Mfumo gani bora wa utawala unaifaa dunia?

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,161
10,877
Wakati duniani kote kuna harakati kubwa za maandamano ya wananchi wanaotaka mabadiliko ya utawala kwa nchi zao.Harakati hizi zinakwenda sambamba na mauwaji makubwa ya waandamanaji kutoka kwa watawala.Wapo ambao baada ya hasara wanazozipata wanafanikiwa kupata wanachokitaka.

Wale ambao hawajafanikiwa kuleta mabadiliko mara nyingi huwa ni sababu ya ukatili mkubwa wa walio madarakani ambao wengi wakishakukalia kiti huwa hawapendi kuondoshwa.

Baadhi ya madai ya waandamanji huwa ni ya msingi na muhimu kusikilizwa kwa namna fulani ikiwemo kujiuzulu kwa watawala.Hata hivyo mengi ya madai ya waandamanaji hao hayana msingi na ni fikra za kisehetani tu kuivuruga dunia.

Hali mojawapo ya kutoridhika kwa wananchi juu ya mifumo inayowatala ni kutokana na kukosa mahitajio muhimu ya kimaisha ikiwemo ya matumizi ya kila siku na hata amani. Wengine huwa wanaandamana kutaka makubwa zaidi ikiwemo uhuru uliopitiliza.

Tukiangalia mifumo ya kiutawala inayoongoza dunia kwa sasa ni mfumo wa kidemokrasia na ule wa ufalme.Tukichukulia kwamba mifumo yote miwili hiyo haijakuwa sababu ya dunia kupata utulivu na kwamba kila mmoja ya mifumo hiyo kwa mifano mbali mbali ina kasoro na ni kweli imekuwa sababu ya matatizo dunia inayoshuhudia kila uchao.

Kwa kuzingatia yale yanayotokea Iran,Marekani,Uiengereza,Tunisia,Sudan.Na yale yanayoendelea Venezuela,Colombia,Chile na kwengineko. Je, upo uwezekano wa kuleta mabadiliko kwenye mifumo hiyo ili kuifanya hali ya dunia iwe shwari ?,na kama haiwezekani.Jee kuna mfumo mwengine wowote utakaofaa kuitawala dunia?.
 
Siku kila mmoja akapata matakwa yake na kuridhika nayo basi dunia haitakuwa tena mahala salama pakuishi. hiyo ni kanuni ya asili
 
Siku kila mmoja akapata matakwa yake na kuridhika nayo basi dunia haitakuwa tena mahala salama pakuishi. hiyo ni kanuni ya asili
Hiyo siku unakisia ni lini wakati kila uchao hali ndiyo inazidi kuharibika.
 
Wakati duniani kote kuna harakati kubwa za maandamano ya wananchi wanaotaka mabadiliko ya utawala kwa nchi zao.Harakati hizi zinakwenda sambamba na mauwaji makubwa ya waandamanaji kutoka kwa watawala.Wapo ambao baada ya hasara wanazozipata wanafanikiwa kupata wanachokitaka.

Wale ambao hawajafanikiwa kuleta mabadiliko mara nyingi huwa ni sababu ya ukatili mkubwa wa walio madarakani ambao wengi wakishakukalia kiti huwa hawapendi kuondoshwa.

Baadhi ya madai ya waandamanji huwa ni ya msingi na muhimu kusikilizwa kwa namna fulani ikiwemo kujiuzulu kwa watawala.Hata hivyo mengi ya madai ya waandamanaji hao hayana msingi na ni fikra za kisehetani tu kuivuruga dunia.

Hali mojawapo ya kutoridhika kwa wananchi juu ya mifumo inayowatala ni kutokana na kukosa mahitajio muhimu ya kimaisha ikiwemo ya matumizi ya kila siku na hata amani. Wengine huwa wanaandamana kutaka makubwa zaidi ikiwemo uhuru uliopitiliza.

Tukiangalia mifumo ya kiutawala inayoongoza dunia kwa sasa ni mfumo wa kidemokrasia na ule wa ufalme.Tukichukulia kwamba mifumo yote miwili hiyo haijakuwa sababu ya dunia kupata utulivu na kwamba kila mmoja ya mifumo hiyo kwa mifano mbali mbali ina kasoro na ni kweli imekuwa sababu ya matatizo dunia inayoshuhudia kila uchao.

Kwa kuzingatia yale yanayotokea Iran,Marekani,Uiengereza,Tunisia,Sudan.Na yale yanayoendelea Venezuela,Colombia,Chile na kwengineko. Je, upo uwezekano wa kuleta mabadiliko kwenye mifumo hiyo ili kuifanya hali ya dunia iwe shwari ?,na kama haiwezekani.Jee kuna mfumo mwengine wowote utakaofaa kuitawala dunia?.
Mimi naona mfumo wa uchifu utakuwa bora zaidi.
 
Mfumo utakao tawala dunia Kwa haki waja, ni pale science itakapo decode Siri ya Mungu wakati anaumba mwanadamu na ulimwengu alikusudia tuhusiane namna gani?!, si mda mrefu haya yatatimia.
Technolojia imefikia hatua kubwa Sana na kuifanya Demokrasia kua outdated kwani msingi mkubwa wa Demokrasia ni udanganyifu na propaganda, hivo hivo na ufalme

Hata hivo dunia ijayo Uongo utakua hauwezekani, kila kitu kitakua bayana na tutatambua Akili kubwa ya muumba ilikusudia nini wakati wa uumbaji.
* String theory inamashiko Sana Kwa sasa. Nadhani wana fizikia mtakua mnanielewa zaidi.

Dunia ijayo itatawaliwa na fact, scientific facts.
Physicist watakua ndio walimu, wahubiri, Kwa maana ya dini zote zitakua replaced na science fact
Wanasheria, wa natural law watakua regulators.
Dini ,democrasia,ufalme nk vitabaki historia

NB. Kwakipindi cha miaka 70 sasa dunia ilitulia kutokana na mfumo wa Demokrasia, hivo mfumo huu unaheshimika Kwa kulinda mstakabali mzima wa ubinadamu duniani.
 
Mfumo unaofaa ni ule ambao rais wa wanyonge anatatua kero za watu wake, baada ya maisha ya watu kuboreka wakivimbiwa sasa watakua na ruksa ya kuomba hayo ya demokrasia na mengine.
 
Back
Top Bottom