Mfahamu Jenerali Mayele na anguko la Zaire

Basi Nenda

JF-Expert Member
Jul 29, 2017
20,159
45,852
unaweza kuwa unajiuliza nini kilipelekea mpaka zaire ikaanguka ?, sababu wengi wanayoijua ni laurent kabila kusaidiwa na rwanda na uganda,lakini anguko la zaire lina mengi, kwa kuanza nitaelezea historia ya aliyekuwa waziri wa ulinzi wa mwisho wa MObutu na mchango wake kwa kuanguka zaire,huyo ni jenerali maHele lieko bokungu,aliyejulikana pia kama donat, wengine humuona kama mzalendo ila alichangia pakubwa kuanguka zaire na kwa sababu hiyo aliuawa mnamo 1997 mwezi wa 5 usiku wa tarehe 16 kwenda 17 katika makao makuu ya jeshi la ulinzi wa mobutu camp tshashi





HISTORIA YA MAHELE

alizaliwa 15/4/1941 huko kinshsasa wakati huo ikiitwa leopoldville katika familia ya kimbuza, wambuza walipewa ofisi za juu katika jeshi la zaire,akiwa na umri mdogo mwaka 1963 akiwa pia na mawazo ya kilumumba alijiunga na the youth organization of the Mouvement national congolais ,miaka miwili baadae mobutu anachukua nchi maHele anapelekwa mafunzoni kwenye kambi ya kitona baadae ndjili paramilitary commandos

mwaka 1968 akiwa second liutenant anajiunga na kikosi cha ulinzi wa rais DSP ,siku moja anakutwa amesinzia mlangoni kwa mobutu usiku badala ya kulinda tukio hili linasababisha ahamishiwe kotakoli commando training center kama mkufunzi,baadae anaenda kusoma ufaransa na mwaka 1984 anarudi zaire akiwa liutenant colonel ,mwisho wa mwaka 1990 anatumwa kama kiongozi wa kikosi kilichotumwa na mobutu kumuokoa rafiki wake raos wa rwanda habyarimana na kuwashushia kipigo RPF wa rwanda, ni kutokana na kichapo walichopata kutoka jeshi la zaire kiongozi wa kwanza wa RPF anauawa fred rwigyema na kupewa cheo cha brigedia jenerali
september 1991 jeshi linaingia mtaani kinshasa na kufanya wizi na uporaji ,mayele anatumwa tena tenaa na mobutu,mobutu akiwa na hasira anamfukuza kazi chief of staff na kumteua mahele

january 1993 jeshi linaingia tena mtaani kuiba vitu lakini hivi sasa ni kikosi cha walinzi wa mobutu na sio FAZ yani jeshi la nchi mayele anaingia mzigoni bila hata kuwapa onyo anatumia mabomu kuwamaliza , DSP hawakumsamehe kwa kitendo hiki na walibaki na chuki nae, week mbili baadae mkuu wa DSP jenerali nzimbi anatumia nafasi ya safari ya mahele kwenda kisangani kukutana na archbishop mosengwo kumchonganisha mahele na mobutu,mahele akiwa huko alisema jeshi sio mali ya mtu binafsi bali ya nchi,mahele anafukuzwa kazi na mobutu na kuteuliwa kuwa mshauri wa kijeshi wa mobutu, kazi hii haikua na maana hasa ukizingatia wakati huu mobutu hana imani na mahele,mahele anaacha kazi na kwenda shambani kwake, ni shamba kubwa lenye thamani ya dolla million 1, humo kuna kila kitu mpaka hospitali na majumba ya kifahari ,je alivipata wapi ? alipewa na mobutu


