Kuondoka kwa Samson Mwigamba katika nafasi ya ukatibu mkuu kuna maana kubwa sana. Hawa ni wale ambao Zitto aliwadanganya kwamba wabunge wengi wa upinzani na CCM wangemfuata baada ya kuanzisha chama chake, aliwaaminisha kwamba Chadema ingekufa baada ya yeye kuondoka hivyo wakamuamini na wakamfuata. Bahati mbaya sana mambo yakawa tofauti, nafasi ya katibu mkuu ikageuka kuwa ya kujitolea pasipo malipo yoyote, uzalendo umemshinda Mwigamba wa kuishi kwa kusubiri hisani ya Zitto huku familia inamtegemea.
Wapi alipo Habib Mchange leo hii kisiasa? Asingedanganywa na Zitto huenda leo ndio angekuwa mbunge kibaha mjini. Lakini leo anatembelea ubavuni mwanaidi CCM apate hisani ya uteuzi bahati Mbaya Zitto alisababisha asimalize hata shule. Yuko wapi Philipo Mwakibinga ambaye alikuwa na ushawishi kiasi cha chama kikajitolea kumsaidia akaja kurubuniwa na Zitto. Yuko wapi Grayson Nyakarungu kijana aliyevuma na washa taa mchana? Yuko wapi Moses Machali? Yuko wapi Mtella Mwampamba? Kitilla Mkumbo huenda leo angekuwa mbunge wa Iramba, lakini na uprofessa wake alirubuniwa akaingia mkenge sasa hivi kazi za chama anafanyia mtandaoni tu huku akiendelea na kazi nyingine za kitaaluma. Poleni sana wote ambao mlihadaika mkauuza utu wenu sababu ya kuwa wafuasi wa Yudah.