BADO MMOJA
JF-Expert Member
- Jul 19, 2012
- 2,196
- 1,338
Habari zenu,
Nachukua Fursa hii adhim kumtakia Kamanda Godbless Lema Siku njema ya X- mass akiwa Gerezani .
Napenda kumhakikishia kuwa haya ni mapambano ya kudai Haki na Uhuru katika nchi hii. Asijisikie upweke Watanzania wenye nia Njema na nchi Tuko pamoja nae.
Mabavu ya watawala tunayaona na imefanywa hivi kwa makusudi kama njia ya kukukomesha uache kusema serikali. Lakini napenda nikuhakikishie Lema we ni miongoni mwa mashujaa wachache katika nchi hii ambao wamejitolea nafsi zao ili kuleta utawala wa haki na demokrasia hapa nchini.Najuwa siku ya leo ulipenda uwe pamoja na familia yako lakini kwa sababu za Kisiasa wameamua ukae ndani.
Usihofu mateso yakizidi Ufalme unakaribia. Pole sana kamanda nakutakia sikukuu Njema ya X-mass ukiwa hapo Gerezani.
Nyie mnampumbaza mwenzenu kumwita kamanda mara shujaa hivi ni shujaaa wa kitu gani hasa mkiulizwa mtasema na dunia imtambue kama SHUJAA?? Au kule kukosa adabu kwake ndiyo mnamwita shujaa? Basi MPUMBAZENI AJIONE NI SHUJAA ATATOKA MWEZI JUNI. Mtu anajitakia mwenyewe kukaa gerezani leo hii mnamwita shujaa for what?? Mwacheni ateseke kwa ujinga wake kwani siasa ni matusi huyo EL mwenyewe sijawahi kumsikia akitukana pamoja na kudai kuibiwa kura huyo jmaa yenu kazi kuropoka tu haya sasa aendelee kuropoka hata humo gerezani kuna radio.