Huyu dogo anahangaika tu mkuu.
Magufuli hawezi fanya kazi na mtu kama Ngeleja, ni mtu wa madili feki sana na mpenda misifa, ni type za kina JK na Nyalandu
Mh. Ngeleja alifanikisha mchakati wa
kupata Sera mpya ya Madini mwaka 2009.
} Mh. Ngeleja alifanikisha mchakato wa
kupata Sheria mpya ya mwaka 2010.
Baadhi ya mambo mapya na muhimu
yalioingizwa katika Sera na Sheria mpya ya
madini ni pamoja na;-
a\ Sharti la Serikali kumiliki hisa za bure
katika migodi(free carried interest), mfano
migodi wa Buckreef Geita, Serikali inamiliki
hisa za bure 45℅ kupiti STAMICO,
Mchuchuma/ Liganga(NDC 20%) Na ngaka
(NDC 30%).
b/ Migodi yote inatakiwa kununua Huduma
na bidhaa mbalimbali nchini badala ya
kuagiza kutoka nje kama ilivyokuwa awali.
c/ Kipindi cha leseni za wachimbaji wadogo
kimeongezwa kutoka 5-7.
d/ Viwango vya mrabaha vimeongezeka, kwa
mfano, dhahabu kwa sasa ni 4% badala ya
3%(migodi ilianza kulipa mrabaha mpya Mei
1, 2012).
} Mh. Ngeleja alisimamia kuifufua STAMICO
mwaka 2008, awali ilikuwa imeorodheshwa
kufutwa kabisa.
} Mh. Ngeleja alisimamia kumpata mwekezaji
katika mgidi wa Makaa ya Mawe na Chuma
wa Mchuchuma/Liganga kwa kushirikiana na
NDC mwaka 2007-2011.
} Mh. Ngeleja alisimamia kuurudisha mgodi
wa kiwira mikononi mwa serikali kupitia
STAMICO Mwaka 2009/11.
} Mh. Ngeleja alisimamia kampuni za madini
kuanza kulipa kodi ya mapato (30℅) mfano,
resolute (Nzega), Geita Gold Mine (Geita),
Tulawaka (Biharamulo) na TanzaniaOne
(Mererani).
} Mh. Ngeleja alihakikisha maeneo zaidi kwa
ajili ya wachimbaji wadogo yanatengwa na
serikali.
} Mh. Ngeleja aliasisi utaratibu wa Mfuko
Maalum wa kusaidia wachimbaji wadogo
nchini.
} Mh. Ngeleja alipiga marufuku usafirishaji
nje ya nchi wa madini ghafi ya Tanzanite
yenye ukubwa unaozidi gramu 1, mwaka
2010 April.
} Mh. Ngeleja ni Muasisi wa utaratibu wa
kutoa hati ya uasili( Certificate of Origin) kwa
wanaouza madini ya Tanzanite.
} Mh. Ngeleja alisimamia uanzishwaji wa
wakala wa ukaguzi wa Migodi, Tanzania
Mineral Audit Agency (TMAA). Mwaka 2009.
Nb; manufaa ya wakala huu yanajulikana.
} Mh. Ngeleja alisimamia mchakato wa
Tanzania kujiunga na tasnia ya uziduaji
duniani (EITI) kuanzia mwaka 2009.
} Mh. Ngeleja alisimamia kuhamishwa kwa
kitengo cha kukata almasi (TRASORT) kutoka
Uingereza na kuhamia nchini mwezi agosti
mwaka 2010.