Mgogoro wa Ethiopia unadhihirisha umadhubuti wa mfumo wetu wa mikoa dhidi ya ule mfumo wa majimbo

nasrimgambo

JF-Expert Member
Jan 10, 2017
1,858
2,348
Habari wanajamvi,

Kama ilivyo kawaida, kufanya tafakuri ya mambo yale mtu anayoyasikia maredioni na magazetini kuhusu yanayoendelea kwenye siasa za nchi mbalimbali.

basi nami nimejikuta nikiyatafakari sana yale yanayoendelea huko Ethiopia na vita vyao vya serikali ya kitaifa na wanamgambo wa jimbo lao la tigrinya, ambapo sasa vita hivyo vimeonekana kuvuta na makundi mengine ya makabila toka majimbo tofauti na tigrinya, tena mbaya zaidi makundi hayo yameanza na kutaka kudai uhuru.

Sasa, nikakumbuka mfumo wao wa uongozi wa Ethiopia wa kutumia majimbo, na kukumbuka jinsi baadhi ya watanzania huwa wanausema mfumo wetu wa mikoa ambao mkuu wa mkoa anateuliwa na rais hivyo kufanya serikali kuu kuwa na mkono wa moja kwa moja kwenye kuongoza mkoa, ambapo ni tofauti na mfumo wa majimbo ambapo kiongozi wa mkoa anapigiwa kura

Ubaya wa majimbo ni kuwa viongozi hao wa majimbo wana kuwa na mamlaka makubwa hata yanawajaa vichwani mara nyingine na kuwa fanya kutaka kuwa juu ya serikali ya kitaifa

Mfano serikali ya jimbo la tigrinya ambalo viongozi wake ndio vinara wa kisapoti waasi wapiganao dhidi ya serikali kuu. Mbaya zaidi mfumo huo wa majimbo unatoa mamlaka ya majimbo kuunda majeshi yao, ndio yanaibuka hayo ya makundi ya kiti gray, ambayo kiukweli ni jeshi la ndani la jimbo la Tigrinya

Kila nikiangalia utulivu wa nchi yetu na jinsi ambavyo serikali ni madhubuti, hivi, hata siuoni mwanya wa mkoa fulani kutuletea vurugu za kujitenga ama kuanzisha mapigano ndivyo ninazidi kuu appreciate mfumo wetu wa mikoa tulio nao

Watanzania badala ya kutumia muda mwingi kuponda mifumo yetu ya kisiasa nashauri tuanze kuisifia, maana ni mifumo inayotuletea amani na umadhubuti wa hali ya juu wa taifa na serikali kuu yake.

Viongozi waasisi wa taifa letu walikuwa na ujiniasi wa kipekee kabisa maana taifa hili walilolisuka baada ya kulipokea toka kwa wakoloni wamelisuka vizuri sana, ulimbukeni wa kukaa na kuona mifumo ya siasa ya wezetu ni bora zaidi ya kwetu tukiuendekeza utafanya siku moja tufumuefumue taifa hili lililosukwa vyema.
 
umeandika sahihi, lakini umejikita kwenye sehemu moja ya aina ya mfumo wa uongozi wa nchi. Lakini changamoto za Ethiopia ni zaidi ya hizo. Kinacholeta ukosefu wa amani ni kwa sababu ya serikali ya Abby kuwa wabinafsi na madikteta. Unajua kwa Nini kabla ya Abby migogoro hii haikuwa na Nguvu au haikuwepo? Ni kwa sababu wenzao Watigray walibalance uongozi bila ubaguzii.

Kitu kingine ni aina ya Wananchi. Watanzania wengi wao ni kama mazombie. Hata uwafanye Nini hawezi kuchukua hatua, Ndio maana unaona Kiongozi anafanya anavyotaka na haguswi, Yaani hawajibishwi na raia. Ndio maana kwenye tozo wakasema Watanzania watazoea tu. Na kweli mmezoea.

