Habari zenu wana mmu.
Wandugu hizi simu ni nzuri sana kwasababu zina turahisishia mawasiliano ukilinganisha na zama zile za barua.
Lakini simu hizi hizi ziki kugeukia utaziona chungu, hasa kwenye suala la mahusiano.
Nimeandika yote hayo hasa baada ya kilichonitokea mimi jana jioni , (ingawa nilikuwa Nasikia tu kwa wengine jinsi simu zilivyovunja ndoa na mahusiano yao)
Jana jioni majira ya saa kumi jioni, nilitoka na mpenzi wangu kwenda kujivinjari maeneo ya kigamboni, mji mwema, kwenye fukwe tulivu za kipepeo beach, mbali na makelele na stress za jiji la Dar es salaam.
Sasa tukiwa huko tunapata vinywaji na vilaji, mpenzi wangu alichukua simu yangu akawa anaiangalia, kwakuwa sina tabia ya kuficha wala kulock simu basi nikamwachia aiangalie.
Wakati anaiangalia-angalia simu yangu, mara message ikaingia, nikaona kabadirika sura ghafla, nilipomuuliza hakunijibu nikaamua kuichukua simu na kuangalia hiyo sms ni ya nani?
Nilipoisoma iliandikwa hivi "mambo baby, vipi uko poa,?! Jana tulipoacha pale Ulifika salama baby? Basi baby, leo jioni tukutane annex bwana , pale pa jana sikupapenda makelele mengi? Sawa baby?
Nilishtuka sana maana kusema ukweli sina mchepuko nje, nikajaribu kumuelewesha mpenzi wangu, kuwa hiyo sms imekosewa lakin hakutaka kuelewe wala nini?
Kukata mzizi wa fitina nikaamua kumpigia simu huyo dada mbele ya mpenz wangu tena nikaweka loud speaker ili naye asikie, sasa yule dada aliyetuma sms akapokea simu alipogundua amekosea sms sijui ni uoga au vipi , akakata simu then akazima kabisa ikawa haipatikani tena.
Sasa akaniachia mzozo na mpenz wangu, najaribu kumwelewesha lakin hataki amenuna, hata kupokea simu yangu hataki na kujibu sms zangu hataki, wakati kusema ukweli kabisa ile sms ilitumwa kimakosa.
Sasa wadau naombeni ushauri nifanyeje ili apate kuniamini.