DOKEZO Mfanyabiashara maarufu Arusha aibiwa Tsh. Milioni 100 kwenye akaunti ya Benki ya NMB

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Watu wana pesa sana wenyeji wa masasi mjini watakuwa wanamfahamu marehemu Chidi boy huyu mwamba alikuwa na pesa ndefu sana wakati kama huu wa mbaazi wengi walikuwa wanaenda kwake anakupa mpaka milion 50 unaenda kukomaa nayo shambani ukishapata mzigo wa mbaazi ni hiyari yako umuuzie yeye chidi au usafirishe upeleke dar pale biasi na hata ukikataa kumuuzia yeye chidi wala hana noma
NDIO MAANA WAKAMUUA CHID BOY
WATU WABAYA SANA
 
Benki za kibongo siziamini.

Mimi mwenyewe kuna rafiki yangu mpaka sasa anakimbizana na watu wa benki moja kubwa Bingo iliyopata tuzo hivi karibuni, kuna kama milioni 250 zake hazijulikani zilipo.

Maafisa wa usalama wa benki badala ya kuona aibu na kufanya kazi kuzirudisha, wanafanya uchunguzi mwezi wa 6 huu.

By comparison, more than 10 years ago, mimi nilishawahi kuibiwa $4,000 Citibank. Kuna jamaa walipata details zangu wakachonga kadi, wakatoa hela Dubai.

Citibank walikuwa so embarassed, niliwapigia simu Alhamisi, Jumatatu hela zikawa zimerudi tayari.

Walichofanya ni kuniuliza tu kuhakiki kama nimempa mtu kadi yangu na pin number. Nikasema sijampa. Wakaniuliza kama nimetoka nje ya Marekani wakati huo, nikasema sijatoka. Wakaangalia wenyewe wakaona mchezo umechezwa Dubai. Halafu wakajua kuwa kuna genge fulani linacheza ule mchezo. Wakanirudishia hela zangu mara moja.

Mpaka leo huniambii kitu kuhusu Citibank na Customer Service yao kwenye haya mambo ya kurudisha hela zinazoibiwa.

Bongo unaibiwa wewe halafu benki bado inakuzungusha haiogopi hata bad publicity!
...... $4,000 Citibank...... Dubai (Kama HushPuppi !!!)
 
Zinatosha kuanzisha ka mtaji
Unajua maana ya kuchomoa kidogo kidogo?. Hana hata 10. Ilikuwa achukue zote kwa pamoja ndio ungekuwa mtaji. Wezi wengi wa hivyo nawaona wajinga tu ksbb mwisho wa siku wanakuwa hawana hata 100. Ksbb ilikuwa akichomia milioni 5 anasikilizia siku kadhaa then anaanza kuipiga. Ikiisha anarudi kwenye kihenge.
 
Ndiyo maana mimi naamini wasimamizi wa mirathi hupewa taarifa za uongo na benki kuhusu pesa walizoacha marehemu hasa wale wa fixed.
Ni kweli. Kuna kesi nyingi za warithi kudhulumiwa na kudanganywa kuhusu kiasi cha fedha kilichokuwa kwenye account ya marehemu.

Binafsi mzee wangu alikuwa anafanya shughuli zake na alikuwa anaweka fedha benki pia Alikuwa mstaafu so alikuwa analipwa Pension yake via NMB. Mwaka ambao mzee alifariki, alivuna mpunga na akauza gunia zaidi ya 500 ambazo alipeleka benki. Baada ya kufariki na tulikaa muda mrefu kupata utaratibu wa mirathi kwenda benki tunaambiwa mzee alikuwa na laki saba tu benki.
 
Inakuwaje pesa zichomolewe asipewe taarifa kwa ujumbe mfupi? Au huyo jamaa alifanya yake zikitolewa asipate taarifa?
Wanachofanya anagushi sahihi yako kisha kila kitu kinaendelea kwa kughushi tu kuanzia kuomba kadi na kuendelea. Naku-mention kwenye uzi mmoja ambao mfanyakazi wa CRDB ubungo aliiba pesa za mteja zaidi ya milioni 100 kwa mtindo huu mwaka 2019.
 
Ni kweli. Kuna kesi nyingi za warithi kudhulumiwa na kudanganywa kuhusu kiasi cha fedha kilichokuwa kwenye account ya marehemu.

Binafsi mzee wangu alikuwa anafanya shughuli zake na alikuwa anaweka fedha benki pia Alikuwa mstaafu so alikuwa analipwa Pension yake via NMB. Mwaka ambao mzee alifariki, alivuna mpunga na akauza gunia zaidi ya 500 ambazo alipeleka benki. Baada ya kufariki na tulikaa muda mrefu kupata utaratibu wa mirathi kwenda benki tunaambiwa mzee alikuwa na laki saba tu benki.
Pia mnahakika kuwa aliweka hiyo hela bank? Maana wazee nao huwa wanamafekeche yao.

Kuna dogo mwaka wa tano huu anafuatilia nyumba pale PPF mwanza Baba yao alinunua. Wamecheck database ya PPF jina halipo, kuja gundua kumbe aliandika jina la bimdogo.
 
Kuchomoa hela kwenye akaunti ya mtu halafu jinai hiyo inafanywa na mtumishi wa bank ni wazi NMB si sehemu salama kuweka akiba
Mtanzania haaminiki kwenye mambo ya fedha. Narudia tena: mtanzania haaminiki kwenye mambo ya fedha. Najua duniani kote binadamu kwenye fedha ni kitu kingine lakini kwa Tanzania ni zaidi. Benki nyingi tu (labda ondoa zile za kimataifa) wafanyakazi wake hawaaminiki. Bongo ukiwa na fedha benki inatakiwa kila uchwao uwe unaangalia balance. Na wakati wa kutoa kama unatoa fedha nyingi uwe makini sana kwani unaweza kuwekewa majambazi.
 
Back
Top Bottom