ndio digdig au ?Mnyama Isha
Isha ni mnyama apatikanae kwenye kundi la wanyama jamii ya swala,anapatikana maeneo ya mashariki na kusini barani Afrika hususani hapa nchini.
SIFA NA TABIA ZA ISHA
Isha ni miongoni mwa swala wenye umbo dogo kama walivo kina taya.
Miili yao ina manyoya mafupi yenye rangi ya dhahabu inayoendana na kahawia au wakati mwingine manyoa yao huonekana kuwa na rangi ya wekundu.
Kwa pamoja madume na majike wana matezi yenye rangi nyeuusi ambayo yanaonekana sehemu ya mbele ya macho yao.
Wana kwato ngumu zilizo chongoka ambazo huwasaidia kuchimba vyakula vyenye asili ya mizizi.
Madume pekee ndo huwa na pembe ambazo zimenyooka, ziko sambamba, nyororo na zilizo chongoka. Pembe hizi hurefuka na kufikia urefu wa sentimita 7 hadi 19.
Hupenda kujisaidia kwenye mashimo na kisha kuyafukia mashimo hayo. Hii huwasaidia wanyama hawa wasigundulike kirahisi maeneo waliyopo hasa kutokana na maadui zao.
Wanapohisi kuna adui wanyama hawa hutulia na kujificha lakini adui anapo wakaribia hukimbia na kutafuta maficho mengine hasa kwenye mashimo yaliyo achwa na wanyama kama mhanga.
Dume na jike huishi mbali mbali na hukutana kipindi wanapotaka kuzaliana tu hivyo dume mmoja huwa na jike mmoja tu na eneo lao huwa na ukubwa wa hekari 4 mpaka 100.
Urefu=Isha mkubwa hufikia urefu wa sentimita 70 hadi 95.
Kimo= kimo cha isha hufikia sentimita 45 hadi 60.
Uzito= wanyama hawa huwa na uzito wa kilogramu 7 hadi 16.
Wanapedelea mazingira yenye majani tu na tafiti zinaonesha kuwa wanyama hawa ni kwa nadra sana kuwaona katika maeneo ambayo kwa asilimia kubwa ardhi imetawaliwa na miti.
Isha ni wanyama walao majani kama walivyo wanyama jamii ya swala wengine. Wana uwezo wakula mizizi pia pamoja na vyakula jamii ya vitunguu.
Wanyama hawa hawapendelei kunywa maji mara kwa mara kwani maji mengi huyapata kupitia chakula au aina ya majani wanayo kula mara kwa mara. Hivyo wana uwezo wa kuishi muda mrefu sana bila kunywa maji.
Mara tuu baaada ya kupandana jike na dume husambaratika na jike hukaa na mimba kwa muda wa miezi 5 hadi 6 kisha huzaa mtoto mmoja tu.
kwa kipindi cha wiki chache za mwanzo mama humficha mtoto eneo salama lenye majani dhidi ya maadui. Mama huondoa kinyesi cha mtoto pamoja na kufukia viashiria vyiovyote vile ambavyo vinaweza kuwafanya maadui kugundua mahali alipo mtoto na kumuuwa.
Huishi miaka 7 na huweza ongezeka ikiwa atafugwa.View attachment 1171743View attachment 1171744View attachment 1171745
Hawa mkuu si wanaliwa km swala wengine waliwavyo????Mnyama Isha
Isha ni mnyama apatikanae kwenye kundi la wanyama jamii ya swala,anapatikana maeneo ya mashariki na kusini barani Afrika hususani hapa nchini.
SIFA NA TABIA ZA ISHA
Isha ni miongoni mwa swala wenye umbo dogo kama walivo kina taya.
Miili yao ina manyoya mafupi yenye rangi ya dhahabu inayoendana na kahawia au wakati mwingine manyoa yao huonekana kuwa na rangi ya wekundu.
Kwa pamoja madume na majike wana matezi yenye rangi nyeuusi ambayo yanaonekana sehemu ya mbele ya macho yao.
Wana kwato ngumu zilizo chongoka ambazo huwasaidia kuchimba vyakula vyenye asili ya mizizi.
Madume pekee ndo huwa na pembe ambazo zimenyooka, ziko sambamba, nyororo na zilizo chongoka. Pembe hizi hurefuka na kufikia urefu wa sentimita 7 hadi 19.
Hupenda kujisaidia kwenye mashimo na kisha kuyafukia mashimo hayo. Hii huwasaidia wanyama hawa wasigundulike kirahisi maeneo waliyopo hasa kutokana na maadui zao.
Wanapohisi kuna adui wanyama hawa hutulia na kujificha lakini adui anapo wakaribia hukimbia na kutafuta maficho mengine hasa kwenye mashimo yaliyo achwa na wanyama kama mhanga.
Dume na jike huishi mbali mbali na hukutana kipindi wanapotaka kuzaliana tu hivyo dume mmoja huwa na jike mmoja tu na eneo lao huwa na ukubwa wa hekari 4 mpaka 100.
Urefu=Isha mkubwa hufikia urefu wa sentimita 70 hadi 95.
Kimo= kimo cha isha hufikia sentimita 45 hadi 60.
Uzito= wanyama hawa huwa na uzito wa kilogramu 7 hadi 16.
Wanapedelea mazingira yenye majani tu na tafiti zinaonesha kuwa wanyama hawa ni kwa nadra sana kuwaona katika maeneo ambayo kwa asilimia kubwa ardhi imetawaliwa na miti.
Isha ni wanyama walao majani kama walivyo wanyama jamii ya swala wengine. Wana uwezo wakula mizizi pia pamoja na vyakula jamii ya vitunguu.
Wanyama hawa hawapendelei kunywa maji mara kwa mara kwani maji mengi huyapata kupitia chakula au aina ya majani wanayo kula mara kwa mara. Hivyo wana uwezo wa kuishi muda mrefu sana bila kunywa maji.
Mara tuu baaada ya kupandana jike na dume husambaratika na jike hukaa na mimba kwa muda wa miezi 5 hadi 6 kisha huzaa mtoto mmoja tu.
kwa kipindi cha wiki chache za mwanzo mama humficha mtoto eneo salama lenye majani dhidi ya maadui. Mama huondoa kinyesi cha mtoto pamoja na kufukia viashiria vyiovyote vile ambavyo vinaweza kuwafanya maadui kugundua mahali alipo mtoto na kumuuwa.
Huishi miaka 7 na huweza ongezeka ikiwa atafugwa.View attachment 1171743View attachment 1171744View attachment 1171745
poaHapana digidigi ni jamii ya swala pia ni mkubwa kama mbuzi wakati hawa kina Isha ni wadogo..nitamleta tumjue nayeye.
Vipi nyama yake mkuu
Wewe ni mnyamwezi au msukuma maana hilo Nina la nsha na I'd ya itegamatwi
Imenifanya nitambue eneo lako asili
Kuna wale diker wako kule zanzibar piaHapana digidigi ni jamii ya swala pia ni mkubwa kama mbuzi wakati hawa kina Isha ni wadogo..nitamleta tumjue nayeye.
Hakanaga ujanja na mwanga wa touch!!!Watam hao nyama yao ina kachumvi fulani hivi amazing
Umechanganya mkuu, digi digi(dik dik) ndio mdogo 3kgs to 4.5kgs wakati Duker au isha kama unavyowaita wanafika hadi 16kgsHapana digidigi ni jamii ya swala pia ni mkubwa kama mbuzi wakati hawa kina Isha ni wadogo..nitamleta tumjue nayeye.
Hapana digidigi ni jamii ya swala pia ni mkubwa kama mbuzi wakati hawa kina Isha ni wadogo..nitamleta tumjue nayeye.
Sahihi.Nilimsikia mmoja wa nduguzo akiita hivyo pale Kipalapala.Kikwetu tunawaita Nsha