Sasaivi bei ya mbolea juu, hakuna anayeona, watu wanalia kimyakimya, Tanzania Ina mambo mengi ambayo yangeweza kuwafanya waende msituni au waandame ila kwa sababu ya uzombi Ndio maana kila ripoti ikija Tanzania nchi isiyo na furaha sawa na somalia, Libya, Burundi na Kongo kwenye vita.

In short kila mtanzania anaandamana na kupigana na serikali hii motoni mwake. Ndio maana watu wanazidi kuchakaa. Maandamano ya moyoni ni mabaya kuliko maandamano ya dhahiri. Hope nimeeleweka.
 
Mifumo ya majimbo kwa afrika nzima ni tatizo.

Maana mwafrika akishika uongozi anajiona yeye ndio bora kuliko wengine.

Ubinafsi

Kama hivyo akiona kwenye eneo lake kuna mali ujue chochote anafanya.

Wakati mwingine anatamani abaki yeye nafamalia yake tu, kwahiyo hata wengine wakifa hawezi kujali.

Mifumo ya majimbo inafaa kwa walioelimika na waliokomaa kisiasa.
 
Wako ndugu zetu kutoka CHADEMA

Huiona mbeleko pale wanapotanguliza sera za MAJIMBO na kutoa mifano ya nchi nyingi zilizopiga hatua na kutokuwa na migogoro

Ndugu hao hupendelea kutoa mifano ya nchi za ULAYA NA MAGHARIBI kana kwamba Waafrika/Afrika tunafanana nao hao watu

Wengine hutoa mfano wa Afrika ya Kusini(SA) wanasahau kuwa mpaka leo Afrika ya Kusini bado uchumi wao UKO MIKONONI mwa wachache weupe na ndio maana akina Tate Julius Malema na Floyd Shivambu bado wanaona hawajakomboka KIUCHUMI kufikia kuja na chama chao chenye sera za KIKOMUNISTI (EFF) nilidhani wangeiga na hili kwa CHADEMA kuwa na Sera za kikomunisti 🤣🤣🤣...kinyume chake wao CDM wanavaa tu MAKOMBATI NA BERETI(nyekundu) kinyume kabisa na msimamo wao(siasa za Kati)🤣🤣

Chadema wasichokijua ni kuwa nchi za ULAYA karibuni zote zinaendeshwa chini ya UFALME tena ufalme wenye "nasabu-uhusiano" mmoja, japo chini yake kuna serikali ambazo tunaambiwa zina maamuzi yote kuzidi hizo falme(changa la macho hili) 🤣🤣🤣

Mathalani tawala ya kifalme ya ulaya iitwayo Saxe-Coburg-Gotha ilianzia UJERUMANI...ndio haohao watawala wa UBELGIJI(alipokimbilia ndugu wakili msomi Tundu Lissu) ndio haohao watawala wa Uingereza n.

Hakika kinachoendelea Ethiopia kinaweza kuikuta nchi yoyote ya Afrika yenye tawala za kimajimbo....huko Kongo ilipata kutokea Katanga kutaka kujitenga na isisahaulike kuwa leo KONGO inashindwa kutawalika/kuletwa AMANI kwa sababu hizohizo, baadhi ya majimbo YAMETELEKEZWA kufikia baadhi ya MAADUI WA NJE KUYAFANYA MAKAZI YAO.

Kwa hili la MIKOA tuendelee tu KUMUIMBA KWA SIFA lukuki na kummwagia DUA nyingi hayati baba wa taifa Mwalimu Nyerere ,aaaamin aaaamin 🙏

Hakika bila ya hili pengine tungekuwa tumeshayashuhudia ya ETHIOPIA ama yangekuwa yako njiani karibuni kutujia.........

#SIEMPRE JMT
#NCHI KWANZA
#TANZANIA NCHI YA MFANO AFRIKA💪
#TUILINDE AMANI YETU KWA NGUVU ZOTE
#KAZI IENDELEE
 
mifumo ya majimbo kwa afrika nzima ni tatizo.

maana mwafrika akishika uongozi anajiona yeye ndio bora kuliko wengine.

ubinafsi.
kamahivyo akiona kwenye eneo lake kuna mali ujue chochote anafanya.
wakati mwingine anatamani abaki yeye nafamalia yake tu ,kwahiyo hata wengine wakifa hawezi kujali.

mifumo ya majimbo inafaa kwa walioelimika na waliokomaa kisiasa.
Exquisite 😍
 
Wako ndugu zetu kutoka CHADEMA

Huiona mbeleko pale wanapotanguliza sera za MAJIMBO na kutoa mifano ya nchi nyingi zilizopiga hatua na kutokuwa na migogoro.

