Mfahamu the Green Mamba

Mfahamu the Green Mamba

Huwa tunaambiwa sumu yake haina dawa. Kama ndiye basi tumekuwa tunamwonea sana huyu nyoka.

Sumu ina dawa ila muda wa kupata matibabu ndo shida, maana dk 24-48 uwe umefika hospitali tena yenye dawa, ndo msala ulipo.Ila ni nyoka wapole sana wao mda mwingi humkimbia binadamu, na wawapo juu ya mti ukiwa chini na hasa kama una radio inapiga mziki ndo kwaanza haondoki na mwisho akichoka anadondoka na kusepa, ujue nyoka hupanda juu ya mti ila hashuki bali hujiachia na kudondoka. Hawa nyoka green mamba kwa kusema ukweli ni waoga sana mi niliwahi kumshika mkia nikiwa namwagilia ukoka kwenye maua, aliteleza na kukimbia, mikoa mingi iliyolima kahawa walikufa sana baada ya sumu kumpigwa kwenye mikahawa hasa Diasnon,DDT nk.
 
Kwenye mikorosho noma Sana hasa ukipanda juu kutungua bibo utakutana na huyo kiumbe mzito,
Miaka ya 80 nilikutana naye tabata dampo kwenye mikorosho ya watu ebwanae wacha nijirushe toka juu ya mti na kutoka nduki Kali,
Maumivu nilienda kuyasikilizia home!!!
Ila ni kweli hawa nyoka hawana madhara Hadi wachokozwe
Hivi bibo ni nini?
 
Hivi bibo ni nini?
Ni Tunda linalotokana na mikorosho.
Mkorosho huwa unazaa korosho ambayo inakuwa imeambatana na bibo.
Mabibo yanaliwa kama matunda mengine pia yanatumika kutengenezea wine na gongo
1103177
 
Kabila letu hamuamini kuwa ukipishana huyu nyoka ukiwa unaenda safari. Yan akikatiza mbele ya njia unayopita, safari yako inakuwa ya mafanikio.
Huyu nyoka kwa imani za kwetu haturuhusiwi kumwua. Na sijashuhudia MTU yeyote kagongwa na huyo nyoka. Ni mpole sana. Hana ugomvi tofauti na huyo black mamba/ koboko,aka mzee wa bifu.
 
Green mamba hata siyo hatari kama mtoa mada ambayo anataka kutuamininisha na thread yake , nimecheza nao sana , Ukifika machame nkuu muulizie Riri utaambiwa tabia yake ya kuwafuga hawa viumbe since Akiwa std 2 Mpaka sasa hivi kaachana nao kashakuwa mkubwaaa
Mtoa mada yuko sahihi,pamoja na upole huyo nyoka anasumu kali sana. Ni vile tu hapendi kuuma Mara kwa Mara .hadi pale anapohisi hatari
 
Mkuu green mamba wameniuma mara kibao sijawahi pata effect na pia sijawahi kwenda hosp, nimehangaika nao sana hao wadudu, labda nilikuwa nang'atwa na local green mambas siyo intaneshino
Mtoa mada yuko sahihi,pamoja na upole huyo nyoka anasumu kali sana. Ni vile tu hapendi kuuma Mara kwa Mara .hadi pale anapohisi hatari
 
hawa wadudu hawana shida ila kuna mmoja nilikutana nae maeneo fulan hiv juu.ya matofali.. kila nikirusha jiwe... namkosa.. sas akawa anatafuta ni nani anayemzingua..

akawa anasimama wima.. kila nikirusha jiwe namkosa kosa anazidi kusimama wima... mpaka akabakiza sehem ndogo ya mkia ikawa ndio balance kwake.. akawa ana hang.. kishoto..kulia.. ili atrack adui wake... aisee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom