Mfumo wa TCU ni kikwazo

WAKU-GOOGLE

JF-Expert Member
Jan 20, 2015
950
623
Wakuu kabla ya mfumo huu wa TCU wanafunzi waliohitaji kujiunga na vyuo mbalimbali walichukua form za chuo husika na kutuma maombi ya kozi ambazo walihitaji kusomea na hii iliongeza chance ya mtu kusomea kozi inayoendana na malengo yake au dreams zake, lakini kwa sasa kwa kupitia TCU mtu atahitaji kuomba kozi nyingi ( mfano mwanzo ilikuwa kozi 12 ila sasa ni 5 ) ambazo kiuhalisia mtu hawezi kuwa na machaguo mengi kiasi hicho wengi wanakuwa na kozi labda mbili wanazozipenda lakini kwa sababu watahitajika kujaza nafasi nyingi na kati ya hizo nyingi wanakuwa wamejaza ili zijaze nafasi zote 12 au 5 kwa sasa ambazo wanatakiwa kujaza.

Wanapochaguliwa kwenda vyuoni ndo kasheshe inaanzia hapo kwani wengi huenda kusomea kozi wasizozipenda na hivyo mtu kutofikia malengo yake ya maisha kama alivyotarajia.

Pia sekretarieti ya ajira sidhani kama inaumuhimu kwani mwanzo wahitimu wa vyuo waliomba katika halmashauri na hii ilipelekea watu wengi kuajiriwa kwa sababu kila halmashauri inakuwa inajua mahitaji yake ya wafanyakazi hivyo kuajiri kila anapohitajika mfanyakazi..... lakini kwa sekretarieti ya ajira ambayo inasimamia ajira zote TZ hali sivyo kwani nafasi zinazotangazwa huwa hazikizi mahitaji ya wafanyakazi katika sekta mbalimbali nchini.. hebu fikiria sekretarieti inaweza ikatoa tangazo moja la kazi na ikapita wiki nzima bila tangazo lolote lingine la kazi kutangazwa hivi ni kweli Tanzania nzima sekta zote zilizopo, mikoa yote iliyopo kweli wiki itapita bila wafanyakazi kuhitajika?

Mi naona ilitakiwa shughuli hizi ziwe-Decentralized kama ilivyokuwa mwazo badala ya kufanyika centralization inayoendelea hapa Nchini.

Kwa swala la kuomba nafasi vyuoni lingekuwa kama ilivyokuwa mwanzo mwanafunzi anaenda chuo husika kilicho na kozi anayoipenda yenye ndoto zake na mwisho wa siku atafikia malengo yake na si hii bahati nasibu ya TCU unaweza pelekwa kozi ambayo hujawahi wazia.

Nawasilisha mawazo yangu wakuu.
 
Be Specific, naona kama umechanganya mafaili. Mara TCU, Mara ajira. Tujadili nini hapa at a time?
 
Mimi nilichagua course mbili tu ila vyuo vyuo vitano nazote nina malengo nazo.... Sasa uyo kijana wa form six atakayechaguliwa coz asiyokua na malengo nayo....kunaweza kukawa nasababu mbili apo moja ni mbulula yani ana maksi za namba za viatu afu anataka kusoma petroleum udsm, mbili ni mbulula+ kwenye selection zake unakuta ameeka 1.law 2.bcom 3.sociology 4.transport and logistic management 5.ba in english....... Sasa umbulula kama huu kama malengo yake ni law kwani asingeiweka io law udom, udsm, mzumbe, mmu na ushirika ? Kwamba akikosa chuo hichi apate huku malengo yake yawe palepale? Akichaguliwa ba in english atawalilia tcu au? BIG UP KWA TCU.... WABUNGE WALIZOEA KUPELEKA BARUA ZA WATOTO WAO UDSM.....SIKU IZI HOLLA MTAWAPELEKA VYUO VYA UCHOCHORONI ABROAD
 
Yan Tz kla cku inazdi kuharb ikfikiri inajenga TCU haimlengi m2 ktk malengo apart from bht nasib 4real haifai.
 
Yan Tz kla cku inazdi kuharb ikfikiri inajenga TCU haimlengi m2 ktk malengo apart from bht nasib 4real haifai.
TCU imesaidia sana zaman mtu mmoja alkua anachaguliwa ata vyuo vnne na kuzuia chance za wengne option zwe ata 3 wewe mleta mada unataka option kum haupo sriaz
 
TCU imesaidia sana!!! awali wanafunzi walikuwa hawajui vyuo zaidi ya udsm.mzumbe.sua. then imepunguza gharama awali fomu ilikuwa tsh 30000 utaomba vyuo kumi kwa sh 300000. then TCU wamefanya makabila kuchangamana. leo utatoka moshi unaenda iringa...RUCO. aliyeko songea anaenda mwanza....SAUTI. ishu ya kuchagua course yakupasa kuwa makini!!!! ilo la secretariate ya ajira sina jibu. ila naomba serekali iwe makini kwa ilo.
 
Back
Top Bottom