Brightman Jr
JF-Expert Member
- Mar 22, 2009
- 1,225
- 232
Akihojiwa na Othman Miraji wa Deutsche Welle Mh. Shelukindo amekiri kuwa ni kweli mpango wa kuongezwa posho ya Tsh.200,000/=ulifanyika kutokana na ugumu wa maisha ya mjini Dodoma. Akiri rais kukataa kusaini ombi la posho hizo. Na kusisitiza kuwa si kweli kwamba wameanza kulipwa. Amesema tume ya kuangalia upya posho hizo itakutana jumamosi. Haya wadau nafikiri kweli posho hizo bado hazijaanza kutolewa kutokana na kauli za watu zaidi ya wawili kukataa kuwa posho bado. Mwasemaje wanaJf?