johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 104,319
- 183,528
Mgombea ubunge wa CCM jimbo la Tunduru Kaskazini, Injinia Ramo Makani, alianguka jukwaani wakati wa kampeni. Alikuwa anaruka kichurachura kuwathibitishia wapiga kura yuko fiti kiafya ndipo 'aibu' hiyo ilipomkuta.
My take: Acheni Mungu aitwe Mungu!
View attachment 294680
Mgombea ubunge wa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Tunduru Kaskazini,Mhandisi Ramo Makani alianguka jukwaani wakati akijaribu kuruka kichura chura.
Tukio hilo lilitokea katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za mgombea huyo, uliofanyika kwenye viwanja vya baraza la Idd mjini hapa.
Inasadikiwa kuwa alikusudia kunogesha staili ya mgombea urais wa tiketi ya CCM,Dr. John Magufuli ya kupiga Push Up..
Ingawa tukio hilo lilionekana kumfedhehesha,mgombea huyo alijikakamua kuinuka huku akisaidiwa na walinzi wake na kuendelea kunadai sera zake.
Alisema kuwa katika kipindi kilichopita alitekeleza ilani ya chama chake kwa kusimamia ujuenzi wa barabara ya Namtumbo-Tunduru hadi wilayani Nanyumbu inayoendelea kujengwa kwa kiwango cha lami.
Nitasimamia kwa nguvu zangu zote kuhakikisha kuwa mradi wa kusambaza umeme vijijini unaanza'' alisema.
Chanzo: Majira
My take: Acheni Mungu aitwe Mungu!