Meremeta & TANGOLD Revealed!

Ikulu ya Ben Mkapa iliibeba Meremeta

Mwandishi Wetu Aprili 9, 2008
Raia Mwema


SASA ni wazi, uongozi wa awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa ndio ulioshinikiza na kuidhinisha kuanzishwa kwa Kampuni ya Meremeta Gold, inayohusishwa na upotevu wa Sh bilioni 155, ndani ya Benki Kuu (BoT), imefahamika.

Habari za uhakika na nyaraka, zimethibitisha kwamba uongozi huo chini ya Mkapa ulihusika ama kushinikiza moja kwa moja mchakato wa kuanzishwa kwa Meremeta na hatimaye kuitafutia fedha za kufanyia kazi, fedha ambazo hata hivyo sasa zinahofiwa kupotea.

Tayari Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), Ludovick Utouh, ametamka kwamba ofisi yake haijawahi kukagua hesabu za Meremeta Gold, na kampuni hiyo tata haimo katika orodha ya makampuni yanayomilikiwa na Serikali ama Serikali kuwa na hisa.

Raia Mwema imeiona barua kutoka Ikulu, iliyoandikwa na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Matern Lumbanga, kwenda benki moja ya Uingereza, ikieleza kwamba Mkapa kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri mwaka 2000, ndiye aliyetoa idhini ya kuanzishwa kwa shughuli za uchimbani dhahabu katika eneo la Tembo na Buhemba, mkoani Mara.

Katika hali isiyo ya kawaida, Ikulu ndiyo iliyobeba jukumu la kuithibitisha na kuitambulisha Kampuni ya Meremeta kwa Deutch Bank AG London, iliyoko nchini Uingereza kwa nia ya kupata mkopo wa uendeshaji wa mgodi huo ambao kwa sasa umefungwa na kampuni hiyo kufilisiwa.

“Hii ni kuthibitisha kwamba tunafahamu kuwapo kwa hazina kubwa ya dhahabu nchini Tanzania ambayo haijalinufaisha Taifa na Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ilianzisha mradi wa Meremeta kwa nia ya kununua dhahabu kwa wachimbaji wadogo.

“Baadaye mwaka 2000, Rais (Mkapa) kupitia Baraza la Mawaziri aliazimia uchimbaji mkubwa wa chini ya ardhi katika eneo la Tembo na uchimbaji mwingine wa kawaida katika eneo la Buhemba, kaskazini mwa Tanzania,”

inaeleza barua hiyo ambayo kivuli chake kimechapishwa ukurasa wa kwanza wa toleo hili, iliyohitimisha kwa kusema kwamba mradi huo utakuwa na manufaa kwa Taifa.

Hata hivyo, katika barua hiyo inatajwa kampuni ya Nedcor Trade Services Limited ya Afrika Kusini kuwa ndiyo iliyotoa mkopo wa fedha za kuanzishia mradi huo chini ya usimamizi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, iliyokuwa inatajwa sana kuwa mmiliki wa mgodi huo awali kabla ya kubainika kuwapo kwa utata mkubwa.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, Utouh, alisema wazi kwamba Meremeta haimo katika orodha ya makampuni na mashirika ya umma ambayo yamewahi kukaguliwa na ofisi yake, na hivyo kuibua utata mwingine kwa kuwa huko nyuma kampuni hiyo imekuwa ikitajwa kuwa ya umma.

Utata huo unaongezwa na taarifa za kwamba Serikali kupitia Msajili wa Hazina ilitoa cheti ya kuithibitisha Meremeta kuwa kampuni ya umma tokea Oktoba mosi, 1997 baada ya kudaiwa kwamba Serikali ilikuwa na hisa katika kampuni hiyo, hisa zilizokuwa na zinazoendelea kushikiliwa na watendaji wakuu serikalini. Baadhi ya watendaji hao wamo serikalini na wengine sasa wako nje.

Habari zinasema kwamba tayari uchunguzi wa kina umekwisha kuanza kufuatilia hasa zilikokwenda fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni 155/- zikiwa ni nyingi zaidi ya zile zilizochotwa BoT kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA). Sakata la EPA linahusisha Sh bilioni 133/-.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari serikalini, uchunguzi huo umekwenda mbali zaidi baada ya watendaji wakuu ndani ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Wizara ya Ulinzi na JKT, kupata hisia za kuwapo kwa mikono michafu katika mradi wa Meremeta.

Habari zinasema sakata la Meremeta linaweza kuwa kubwa na zito zaidi kutokana na maelezo ya uwezekano wa kuwapo wahusika wanaofahamika duniani katika biashara chafu na hivyo kuibua mjadala mwingine mkubwa utakaovuka nje ya mipaka ya Tanzania.

Kampuni ya Nedcor Trade Services Limited ya Afrika Kusini, inaelezwa kuwa na uhusiano na benki ya Nedbank ya Afrika Kusini ambako sehemu ya fedha hizo zilipelekwa kutoka BoT. Baadhi ya watumishi wa benki hiyo wamekuwa wakitajwa kuwa wakurugenzi wa kampuni nyingine tata ya Deep Green Finance Limited, ambayo sasa haipo.

Deep Green Finance Limited ilisajiliwa nchini, ikachota fedha kutoka BoT, kabla ya kufilisiwa bila ya maelezo ya kutosha ya madhumuni hasa ya kuanzishwa kwa kampuni hiyo katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2005.

Kashfa ya Meremeta inaelezwa kuwa kubwa zaidi ya ile ya EPA kutokana na kwamba uwezekano wa kurejesha fedha hizo ni mdogo kutokana na kwamba ziliingia katika mkondo unaoihusisha zaidi Serikali yenyewe na watendaji wake na wafanyabiashara wa kimataifa.

Tayari Kamati ya Rais inayochunguza sekta ya Madini, chini ya uongozi wa Jaji Mark Bomani, imeufuatilia mradi huo kwa kwenda Buhemba na pia kuwaita watendaji kadhaa wa Serikali akiwamo Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, ambaye inadaiwa taarifa hizo zimemshitua.

