Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Jeshi la Polisi Mkoani Arusha linamshikilia Afisa Mikopo wa Benki ya NMB Tawi la Clock Tower Jijini Arusha , Geroge Kifaruka kwa tuhuma za kumweka uyumba na kumlawiti mwanafunzi wa kiume wa shule ya sekondari aliyekuwa na umri wa chini ya miaka kumi na nane kwa zaidi ya miaka miwili kwa kile alichodai malipo ya kumsomesha shule.
Kwa mujibu wa vyanzo vya habari ndani ya jeshi la polisi Arusha vilisema kuwa Kifaruka alikamatwa julai 12 mwaka huu baada taarifa fiche kutoka kwa Mwalimu wa Sekondari ya shule ya Sinoni iliyopo Jijini Arusha kutoa kwa Polisi Arusha na mtuhumiwa kukamatwa.
Kamanda wa polisi Mkoani Arusha,Kamishina Msaidizi wa Jeshi la polisi Nchini Justin Masejo alipoulizwa juu ya tukio hilo alisema kuwa mezani kwake taarifa hiyo haijamfikia ila akiipata ataitolea taarifa.
‘’Kwa sasa tukio hilo haliko mezani kwangu ila ikija ntakupa taarifa zima tufanye subira’’ alisema Kamanda Msejo
Taarifa kutoka ndani ya Jeshi la Polisi Arusha na benki ya NMB zinadai kuwa tukio la Kifaruka linafanywa kuwa siri kubwa huku kaka yake na mtuhumiwa ambaye ni askari wa jeshi la wananchi JWTZ(jina linahifadhiwa)kwa kushirikiana na afisa mikopo mwenzake aliyefahamika kwa jina moja la Devi walikuwa wakihaha kutafuta fedha ili kumaliza tukio hilo polisi na idara ya ustawi wa jamii ambao wamelivalia njuga.
"Hadi juzi asubuhi alikuwa bado yuko rumande na kwamba jitihada za ziada zinafanyika kuzima tukio hilo kati ya polisi na Maofisa wakubwa wa benki hiyo Jijini Arusha"kilisema chanzo ndani ya jeshi la polisi
Mtoa taarifa ndani ya jeshi hilo ambaye anadai kuumizwa na kitendo cha mwanafunzi huyo ambaye anatembea akiwa amevaa pampasi baada ya kuharibiwa vibaya alisema haridhishwi na namna jambo hilo linavyoendeshwa kituoni hapo ikiwemo jalada la tukio kuitishwa Mkoani kinyume na utaratibu kwani majalada mengine huchunguzwa na askari wa wilayani
Alisema hatua hiyo inatia shaka haki kutotendeka na kuwaomba waandishi wa habari pamoja na jamii zinazopinga ukatili kuingilia kati ili kukomesha matukio ya aina hiyo ambayo yanazidi kukithiri huku hatua kali zikiwa bado hazijachukuliwa ipasavyo.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya Polisi vinasema kuwa tayari mwanafunzi huyo ameshapimwa na daktarin wa Hospital ya Mount Meru na baadhi ya walimu walioona mwenendo usioridhisha wa mwanafunzi huyo wameshatoa maelezo polisi lakini jalada halijaenda kwa Mwanasheria Mkuu wa serikali kwa ajili ya kufunguliwa mashitaka.
Habari kutoka shuleni Sinoni kwa Mwanafunzi huyo zilisema kuwa wale waliotoa taarifa wameliachia kazi Jeshi la Polisi Arusha kufanya kazi yake na ikiwa vinginevyo wataandamana kwa waziri anayehusika.
Meneja wa banking ya NMB tawi la Clock Tower, aliyejitaja kwa jina moja la Bahati alikiri kuwa George kifaruka ni mfanyakazi wa benki hiyo na taarifa za tukio hilo amefanya kuzisikia ila kwa kuwa alikuwa amesafiri atafuatilia.
Baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wamedai kitendo kilichofanywa na mfanyakazi mwenzao George na kulifanya tukio hilo siri hakikubaliki na kinaitia aibu Benki hiyo kubwa nchini na kuomba sheria kuchukua mkondo wake.
Kwa mujibu wa vyanzo vya habari ndani ya jeshi la polisi Arusha vilisema kuwa Kifaruka alikamatwa julai 12 mwaka huu baada taarifa fiche kutoka kwa Mwalimu wa Sekondari ya shule ya Sinoni iliyopo Jijini Arusha kutoa kwa Polisi Arusha na mtuhumiwa kukamatwa.
Kamanda wa polisi Mkoani Arusha,Kamishina Msaidizi wa Jeshi la polisi Nchini Justin Masejo alipoulizwa juu ya tukio hilo alisema kuwa mezani kwake taarifa hiyo haijamfikia ila akiipata ataitolea taarifa.
‘’Kwa sasa tukio hilo haliko mezani kwangu ila ikija ntakupa taarifa zima tufanye subira’’ alisema Kamanda Msejo
Taarifa kutoka ndani ya Jeshi la Polisi Arusha na benki ya NMB zinadai kuwa tukio la Kifaruka linafanywa kuwa siri kubwa huku kaka yake na mtuhumiwa ambaye ni askari wa jeshi la wananchi JWTZ(jina linahifadhiwa)kwa kushirikiana na afisa mikopo mwenzake aliyefahamika kwa jina moja la Devi walikuwa wakihaha kutafuta fedha ili kumaliza tukio hilo polisi na idara ya ustawi wa jamii ambao wamelivalia njuga.
"Hadi juzi asubuhi alikuwa bado yuko rumande na kwamba jitihada za ziada zinafanyika kuzima tukio hilo kati ya polisi na Maofisa wakubwa wa benki hiyo Jijini Arusha"kilisema chanzo ndani ya jeshi la polisi
Mtoa taarifa ndani ya jeshi hilo ambaye anadai kuumizwa na kitendo cha mwanafunzi huyo ambaye anatembea akiwa amevaa pampasi baada ya kuharibiwa vibaya alisema haridhishwi na namna jambo hilo linavyoendeshwa kituoni hapo ikiwemo jalada la tukio kuitishwa Mkoani kinyume na utaratibu kwani majalada mengine huchunguzwa na askari wa wilayani
Alisema hatua hiyo inatia shaka haki kutotendeka na kuwaomba waandishi wa habari pamoja na jamii zinazopinga ukatili kuingilia kati ili kukomesha matukio ya aina hiyo ambayo yanazidi kukithiri huku hatua kali zikiwa bado hazijachukuliwa ipasavyo.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya Polisi vinasema kuwa tayari mwanafunzi huyo ameshapimwa na daktarin wa Hospital ya Mount Meru na baadhi ya walimu walioona mwenendo usioridhisha wa mwanafunzi huyo wameshatoa maelezo polisi lakini jalada halijaenda kwa Mwanasheria Mkuu wa serikali kwa ajili ya kufunguliwa mashitaka.
Habari kutoka shuleni Sinoni kwa Mwanafunzi huyo zilisema kuwa wale waliotoa taarifa wameliachia kazi Jeshi la Polisi Arusha kufanya kazi yake na ikiwa vinginevyo wataandamana kwa waziri anayehusika.
Meneja wa banking ya NMB tawi la Clock Tower, aliyejitaja kwa jina moja la Bahati alikiri kuwa George kifaruka ni mfanyakazi wa benki hiyo na taarifa za tukio hilo amefanya kuzisikia ila kwa kuwa alikuwa amesafiri atafuatilia.
Baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wamedai kitendo kilichofanywa na mfanyakazi mwenzao George na kulifanya tukio hilo siri hakikubaliki na kinaitia aibu Benki hiyo kubwa nchini na kuomba sheria kuchukua mkondo wake.