Elections 2015 Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli

Wanabodi,

Leo nimekutana na rafiki yangu wa siku nyingi, ambaye ni mtu wa kuaminika na ni kada wa Chama cha Mapinduzi-CCM, akanieleza seriously habari za kushtusha kidogo ambazo mimi pia zimenihuzunisha, kunisikitisha na kunisononesha!, kuwa eti imeishaamuliwa mgombea wa urais wa mwaka 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi-CCM ni Mhe. John Pombe Magufuli!.

Kilichonistua, kunihuzunisha, kunisikitisha na kunisononesha, ni the reasons behind alizonitajia ambazo ndizo zimepelekea CCM kuamua why ni lazima awe Magufuli tuu, and no one else!.

Kwa vile sababu hizo alizonitajia, baadhi ni justifiable na nyingine sio tuu ni unjustifiable!, bali hazikubaliki kabisa katika Tanzania ya leo!. Naomba kwa sasa nisizitaje kwanza, kwa sababu habari zenyewe nimezisikia from a single source, nahitaji kwanza kufanya collaborative verification na kupata attribution ili nijiridhishe kuwa ni za kweli na kuthibitisha kuwa hivyo ndivyo CCM inavyoweza kufikia maamuzi based on hayo niliyoyasikia!, then nitaziweka hadharani hizo sababu za CCM on Why ni Magufuli!.

Kwa kawaida sisi waandishi, ukipata taarifa kama hii, huwa inaitwa "news tip", haukimbilii kuiandika mbio mbio mpaka kwanza uifanyie verification kuthibitisha ukweli wa taarifa yenyewe, lakini kwa vile sasa tunaishi kwenye "the world of information age", nimeamua kuileta hii "news tip" humu jf, hivi hivi ikiwa kwenye hatua ya "tip" kabla hata ya verification, ili wewe kama mwana JF, uipate ile advantage ya JF, "be the first to know!", hivyo nawaombeni tuu sasa mkae mkijua, "Mgombea wa CCM 2015 ni John Pombe Magufuli!"

Nikiisha "confirm" neno "tetesi" litaondolewa na kuwa replaced na neno "confirmed!", na nitaziweka hizo sababu ila sasa ndio zijadiliwe!, na nawahakikishia wale wote wenye mapenzi mema na taifa hili, mkizisikia hizo sababu za CCM!, na nyinyi pia zitawashtua, kuwahuzunisha, kuwasikitisha na kuwasononesha!. Naomba nisiwatajie jina la huyo source wangu chini ya kinga ya kihabari inayoitwa "The Confidentiality of the source".

NB. Sio kila thread ni lazima ichangiwe, saa nyingine itoshe kujisomea tuu na kujipitia bila kuchangia chochote!. Hii ni just a news tip, kwa vile nimewaahidi naifanyia verification kuithibitisha, nawaombeni msiniulize swali lolote at this stage, kwa sababu sitajibu chochote!, and if possible nawashauri na nyingi msome FYE only na sio lazime mchangie kwa sasa na badala yake mvute subira kusubiria verification.

Sababu ya kuiwahisha humu JF kabla ya verification ni ili tuu wewe kama mwana JF to be the first to know!. Information is power!, if you are the first to know, then you'll have the powers to make good things happen or not to happen if they are bad things!.


Asante.
Pasco.

Update 12/07/2015
Leo hili limetimia ni kweli aliyepita ni Magufuli, nimezitafakari sababu nilizotajiwa ile siku napewa tetesi hii, na kuzipima na hiki kilichotokea, nimejikuta nimelazimika kutoziamini kuwa zile nilizosikia ndizo sababu zenyewe halisi.

Kwa sisi waandishi tuna kanuni, ukilisikia jambo, kama huliamini, then usiliseme wala kuliandika, hivyo hizo sababu nilisopewa siku hiyo, why Magufuli, siziamini, naomba nisiziseme hivyo chukulie kupitishwa kwa Magufuli kumetokea tuu natural, bila any pre meditated moves, na hili bandiko lichukuliwa tuu kama just a coincidence, nilisema ni Magufuli na akawa coincidentally.

Kwa mtakaonielewa asanteni, kwa msio nielewa samahanini sana!.

Hongera Magufuli!.

Pasco

Pasco wewe si ulikuwa kambi ya mzee wa mafuriko?
 
Pasco wewe si ulikuwa kambi ya mzee wa mafuriko?
Sijawahi kuwemo kwenye kambi ya mgombea yoyote, ila kwenye CCM nilikuwa namkubali sana EL na kumsupport humu jf!, ila kiukweli JPM ni jembe kuliko hata EL!.

Tena nawaombeni msije kunifananisha na Petro aliyemkana Yesu mara tatu kabla jogoo hajawika, mimi sijawahi kuwepo kwenye kambi ya mtu yoyote na sijawahi kupokea senti tano ya mgombea yoyote!.

Pasco
 
...tatizo la magufuli ni kwamba yeye ni one-man-show. Hata pale anapotekeleza sheria anafanya kwa namna ya kukomoa au kikatili-katili.

..huyu ni mtu ambaye anatakiwa kuwa checked mara kwa mara. Naamini ni mtu hatari kupewa madaraka bila ya kuwa na mtu wa juu yake atakayemdhibiti.

Cc Kishimbe wa Kishimbe, Nguruvi3
Tanzania hapa tulipofika tunamhitaji tulikuwa tunahitaji benevolent dictator, Mungu katupatia a real dictaor!, Tanzania ili tubadilike, na ili tuende, tunahitaji mtu kama Magufuli!, atatawala kwa an iron hand ni heshima na adabu!.

Pasco
 
Sijawahi kuwemo kwenye kambi ya mgombea yoyote, ila kwenye CCM nilikuwa namkubali sana EL na kumsupport humu jf!, ila kiukweli JPM ni jembe kuliko hata EL!.

Tena nawaombeni msije kunifananisha na Petro aliyemkana Yesu mara tatu kabla jogoo hajawika, mimi sijawahi kuwepo kwenye kambi ya mtu yoyote na sijawahi kupokea senti tano ya mgombea yoyote!.

Pasco
Mpaka huu uchaguzi uishe Mamvii atakanwa sana, namhurumia sana.
 
Tanzania hapa tulipofika tunamhitaji tulikuwa tunahitaji benevolent dictator, Mungu katupatia a real dictaor!, Tanzania ili tubadilike, na ili tuende, tunahitaji mtu kama Magufuli!, atatawala kwa an iron hand ni heshima na adabu!.

Pasco
Maamuzi ya kukurupuka ndiyo unayaita ya kidikteta?
Mwambie alipie kwanza ile hasara ya bil 40 za samaki aliyotusababishia Watanzania.
 
..tunahitaji raisi anayeweza kujenga taasisi mbalimbali na mfumo utakaowezesha nchi kusonga mbele.

..it is very dangerous kwa nchi kama tanzania kutegemea mtu mmoja badala ya mifumo ya kitaasisi.

..tatizo la magufuli ni kwamba yeye ni one-man-show. Hata pale anapotekeleza sheria anafanya kwa namna ya kukomoa au kikatili-katili.

..huyu ni mtu ambaye anatakiwa kuwa checked mara kwa mara. Naamini ni mtu hatari kupewa madaraka bila ya kuwa na mtu wa juu yake atakayemdhibiti.

..bongo fleva is not a bad thing. Too much of it ndiyo a bad thing. Mafanikio tuliyoyapata ktk bongo fleva tunatakiwa tuya replicate ktk science,engineering, technology, mathematics, and sports.

Cc Kishimbe wa Kishimbe, Nguruvi3


You can say that again
 
Kidogo nilipata madokezo kama hayo

Ni habari iliyoenea sana katika ngazi za juu, kwamba kufanikiwa kwa Magufuli kupeperusha bendera ya CCM kwenye kugombea raisi nguvu kubwa nyuma yake ni Raisi mstaafu Benjamin Mkapa. Kuna sababu kadhaa zinazotolewa, na jinsi Mkapa alivyofanya kufanikisha hili.

