GE2025 Mgombea Udiwani ajenga kiwanda cha bilioni 14

GE2025 Mgombea Udiwani ajenga kiwanda cha bilioni 14

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Mgombea nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Musa Musa ambaye ameteuliwa na Chama hicho Kata ya Lugelele Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Mkoa wa Mbeya, amejenga kiwanda cha bilioni kumi na nne kitakachoajiri vijana 400 na kusaidia kutatua changamoto ya ajira.

Bw. Musa baada ya kuchukua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi ya Udiwani Oktoba 2025 amebainisha vipaumbele vyake huku akisema endapo wananchi watampa ridhaa ya kuwa Diwani wa Kata hiyo hatowaacha wanawake pamoja na vijana.
 
Back
Top Bottom