Kwa mujibu wa Gavana Profesa Ndulu, kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za malipo ya fedha hizo za Meremeta ambazo ni zaidi ya zile za EPA zilizolipwa kwa utaratibu wa Dhamana za Hazina (Treasury Bonds).

Jaji Bomani aliliambia Raia Mwema hivi karibuni kwamba Kamati yake haitaficha kitu na kwamba baada ya kutembelea Buhemba na kuchunguza mambo yanayohusiana na mgodi huo, itatoa mapendekezo yake katika ripoti.

Baadhi ya wakurugenzi wa Kampuni ya Meremeta ambao wanaelezwa kuwa katika nafasi hizo kutokana na nyadhifa zao bado wanaendelea kushikilia hisa hizo akiwamo Gavana wa zamani wa Benki Kuu, Dk. Daudi Ballali, ambaye ajira yake ilisitishwa na Rais Jakaya Kikwete.

Tayari kuna habari kwamba kumekuwapo na juhudi za makusudi zinazofanywa na baadhi ya watendaji serikalini ambao wanajipanga kuzuia kuanikwa kwa ufisadi huo mkubwa.

Fedha hizo ambazo zilibadilishwa kuwa Dola za Marekani 131,736,628.73 kwa maelekezo yaliyotolewa Desemba 20, 2005, siku moja kabla ya kuapishwa kwa Rais Jakaya Kikwete, zilihamishwa kwenda Afrika Kusini na kuingizwa Nedbank, na nyingine kuingizwa katika akaunti za kampuni ya Tangold na Meremeta.

Taarifa za wakaguzi zinaonyesha kwamba baada ya ununuzi huo wa dhamana, Benki Kuu ilizibadilisha sehemu ya dhamana hizo kuwa dola za Marekani 118,396,460.36 ambazo zilipelekwa kwenye akaunti moja isiyojulikana ya Nedbank Ltd. ya Afrika Kusini, benki hiyo ikiwa imezipokea fedha hizo kupitia HSB Bank ya New York, Marekani zikitajwa kuwa malipo ya madeni ya kampuni mufilisi ya Meremeta Ltd.

Nyaraka ambazo Raia Mwema imeziona zinaonyesha kwamba sehemu nyingine ya fedha hizo zipatazo Dola za Marekani 13,736,628.73 zililipwa kwa kampuni ya TANGOLD kwenye akaunti ya kampuni hiyo iliyoko Benki ya NBC Corporate Branch, Dar es Salaam.

Mbali ya kamati ya madini na wakaguzi, kwa nyakati tofauti, kuhoji malipo hayo, bado usiri na juhudi kubwa za kufunika masuala hayo zimekuwa zikiendelea kufanywa.

Mwaka jana Mbunge wa Karatu Dk. Willibrod Slaa (CHADEMA), aliliingiza suala hilo katika hoja yake iliyokuja kugonga mwamba baadaye.

Katika hoja yake hiyo, Dk. Slaa alibainisha kwamba Meremeta Ltd. ni kampuni binafsi ya kigeni iliyoandikishwa Agosti 19, 1997 katika kisiwa cha Isle of Man nchini Uingereza na kupewa namba ya usajili 3424504, ikimilikiwa na TRIENNEX (PTY) LTD ya Afrika Kusini yenye asilimia 50 ya hisa za kawaida na Msajili wa Hazina (Treasury Registrar) akiwa na asilimia 50.

Kwa upande wa Tanzania, Dk. Slaa alisema Meremeta ilipewa Hati ya kutimiza masharti (Certificate of Compliance) Oktoba, 1997 lakini akasema kwamba Meremeta ilifilisiwa Uingereza Januari 2006.

Hata hivyo, Dk. Slaa ameeleza kwamba pamoja na kampuni hiyo kufilisiwa nchini Uingereza, hakuna ushahidi kuwa kwa upande wa Tanzania kampuni hiyo imefilisiwa au la kutokana na kutajwa katika marejeo mbalimbali kuwa moja ya makampuni yanayozalisha dhahabu.

“Taarifa na takwimu muhimu kuhusu Sekta za Nishati na Madini’, ya Julai, 2007, inaonyesha kuwa Meremeta bado inafanya kazi, na inazalisha tani 2.27 za dhahabu. Kama Serikali inasema Meremeta imefilisiwa na mali zake kuhamishiwa TANGOLD hali hii inaelezwa vipi? Taarifa hizi za utata zinaashiria nini?” alihoji Dk. Slaa.

Maelezo mengine yanayoibua utata zaidi na ambao Kamati ya Rais inayopitia mikataba ya madini itapata wakati mgumu kuitolea taarifa ni kuhusu Meremeta kudaiwa kuwa ni kampuni iliyoanzishwa kwa lengo la kusaidia JWTZ, Kikosi cha Nyumbu wakati ikiwa imeandikishwa nje ya nchi.

Taarifa ya awali ya wakaguzi waliokagua BoT, Juni 2006, iliibua sakata hilo la Meremeta pamoja na kashfa nyingine lakini haikuweza kufahamika ripoti hiyo ya wakaguzi ilivyoyeyuka na kutoanikwa hadharani kabla ya wakaguzi wengine wa nje kuibua suala la EPA pekee miongoni mwa uchafu mwingi ndani ya BoT na serikalini.

Taarifa hiyo ya wakaguzi ilibainisha kwamba Serikali ilitoa fedha hizo kiasi cha Sh. bilioni 155 kwa njia ya dhamana ya hazina ambayo inatakiwa kulipiwa riba ya asilimia 14.92 kila mwaka lakini hakukuwa na makubaliano yoyote rasmi kati ya Serikali na Meremeta hali inayoibua zaidi utata na kuonyesha hakuna njia yoyote ya kuweza kuzipata fedha hizo.

Ndani ya BoT bado kuna mianya mingi ambayo huenda ikaendelea kuibuka siku hadi siku hususan baada ya Bunge kuonyesha njia kwa kushughulikia sakata la umeme wa dharura uliokabidhiwa kwa kampuni ya Richmond Development LLC ya Marekani, sakata lililosababisha kuanguka kwa mawaziri watatu akiwamo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Wakati hayo yote yakiendelea, imefahamika kwamba Kamati ya Rais inayochunguza sekta ya madini, inatarajiwa kukabidhi ripoti yake wiki hii lakini Raia Mwema halikuweza kujua undani wa taarifa hiyo kutokana na usiri mkubwa wa yanayojiri ndani ya kamati hiyo.
 