La kwanza inasemwa Mkapa ilibidi amshawishi JK kwamba Magufuli kuwa raisi ajaye ni kwa faida yao wote, kwamba mojawapo ni Magufuli pekee ambaye watakuwa na uhakika wa asilimia 100% kwamba atawalinda kutokana na lolote ambalo wanaweza kusakamwa nalo (mfano suala la Kiwira, nk nk). Kulikuwa na suala la athari ya yale Magufuli aliyofanya, mfano kuhusiana na uuzaji wa nyumba za serikali - kutia ndani na kumuuzia ndugu yake - lakini ilionwa kwamba hilo si jambo kubwa, hasa ukizingatia kwamba pamoja na hayo bado Magufuli alikuwa ana mashabiki wengi katika watu wa kawaida.

Pia ilionekana wazi kwamba JK hakuwa na mtu chaguo lake ambaye aidha alikubalika kwa watu na angeweza kufanya kazi kwa maslahi ya maraisi waliopita - kutia ndani kuwasikiliza. Hatimaye makubaliano yalifikiwa, kwamba na iwe Magufuli. Magufuli aliambiwa juu ya hili, na hata kushauriwa namna ya kujitokeza kuwa mgombea - kimya kimya kabisa.

Lakini sasa, tutarajie kiasi gani cha influence ya Mkapa au JK kwa maamuzi ya Magufuli akiwa raisi? Inasemwa kwamba Magufuli ni mtu wa Mkapa 100%, na sio vibaya kutarajia chochote Mkapa atakachosema Magufuli atafanya, akijua wazi bila Mkapa yeye Magufuli asingekuwa alipo leo. Influence ya JK kwa Magufuli ni kidogo sana, na hata ile kidogo lazima iwe na baraka za Mkapa.

Kwa nini Mkapa awe na influence kiasi hicho kwa Magufuli? Inasemwa kwamba influence hiyo inatokana na urafiki wao binafsi. Wengine wanadai Magufuli alikuwa kwenye "system", yaani intelijensia ya Mkapa na serikali kabla hata hajawa Mbunge na kuteuliwa Waziri Mdogo, toka enzi Magufuli akiwa mwalimu.

Lakini watu wanaomfahamu wanamuonaje Magufuli kama Raisi? Wengi wanaona Tanzania ilipofikia inahitaji raisi kama Magufuli - namna fulani ya bulldozer ambalo linatumia nguvu bila kuangalia lojiki. Hata hivyo, wengi wana wasiwasi sana na influence ya Mkapa kwa Magufuli - kwamba itakuwa kama Makapa karudi kwenye uraisi, na wengi hilo hawalitaki.

Na wengine wana wasiwasi sana juu ya silka ya Magufuli katika kufanya maamuzi, wakisema ingekuwa Magufuli ndiye raisi kipindi cha JK, Tanzania ingekuwa imeshapigana vita na Rwanda na Malawi. Kuna wengine wanakumbusha jinsi Magufuli alivyokataa bila kushaurika kusafirishwa kwa boat za Azam kwenda Ziwa Victoria, ikabidi Mwandosya awaombe Kenya zile boti ziende ziwa Victoria kupitia barabara za Kenya. Na wengine wanakumbusha jinsi alivyokataa mabasi ya Zambia kupita barabara ya Tanzania Zambia, wakakwaruzana na Mwakyembe. Wengine wanadai ana silka ya kulipiza kisasi. Kuna mtu aligusia kwamba anaweza kukusweka ndani kwa sababu binafsi (eti alishaweka mume wa mtu ndani kwa sababu za ugomvi wa kimapenzi)

Vipi kuhusu mitandao kama JF? Kuna wengine hata wanasema katika uraisi wa Magufuli, uhai wa Mitandao ya Jamii kama JF uko mashakani sana!

