripoti then inawekwa kwenye mashelf.ni kamati gani ambayo matokeo na ushauri wao umefanyiwa kazi?hizi tume zimekuwa zikitumika kuaadaa wananchi kuwaonyesha kuwa serikali hi sikivu kumbe wapi.

Mkuu, uliyosema ni kweli! Pamoja na ukweli huo, bado Maridhiano ni lazima. Tusiendelee kulaumu tulipo anguka ima kugalagala chini, bali tuinuke na kuchukua hatua! Na hatua ya Mwanzo ni Tume ya maridhiano! Hatuna Nchi nyingine zaidi ya hii, ambayo MMungu ametupa itutunze tukiwa Hai na baadaye tukifa tuzikwe Humo.
 
Hao wabunge wa CHADEMA sio wajinga, ni heri wangepewa uhuru bungeni wasikilizwe wanachodai. Kumbukeni hao ni watu wazima na sio watoto wadogo, na wengine ni wanasheria. Mimi naona madai yao ni ya msingi
 
Hao wabunge wa CHADEMA sio wajinga, ni heri wangepewa uhuru bungeni wasikilizwe wanachodai. Kumbukeni hao ni watu wazima na sio watoto wadogo, na wengine ni wanasheria. Mimi naona madai yao ni ya msingi

Hata wakiwachukulia hivyo! Isiwe sababu ya kuwakejeli na kuwatusi! Bado nchi hii ni yetu wote na tunastahili heshima, hilo nalo gumu? Kwa nini tusishindane kwa hoja ili wananchi tupime hoja, na sio kejeli na matusi?
 
Wakubwa bado sababu ipo!Tusiwe kama yule mnyama mbwa mwenye watoto4 ambao wanatoana damu kunyonya wakati mama yao ana matiti12! Wangeridhiana matiti8 hayana mnyonyaji!Kilichofisadiwa ni kidogo sana kuliko kilicho bakia, tukiridhiana nchi hii tutakopesha badala ya kukopa! Tukishindwa kuridhiana itakuwa vita ya panzi manufaa kwa kunguru! I N A W E Z E K A N A!
 
Hamna haja ya tume wala maridhiano hapa kwa kuwa tuna uzoefu wa tume nyingi kwa muda mrefu. Kinachotakiwa hapa ni JK na NEC yake kuacha style za kizamani za kuthibiti democrasia. Wao waiche M4C iendelee na wape support ya ulinzi wa kweli si vita na wao ccm wajiandae kupangua hoja za M4C wakishindwa wajiandae kuachia madaraka kwa amani. Hii ndiyo hekima na usitarabu kwa mtawala asiyedikiteita si tume za kuzidi kutupotezea muda na pesa.
 
CDM Ni SAUTI ya wengi wasiokuwa na SAUTI.

Viongozi wengi walio jifungia Ikulu na kusikia tu sauti nzuri za wapambe na kushindwa kutambua sauti ya wengi niipate vipi, WAMEANGUKA bila ya kujua sababu la anguko, na hawakuinuka tena.

Hivyo basi CDM inawakilisha ule umati ulio andamana, wana haki ya kusikilizwa wanacho dai na kukifanyia kazi.

Ushauri unda tume huru ambayo haitakuwa na wapambe kutambua ULIPO JIKWAA ILI KISIKI KING'OLEWE TUANZE UPYA.

INAWEZEKANA.
Hawezi kuunda hiyo tume kwani anamanufaa gani na maafikiano wakati muda wake wa kutawala unaishia 2015 na kama ni utajiri alishaukwaa na kumilikisha wanawe njia za uchumi na kuweka mademu wake kwenye vyeo. Ni sisi wapenda maendeleo na mageuzi tushikamane tuupinge huu utawala kwa nguvu ikiwezekana hata kuingia msituni.
 
kikwete hawezi kuunda tume kwani mauaji haya ana maslahi nayo kisiasa kwani walipanga wote ikuli wakiwa na tendwa, IGP mwema na wenzake, kuna nepi,na wengineo muhimu katika serikali ili wawasaidie kuwadhibiti chadema. haya mauaji ni ya kimkakati.
jk tunaomba umalize kwa amani acha watu wafanye siasa kwa amani. cha muhimu sasa kaa na vyombo vyako vya ulinzi uwakataze na fanya kikao cha vyama vyote kama wewe ni mpatanishi kweli. kenya uliweza kwako unamaslahi gani na fujo. sisi tunataka uondoke kwa amani 2015 ila kama utaendelea na sera za kina nepi na kina tendwa shairi yako huo ni ushauri wa bure
 
CDM Ni SAUTI ya wengi wasiokuwa na SAUTI.

Viongozi wengi walio jifungia Ikulu na kusikia tu sauti nzuri za wapambe na kushindwa kutambua sauti ya wengi niipate vipi, WAMEANGUKA bila ya kujua sababu la anguko, na hawakuinuka tena.

Hivyo basi CDM inawakilisha ule umati ulio andamana, wana haki ya kusikilizwa wanacho dai na kukifanyia kazi.

Ushauri unda tume huru ambayo haitakuwa na wapambe kutambua ULIPO JIKWAA ILI KISIKI KING'OLEWE TUANZE UPYA.

INAWEZEKANA.

kweli kuna watu mnaona wanaokufa kama vile ni mbuzi
 
Back
Top Bottom