VITA YA KWANZA YA CONGO / UVAMIZI WA ZAIRE
augost 1996 mobutu anafanyiwa surgery ya saratani huko lausanne ,mwezi october vita vinatokea mashariki mwa kivu dhidi ya majeshi ya muungano wa kina kabila,na mwezi november goma na bukavu inachukuliwa na waasi,mobutu akiwa nyumbani kwake Roquebrune-Cap-Martin ufaransa akiwa amepumzika kutokana na maradhi,anamfukuza kazi chief of staff na kumteua jenerali baramoto,hali ni mbaya majeshi ya zaire yanashindwa vita kila siku na dsp kikosi cha ulinzi wa mobutu kinatumia muda wake kupigana na vikosi vingine vya jeshi la zaire wakishindana kuiba vitu

17 december 1996 mobutu anarudi zaire,baada ya kushauriwa sana kumteua mahele kuongoza jeshi,huku akiwa hataki kabisa hatimae mobutu anakubali,mayele anateuliwa ila anahofia usalama wake, anashauriwa baadhi ya mambo ikiwemo kuhama nyumba yake iliyo karibu na kambi ya tshasi/camp tshashi makao makuu ya maadui wake ambao ni dsp walinzi wa mobutu pili kuacha kwenda mstari wa mbele vitani na tatu ahame ofisi zilizo karibu na dsp

mahele anaenda kisangani na kuwashawishi wanajeshi wa zaire wasipambane ni march 15,na wanakubali siku tatu baadae kisangani inatwaliwa na waasi


USALITI
mmoja wa marafiki wa mahele anamuunganisha mahele wafanye mazungumzo na juliana lumumba,binti wa patrice lumumba ambaye anafanya mAwasiliano na vikosi vya kabila, wanawasiliana na makao makuu ya waasi huko goma kuwa wako tayri kufanya mazungumzo .mayele anadai anawasiwasi mazungumzo yao yasijedukuliwa na serikali,marekani inampa mahele simu ya satellite, siku moja january 3 simu ya mahele inaita aliyepiga ni laurent kabila kiongozi wa waasi

vita vimepamba moto, jonas savimbi anatoa usd 20 million kusaidia vita upande wa rafiki yake mobutu,na silaha pamoja na wanajeshi 3000 wa UNITA ushindi unaonekana upande wa zaire, dsp wana silaha mpya na nzito ,majeshi ya kabila na rwanda ,uganda na angola yanachapwa mno na majeshi ya zaire , kabila anamtafuta mahele mahele anampa taarifa za sili za jeshi, vikosi vya mobutu vinapoteza pambano

thursday may 15 wakati vikosi vya mobutu vilivopigwa kenge kutokana na mahele kutoa taarifa za kiintelijensia kwa kabila vinaludi kinshasa,mobutu anaweka kikao camp tshashi na majenerali wake, mahele likulia na ilunga wanamshauri mobutu aondoke kinshasa aende mji wa gbadolite nyumbani kwake kwa sababu akiwa kinshasa hawawezi kumuakikishia usalama wake aende gbadolite huku wakiangalia njia za kupambana na adui, mobutu anakataa na kusema ukiwa mwanajeshi ni uwawe au ujisalimishe ila haukimbii, kikao hiki kinaisha,na baada ya muda mobutu anaitisha kingine usiku wa manane

kikao cha pili anakaa na majenerali wa kabila lake la ngbandi ambapo wanadai kuna wasaliti na wakataka watajwe,mobutu anaamua yaishe anakubali kesho yake ataondoka,kikao kinaisha majenerali wanaenda nyumbani kwa baramoto kufanya kikao ch tatu ambacho kinaisha saa kumi na moja alfajili ,katika kikao hicho majina ya wasaliti yanatajwa na mahele anakua namba moja