Tutafika wakati ambapo utakuta kila unayemgusa either ana kasoro au ni FISADI.

Kuna mtu mmoja alisha sema pesa walizonazo viongozi wa nchi masikini ni kubwa muno hata hazilingani na viongozi wa nchi zilizoendelea pamoja na kwamba wao ni maili ktk kuomba misaada kutoka nchi zilizoendelea.

Ukisoma taarifa kama hizi huna haja ya kuendelea kuuliza. Conclusion yake inaonyesha sisi hatuna watawala hila tuna majambazi waliojivika kilemba cha utawala.
 
du mi hadi naogopa jamani siku zinavyozidi kuongezekaa..ndioo mambo yanapokuwa hadharani...jamani nyie tutafika wapi??jamani nyieee.......
 
Inafurahisha kuona Ikulu yetu imekuwa wazi kiasi cha Document za wakuu zinaanikwa ktk magazeti!!!!

Ipo siku tutaona picha wakuu wakiwa wamelala usingizi vyumbani huko ikulu nazo magazetini,hii ni hatari kuliko salama.
 
Inafurahisha kuona Ikulu yetu imekuwa wazi kiasi cha Document za wakuu zinaanikwa ktk magazeti!!!!

Ipo siku tutaona picha wakuu wakiwa wamelala usingizi vyumbani huko ikulu nazo magazetini,hii ni hatari kuliko salama.

Kwani ikulu ikiwa wazi wewe una wasiwasi gani maana hazikai pesa pale na hakuna mtu mwenye haja ya kuiba ikulu wasiwasi mkubwa nilio nao ni mbona benk kuu imekuwa wazi sana kiasi kila mtu anajichotea anavyotaka? au ndiyo maana kipindi fulani iliandikwa kuwa watendaji wote wa benk kuu wana uhusiano na viongozi wakuu wa serikali kwa hiyo hata wananchi walipe vipi kodi haisaidii maana kodi hizi wanagawana watu kama 20 hapo tanzania. na ndiyo maana kila anayeingia hapo ikulu hupagawa na huo mgawo na kusahau ahadi zote alizotoa kwa wananchi. wewe ulitegemea mkapa angefanya aliyoyafanya jinsi tulivyomwamini na tena alitukabidhi Mwalimu na akasema ni mr clean.au unaweza kufikiri unaota kwa mambo ambayo jk anayafanya sasa hivi maana kabla ya kuchaguliwa alikuwa ni kipenzi cha wananchi.angalia jinsi alivyowageuka you can't believe
 
SASA ni wazi, uongozi wa awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa ndio ulioshinikiza na kuidhinisha kuanzishwa kwa Kampuni ya Meremeta Gold, inayohusishwa na upotevu wa Sh bilioni 155, ndani ya Benki Kuu (BoT), imefahamika.

Habari za uhakika na nyaraka, zimethibitisha kwamba uongozi huo chini ya Mkapa ulihusika ama kushinikiza moja kwa moja mchakato wa kuanzishwa kwa Meremeta na hatimaye kuitafutia fedha za kufanyia kazi, fedha ambazo hata hivyo sasa zinahofiwa kupotea.

Tayari Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), Ludovick Utouh, ametamka kwamba ofisi yake haijawahi kukagua hesabu za Meremeta Gold, na kampuni hiyo tata haimo katika orodha ya makampuni yanayomilikiwa na Serikali ama Serikali kuwa na hisa.

Raia Mwema imeiona barua kutoka Ikulu, iliyoandikwa na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Matern Lumbanga, kwenda benki moja ya Uingereza, ikieleza kwamba Mkapa kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri mwaka 2000, ndiye aliyetoa idhini ya kuanzishwa kwa shughuli za uchimbani dhahabu katika eneo la Tembo na Buhemba, mkoani Mara.

Katika hali isiyo ya kawaida, Ikulu ndiyo iliyobeba jukumu la kuithibitisha na kuitambulisha Kampuni ya Meremeta kwa Deutch Bank AG London, iliyoko nchini Uingereza kwa nia ya kupata mkopo wa uendeshaji wa mgodi huo ambao kwa sasa umefungwa na kampuni hiyo kufilisiwa.

“Hii ni kuthibitisha kwamba tunafahamu kuwapo kwa hazina kubwa ya dhahabu nchini Tanzania ambayo haijalinufaisha Taifa na Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ilianzisha mradi wa Meremeta kwa nia ya kununua dhahabu kwa wachimbaji wadogo.

“Baadaye mwaka 2000, Rais (Mkapa) kupitia Baraza la Mawaziri aliazimia uchimbaji mkubwa wa chini ya ardhi katika eneo la Tembo na uchimbaji mwingine wa kawaida katika eneo la Buhemba, kaskazini mwa Tanzania,”

inaeleza barua hiyo ambayo kivuli chake kimechapishwa ukurasa wa kwanza wa toleo hili, iliyohitimisha kwa kusema kwamba mradi huo utakuwa na manufaa kwa Taifa.

Hata hivyo, katika barua hiyo inatajwa kampuni ya Nedcor Trade Services Limited ya Afrika Kusini kuwa ndiyo iliyotoa mkopo wa fedha za kuanzishia mradi huo chini ya usimamizi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, iliyokuwa inatajwa sana kuwa mmiliki wa mgodi huo awali kabla ya kubainika kuwapo kwa utata mkubwa.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, Utouh, alisema wazi kwamba Meremeta haimo katika orodha ya makampuni na mashirika ya umma ambayo yamewahi kukaguliwa na ofisi yake, na hivyo kuibua utata mwingine kwa kuwa huko nyuma kampuni hiyo imekuwa ikitajwa kuwa ya umma.

