Mfahamu Baharia wa meli, Idara za meli na nafasi za mabaharia katika meli

Mfano mimi Nina Bachelor na Diploma za Electrical and Electronic Engineering nikienda DMI kusoma Postgraduate Diploma ya Marine Engineering nikimaliza kusoma nikapata seatime ya mwaka nikitaka kusoma CoC (Certificates of Competency) upande was Engine Room nitasoma ipi Kati ya Fourth Engineer,Third Engineer au Second Engineer?
 
Class III yaani third engineer
 
Dah ni noma je nikienda na background ya electrical itakuaje au ndio nitaambiwa nianze mandatory courses then rating
Mandatories zote ni lazima mfan survival at sea, pssr nakadhalika. Mfano pssr ni muhimu sana maana kule mara nyingi tunafanya kazi na watu wa mataifa mbalimbali na wenye tamaduni tofauti tofauti. Jana tu nimeshuhudia ugomvi mkubwa baina ya watu ushwahilini hadi ndundi zikawaka kiasa! mmoja wao wakati wa mabishano alimyooshea kidole mwenzake kumbe yule jamaa kikwao huko kanda ya ziwa ni dharau kufanya hivyo. Mfano mwingine niaye rafiki yangu wa karibu sana miaka ya nyuma aliwahi kufanya kazi kama nahodha kwenye meli moja na crew members wengi walikuwa wahindi. Basi siku moja kulitokea sintofahamu melini baada ya nahodha kuonwa anakunywa maziwa fresh na samaki wa kukaanga kumbe wale wahindi kwa imani yao ukichanganya vyakula hivyo hautaishi muda mrefu utakufa. Daaah ilichukuwa juhudi kubwa sana kuwaelimisha hatimae wakatuliwa ingawa walikuwa bado wanasikilizia captain atakufa saa ngapi. Kwahiyo masomo yote pale ni muhimu
 
Sawa kaka ngoja nijipange mwakani niingie dmi.
 
Na
Naweza kukusaidia kwa mambo mawili matatu kwasababu niko kwenye fani karibu miaka 30 na nimesaidia wengi hadi sasa najivunia kuwa na ndugu wengi sana. Yaani ukoo wangu mkubwa sasa hivi
Naomba kufahamu upatikanaji wake wa ajira kwa ujumla hasa nje ya nchi.
 
Na
Naomba kufahamu upatikanaji wake wa ajira kwa ujumla hasa nje ya nchi.
Kazi zipo tele katika nchi ambazo ni maritime oriented na hii fani ni ya kimataifa. Ila unatakiwa kuchangamka kwa kuipenda fani, kuwa bora kwenye fani na kuwa huru kufanya popote duniani. Ukitegemea hapa kwetu sijui victoria sijui nini nini huko utachanganyikiwa. Unaweza kukuta boss wako ana fani ya uinjinia wa magodauni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…