Mgombea Ubunge Chadema Jimbo la Bukene atishiwa kutekwa na kunyang'anywa Fomu

Mgombea Ubunge wa Chadema Jimbo la Bukene Lumola Stephen Kahumbi amepokea taarifa za vitisho vya kutekwa na kunyang'anywa Fomu za Uteuzi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Katika taarifa yake kwa Umma Lumola amesema tayari ameshawasilisha taarifa hizo kwa Jeshi la Polisi ili zifanyiwe kazi.

Lumola ameonya kwamba atatumia njia yoyote kujilinda ili fomu zake zisiporwe na akasema Yuko tayari kufa kuliko wampore fomu hizo.

WITO
Kutokana na Mara kadhaa wagombea wa Upinzani kufanyiwa hujuma za kutekwa na kuporwa fomu Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kupitia Kanda zake zote 10 wanapaswa kuandaa taratibu za kuwalinda wagombea wao wote wa Ubunge na Udiwani Kati ya leo mpaka siku ya Jumanne siku ya kurejesha fomu.
October 28 CCM hawachomoi
 
Kwa kawaida raia akitoa taarifa polisi kuwa kuna mazingira ambayo yanatoa tishio la usalama wake au mali zake, polisi wanalazimika kumpa ulinzi mtu huyo mpaka wanapojiridhisha kuwa mtu huyo yupo salama.

Bahati iliyopo ni kuwa, mara kadhaa polisi hao hao wanaitakiwa kutoa hakikisho la usalama, huwa ni sehemu ya hayo matukio machafu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndivyo inavyotakiwa.
 
Sheria ya uchaguzi iende mbali kuwa wote waliochukua fomu wapewe ulinzi na Polisi 24/7 mpaka 28 .10.2020.

Kama kipengele hicho cha sheria hakipo basi Kamati ya Ulinzi na Usalama za Mikoa na Wilaya wafanye kujiongeza ili matukio haya ya kutishia demokrasia yasiwepo.
Ni hatari Sana kwa ustawi wa Demokrasia yetu
 
Pole sana ndugu yangu Lumola kahumbi, ila usiwaze sana Robert Amsterdam huu mwaka wameshajiapiza kuwa hawatocheka na kima tena.
 
Pole sana Lumola, Usikate tamaa na wala usitishwe Mapambano yanaendelea
 
Mgombea Ubunge wa Chadema Jimbo la Bukene Lumola Stephen Kahumbi amepokea taarifa za vitisho vya kutekwa na kunyang'anywa Fomu za Uteuzi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Katika taarifa yake kwa Umma Lumola amesema tayari ameshawasilisha taarifa hizo kwa Jeshi la Polisi ili zifanyiwe kazi.

Lumola ameonya kwamba atatumia njia yoyote kujilinda ili fomu zake zisiporwe na akasema Yuko tayari kufa kuliko wampore fomu hizo.

WITO
Kutokana na Mara kadhaa wagombea wa Upinzani kufanyiwa hujuma za kutekwa na kuporwa fomu Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kupitia Kanda zake zote 10 wanapaswa kuandaa taratibu za kuwalinda wagombea wao wote wa Ubunge na Udiwani Kati ya leo mpaka siku ya Jumanne siku ya kurejesha fomu.

Updates Leo Jumapili 23/8/20

*_UTEKAJI WA MGOMBEA UDIWANI KEREGE- BAGAMOYO_*

Taarifa kutoka kwa Baraka Mwago Mwenyekiti Kanda ya Pwani

Makamanda Salama,
Watu wanaojiita Polisi walifika nyumbani kwa Mgombea wetu wa Udiwani kata ya Kerege - Bagamoyo Mhe. *_Martin Sultani Anney_* saa 03 usiku na kujitambulisha kuwa ni polisi na wamefika kumkamata ili kumpeleka Polisi akatoe maelezo ya makosa ya uhalifu aliyofanya huko Morogoro.

Watekaji hao walikuwa na dhamira ya kumpeleka Morogoro ili asiweze kurudisha fomu ya kugombea. Makamanda wa Bagamoyo walimsaka usiku kucha vituo vyote polisi Bagamoyo na vile vya DSM vilivyopo karibu na Bagamoyo na polisi walikana kuwa na mpiganaji mwenzetu.

Watekaji wakiwa na hofu ya kukamatwa/kufuatiliwa na polisi au CHADEMA walijikuta wanapita njia isiyotoka iliyopelekea kumtelekeza Mgombea wetu pamoja na gari yao mpaka alipopata msaada wa Bodaboda.

Kwasasa wako polisi Mlandizi na dereva wa watekaji ameweza kukamatwa aliporudi kujaribu kuchukua gari walilotelekeza na kwa maelezo ya awali ya dereva wa watekaji anakiri wametumwa na viongozi wa CCM ili kuzuia mgombea wetu asiweze kurudisha fomu na wao wapitwe bila kupingwa.

Tutaendelea kupeana taarifa kwa kila kinachojiri
Vitendo Kama hivi sio vizuri Kama havikemewi kwa nguvu zote, maana vinaikaribisha CIA Tanzania
 
Back
Top Bottom