SAFARI YA KUONDOKA KINSHASA
ijumaa may tarehe 16 saa nane mchana rais mobutu na familia yake wapo uwanja wa ndege wa ndjili wakingoja kwenda gbadolite, mobutu ana hasira anauliza pesa zipo wapi ? kwa sababu siku moja kabla operation kubwa ya ukusanywaji pesa ilifanyika kutoka bank kuu na ofisi ya waziri mkuu nk ,dolla 40 million zilikuwa zimekusanywa ndani ya masaa machache , mobutu anazitaka,ila tatizo kila aliyetumwa kachukua chake na kiasi kilicholetwa ni kidogo kuliko rais alichotarajia
ila ni lazima waondoke, wakati wanapanda ngazi za ndege bobi ladawa mke wa mobutu anamgeukia mahele na kusema <donat tunajua ulichofanya,hivyo ndivo unamlipa baba baada ya yote aliyokufanyia> mahele hajibu kitu, mobutu alisikia maneno hayo akatikisa tu kichwa , ni saa tisa na nusu mchana ndege inaruka ila inatumia njia tofauti kuna tishio la shambulizi <nimeshalielezea kwenye moja ya nyzi>



KIFO CHA MAHELE,MAUAJI CAMP TSHASHI
kila mtu anarudi kwake baada ya kumsindikiza mobutu akienda kujiandaa kutoroka kwa sababu waasi wa kabila wapo kilomita 40 katika barabara ya kenge wanakuja kuichukua kinshasa, mahele anaenda kwake la gombe baadae anaenda nyumbani kwa waziri mkuu likulia,wanajadili kuwatumia pesa wanajeshi kwa ajili ya chakula nk
baadae anarudi kwake,simu inaita anapigiwa na mtu wake kutoka waasi wa kabila na wanajadili kumkabidhi nchi kabila,


11pm,thursday may 16 1997 waziri mkuu likulia bolongo anampigia simu mahele na kumtaarifu dalili za uasi katika kambi ya tshashi ambayo ni makao makuu ya walinzi wa mobutu, mahele anasema anaenda kuongea na hao wanajeshi licha ya kutaadharishwa anatoka kwake na gari mbili moja ya walinzi kumi, na moja amepanda yeye,dereva na bodyguard wake,alipofika camp tshashi gari ya walinzi ikabaki nje, akaingia na gari moja
mahele anakutana na mamia ya wanajeshi wa DSP wanaogoma kumpa heshima za kijeshi, mmoja wao ni jenerali wezago aliyeshiriki kile kikao cha kutaja wasaliti ,wezago anamkalipia mahele umefata nini hapa wewe msaliti hukupigana vita, mahele anajibu punguza jazba AFDL wapo njiani watakua hapa kesho hivo huna jinsi shusha chini silaha

wezago anajibu,inawezezekana vipi wewe uliyeruhusu dsp wafe unanipa orders, akatoa pistol na kumpiga mkuuni mahele
,mlinzi wa mahele anaingilia kati naye anapigwa risasi,dereva wa mahele kashakimbia sasa mahele yupo peke yake akajificha chini ya uvungu wa gari, wezago hakutaka kumuacha akachukua tochi kumtafuta,wanajeshi wakasema mahele ana ushirikina mkubwa amepotea, lakini hii haikumzuia wezago kumtafuta hatimae wakampata uvunguni wa gari na kumpigisha magoti, walinzi wa mahele waliposikia risasi walikimbia kumuita kongolu mobutu a.k.a saddam hussein aliyefika haraka ila kabla hajafika, pale mahele alipopigishwa magoti alitokea ofisa wa juu wa DSP akampiga risasi ya shingo mahele akafa hapo hapo


huo ndio mwisho wa mahele,mwanajeshi shupavu aliyeisaliti nchi yake

NB
KATIKA HIYO PICHA HUYO MZEE MWENYE MUSTACHE ALIYE UPANDE WA KULIA WA MAHELE NDIYE JENERALI WEZAGO AMBAYE ALIMPIGA RISASI MAHELE
 

Attachments

  • mahele1.jpg
    mahele1.jpg
    285 KB · Views: 147
Tunawalaumu sana watu wa nje wakati tatizo tunalo sie wenyewe

mpuuzi mpuuzi tu
mkuu, tatizo ni rwanda na mzungu tu, zaire ilipata maendeleo ikahujumiwa na wazungu, haya ma ndege magu anayonunua yalikuwepo zaire makubwa zaidi ya haya tuliyonayo, wazaire wengi wa mijini wali enjoy maisha, mpaka mwanzoni mwa miaka ya 90 ndio tabu ikaanza, mzungu akaweka figisu bei za madini ya congo zikashuka,akakata misaada,akaleta na waasi
 
unaweza kuwa unajiuliza nini kilipelekea mpaka zaire ikaanguka ?, sababu wengi wanayoijua ni laurent kabila kusaidiwa na rwanda na uganda,lakini anguko la zaire lina mengi, kwa kuanza nitaelezea historia ya aliyekuwa waziri wa ulinzi wa mwisho wa MObutu na mchango wake kwa kuanguka zaire,huyo ni jenerali maHele lieko bokungu,aliyejulikana pia kama donat, wengine humuona kama mzalendo ila alichangia pakubwa kuanguka zaire na kwa sababu hiyo aliuawa mnamo 1997 mwezi wa 5 usiku wa tarehe 16 kwenda 17 katika makao makuu ya jeshi la ulinzi wa mobutu camp tshashi





HISTORIA YA MAHELE

alizaliwa 15/4/1941 huko kinshsasa wakati huo ikiitwa leopoldville katika familia ya kimbuza, wambuza walipewa ofisi za juu katika jeshi la zaire,akiwa na umri mdogo mwaka 1963 akiwa pia na mawazo ya kilumumba alijiunga na the youth organization of the Mouvement national congolais ,miaka miwili baadae mobutu anachukua nchi maHele anapelekwa mafunzoni kwenye kambi ya kitona baadae ndjili paramilitary commandos

mwaka 1968 akiwa second liutenant anajiunga na kikosi cha ulinzi wa rais DSP ,siku moja anakutwa amesinzia mlangoni kwa mobutu usiku badala ya kulinda tukio hili linasababisha ahamishiwe kotakoli commando training center kama mkufunzi,baadae anaenda kusoma ufaransa na mwaka 1984 anarudi zaire akiwa liutenant colonel ,mwisho wa mwaka 1990 anatumwa kama kiongozi wa kikosi kilichotumwa na mobutu kumuokoa rafiki wake raos wa rwanda habyarimana na kuwashushia kipigo RPF wa rwanda, ni kutokana na kichapo walichopata kutoka jeshi la zaire kiongozi wa kwanza wa RPF anauawa fred rwigyema na kupewa cheo cha brigedia jenerali
september 1991 jeshi linaingia mtaani kinshasa na kufanya wizi na uporaji ,mayele anatumwa tena tenaa na mobutu,mobutu akiwa na hasira anamfukuza kazi chief of staff na kumteua mahele

january 1993 jeshi linaingia tena mtaani kuiba vitu lakini hivi sasa ni kikosi cha walinzi wa mobutu na sio FAZ yani jeshi la nchi mayele anaingia mzigoni bila hata kuwapa onyo anatumia mabomu kuwamaliza , DSP hawakumsamehe kwa kitendo hiki na walibaki na chuki nae, week mbili baadae mkuu wa DSP jenerali nzimbi anatumia nafasi ya safari ya mahele kwenda kisangani kukutana na archbishop mosengwo kumchonganisha mahele na mobutu,mahele akiwa huko alisema jeshi sio mali ya mtu binafsi bali ya nchi,mahele anafukuzwa kazi na mobutu na kuteuliwa kuwa mshauri wa kijeshi wa mobutu, kazi hii haikua na maana hasa ukizingatia wakati huu mobutu hana imani na mahele,mahele anaacha kazi na kwenda shambani kwake, ni shamba kubwa lenye thamani ya dolla million 1, humo kuna kila kitu mpaka hospitali na majumba ya kifahari ,je alivipata wapi ? alipewa na mobutu


VITA YA KWANZA YA CONGO / UVAMIZI WA ZAIRE
augost 1996 mobutu anafanyiwa surgery ya saratani huko lausanne ,mwezi october vita vinatokea mashariki mwa kivu dhidi ya majeshi ya muungano wa kina kabila,na mwezi november goma na bukavu inachukuliwa na waasi,mobutu akiwa nyumbani kwake Roquebrune-Cap-Martin ufaransa akiwa amepumzika kutokana na maradhi,anamfukuza kazi chief of staff na kumteua jenerali baramoto,hali ni mbaya majeshi ya zaire yanashindwa vita kila siku na dsp kikosi cha ulinzi wa mobutu kinatumia muda wake kupigana na vikosi vingine vya jeshi la zaire wakishindana kuiba vitu

17 december 1996 mobutu anarudi zaire,baada ya kushauriwa sana kumteua mahele kuongoza jeshi,huku akiwa hataki kabisa hatimae mobutu anakubali,mayele anateuliwa ila anahofia usalama wake, anashauriwa baadhi ya mambo ikiwemo kuhama nyumba yake iliyo karibu na kambi ya tshasi/camp tshashi makao makuu ya maadui wake ambao ni dsp walinzi wa mobutu pili kuacha kwenda mstari wa mbele vitani na tatu ahame ofisi zilizo karibu na dsp

mahele anaenda kisangani na kuwashawishi wanajeshi wa zaire wasipambane ni march 15,na wanakubali siku tatu baadae kisangani inatwaliwa na waasi


USALITI
mmoja wa marafiki wa mahele anamuunganisha mahele wafanye mazungumzo na juliana lumumba,binti wa patrice lumumba ambaye anafanya mAwasiliano na vikosi vya kabila, wanawasiliana na makao makuu ya waasi huko goma kuwa wako tayri kufanya mazungumzo .mayele anadai anawasiwasi mazungumzo yao yasijedukuliwa na serikali,marekani inampa mahele simu ya satellite, siku moja january 3 simu ya mahele inaita aliyepiga ni laurent kabila kiongozi wa waasi

vita vimepamba moto, jonas savimbi anatoa usd 20 million kusaidia vita upande wa rafiki yake mobutu,na silaha pamoja na wanajeshi 3000 wa UNITA ushindi unaonekana upande wa zaire, dsp wana silaha mpya na nzito ,majeshi ya kabila na rwanda ,uganda na angola yanachapwa mno na majeshi ya zaire , kabila anamtafuta mahele mahele anampa taarifa za sili za jeshi, vikosi vya mobutu vinapoteza pambano

thursday may 15 wakati vikosi vya mobutu vilivopigwa kenge kutokana na mahele kutoa taarifa za kiintelijensia kwa kabila vinaludi kinshasa,mobutu anaweka kikao camp tshashi na majenerali wake, mahele likulia na ilunga wanamshauri mobutu aondoke kinshasa aende mji wa gbadolite nyumbani kwake kwa sababu akiwa kinshasa hawawezi kumuakikishia usalama wake aende gbadolite huku wakiangalia njia za kupambana na adui, mobutu anakataa na kusema ukiwa mwanajeshi ni uwawe au ujisalimishe ila haukimbii, kikao hiki kinaisha,na baada ya muda mobutu anaitisha kingine usiku wa manane

kikao cha pili anakaa na majenerali wa kabila lake la ngbandi ambapo wanadai kuna wasaliti na wakataka watajwe,mobutu anaamua yaishe anakubali kesho yake ataondoka,kikao kinaisha majenerali wanaenda nyumbani kwa baramoto kufanya kikao ch tatu ambacho kinaisha saa kumi na moja alfajili ,katika kikao hicho majina ya wasaliti yanatajwa na mahele anakua namba moja


SAFARI YA KUONDOKA KINSHASA
ijumaa may tarehe 16 saa nane mchana rais mobutu na familia yake wapo uwanja wa ndege wa ndjili wakingoja kwenda gbadolite, mobutu ana hasira anauliza pesa zipo wapi ? kwa sababu siku moja kabla operation kubwa ya ukusanywaji pesa ilifanyika kutoka bank kuu na ofisi ya waziri mkuu nk ,dolla 40 million zilikuwa zimekusanywa ndani ya masaa machache , mobutu anazitaka,ila tatizo kila aliyetumwa kachukua chake na kiasi kilicholetwa ni kidogo kuliko rais alichotarajia
ila ni lazima waondoke, wakati wanapanda ngazi za ndege bobi ladawa mke wa mobutu anamgeukia mahele na kusema <donat tunajua ulichofanya,hivyo ndivo unamlipa baba baada ya yote aliyokufanyia> mahele hajibu kitu, mobutu alisikia maneno hayo akatikisa tu kichwa , ni saa tisa na nusu mchana ndege inaruka ila inatumia njia tofauti kuna tishio la shambulizi <nimeshalielezea kwenye moja ya nyzi>



KIFO CHA MAHELE,MAUAJI CAMP TSHASHI
kila mtu anarudi kwake baada ya kumsindikiza mobutu akienda kujiandaa kutoroka kwa sababu waasi wa kabila wapo kilomita 40 katika barabara ya kenge wanakuja kuichukua kinshasa, mahele anaenda kwake la gombe baadae anaenda nyumbani kwa waziri mkuu likulia,wanajadili kuwatumia pesa wanajeshi kwa ajili ya chakula nk
baadae anarudi kwake,simu inaita anapigiwa na mtu wake kutoka waasi wa kabila na wanajadili kumkabidhi nchi kabila,


11pm,thursday may 16 1997 waziri mkuu likulia bolongo anampigia simu mahele na kumtaarifu dalili za uasi katika kambi ya tshashi ambayo ni makao makuu ya walinzi wa mobutu, mahele anasema anaenda kuongea na hao wanajeshi licha ya kutaadharishwa anatoka kwake na gari mbili moja ya walinzi kumi, na moja amepanda yeye,dereva na bodyguard wake,alipofika camp tshashi gari ya walinzi ikabaki nje, akaingia na gari moja
mahele anakutana na mamia ya wanajeshi wa DSP wanaogoma kumpa heshima za kijeshi, mmoja wao ni jenerali wezago aliyeshiriki kile kikao cha kutaja wasaliti ,wezago anamkalipia mahele umefata nini hapa wewe msaliti hukupigana vita, mahele anajibu punguza jazba AFDL wapo njiani watakua hapa kesho hivo huna jinsi shusha chini silaha

wezago anajibu,inawezezekana vipi wewe uliyeruhusu dsp wafe unanipa orders, akatoa pistol na kumpiga mkuuni mahele
,mlinzi wa mahele anaingilia kati naye anapigwa risasi,dereva wa mahele kashakimbia sasa mahele yupo peke yake akajificha chini ya uvungu wa gari, wezago hakutaka kumuacha akachukua tochi kumtafuta,wanajeshi wakasema mahele ana ushirikina mkubwa amepotea, lakini hii haikumzuia wezago kumtafuta hatimae wakampata uvunguni wa gari na kumpigisha magoti, walinzi wa mahele waliposikia risasi walikimbia kumuita kongolu mobutu a.k.a saddam hussein aliyefika haraka ila kabla hajafika, pale mahele alipopigishwa magoti alitokea ofisa wa juu wa DSP akampiga risasi ya shingo mahele akafa hapo hapo


huo ndio mwisho wa mahele,mwanajeshi shupavu aliyeisaliti nchi yake

NB
KATIKA HIYO PICHA HUYO MZEE MWENYE MUSTACHE ALIYE UPANDE WA KULIA WA MAHELE NDIYE JENERALI WEZAGO AMBAYE ALIMPIGA RISASI MAHELE
Hii inatufundisha wajeda ndio wenye nchi wakikosa udhibiti ni noma
 
Back
Top Bottom