Lakini kwa ujumla, watu wanasema huenda ni wakati muafaka kwa Tanzania kuwa na raisi kama Magufuli. Nchi imeharibika sana.
 
The Boss, wewe mtazamo wako ni upi kwenye mambo yanavyokwenda? Naamini tunamuhitaji mtu atakayebadilisha approach yetu kwenye mambo ya msingi. We need a person like JPM


Mimi naamini hafai
but wengine hawafai zaidi
in the end amekuwa kama 'malaika' mbele ya 'mashetani'

So bora nusu shari tu for now,tusubiri tuone
but aki fail sitashangaa
 
Mimi naamini hafai
but wengine hawafai zaidi
in the end amekuwa kama 'malaika' mbele ya 'mashetani'

So bora nusu shari tu for now,tusubiri tuone
but aki fail sitashangaa

Indeed...katika wale watano, hakukuwa na namna...ni heri nusu shari. Sijui vigezo gani vinatumika, ila ndio hivyo tena.
 
Hahahahaha lol!!!! Sijui siye Watanzania tulimkosea nini Mungu mpaka tupate watu wa ajabu ajabu ambao hawana hata sifa moja ya uongozi kuliongoza Taifa letu.

SABABU NI UVAMIZI WA zANZIBAR NA KUIINGIZA TANGANYIKA CHINI YA MWAVULI WA MUUNGANO FEKI
 
..Magufuli ni mropokaji.

..hana kabisa breki ya mdomo.

..pia inaonekana hajatulia kimawazo, na Uraisi hauhitaji mtu wa namna hiyo.

Mkuu joka kuu, nimetafakari sana capabilities za Magufuli kwenye Urais hasa kwenye kipengele cha mahusiano na majirani zetu.
Magufuli ni kama 'ndugu' wa Raila Odinga ambapo pia Kenya haijatulia 'kivile'. Uganda nayo kuna chokochoko za chini chini, Burundi na Rwanda hali tete, Malawi na sisi bado shughuli ni mbichi, Somalia, Sudan bado wanaweza kuisumbua EA.
Uzoefu unaonyesha Tanzania huwa ni mpatanishi. Ilikuwa hivyo kwa Mwinyi, Ben na sasa Kikwete.
Hawa viongozi watatu walikuwa wana Diplomatic Capabilities. Magufuli kwa historia hana hizo.
Ametoka kufundisha, kagombea ubunge, kapewa uwaziri na sasa anataka kuwa rais. Akiwa rais atakuwa na uwezo wa ku-manage haya mambo?
Mkandara
Pasco
Mag3
Somoche
 
Last edited by a moderator:
Mkuu joka kuu, nimetafakari sana capabilities za Magufuli kwenye Urais hasa kwenye kipengele cha mahusiano na majirani zetu.
Magufuli ni kama 'ndugu' wa Raila Odinga ambapo pia Kenya haijatulia 'kivile'. Uganda nayo kuna chokochoko za chini chini, Burundi na Rwanda hali tete, Malawi na sisi bado shughuli ni mbichi, Somalia, Sudan bado wanaweza kuisumbua EA.
Uzoefu unaonyesha Tanzania huwa ni mpatanishi. Ilikuwa hivyo kwa Mwinyi, Ben na sasa Kikwete.
Hawa viongozi watatu walikuwa wana Diplomatic Capabilities. Magufuli kwa historia hana hizo.
Ametoka kufundisha, kagombea ubunge, kapewa uwaziri na sasa anataka kuwa rais. Akiwa rais atakuwa na uwezo wa ku-manage haya mambo?
Mkandara
Pasco
Mag3
Somoche
Usishangae Mzito Kabwela, CCM inazama na ninavyojua mfa maji hutapatapa na hata majani atajaribu kuyang'ang'ania katika jitihada za kujaribu kujiokoa. Hiyo ndiyo sababu kubwa kwa nini wanamng'ang'ania Magufuli, completely a non starter...heri hata Ben alianza on a clean slate (so we were told), huyu jamaa anaanza na gunia la kashfa, next to nothing diplomacy na hata kuongea tu hajui. Lakini linalosikitisha zaidi ni kwamba huyo aliye msafi CCM hii tunayoijua imtoe wapi?
 
Last edited by a moderator:
Kwa harakaharaka Mh JPM anaonekana ni mtu asiye shaurika kirahisi, na pia asiyeweza kukontrol hasira zake. Hii ni hatari kwa mtu wa namna hii kupewa madaraka ya juu kabisa nchini.
 
Mkuu joka kuu, nimetafakari sana capabilities za Magufuli kwenye Urais hasa kwenye kipengele cha mahusiano na majirani zetu.
Magufuli ni kama 'ndugu' wa Raila Odinga ambapo pia Kenya haijatulia 'kivile'. Uganda nayo kuna chokochoko za chini chini, Burundi na Rwanda hali tete, Malawi na sisi bado shughuli ni mbichi, Somalia, Sudan bado wanaweza kuisumbua EA.
Uzoefu unaonyesha Tanzania huwa ni mpatanishi. Ilikuwa hivyo kwa Mwinyi, Ben na sasa Kikwete.
Hawa viongozi watatu walikuwa wana Diplomatic Capabilities. Magufuli kwa historia hana hizo.
Ametoka kufundisha, kagombea ubunge, kapewa uwaziri na sasa anataka kuwa rais. Akiwa rais atakuwa na uwezo wa ku-manage haya mambo?
Mkandara
Pasco
Mag3
Somoche
Mara nyingi rais huwa na washauri wake wa mambo mbali mbali lakini huchukua maamuzi sahihi baada ya kushauriwa. Hivyo usitegemee kwamba Mwinyi, Mkapa na Kikwete walikuwa wakifanya maamuzi yao wenyewe, zaidi ya hapo Upatanishi ni kipaji kinachotokana na hekima na Busara sio wadhifa ama Elimu .. Na uwezo wa mtu kaitka hili inategema anaheshimika vipi..
 
Mkuu joka kuu, nimetafakari sana capabilities za Magufuli kwenye Urais hasa kwenye kipengele cha mahusiano na majirani zetu.
Magufuli ni kama 'ndugu' wa Raila Odinga ambapo pia Kenya haijatulia 'kivile'. Uganda nayo kuna chokochoko za chini chini, Burundi na Rwanda hali tete, Malawi na sisi bado shughuli ni mbichi, Somalia, Sudan bado wanaweza kuisumbua EA.
Uzoefu unaonyesha Tanzania huwa ni mpatanishi. Ilikuwa hivyo kwa Mwinyi, Ben na sasa Kikwete.
Hawa viongozi watatu walikuwa wana Diplomatic Capabilities. Magufuli kwa historia hana hizo.
Ametoka kufundisha, kagombea ubunge, kapewa uwaziri na sasa anataka kuwa rais. Akiwa rais atakuwa na uwezo wa ku-manage haya mambo?
Mkandara
Pasco
Mag3
Somoche

..hilo la kuwa mpatanishi sidhani kama analiweza.

..lakini kuna suala kubwa zaidi, nalo ni nafasi na maslahi ya Tz ktk EAC.

..raisi wa Tz ajaye lazima awe makini kwamba hachukui maamuzi ambayo yatawaumiza wa-Tz ktk EAC.

..hii jumuiya imekaa kiujanja-ujanja, ambapo kila mwanachama anavutia kwake. sasa Raisi ajaye ni lazima aelewe kinachoendela ktk jumuiya.

cc Geza Ulole, Mkandara, Mag3
 
Magufuli pamoja na utendaji wake kawekwa pale kulinda maslahi ya waliopita! Hilo pekee linaanza kumletea shida na kama fununu tunazozisikia juu ya EL zikiwa kweli, mpambano huu utakuwa mtamuu ile mbaya tatizo CUF wana nia ya kuharibu hizi mbio tena wako radhi kucheza kadi za udini!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom