Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Mfanyabiashara maarufu jijini Arusha,Philemon Mollel (Monaban)amelalamikia hatua ya baadhi ya Mali zake zilizoko katika Kiwanda cha kusagisha nafaka cha NMC kuanza kuhujumiwa na kuuzwa mitaani kinyume na utaratibu.
Mollel ametoa kilio hicho wakati akiongea na waandishi wa habari Mara baada ya kukamata mifuko ya vifungashio zaidi ya 1,000,000 aliyokua ameagiza kutoka ndani na nje ya nchi na mingine aliyozalisha katika kiwanda hicho kabla ya Serikali kumpokonya ikiwa inauzwa mtaani na wafanyabiashara wadogo.
Pia Mollel ameingiwa na wasiwasi kuhusiana na Mali zakr zingine alizoacha kiwandani hapo yakiwemo Mahindi,Mtama ,Ngano na Vipuri na spare za Machine ambazo zipo ndani ya kiwanda hicho wakati akisubiri shauri la maridhiano baina yake na Bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko lililopo mahakamani.
"Nimesikitishwa kuona Mali zangu zikihujumiwa na sielewi Nani anahusika kuzitoa kiwandani hapo huu ni uonevu mkubwa na unania mbaya ya kunidhoofisha kibiashara" amesema Mollel
Amesema kuwa hatua hiyo ilimlazimu kuingia mtaani kufanya msako kwenye masoko akiwa na askari polisi na kufanikiwa kuwakamata vijana wapatao 13 wanayoisambaza mtaani wakiwemo wauza chipsi wanaoitumia kufungashia chips wateja wao.
Mfanyabiashara huyo amesema kuwa Mara baada ya serikali kumpokonya Kiwanda hicho na kuikabidhi Bodi ya Nafaka na mazao mchanganyiko aliacha Mali nyingi alizokuwa amezalisha ambazo kimsingi hazihusiani na mgogoro wake na Bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko,lakini ameshangaa kuona Mali hizo zikizagaa mtaani.
Amesema shauri la mgogoro huo bado lipo mahakamani na wanasubiri uamuzi wa Mahakama kuhusu mkataba wake was uoangaji katika kiwanda hicho pamoja na Mali zake lakini ameshangazwa kuona Mali hizo zikiuzwa na wamachinga mtaani.
"Nasikitika kuona Mali zangu zikihujumiwa wakati jambo hili bado lipo mahakamani ,naiomba Serikali isaidie Mali zangu zisije zikapotea " Amesema Mollel.
Molel ameiomba Serikali kupitia Vyombo Vya dola kuchunguza kwa makini jambo hilo na kuwachukulia hatua waliohusika kutoa Mali hizo kiwandani na kuziuza nje kinyume na utaratibu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ,Jonathan Shana amesema jambo hilo lipo katika hatua za uchunguzi ili kubaini wahusika halisi wa tukio hilo.
Na pindi upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.
Ends...
Sent using Jamii Forums mobile app
Mollel ametoa kilio hicho wakati akiongea na waandishi wa habari Mara baada ya kukamata mifuko ya vifungashio zaidi ya 1,000,000 aliyokua ameagiza kutoka ndani na nje ya nchi na mingine aliyozalisha katika kiwanda hicho kabla ya Serikali kumpokonya ikiwa inauzwa mtaani na wafanyabiashara wadogo.
Pia Mollel ameingiwa na wasiwasi kuhusiana na Mali zakr zingine alizoacha kiwandani hapo yakiwemo Mahindi,Mtama ,Ngano na Vipuri na spare za Machine ambazo zipo ndani ya kiwanda hicho wakati akisubiri shauri la maridhiano baina yake na Bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko lililopo mahakamani.
"Nimesikitishwa kuona Mali zangu zikihujumiwa na sielewi Nani anahusika kuzitoa kiwandani hapo huu ni uonevu mkubwa na unania mbaya ya kunidhoofisha kibiashara" amesema Mollel
Amesema kuwa hatua hiyo ilimlazimu kuingia mtaani kufanya msako kwenye masoko akiwa na askari polisi na kufanikiwa kuwakamata vijana wapatao 13 wanayoisambaza mtaani wakiwemo wauza chipsi wanaoitumia kufungashia chips wateja wao.
Mfanyabiashara huyo amesema kuwa Mara baada ya serikali kumpokonya Kiwanda hicho na kuikabidhi Bodi ya Nafaka na mazao mchanganyiko aliacha Mali nyingi alizokuwa amezalisha ambazo kimsingi hazihusiani na mgogoro wake na Bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko,lakini ameshangaa kuona Mali hizo zikizagaa mtaani.
Amesema shauri la mgogoro huo bado lipo mahakamani na wanasubiri uamuzi wa Mahakama kuhusu mkataba wake was uoangaji katika kiwanda hicho pamoja na Mali zake lakini ameshangazwa kuona Mali hizo zikiuzwa na wamachinga mtaani.
"Nasikitika kuona Mali zangu zikihujumiwa wakati jambo hili bado lipo mahakamani ,naiomba Serikali isaidie Mali zangu zisije zikapotea " Amesema Mollel.
Molel ameiomba Serikali kupitia Vyombo Vya dola kuchunguza kwa makini jambo hilo na kuwachukulia hatua waliohusika kutoa Mali hizo kiwandani na kuziuza nje kinyume na utaratibu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ,Jonathan Shana amesema jambo hilo lipo katika hatua za uchunguzi ili kubaini wahusika halisi wa tukio hilo.
Na pindi upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.
Ends...
Sent using Jamii Forums mobile app