View attachment 1102622
Huyu mmoja kati ya nyoka hatari sana anayepeatikana mashariki mwa Afrika, ana ufanano wa karibu sana na yule black mamba
Kitaalamu huitwa "'Dedroaspis angusticep"' nyoka huyu huingia katika kundi la wanyama waishio juu ya miti yaani ARBOREAL kwa mara ya kwanza species hii iligunduliwa kwenye miaka ya 1840 hivi na zoologist mmoja aliyeitwa Dr Andrew katika kundi hili la hawa nyoka kuna species ambayo imepotea tayari ambao inasadikiwa ndio walikuwa hatari zaidi,
Sasa hawa huitwa green mamba kutokana na ufanano na wale black mamba "' koboko"' lakini hawa midomo yao ni meupe na meno yaliyojikunja hivi na yako hivi kwa ajili ya kuingizia sumu pale anapokuwa amemshambulia adui yake, jike urefu wake hufikia karibu futi 6.5 hivi na dume hufikia futi 5.7
Kwa kawaida Mungu alivyo wa ajabu pamoja na kuwaweka viumbe hatari mbali na makazi ya binadamu pia nyoka hawa wanaodaiwa kuwa na sumu kali ni wapole kupita kiasi na hushambulia pale wanapochokozwa na kwa viumbe vilivyowazidi ukubwa kama binadamu nyoka hawa hutoa tahadhari zaidi ya mara tatu kabla ya shambulio mfano kuna nyoka hutoa sauti ziitwazo '" sound of death'' mfano wa tairi lenye pancha hivyo ukisikia hivyo kaa mbali kitendo cha kumsogele ni kukiuka amri halali kwa hiyo shambilio lolote hatalaumiwa.
Nyoka huyu huweza kukushambulia kwa haraka hata zaidi ya mara tatu pale anapochokozwa
VIPI KUHUSU SUMU YAKE
Kama ulikuwa hujui huyu ana sumu mbaya na kali kuliko koboko ama black mamba, wakati black mamba akiwa na sumu yenye mchanganyiko wa sumu mbili huyu ni balaa zaidi kwani ana sumu yenye mchanganyiko wa aina NNE.....
Aina ya kwanza ni NEURO TOXIC VENON, pigo moja lenye ujazo wa gramm 90 likiwa na hii sumu linatosha kuathiri mfumo mzima wa neva za kiumbe aliyeshambuliwa sasa aina hii ya sumu pia anayo black mamba kinachowatofautisha na kumfanya green mamba awe tofauti na hatari ni hii sumu ya pili
Aina ya pili huitwa DENDROTOXIN VENON.....hii sasa ndo hatari kwani ndani yake ni mchanganyiko wa sumu aina tatu ambazo ni CALCICLUDINE, CARDIOTOXIN, na FASCICICULIN.....sasa ona balaa lake hapo unadungwa jino moja unakula mchanganyiko wa sumu zote hizo kweli huyu ni hatari jaribu kufikiri kama hiyo CARDIOTOXIN yenyewe ikiingia kwenye damu hukimbilia kuharibu mfumo wa moyo unaweza kukisia ni dakika ngapi zitakutosha kutubu dhambi zako maana kama usipopata matibabu mapema ni dakika 20 hadi 30 zinakutosha kuuona ulimwengu huu kwa mara ya mwisho.
Moja kati ya madhara utakayoyapata baada ya shambulio la nyoka huyu ni kuathiri mapigo ya moyo, kushindwa kupumua, kuvimba mwili mzima, na kupooza dah aisee huyu kiumbe ni hatari ila mpole hahahahah......
Baada ya mating jike hutaga mayai kati 4 hadi 17 na huanguliwa baada ya wiki 12 na kwa kawaida huishi hadi miaka 16
TAHADHARI
Mara unapokutana na nyoka huyu usijaribu kumshambulia maana kama nilivysema hapo awali aina hii ya hawa nyoka wana kasi ya ajabu na yeye akuonapo hujificha hivyo wale wenzangu na mimi wanapoona nyoka hukimbilia silaha kutaka kummaliza angalia usije kumalizwa kuwa mpole relax maana nyoka wana kitu inaitwa SENSE OF HEAT wanajua kama wanataka kushambuliwa maana bianadamu anapoona kitu cha kuopesha hushituka na joto la mwili hupanda kutokana na kuongezeka kwa mapigo ya moyo sasa hapa nyoka huhisi hii kitu ndio maana nyoka huweza kucheza na mtoto kwa sababu anajua hawezi shambuliwa
Tuwapende na tuwalinde wanyama na viumbe vilivyopo ndani ya Dunia yetu maana Mungu aliviweka ili viupendezeshe ulimwengu pia tujifunze kupenda utalii wa ndani Tanzania tuna utajiri wa viumbe na wanyama wakutosha tuwalinde kwa faida ya vizazi vijavyo.