Ndugu hao hupendelea kutoa mifano ya nchi za ULAYA NA MAGHARIBI kana kwamba Waafrika/Afrika tunafanana nao hao watu.

Wengine hutoa mfano wa Afrika ya Kusini(SA)...wanasahau kuwa mpaka leo Afrika ya Kusini bado uchumi wao UKO MIKONONI mwa wachache....weupe.... na ndio maana akina Tate Julius Malema na Floyd Shivambu bado wanaona hawajakomboka KIUCHUMI kufikia kuja na chama chao chenye sera za KIKOMUNISTI (EFF)....nilidhani wangeiga na hili kwa CHADEMA kuwa na Sera za kikomunisti ...kinyume chake wao wanavaa tu MAKOMBATI NA BERETI(nyekundu) kinyume kabisa na msimamo wao(siasa za Kati)

Chadema wasichokijua ni kuwa nchi za ULAYA karibuni zote zinaendeshwa chini ya UFALME tena ufalme wenye "nasabu-uhusiano" mmoja....japo chini yake kuna serikali ambazo tunaambiwa zina maamuzi yote kuzidi hizo falme(changa la macho hili)

Mathalani tawala ya kifalme ya ulaya iitwayo Saxe-Coburg-Gotha ilianzia UJERUMANI...ndio haohao watawala wa UBELGIJI(alipokimbilia ndugu wakili msomi Tundu Lissu)....ndio haohao watawala wa Uingereza n.k

Hakika kinachoendelea Ethiopia kinaweza kuikuta nchi yoyote ya Afrika yenye tawala za kimajimbo....huko Kongo ilipata kutokea Katanga kutaka kujitenga na isisahaulike kuwa leo KONGO inashindwa kutawalika/kuletwa AMANI kwa sababu hizohizo, baadhi ya majimbo YAMETELEKEZWA kufikia baadhi ya MAADUI WA NJE KUYAFANYA MAKAZI YAO.

Kwa hili la MIKOA tuendelee tu KUMUIMBA KWA SIFA lukuki na kummwagia DUA nyingi hayati baba wa taifa Mwalimu Nyerere ,aaaamin aaaamin

Hakika bila ya hili pengine tungekuwa tumeshayashuhudia ya ETHIOPIA ama yangekuwa yako njiani karibuni kutujia.

#SIEMPRE JMT
#NCHI KWANZA
#TANZANIA NCHI YA MFANO AFRIKA
#TUILINDE AMANI YETU KWA NGUVU ZOTE
#KAZI IENDELEE
Uchambuzi mzuri

Hawa watu wa Chama kikuu cha upinzani wanakasumba ya kukosoa kiiila jambo la mifumo yetu ya kiongozi kama taifa
 
Mifumo ya mikoa hupelekea nchi kuvunjika ndiyo maana watu huopt mfumo wa majimbo. Mfumo wa majimbo huwa haisababishi nchi kusambaratika bali huwekwa ili kuokoa nchi kusambaratika sababu ya mfumo mbovu wa mikoa. Mtazamo wako unaangalia vitu kinyumenyume. Kwa sababu mfumo ulikuwepo mara tu kabla ya nchi kuchafuka, haimaanishi ndiyo umeleta machafuko. Inahitaji umakini unapoangalia cause and effects.

Nchi kama Mynamar inafikiria kuingia kwenye mfumo wa majimbo sababu mfumo wa mikoa unataka kuvunja nchi.
 
Uchambuzi mzuri,
Hawa watu wa Chama kikuu cha upinzani wanakasumba ya kukosoa kiiila jambo la mifumo yetu ya kiongozi kama taifa
Hakika kamarada

Yaani unaweza kuwasikiliza vijana wenzetu wa CHADEMA na kuishia kucheka tu.....tatizo lao wengi wao wanaongozwa na MIHEMKO NA HISIA katika mambo yanayohitaji UHALISIA......mathalani "ari ya ujana" inawasumbua Sana....kwani ni kipindi Cha ujana ambacho tuna nguvu kubwa ya KUKOSOA TU....KUKUSOA TU.....tena kukosoa KIMAKUNDI.... ndio maana wengi wa wafuasi wa CHADEMA utawakuta wako vyuo vikuu.....na mara nyingi huendelea na misimamo yao miaka isiyozidi 5 baada ya kumaliza vyuo(UHALISIA WA MAISHA).....

Wengi wa vijana wa CHADEMA wameathiriwa na WANAHARAKATI(NGOs).....ambao hupata "fedha nyingi" kwa ajili ya SHUGHULI ZAO.....wakati mwingine baadhi ya NGOs hutumikia MAELEKEZO YA WASIOPENDA AMANI YETU NA KULETA MISUGUANO ILI KUTOKEE "COUP D ETAT".....mifano iko mingi mathalani iko TAASISI moja kubwa ilishawahi kusababisha hayo huko INDONESIA....kwa harakati zilizoanzia vyuo vikuu.


Siempre JMT
ford.png
 
Nidhamu ya woga ndo inafanya CCM kuogopa mfumo wa majimbo.
Faida za mfumo wa majimbo ni lukuki kuliko hasara zake.
Imagine jimbo la victoria (MWANZA, SHINYANGA,MARA,KAGERA) wasimamie rasilimali zao kwa ajili ya wananchi wao.
Bulyanhulu,almasi,ziwa Victoria, serengeti.
Jimbo la kaskazini (Arusha,Kilimanjaro,Tanga)
Wasimamie rasilimali zao mlima,mbuga,bandari,tanzanite.
JIMBO LA KUSINI (Mtwara,lindi,Ruvuma)
Wasimamie Korosho,Gesi,Mawese,Tumbaku.
Jimbo la Nyanda za juu kusini (Iringa,Mbeya,Songwe)
Wasimamie wenyewe rasilimali zao Kilimo cha mazao ya chakula, kilimo cha miti.
Jimbo la Pwani (Dar es Salaam, Pwani)
Wasimamie rasilimali zao Pwani ni eneo la Viwanda, Bandari ya Dar.
ETC.
na majimbo mengine yoote.
DODOMA IBAKI KUWA JIMBO HURU. FREE STATE SHUGHULI ZOTE ZA SERIKALI KUU ZIWE ZINAFANYIKA DODOMA BILA KUATHIRIWA NA SERIKALI ZA MAJIMBO.
Serikali kuu iwe msimamizi wa shughuli za serikali za majimbo...
Serikali za majimbo ziwe na maamuzi juu ya shughuli kwayo.
CCM wanafaidika sana na huu mfumo wa mikoa kwa sababu unaendeleza umaskini wa kupindukia mtaji wa CCM ni masikini the so called Wanyonge... Uwepo wa wanyonge wengi ndo uhai wa CCM.
FAIDA YA MAJIMBO NI FREE AND FAIR COMPETITION MAJIMBO YATAPAMBANA KUVUTIA WAWEKEZAJI MFANO JIMBO LA KASKAZINI LITAPAMBANA KUVUTIA WATALII... shughuli za kuvutia watalii hazitasimamiwa na TANAPA BALI NA TOURISM DEPARTMENT YA JIMBO HUSIKA.
JIMBO LA KASKAZINI LITAPAMBANA KUHAKIKISHA WANAKUWA NA KILIMANJARO AIRWAYS.

HUU MFUMO WA MAJIMBO NI HATARI SANA KWA UHAI WA CCM KWANI LITAWAFUMBUA MACHO HADI MAJIMBO YENYE RASILIMALI CHACHE KUPAMBANA.
CCM hawahitaji nchi hii iwe na raia wengi matajiri ndo maana wamachinga,bodaboda,wanaobadilisha fedha za kigeni walisumbuliwa sana kipindi cha mwendazake.
Mfumo wa sasa wa mikoa umewekwa kuhakikisha unaipa pumzi CCM.
Mtaji wa CCM ni umaskini,ujinga na maradhi. Hivi vikitoweka na CCM itatoweka.

#KATIBAMPYANISASA
 
mifumo ya majimbo kwa afrika nzima ni tatizo.

maana mwafrika akishika uongozi anajiona yeye ndio bora kuliko wengine.

ubinafsi.
kamahivyo akiona kwenye eneo lake kuna mali ujue chochote anafanya.
wakati mwingine anatamani abaki yeye nafamalia yake tu ,kwahiyo hata wengine wakifa hawezi kujali.

mifumo ya majimbo inafaa kwa walioelimika na waliokomaa kisiasa.

Sentensi yako ya mwisho inalihukumu bara la Afrika kuwa nyonge daima. Kuwa bara la wajinga (ignorants) wasiokuwa na weledi wa kisiasa (lacking political savvy). Kihivyo, hakuna namna Waafrika wanaweza kuwa na jeuri ya kutembea kifua mbele, kujitegemea na kushindana kwenye soko la kimataifa.

Halafu ni kupotosha kufikiri viongozi wa majimbo wanakuwa na madaraka yote juu ya taasisi na vyombo vyote vya dola. Mfano hapa Tanzania. Rais wa Zanzibar SI amiri mkuu wa majeshi na si mkuu wa Mambo ya Nje wala ya Ndani. Mamlaka hayo ni ya Rais wa JMT pekee.

Utawala wa Ethiopia ya leo unaundwa na vikundi vya wapigania uhuru wa majimbo ya kikabila yaliyokuwa mwanzoni chini ya utawala wa kifalme na baadaye chini ya utawala wa kidikteta/kikomunisti na mwishowe Federation.

Tatizo lao kuu si majimbo bali ni kuendelea kuwepo kwa vikundi vya kijeshi chini ya miamvuli ya vyama vya siasa vya kikabila vinavyotawala majimbo. Ethiopia huwezi kuwa na chama cha siasa ambacho sio cha kikabila. Na wako tayari kwa mapambano hata kumwaga damu wakihisi wanaonewa.

Tanzania hatuna vikundi vya kijeshi vya kikabila. Vyama vya siasa si vya kikabila. Rais wa JMT ndiye mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama. Watanzania wameshachanganyika sana kijamii, kisiasa na kijiografia. Hakuna namna mgawanyiko kama wa Ethiopia unaweza kutokea.
 
umeandika sahihi, lakini umejikita kwenye sehemu moja ya aina ya mfumo wa uongozi wa nchi. Lakini changamoto za Ethiopia ni zaidi ya hizo. Kinacholeta ukosefu wa amani ni kwa sababu ya serikali ya Abby kuwa wabinafsi na madikteta. Unajua kwa Nini kabla ya Abby migogoro hii haikuwa na Nguvu au haikuwepo? Ni kwa sababu wenzao Watigray walibalance uongozi bila ubaguzii.

Kitu kingine ni aina ya Wananchi. Watanzania wengi wao ni kama mazombie. Hata uwafanye Nini hawezi kuchukua hatua, Ndio maana unaona Kiongozi anafanya anavyotaka na haguswi, Yaani hawajibishwi na raia. Ndio maana kwenye tozo wakasema Watanzania watazoea tu. Na kweli mmezoea. Sasaivi bei ya mbolea juu, hakuna anayeona, watu wanalia kimyakimya, Tanzania Ina mambo mengi ambayo yangeweza kuwafanya waende msituni au waandame ila kwa sababu ya uzombi Ndio maana kila ripoti ikija Tanzania nchi isiyo na furaha sawa na somalia, Libya, Burundi na Kongo kwenye vita.
In short kila mtanzania anaandamana na kupigana na serikali hii motoni mwake. Ndio maana watu wanazidi kuchakaa. Maandamano ya moyoni ni mabaya kuliko maandamano ya dhahiri. Hope nimeeleweka.
Duuuh 😳😳😳

Hayati Meles Zenawi alitokea Tigray......aliitawala hiyo nchi kwa MKONO WA CHUMA......

Unajua ni kwanini alifanya hayo ?!!!

Kwa sababu Ethiopia ni nchi ya kikabila na matabaka....matabaka makubwa ni OROMO na AMHARA ambao huwa wanadai "share" kubwa kwa sababu ya WINGI wao .....Meles Zenawi aliiongoza nchi hiyo kwa MKONO WA CHUMA Kama afanyavyo ABIY AHMED.....na la kushangaza ABIY AHMED ni mchanganyiko wa kutoka OROMO na AMHARA....ndugu zake hao wanamuona kama mtu msaliti aliyewageuka....wao walitegemea ANGEWABEBA KIKANDA......

Ikumbukwe alipoondoka Meles Zenawi Watigrinya walikuwa ni KABILA hodhi ya kila eneo la kimkakati nchini Ethiopia ijapokuwa ni kabila DOGO.........

Leo wameungana(ajabu kabisa) wanamshambulia ndugu yao Abiy Ahmed wakiwa bega kwa bega na kundi lililofaidika kipindi cha hayati Zenawi(TPLF)....

Hapa ndipo tunapopinga Sera za MAJIMBO kwani hutokea siku isiyo na jina WANASIASA kwa tamaa na ULAFI WAO huiingiza nchi matatizoni....wanaoumia ni wazee ,wanawake na watoto!!!!

SIEMPRE JMT
 
Mifumo ya mikoa hupelekea nchi kuvunjika ndiyo maana watu huopt mfumo wa majimbo. Mfumo wa majimbo huwa haisababishi nchi kusambaratika bali huwekwa ili kuokoa nchi kusambaratika sababu ya mfumo mbovu wa mikoa. Mtazamo wako unaangalia vitu kinyumenyume. Kwa sababu mfumo ulikuwepo mara tu kabla ya nchi kuchafuka, haimaanishi ndiyo umeleta machafuko. Inahitaji umakini unapoangalia cause and effects.

Nchi kama Mynamar inafikiria kuingia kwenye mfumo wa majimbo sababu mfumo wa mikoa unataka kuvunja nchi.
Burma au Myanmar tatizo ni Military Junta kupindua serikali za kiraia na sio suala la majimbo.
Wewe ndie unajadili kinyume nyume.
 
umeandika sahihi, lakini umejikita kwenye sehemu moja ya aina ya mfumo wa uongozi wa nchi. Lakini changamoto za Ethiopia ni zaidi ya hizo. Kinacholeta ukosefu wa amani ni kwa sababu ya serikali ya Abby kuwa wabinafsi na madikteta. Unajua kwa Nini kabla ya Abby migogoro hii haikuwa na Nguvu au haikuwepo? Ni kwa sababu wenzao Watigray walibalance uongozi bila ubaguzii.

Kitu kingine ni aina ya Wananchi. Watanzania wengi wao ni kama mazombie. Hata uwafanye Nini hawezi kuchukua hatua, Ndio maana unaona Kiongozi anafanya anavyotaka na haguswi, Yaani hawajibishwi na raia. Ndio maana kwenye tozo wakasema Watanzania watazoea tu. Na kweli mmezoea.

Sasaivi bei ya mbolea juu, hakuna anayeona, watu wanalia kimyakimya, Tanzania Ina mambo mengi ambayo yangeweza kuwafanya waende msituni au waandame ila kwa sababu ya uzombi Ndio maana kila ripoti ikija Tanzania nchi isiyo na furaha sawa na somalia, Libya, Burundi na Kongo kwenye vita.

In short kila mtanzania anaandamana na kupigana na serikali hii motoni mwake. Ndio maana watu wanazidi kuchakaa. Maandamano ya moyoni ni mabaya kuliko maandamano ya dhahiri. Hope nimeeleweka.
Kama "uzombi" wa watanzania ndiyo unaofanya tuwe na amani hii tuliyonayo na stability hii tuliyonayo, basi si uzombi bali ni akili.

