Vitalis Msungwite
JF-Expert Member
- May 11, 2014
- 3,269
- 7,771
Kuna mgogoro umemkumba jirani yetu hapa na ulipofikia anahitaji msaada wa kisheria. Huyu mama ana mtoto wa miaka 6 na Mme wake alifariki mwaka 2016. Marehemu aliacha watoto 5 na wake wawili na huyu mama ni mke wa pili. Kwa mke mkubwa Mali zilizoachwa na marehemu ni; nyumba, powertiller , ng'ombe 35, pikipiki, shamba la mahindi hekari 15, shamba la mpunga hekari 16. Kwa mke mdogo aliacha nyumba ambayo haijaisha ukarabati na shamba la mpunga hekari 10, ikumbukwe shamba hili alilitafuta marehemu na mke mdogo.
Wakati wa msiba ndugu walizuia taratibu za kumaliza msiba na kuomba kila mke atunze kile alichoachiwa na marehemu wakati taratibu za milathi na kumaliza msiba ziliposimama. Hapo kwamaana kuwa wataendeleza vile alivyoacha marehemu. Mke mkubwa aliuza ng'ombe 20 ndani ya mwaka mmoja na huku akiendelea kusimamia mashamba. Huku mke mdogo nae akiendelea kulima shamba la mpunga zile hekari 10.
Tarehe 28/08/2018 mtoto mkubwa wa marehemu alifungua shtaka katika baraza la ardhi la kijiji akitaka mama yake mdogo amkabidhi shamba la mpunga. Baraza lilisikiliza maelezo ya pande zote mbili, huku mlalamikaji akidai kuwa mama yake (mke mkubwa) ameishiwa kiuchumi na sasa anachoma mkaa kujinusuru hivyo analihitaji hilo shamba alime ili amuinue. Maamuzi ya baraza la kijiji ni kuwa maamuzi ya kikao cha mwisho cha familia yafuatwe kwamaana kuwa kila mmoja asimamie alichoachiwa mpaka milathi itakapo toka.
Leo tar 18/09/2018 amemfikisha mama yake mdogo katika baraza la ardhi la kata. Baada ya kusomewa shtaka la kuzuia ardhi mke mdogo amekana mashtaka. Baraza limemtaka mlalamikaji kulipa sh 15000/= kama ghalama za kufungulia mashtaka. Pia limewataka kutoa kila mmoja kiasi cha sh 200,000/=(laki mbili) jumla laki NNE kama ghalama za kufika eneo la shamba lililopo umbali wa km 12.
Msaada unahitajika katika mambo yafuatayo.
1: Kesi hii kwa mtazamo wa kisheria ni nani mwenye uhalali wa kulimiliki na kulima kwasasa?
2: Je ghalama hizi ni sahihi au kuna dalili za utapeli?
3: Maamuzi ya ndugu wakati wa kumaliza msiba yataweza kutengua hukumu itakayotolewa baada ya kesi hii?.
4:Mama huyu afanyeje amilikishwe eneo yeye?
Wakati wa msiba ndugu walizuia taratibu za kumaliza msiba na kuomba kila mke atunze kile alichoachiwa na marehemu wakati taratibu za milathi na kumaliza msiba ziliposimama. Hapo kwamaana kuwa wataendeleza vile alivyoacha marehemu. Mke mkubwa aliuza ng'ombe 20 ndani ya mwaka mmoja na huku akiendelea kusimamia mashamba. Huku mke mdogo nae akiendelea kulima shamba la mpunga zile hekari 10.
Tarehe 28/08/2018 mtoto mkubwa wa marehemu alifungua shtaka katika baraza la ardhi la kijiji akitaka mama yake mdogo amkabidhi shamba la mpunga. Baraza lilisikiliza maelezo ya pande zote mbili, huku mlalamikaji akidai kuwa mama yake (mke mkubwa) ameishiwa kiuchumi na sasa anachoma mkaa kujinusuru hivyo analihitaji hilo shamba alime ili amuinue. Maamuzi ya baraza la kijiji ni kuwa maamuzi ya kikao cha mwisho cha familia yafuatwe kwamaana kuwa kila mmoja asimamie alichoachiwa mpaka milathi itakapo toka.
Leo tar 18/09/2018 amemfikisha mama yake mdogo katika baraza la ardhi la kata. Baada ya kusomewa shtaka la kuzuia ardhi mke mdogo amekana mashtaka. Baraza limemtaka mlalamikaji kulipa sh 15000/= kama ghalama za kufungulia mashtaka. Pia limewataka kutoa kila mmoja kiasi cha sh 200,000/=(laki mbili) jumla laki NNE kama ghalama za kufika eneo la shamba lililopo umbali wa km 12.
Msaada unahitajika katika mambo yafuatayo.
1: Kesi hii kwa mtazamo wa kisheria ni nani mwenye uhalali wa kulimiliki na kulima kwasasa?
2: Je ghalama hizi ni sahihi au kuna dalili za utapeli?
3: Maamuzi ya ndugu wakati wa kumaliza msiba yataweza kutengua hukumu itakayotolewa baada ya kesi hii?.
4:Mama huyu afanyeje amilikishwe eneo yeye?