Elections 2010 Mgombea CHADEMA afariki

DICTATOR

JF-Expert Member
Sep 17, 2010
391
3
na Ali Lityawi, Kahama

Source: Tanzania Daima

MGOMBEA udiwani wa Kata ya Igunda, Wilaya ya Kahama kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Charles Malecha Kasonha (43), amefariki dunia jana majira ya saa 10:30 alfajiri katika hospitali ya serikali wilayani hapa.

Kasonha alifikwa na mauti baada ya kusumbuliwa na maradhi ya tumbo na kulazwa kwa muda wa siku tatu.

Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Kahama, Juma Ntahimpera, alisema mgombea huyo aliyekuwa akiwania kata hiyo mpya iliyogawanywa kutoka Kata ya Nyandekwa, alifikwa na mauti hayo alfajiri ya Ntahimpera alisema marehemu Kasonha aliugua tumbo ghafla mara baada ya uzinduzi wa kampeni za mgombea Ubunge wa chama hicho, Jimbo la Kahama.

“Baada ya uzinduzi huo, marehemu alijisikia tumbo kumsokota, alitutaarifu tukampeleka hospitali… alilazwa hadi alipofikwa na mauti,” alisema Ntahimpera.

Mwenyekiti huyo wa CHADEMA wa Wilaya alisema marehemu huyo aliyeacha mjane mmoja na watoto sita atazikwa kesho saa nne asubuhi katika kijiji alichozaliwa cha Bunasani, Kata ya Igunda. Katika kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya udiwani kwenye kata hiyo, marehemu alikuwa akichuana vikali na wagombea wawili wa vyama vya CUF na CCM.

Swali langu: Vipi wadau hapo sheria inasemaje kuhusu kuweka mgombea mbadala au utaratibu ni upi hapo? Nawaombeni ufafanuzi hapo.
 
na ali lityawi, kahama


source: Tanzania daima.
amka2.gif
mgombea udiwani wa kata ya igunda, wilaya ya kahama kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (chadema), charles malecha kasonha (43), amefariki dunia jana majira ya saa 10:30 alfajiri katika hospitali ya serikali wilayani hapa.
Kasonha alifikwa na mauti baada ya kusumbuliwa na maradhi ya tumbo na kulazwa kwa muda wa siku tatu.
Mwenyekiti wa chadema wilaya ya kahama, juma ntahimpera, alisema mgombea huyo aliyekuwa akiwania kata hiyo mpya iliyogawanywa kutoka kata ya nyandekwa, alifikwa na mauti hayo alfajiri ya ntahimpera alisema marehemu kasonha aliugua tumbo ghafla mara baada ya uzinduzi wa kampeni za mgombea ubunge wa chama hicho, jimbo la kahama.
"baada ya uzinduzi huo, marehemu alijisikia tumbo kumsokota, alitutaarifu tukampeleka hospitali… alilazwa hadi alipofikwa na mauti," alisema ntahimpera.
Mwenyekiti huyo wa chadema wa wilaya alisema marehemu huyo aliyeacha mjane mmoja na watoto sita atazikwa kesho saa nne asubuhi katika kijiji alichozaliwa cha bunasani, kata ya igunda. Katika kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya udiwani kwenye kata hiyo, marehemu alikuwa akichuana vikali na wagombea wawili wa vyama vya cuf na ccm.


Swali langu: Vipi wadau hapo sheria inasemaje kuhusu kuweka mgombea mbadala au utaratibu ni upi hapo? Nawaombeni ufafanuzi hapo.


shaka ondoa mkuu jina la marehemu litakuwepo kwenye kinyanganyiro na akiishinda tu wanatangaza kuwa wazi hivyo tunarudia tena uchaguzi hapo yoyote anaruhusiwa
rip
kamanda
 
god is there for those in need,mungu ailaze roho yake mahali pema peponi,wanachadema pls msikate tamaa
 
Back
Top Bottom