Kwani wewe unadhani hili usionekane zombi basi lazima ulalamikelalamike? Kitu gani ambacho serikali hii imefanya ambacho hakikupasi kama wewe mwanachi ukifanye? Kama hutaki kutozwa tozo basi usitoe tozo na hakuna aliyekulazimisha utoe tozo. Watanzania tunaishi kwa kanuni ya "contentment", tunahitaji amani, tunahitaji stability, vinginevyo vitafuata kwa juhudi binafsi na maarifa. Basi.
 
Vijana wa Lumumba baada ya kukosekana kwenye teuzi za chama Sasa wanajikuta kukosoa tawala za mfumo wa majimbo ili waonekane na wazidi kuvutia mamlaka za uteuzi. Suala la Ethiopia tatizol la utawala wa majimbo wala halina nguvu katika fukuto lote pale. Ukabila ndio tatizo kubwa.

Go and study mjue sababu zilizopelekea Mengetsu Haile Mariam mpaka anamzika chooni Haile Selassie sababu alizozitoa zilikuwa ni majimbo ama la.
 
kwa takwimu zipi hasa ukiangalia dunia nzima?

dunia nzima yote ipo kwenye majimbo,then inatokea nchi moja kati ya 400 inapata tatizo unasema 1/400 ni best probability?

Hivi ulisoma Statistics and Probability shule ya chooni?

Na mgogoro wa Tigray sababu yake ni ingine kabisa compared na unachoongea hapa
Nchi 54 za Afrika ni nchi 5 tu zenye mfumo huo.......

Nchi 48 za bara la Asia ni nchi 5 tu zenye huo mfumo wa kimajimbo......

India na ndugu yake Pakistan.....

Nepal na Burma pamoja na Iraq.....

✓India mpaka Leo uchumi wake haujawa sawa kimajimbo na Kuna matabaka sugu ya kutosha tu......

✓Iraq toka enzi ya Saddam kumekuwa na msuguano na WAKURDI wanaotaka kujitenga.....

Kule Amerika ya kusini ,Kati ya 12 ni 4 tu ( Venezuela ,Mexico ,Argentina na Brazil)......

✓Jimbo la ZULIA nchini Venezuela wanapambana kujitenga(vikundi viko active)
✓Argentina kule Patagonia wanataka kujitenga (vikundi vya silaha)
✓Brazil Jimboni Sao Paulo(vikundi vya silaha)
✓Mexico imefurutu ADA ya madawa ya kulevya.....

SIEMPRE JMT
 
Vijana wa Lumumba baada ya kukosekana kwenye teuzi za chama Sasa wanajikuta kukosoa tawala za mfumo wa majimbo ili waonekane na wazidi kuvutia mamlaka za uteuzi. Suala la Ethiopia tatizol la utawala wa majimbo wala halina nguvu katika fukuto lote pale. Ukabila ndio tatizo kubwa.

Go and study mjue sababu zilizopelekea Mengetsu Haile Mariam mpaka anamzika chooni Haile Selassie sababu alizozitoa zilikuwa ni majimbo ama la.
Yaani tusitoe mawazo yetu ya kujenga nchi kwa kuogopa kuwa tutaitwa tunajipendekeza ?!!! Khaaa 😳😳

Mawazo ya ajabu kabisa haya duuuh 😳😳

CCM ina vijana wengi....yaani wote wateuliwe ilihali uteuzi si tu kwa ajili ya vijana ?!!

Hapa tunajadili mapungufu ya Sera za MAJIMBO hususani barani Afrika kwa mustakabali mwema wa taifa letu na kukua kwake zaidi ya hizo nafasi za uteuzi na maslahi ya mtu mmoja mmoja......

Amka wewe......

