Mgomo wa Walimu Tanzania: Ripoti toka Maeneo mbalimbali ya nchi

Katika ile thread yangu ya 'Kwanini moyo wa rais uwe mgumu kama wa pharao" nilimaanisha kuwa KIONGOZI wetu huwa ama hajali mambo ya msingi au anafanya makusudi..Kwanini huwa hapendi kuusikiliza umma na mahitaji yake?..anabaki kusema umma wa watanzania....au amestaafishwa kwa manufaa ya umma,...umma upi? sasa ni huo umma ndio unamuaibisha....Na kingine ni kwanini huwa HANA UWEZO AU ANAO ILA HAPENDI KUUTUMIA, UWEZO WA KUFANYA MAAMUZI MAGUMU, kama hili la waalimu. Kwani waalimu wameanza kulalamika leo? Kwanini asubiri hadi mambo YAFIKIE HAPO YALIPO ndio atafute nini cha kuongea?.....jamani mimi nina maswali yasiyoisha, mwenye namba zake anitumie kwani nilizo nazo labda hazitumii tena au kabadili namba.......nitampigia sasa hivi nimuulize au nisaidie kumshauri kidogo,,,huenda akanisikiliza au Mungu akamgusa kutenda tofauti na kawaida.

Walimu wote nchini:
Jipeni moyo kwani saa ya ukombozi wenu imekaribia

Wanafunzi wote nchini:
Hao waalimu ni mama zenu na baba zenu, wanagoma ili wawezeshwe na serikali ili wawafundishe vizuri, msiwalaumu.

Jingine ni kile kichefuchefu cha mafao yetu kwenye hii mifuko fisadi ya pensheni...kwani rais alishindwa kuusikiliza umma unataka nini?...

Kwa hili, nimechefukwa na roho sana, ila nikafarijiwa na mbunhge wa kisarawe, Mhe Jafo. nilijaribu kumpigia simu yake ikawa haipatikani, nadhani alikuwa kwenye "session" kule bungeni. Lengo lilikuwa ni kujua amefikia wapi kuhusu kuorodhesha malalamiko ya umma kwa mwenyekiti wa bunge, Mhe. Jenista Mhagama...

Au jamani rais kwa kuwa anamaliza muda wa utawala wake hivyo anaona hana haja ya kuusikiliza umma.

umenisuuza sana, ukimpata jefo, nimp nmpe yangu
 
Kila. Mtanzania now mwanasiasa, maneno mengi. Mdomoni. Kchwani akili hamna. Ni Masaburi tu! Mkoba tuko pamoja!
 
leo nipo kasulu mkoani kigoma mgomo huku naona upo kwa 99.99% shule karibu zote hazina hata mwalimu mkuu, watoto wamezagaa mitaani bila msaada wowote. Kikwete inapidi atafute mwafaka haraka sana kwani siku zinavyozidi kwenda ndio na mgomo unazidi kushika kasi zaidi.
 
Hivi hao waalimu wanaokwenda shule, wanaenda kumfundisha nani wakati hao hao wanafunzi wenyewe wame-respond kwa maandamano?
 
Serikali iache mara moja kuchezea walimu, wakiamua hakuna kurudi nyuma. Tunasubiri maandamano ya wazazi wa wanafunzi nchi nzima
 
Mfa maji haachi kutapatapa,Wahenga walisema. Imekuwa kawaida kwa CCM, Bwana Kikwete na wana-Propaganda wake kutafuta mchawi wa migomo na migogoro mbalimbali badala ya kutafuta suluhisho la kudumu la ufumbuzi wake. Mtakumbuka matukio kadhaa yalitokea,mfano:

1. Maandamano ya Wanavyuo,kudai mikopo na kuboreshwa mazingira.. Walijitokeza watetezi wengi na makada wa CCM kudai ati ni Chadema wanaohusika. (impact yake- ccm kupoteza kukubalika vyuoni).
2. Ukaja mgomo wj madaktari na crucifiction ya bwana-Daktari Ulimboka. Hapa Kikwete, CCM yake na vibaraka wao TISS waliwatuhumu Chadema kuwa nyuma ya wadai haki zao (madaktari). (Impact yake- CCM kuonekana bulshit katika jamii ya madaktari)!
3. Mgomo wa Walimu.. Hali inavyoelekea,si punde itatamkwa Chadema wapo nyuma ya wadai haki hawa. Natamani sana wataalam wa propaganda wa bwana JMK na chama lake wajitokeze na kuwakemea walim waache kutumiwa na CHADEMA..

My take:- Ni uwezo mdogo wa kiuongozi na utawala alionao kikwete,kukimbilia visingizio kama chaka la kuficha udhaifu.
:- Natoa wito kwa walim kwa kuwa wapo wengi,na wana mtandao mkubwa kila kona ya nchi, basi wawe mashuhuda wa kuwa CHADEMA ndio watetezi wa haki kwani hata CCM wanakiri hivyo,na kubwa zaidi thamani yenu mbele ya chama tawala ni ndogo mno.

Well said,tayari kwenye baadhi ya mikoa propaganda za kuihusisha chadema zimeanza
 
huu ni uonevu kwa walimu, mwalimu ndio kila kitu katika zama hizi ,bila msingi mzuri kutoka kwa walimu hawa ma proffessions wasingekuwa hapo.
just Maoni tu.
 
Back
Top Bottom