Utata huo unaongezwa na taarifa za kwamba Serikali kupitia Msajili wa Hazina ilitoa cheti ya kuithibitisha Meremeta kuwa kampuni ya umma tokea Oktoba mosi, 1997 baada ya kudaiwa kwamba Serikali ilikuwa na hisa katika kampuni hiyo, hisa zilizokuwa na zinazoendelea kushikiliwa na watendaji wakuu serikalini. Baadhi ya watendaji hao wamo serikalini na wengine sasa wako nje.

Habari zinasema kwamba tayari uchunguzi wa kina umekwisha kuanza kufuatilia hasa zilikokwenda fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni 155/- zikiwa ni nyingi zaidi ya zile zilizochotwa BoT kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA). Sakata la EPA linahusisha Sh bilioni 133/-.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari serikalini, uchunguzi huo umekwenda mbali zaidi baada ya watendaji wakuu ndani ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Wizara ya Ulinzi na JKT, kupata hisia za kuwapo kwa mikono michafu katika mradi wa Meremeta.

Habari zinasema sakata la Meremeta linaweza kuwa kubwa na zito zaidi kutokana na maelezo ya uwezekano wa kuwapo wahusika wanaofahamika duniani katika biashara chafu na hivyo kuibua mjadala mwingine mkubwa utakaovuka nje ya mipaka ya Tanzania.

Kampuni ya Nedcor Trade Services Limited ya Afrika Kusini, inaelezwa kuwa na uhusiano na benki ya Nedbank ya Afrika Kusini ambako sehemu ya fedha hizo zilipelekwa kutoka BoT. Baadhi ya watumishi wa benki hiyo wamekuwa wakitajwa kuwa wakurugenzi wa kampuni nyingine tata ya Deep Green Finance Limited, ambayo sasa haipo.

Deep Green Finance Limited ilisajiliwa nchini, ikachota fedha kutoka BoT, kabla ya kufilisiwa bila ya maelezo ya kutosha ya madhumuni hasa ya kuanzishwa kwa kampuni hiyo katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2005.

Kashfa ya Meremeta inaelezwa kuwa kubwa zaidi ya ile ya EPA kutokana na kwamba uwezekano wa kurejesha fedha hizo ni mdogo kutokana na kwamba ziliingia katika mkondo unaoihusisha zaidi Serikali yenyewe na watendaji wake na wafanyabiashara wa kimataifa.

Tayari Kamati ya Rais inayochunguza sekta ya Madini, chini ya uongozi wa Jaji Mark Bomani, imeufuatilia mradi huo kwa kwenda Buhemba na pia kuwaita watendaji kadhaa wa Serikali akiwamo Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, ambaye inadaiwa taarifa hizo zimemshitua.

Kwa mujibu wa Gavana Profesa Ndulu, kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za malipo ya fedha hizo za Meremeta ambazo ni zaidi ya zile za EPA zilizolipwa kwa utaratibu wa Dhamana za Hazina (Treasury Bonds).

Jaji Bomani aliliambia Raia Mwema hivi karibuni kwamba Kamati yake haitaficha kitu na kwamba baada ya kutembelea Buhemba na kuchunguza mambo yanayohusiana na mgodi huo, itatoa mapendekezo yake katika ripoti.

Baadhi ya wakurugenzi wa Kampuni ya Meremeta ambao wanaelezwa kuwa katika nafasi hizo kutokana na nyadhifa zao bado wanaendelea kushikilia hisa hizo akiwamo Gavana wa zamani wa Benki Kuu, Dk. Daudi Ballali, ambaye ajira yake ilisitishwa na Rais Jakaya Kikwete.

Tayari kuna habari kwamba kumekuwapo na juhudi za makusudi zinazofanywa na baadhi ya watendaji serikalini ambao wanajipanga kuzuia kuanikwa kwa ufisadi huo mkubwa.

Fedha hizo ambazo zilibadilishwa kuwa Dola za Marekani 131,736,628.73 kwa maelekezo yaliyotolewa Desemba 20, 2005, siku moja kabla ya kuapishwa kwa Rais Jakaya Kikwete, zilihamishwa kwenda Afrika Kusini na kuingizwa Nedbank, na nyingine kuingizwa katika akaunti za kampuni ya Tangold na Meremeta.

Taarifa za wakaguzi zinaonyesha kwamba baada ya ununuzi huo wa dhamana, Benki Kuu ilizibadilisha sehemu ya dhamana hizo kuwa dola za Marekani 118,396,460.36 ambazo zilipelekwa kwenye akaunti moja isiyojulikana ya Nedbank Ltd. ya Afrika Kusini, benki hiyo ikiwa imezipokea fedha hizo kupitia HSB Bank ya New York, Marekani zikitajwa kuwa malipo ya madeni ya kampuni mufilisi ya Meremeta Ltd.

Nyaraka ambazo Raia Mwema imeziona zinaonyesha kwamba sehemu nyingine ya fedha hizo zipatazo Dola za Marekani 13,736,628.73 zililipwa kwa kampuni ya TANGOLD kwenye akaunti ya kampuni hiyo iliyoko Benki ya NBC Corporate Branch, Dar es Salaam.

Mbali ya kamati ya madini na wakaguzi, kwa nyakati tofauti, kuhoji malipo hayo, bado usiri na juhudi kubwa za kufunika masuala hayo zimekuwa zikiendelea kufanywa.

Mwaka jana Mbunge wa Karatu Dk. Willibrod Slaa (CHADEMA), aliliingiza suala hilo katika hoja yake iliyokuja kugonga mwamba baadaye.

Katika hoja yake hiyo, Dk. Slaa alibainisha kwamba Meremeta Ltd. ni kampuni binafsi ya kigeni iliyoandikishwa Agosti 19, 1997 katika kisiwa cha Isle of Man nchini Uingereza na kupewa namba ya usajili 3424504, ikimilikiwa na TRIENNEX (PTY) LTD ya Afrika Kusini yenye asilimia 50 ya hisa za kawaida na Msajili wa Hazina (Treasury Registrar) akiwa na asilimia 50.

Kwa upande wa Tanzania, Dk. Slaa alisema Meremeta ilipewa Hati ya kutimiza masharti (Certificate of Compliance) Oktoba, 1997 lakini akasema kwamba Meremeta ilifilisiwa Uingereza Januari 2006.

Hata hivyo, Dk. Slaa ameeleza kwamba pamoja na kampuni hiyo kufilisiwa nchini Uingereza, hakuna ushahidi kuwa kwa upande wa Tanzania kampuni hiyo imefilisiwa au la kutokana na kutajwa katika marejeo mbalimbali kuwa moja ya makampuni yanayozalisha dhahabu.

“Taarifa na takwimu muhimu kuhusu Sekta za Nishati na Madini’, ya Julai, 2007, inaonyesha kuwa Meremeta bado inafanya kazi, na inazalisha tani 2.27 za dhahabu. Kama Serikali inasema Meremeta imefilisiwa na mali zake kuhamishiwa TANGOLD hali hii inaelezwa vipi? Taarifa hizi za utata zinaashiria nini?” alihoji Dk. Slaa.

Maelezo mengine yanayoibua utata zaidi na ambao Kamati ya Rais inayopitia mikataba ya madini itapata wakati mgumu kuitolea taarifa ni kuhusu Meremeta kudaiwa kuwa ni kampuni iliyoanzishwa kwa lengo la kusaidia JWTZ, Kikosi cha Nyumbu wakati ikiwa imeandikishwa nje ya nchi.

Taarifa ya awali ya wakaguzi waliokagua BoT, Juni 2006, iliibua sakata hilo la Meremeta pamoja na kashfa nyingine lakini haikuweza kufahamika ripoti hiyo ya wakaguzi ilivyoyeyuka na kutoanikwa hadharani kabla ya wakaguzi wengine wa nje kuibua suala la EPA pekee miongoni mwa uchafu mwingi ndani ya BoT na serikalini.

Taarifa hiyo ya wakaguzi ilibainisha kwamba Serikali ilitoa fedha hizo kiasi cha Sh. bilioni 155 kwa njia ya dhamana ya hazina ambayo inatakiwa kulipiwa riba ya asilimia 14.92 kila mwaka lakini hakukuwa na makubaliano yoyote rasmi kati ya Serikali na Meremeta hali inayoibua zaidi utata na kuonyesha hakuna njia yoyote ya kuweza kuzipata fedha hizo.

Ndani ya BoT bado kuna mianya mingi ambayo huenda ikaendelea kuibuka siku hadi siku hususan baada ya Bunge kuonyesha njia kwa kushughulikia sakata la umeme wa dharura uliokabidhiwa kwa kampuni ya Richmond Development LLC ya Marekani, sakata lililosababisha kuanguka kwa mawaziri watatu akiwamo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Wakati hayo yote yakiendelea, imefahamika kwamba Kamati ya Rais inayochunguza sekta ya madini, inatarajiwa kukabidhi ripoti yake wiki hii lakini Raia Mwema halikuweza kujua undani wa taarifa hiyo kutokana na usiri mkubwa wa yanayojiri ndani ya kamati hiyo.


http://www.raiamwema.co.tz/08/04/09/1.php

Mimi naona nchi hii iuzwe kila mtu achukue chake, maana naona ni wachache tu wanachukua chao, sisi je?
 
SASA ni wazi, uongozi wa awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa ndio ulioshinikiza na kuidhinisha kuanzishwa kwa Kampuni ya Meremeta Gold, inayohusishwa na upotevu wa Sh bilioni 155, ndani ya Benki Kuu (BoT), imefahamika.

Habari za uhakika na nyaraka, zimethibitisha kwamba uongozi huo chini ya Mkapa ulihusika ama kushinikiza moja kwa moja mchakato wa kuanzishwa kwa Meremeta na hatimaye kuitafutia fedha za kufanyia kazi, fedha ambazo hata hivyo sasa zinahofiwa kupotea.

Tayari Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), Ludovick Utouh, ametamka kwamba ofisi yake haijawahi kukagua hesabu za Meremeta Gold, na kampuni hiyo tata haimo katika orodha ya makampuni yanayomilikiwa na Serikali ama Serikali kuwa na hisa.

Raia Mwema imeiona barua kutoka Ikulu, iliyoandikwa na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Matern Lumbanga, kwenda benki moja ya Uingereza, ikieleza kwamba Mkapa kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri mwaka 2000, ndiye aliyetoa idhini ya kuanzishwa kwa shughuli za uchimbani dhahabu katika eneo la Tembo na Buhemba, mkoani Mara.

Katika hali isiyo ya kawaida, Ikulu ndiyo iliyobeba jukumu la kuithibitisha na kuitambulisha Kampuni ya Meremeta kwa Deutch Bank AG London, iliyoko nchini Uingereza kwa nia ya kupata mkopo wa uendeshaji wa mgodi huo ambao kwa sasa umefungwa na kampuni hiyo kufilisiwa.

“Hii ni kuthibitisha kwamba tunafahamu kuwapo kwa hazina kubwa ya dhahabu nchini Tanzania ambayo haijalinufaisha Taifa na Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ilianzisha mradi wa Meremeta kwa nia ya kununua dhahabu kwa wachimbaji wadogo.

“Baadaye mwaka 2000, Rais (Mkapa) kupitia Baraza la Mawaziri aliazimia uchimbaji mkubwa wa chini ya ardhi katika eneo la Tembo na uchimbaji mwingine wa kawaida katika eneo la Buhemba, kaskazini mwa Tanzania,”

inaeleza barua hiyo ambayo kivuli chake kimechapishwa ukurasa wa kwanza wa toleo hili, iliyohitimisha kwa kusema kwamba mradi huo utakuwa na manufaa kwa Taifa.

Hata hivyo, katika barua hiyo inatajwa kampuni ya Nedcor Trade Services Limited ya Afrika Kusini kuwa ndiyo iliyotoa mkopo wa fedha za kuanzishia mradi huo chini ya usimamizi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, iliyokuwa inatajwa sana kuwa mmiliki wa mgodi huo awali kabla ya kubainika kuwapo kwa utata mkubwa.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, Utouh, alisema wazi kwamba Meremeta haimo katika orodha ya makampuni na mashirika ya umma ambayo yamewahi kukaguliwa na ofisi yake, na hivyo kuibua utata mwingine kwa kuwa huko nyuma kampuni hiyo imekuwa ikitajwa kuwa ya umma.

Utata huo unaongezwa na taarifa za kwamba Serikali kupitia Msajili wa Hazina ilitoa cheti ya kuithibitisha Meremeta kuwa kampuni ya umma tokea Oktoba mosi, 1997 baada ya kudaiwa kwamba Serikali ilikuwa na hisa katika kampuni hiyo, hisa zilizokuwa na zinazoendelea kushikiliwa na watendaji wakuu serikalini. Baadhi ya watendaji hao wamo serikalini na wengine sasa wako nje.

Habari zinasema kwamba tayari uchunguzi wa kina umekwisha kuanza kufuatilia hasa zilikokwenda fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni 155/- zikiwa ni nyingi zaidi ya zile zilizochotwa BoT kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA). Sakata la EPA linahusisha Sh bilioni 133/-.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari serikalini, uchunguzi huo umekwenda mbali zaidi baada ya watendaji wakuu ndani ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Wizara ya Ulinzi na JKT, kupata hisia za kuwapo kwa mikono michafu katika mradi wa Meremeta.

Habari zinasema sakata la Meremeta linaweza kuwa kubwa na zito zaidi kutokana na maelezo ya uwezekano wa kuwapo wahusika wanaofahamika duniani katika biashara chafu na hivyo kuibua mjadala mwingine mkubwa utakaovuka nje ya mipaka ya Tanzania.

Kampuni ya Nedcor Trade Services Limited ya Afrika Kusini, inaelezwa kuwa na uhusiano na benki ya Nedbank ya Afrika Kusini ambako sehemu ya fedha hizo zilipelekwa kutoka BoT. Baadhi ya watumishi wa benki hiyo wamekuwa wakitajwa kuwa wakurugenzi wa kampuni nyingine tata ya Deep Green Finance Limited, ambayo sasa haipo.

Deep Green Finance Limited ilisajiliwa nchini, ikachota fedha kutoka BoT, kabla ya kufilisiwa bila ya maelezo ya kutosha ya madhumuni hasa ya kuanzishwa kwa kampuni hiyo katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2005.

Kashfa ya Meremeta inaelezwa kuwa kubwa zaidi ya ile ya EPA kutokana na kwamba uwezekano wa kurejesha fedha hizo ni mdogo kutokana na kwamba ziliingia katika mkondo unaoihusisha zaidi Serikali yenyewe na watendaji wake na wafanyabiashara wa kimataifa.

Tayari Kamati ya Rais inayochunguza sekta ya Madini, chini ya uongozi wa Jaji Mark Bomani, imeufuatilia mradi huo kwa kwenda Buhemba na pia kuwaita watendaji kadhaa wa Serikali akiwamo Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, ambaye inadaiwa taarifa hizo zimemshitua.

Kwa mujibu wa Gavana Profesa Ndulu, kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za malipo ya fedha hizo za Meremeta ambazo ni zaidi ya zile za EPA zilizolipwa kwa utaratibu wa Dhamana za Hazina (Treasury Bonds).

Jaji Bomani aliliambia Raia Mwema hivi karibuni kwamba Kamati yake haitaficha kitu na kwamba baada ya kutembelea Buhemba na kuchunguza mambo yanayohusiana na mgodi huo, itatoa mapendekezo yake katika ripoti.

Baadhi ya wakurugenzi wa Kampuni ya Meremeta ambao wanaelezwa kuwa katika nafasi hizo kutokana na nyadhifa zao bado wanaendelea kushikilia hisa hizo akiwamo Gavana wa zamani wa Benki Kuu, Dk. Daudi Ballali, ambaye ajira yake ilisitishwa na Rais Jakaya Kikwete.

Tayari kuna habari kwamba kumekuwapo na juhudi za makusudi zinazofanywa na baadhi ya watendaji serikalini ambao wanajipanga kuzuia kuanikwa kwa ufisadi huo mkubwa.

Fedha hizo ambazo zilibadilishwa kuwa Dola za Marekani 131,736,628.73 kwa maelekezo yaliyotolewa Desemba 20, 2005, siku moja kabla ya kuapishwa kwa Rais Jakaya Kikwete, zilihamishwa kwenda Afrika Kusini na kuingizwa Nedbank, na nyingine kuingizwa katika akaunti za kampuni ya Tangold na Meremeta.

Taarifa za wakaguzi zinaonyesha kwamba baada ya ununuzi huo wa dhamana, Benki Kuu ilizibadilisha sehemu ya dhamana hizo kuwa dola za Marekani 118,396,460.36 ambazo zilipelekwa kwenye akaunti moja isiyojulikana ya Nedbank Ltd. ya Afrika Kusini, benki hiyo ikiwa imezipokea fedha hizo kupitia HSB Bank ya New York, Marekani zikitajwa kuwa malipo ya madeni ya kampuni mufilisi ya Meremeta Ltd.

Nyaraka ambazo Raia Mwema imeziona zinaonyesha kwamba sehemu nyingine ya fedha hizo zipatazo Dola za Marekani 13,736,628.73 zililipwa kwa kampuni ya TANGOLD kwenye akaunti ya kampuni hiyo iliyoko Benki ya NBC Corporate Branch, Dar es Salaam.

Mbali ya kamati ya madini na wakaguzi, kwa nyakati tofauti, kuhoji malipo hayo, bado usiri na juhudi kubwa za kufunika masuala hayo zimekuwa zikiendelea kufanywa.

Mwaka jana Mbunge wa Karatu Dk. Willibrod Slaa (CHADEMA), aliliingiza suala hilo katika hoja yake iliyokuja kugonga mwamba baadaye.

Katika hoja yake hiyo, Dk. Slaa alibainisha kwamba Meremeta Ltd. ni kampuni binafsi ya kigeni iliyoandikishwa Agosti 19, 1997 katika kisiwa cha Isle of Man nchini Uingereza na kupewa namba ya usajili 3424504, ikimilikiwa na TRIENNEX (PTY) LTD ya Afrika Kusini yenye asilimia 50 ya hisa za kawaida na Msajili wa Hazina (Treasury Registrar) akiwa na asilimia 50.

Kwa upande wa Tanzania, Dk. Slaa alisema Meremeta ilipewa Hati ya kutimiza masharti (Certificate of Compliance) Oktoba, 1997 lakini akasema kwamba Meremeta ilifilisiwa Uingereza Januari 2006.

Hata hivyo, Dk. Slaa ameeleza kwamba pamoja na kampuni hiyo kufilisiwa nchini Uingereza, hakuna ushahidi kuwa kwa upande wa Tanzania kampuni hiyo imefilisiwa au la kutokana na kutajwa katika marejeo mbalimbali kuwa moja ya makampuni yanayozalisha dhahabu.

“Taarifa na takwimu muhimu kuhusu Sekta za Nishati na Madini’, ya Julai, 2007, inaonyesha kuwa Meremeta bado inafanya kazi, na inazalisha tani 2.27 za dhahabu. Kama Serikali inasema Meremeta imefilisiwa na mali zake kuhamishiwa TANGOLD hali hii inaelezwa vipi? Taarifa hizi za utata zinaashiria nini?” alihoji Dk. Slaa.

Maelezo mengine yanayoibua utata zaidi na ambao Kamati ya Rais inayopitia mikataba ya madini itapata wakati mgumu kuitolea taarifa ni kuhusu Meremeta kudaiwa kuwa ni kampuni iliyoanzishwa kwa lengo la kusaidia JWTZ, Kikosi cha Nyumbu wakati ikiwa imeandikishwa nje ya nchi.

Taarifa ya awali ya wakaguzi waliokagua BoT, Juni 2006, iliibua sakata hilo la Meremeta pamoja na kashfa nyingine lakini haikuweza kufahamika ripoti hiyo ya wakaguzi ilivyoyeyuka na kutoanikwa hadharani kabla ya wakaguzi wengine wa nje kuibua suala la EPA pekee miongoni mwa uchafu mwingi ndani ya BoT na serikalini.

Taarifa hiyo ya wakaguzi ilibainisha kwamba Serikali ilitoa fedha hizo kiasi cha Sh. bilioni 155 kwa njia ya dhamana ya hazina ambayo inatakiwa kulipiwa riba ya asilimia 14.92 kila mwaka lakini hakukuwa na makubaliano yoyote rasmi kati ya Serikali na Meremeta hali inayoibua zaidi utata na kuonyesha hakuna njia yoyote ya kuweza kuzipata fedha hizo.

Ndani ya BoT bado kuna mianya mingi ambayo huenda ikaendelea kuibuka siku hadi siku hususan baada ya Bunge kuonyesha njia kwa kushughulikia sakata la umeme wa dharura uliokabidhiwa kwa kampuni ya Richmond Development LLC ya Marekani, sakata lililosababisha kuanguka kwa mawaziri watatu akiwamo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Wakati hayo yote yakiendelea, imefahamika kwamba Kamati ya Rais inayochunguza sekta ya madini, inatarajiwa kukabidhi ripoti yake wiki hii lakini Raia Mwema halikuweza kujua undani wa taarifa hiyo kutokana na usiri mkubwa wa yanayojiri ndani ya kamati hiyo.


http://www.raiamwema.co.tz/08/04/09/1.php

Mimi naona nchi hii iuzwe kila mtu achukue chake, maana naona ni wachache tu wanachukua chao, sisi je?



Inasikitisha kuona kuwa hata ufisadi wa EPA bado ni mdogo, ukilinganisha na yanayoendelea kuibuka. Sijui tukipekuwa zaidi files za BoT tutakuta nini? Naona hivi sasa inahitajika independent auditing mpya ifanyike kwa amri ya Bunge na sio tena serikali.
 
Nani wa kutoa amri huyo wakati wote hao ni wezi, rpstam kataka kuongea hukohuko bungeni na amepigwa chini, bunge lipi hasa litakalo amuru?
 
Wale waandishi wa Vitabu vya ukombozi wa tanzania itakuwa siyo Busara kama Jina la Dr. Slaa litakosa ktk Vitabu hivyo. Huyu ni Mtanzania ambaye anatakiwa kuwekwa ktk Historia ya Taifa kwa kusimama kidete bila kutetereka na kutoa kauli nzito juu ya Mafisadi.

Kila alicho kisema sasa hivi kinadhihirika ni kweli.

Mungu ambariki mpiganaji huyu. Maana ilikuwa rahisi kupigana na Mkoloni Mweupe kuliko Mkoloni Mweusi.
 
Ikulu ya Ben Mkapa iliibeba Meremeta

Mwandishi Wetu Aprili 9, 2008 (www.raiamwema.co.tz



SASA ni wazi, uongozi wa awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa ndio ulioshinikiza na kuidhinisha kuanzishwa kwa Kampuni ya Meremeta Gold, inayohusishwa na upotevu wa Sh bilioni 155, ndani ya Benki Kuu (BoT), imefahamika.

Habari za uhakika na nyaraka, zimethibitisha kwamba uongozi huo chini ya Mkapa ulihusika ama kushinikiza moja kwa moja mchakato wa kuanzishwa kwa Meremeta na hatimaye kuitafutia fedha za kufanyia kazi, fedha ambazo hata hivyo sasa zinahofiwa kupotea.

Tayari Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), Ludovick Utouh, ametamka kwamba ofisi yake haijawahi kukagua hesabu za Meremeta Gold, na kampuni hiyo tata haimo katika orodha ya makampuni yanayomilikiwa na Serikali ama Serikali kuwa na hisa.

Raia Mwema imeiona barua kutoka Ikulu, iliyoandikwa na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Matern Lumbanga, kwenda benki moja ya Uingereza, ikieleza kwamba Mkapa kupitia kikao cha Baraza la Mawaziri mwaka 2000, ndiye aliyetoa idhini ya kuanzishwa kwa shughuli za uchimbani dhahabu katika eneo la Tembo na Buhemba, mkoani Mara.