SIEMPRE JMT
 
Habari wanajamvi,

Kama ilivyo kawaida, kufanya tafakuri ya mambo yale mtu anayoyasikia maredioni na magazetini kuhusu yanayoendelea kwenye siasa za nchi mbalimbali.

basi nami nimejikuta nikiyatafakari sana yale yanayoendelea huko Ethiopia na vita vyao vya serikali ya kitaifa na wanamgambo wa jimbo lao la tigrinya, ambapo sasa vita hivyo vimeonekana kuvuta na makundi mengine ya makabila toka majimbo tofauti na tigrinya, tena mbaya zaidi makundi hayo yameanza na kutaka kudai uhuru.

Sasa, nikakumbuka mfumo wao wa uongozi wa Ethiopia wa kutumia majimbo, na kukumbuka jinsi baadhi ya watanzania huwa wanausema mfumo wetu wa mikoa ambao mkuu wa mkoa anateuliwa na rais hivyo kufanya serikali kuu kuwa na mkono wa moja kwa moja kwenye kuongoza mkoa, ambapo ni tofauti na mfumo wa majimbo ambapo kiongozi wa mkoa anapigiwa kura

Ubaya wa majimbo ni kuwa viongozi hao wa majimbo wana kuwa na mamlaka makubwa hata yanawajaa vichwani mara nyingine na kuwa fanya kutaka kuwa juu ya serikali ya kitaifa

Mfano serikali ya jimbo la tigrinya ambalo viongozi wake ndio vinara wa kisapoti waasi wapiganao dhidi ya serikali kuu. Mbaya zaidi mfumo huo wa majimbo unatoa mamlaka ya majimbo kuunda majeshi yao, ndio yanaibuka hayo ya makundi ya kiti gray, ambayo kiukweli ni jeshi la ndani la jimbo la Tigrinya

Kila nikiangalia utulivu wa nchi yetu na jinsi ambavyo serikali ni madhubuti, hivi, hata siuoni mwanya wa mkoa fulani kutuletea vurugu za kujitenga ama kuanzisha mapigano ndivyo ninazidi kuu appreciate mfumo wetu wa mikoa tulio nao

Watanzania badala ya kutumia muda mwingi kuponda mifumo yetu ya kisiasa nashauri tuanze kuisifia, maana ni mifumo inayotuletea amani na umadhubuti wa hali ya juu wa taifa na serikali kuu yake.

Viongozi waasisi wa taifa letu walikuwa na ujiniasi wa kipekee kabisa maana taifa hili walilolisuka baada ya kulipokea toka kwa wakoloni wamelisuka vizuri sana, ulimbukeni wa kukaa na kuona mifumo ya siasa ya wezetu ni bora zaidi ya kwetu tukiuendekeza utafanya siku moja tufumuefumue taifa hili lililosukwa vyema.
Mabeberu wanataka kurudi na kutawala upya kupitia migogoro yetu kama hiyo ya Ethiopia tayari Marekani wanampango wa kupeleka ASKARI Ethiopia. Next ni Kenya baada ya uchaguzi wa mwaka kesho tutegemee the same problem. Hapa Tanzania tayari sera ya majimbo CHADEMA ndio wanaotaka
 
LIES!

Stop this nonsense
Umetaka takwimu kutoka kwa mtoa hoja.....nimekupatia na uchambuzi wake......

Nilichotegemea unipinge kwa HOJA badala yake umekuja na ARGUMENTUM AD HOMINEM kuwa NINADANGANYA tu duuuh 😳😳😳🤣🤣

Nisalimie Marekani huko......
 
Yaani tusitoe mawazo yetu ya kujenga nchi kwa kuogopa kuwa tutaitwa tunajipendekeza ?!!! Khaaa 😳😳

Mawazo ya ajabu kabisa haya duuuh 😳😳

CCM ina vijana wengi....yaani wote wateuliwe ilihali uteuzi si tu kwa ajili ya vijana ?!!

Hapa tunajadili mapungufu ya Sera za MAJIMBO hususani barani Afrika kwa mustakabali mwema wa taifa letu na kukua kwake zaidi ya hizo nafasi za uteuzi na maslahi ya mtu mmoja mmoja......

Amka wewe......

SIEMPRE JMT
Tayari jiwe lishampata mtu. Chezea shabaha gizani wewe.
 
Back
Top Bottom