Katika hali isiyo ya kawaida, Ikulu ndiyo iliyobeba jukumu la kuithibitisha na kuitambulisha Kampuni ya Meremeta kwa Deutch Bank AG London, iliyoko nchini Uingereza kwa nia ya kupata mkopo wa uendeshaji wa mgodi huo ambao kwa sasa umefungwa na kampuni hiyo kufilisiwa.

“Hii ni kuthibitisha kwamba tunafahamu kuwapo kwa hazina kubwa ya dhahabu nchini Tanzania ambayo haijalinufaisha Taifa na Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ilianzisha mradi wa Meremeta kwa nia ya kununua dhahabu kwa wachimbaji wadogo.

“Baadaye mwaka 2000, Rais (Mkapa) kupitia Baraza la Mawaziri aliazimia uchimbaji mkubwa wa chini ya ardhi katika eneo la Tembo na uchimbaji mwingine wa kawaida katika eneo la Buhemba, kaskazini mwa Tanzania,”

inaeleza barua hiyo ambayo kivuli chake kimechapishwa ukurasa wa kwanza wa toleo hili, iliyohitimisha kwa kusema kwamba mradi huo utakuwa na manufaa kwa Taifa.

Hata hivyo, katika barua hiyo inatajwa kampuni ya Nedcor Trade Services Limited ya Afrika Kusini kuwa ndiyo iliyotoa mkopo wa fedha za kuanzishia mradi huo chini ya usimamizi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, iliyokuwa inatajwa sana kuwa mmiliki wa mgodi huo awali kabla ya kubainika kuwapo kwa utata mkubwa.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, Utouh, alisema wazi kwamba Meremeta haimo katika orodha ya makampuni na mashirika ya umma ambayo yamewahi kukaguliwa na ofisi yake, na hivyo kuibua utata mwingine kwa kuwa huko nyuma kampuni hiyo imekuwa ikitajwa kuwa ya umma.

Utata huo unaongezwa na taarifa za kwamba Serikali kupitia Msajili wa Hazina ilitoa cheti ya kuithibitisha Meremeta kuwa kampuni ya umma tokea Oktoba mosi, 1997 baada ya kudaiwa kwamba Serikali ilikuwa na hisa katika kampuni hiyo, hisa zilizokuwa na zinazoendelea kushikiliwa na watendaji wakuu serikalini. Baadhi ya watendaji hao wamo serikalini na wengine sasa wako nje.

Habari zinasema kwamba tayari uchunguzi wa kina umekwisha kuanza kufuatilia hasa zilikokwenda fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni 155/- zikiwa ni nyingi zaidi ya zile zilizochotwa BoT kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA). Sakata la EPA linahusisha Sh bilioni 133/-.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari serikalini, uchunguzi huo umekwenda mbali zaidi baada ya watendaji wakuu ndani ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Wizara ya Ulinzi na JKT, kupata hisia za kuwapo kwa mikono michafu katika mradi wa Meremeta.

Habari zinasema sakata la Meremeta linaweza kuwa kubwa na zito zaidi kutokana na maelezo ya uwezekano wa kuwapo wahusika wanaofahamika duniani katika biashara chafu na hivyo kuibua mjadala mwingine mkubwa utakaovuka nje ya mipaka ya Tanzania.

Kampuni ya Nedcor Trade Services Limited ya Afrika Kusini, inaelezwa kuwa na uhusiano na benki ya Nedbank ya Afrika Kusini ambako sehemu ya fedha hizo zilipelekwa kutoka BoT. Baadhi ya watumishi wa benki hiyo wamekuwa wakitajwa kuwa wakurugenzi wa kampuni nyingine tata ya Deep Green Finance Limited, ambayo sasa haipo.

Deep Green Finance Limited ilisajiliwa nchini, ikachota fedha kutoka BoT, kabla ya kufilisiwa bila ya maelezo ya kutosha ya madhumuni hasa ya kuanzishwa kwa kampuni hiyo katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2005.

Kashfa ya Meremeta inaelezwa kuwa kubwa zaidi ya ile ya EPA kutokana na kwamba uwezekano wa kurejesha fedha hizo ni mdogo kutokana na kwamba ziliingia katika mkondo unaoihusisha zaidi Serikali yenyewe na watendaji wake na wafanyabiashara wa kimataifa.

Tayari Kamati ya Rais inayochunguza sekta ya Madini, chini ya uongozi wa Jaji Mark Bomani, imeufuatilia mradi huo kwa kwenda Buhemba na pia kuwaita watendaji kadhaa wa Serikali akiwamo Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, ambaye inadaiwa taarifa hizo zimemshitua.

Kwa mujibu wa Gavana Profesa Ndulu, kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za malipo ya fedha hizo za Meremeta ambazo ni zaidi ya zile za EPA zilizolipwa kwa utaratibu wa Dhamana za Hazina (Treasury Bonds).

Jaji Bomani aliliambia Raia Mwema hivi karibuni kwamba Kamati yake haitaficha kitu na kwamba baada ya kutembelea Buhemba na kuchunguza mambo yanayohusiana na mgodi huo, itatoa mapendekezo yake katika ripoti.

Baadhi ya wakurugenzi wa Kampuni ya Meremeta ambao wanaelezwa kuwa katika nafasi hizo kutokana na nyadhifa zao bado wanaendelea kushikilia hisa hizo akiwamo Gavana wa zamani wa Benki Kuu, Dk. Daudi Ballali, ambaye ajira yake ilisitishwa na Rais Jakaya Kikwete.

Tayari kuna habari kwamba kumekuwapo na juhudi za makusudi zinazofanywa na baadhi ya watendaji serikalini ambao wanajipanga kuzuia kuanikwa kwa ufisadi huo mkubwa.

Fedha hizo ambazo zilibadilishwa kuwa Dola za Marekani 131,736,628.73 kwa maelekezo yaliyotolewa Desemba 20, 2005, siku moja kabla ya kuapishwa kwa Rais Jakaya Kikwete, zilihamishwa kwenda Afrika Kusini na kuingizwa Nedbank, na nyingine kuingizwa katika akaunti za kampuni ya Tangold na Meremeta.

Taarifa za wakaguzi zinaonyesha kwamba baada ya ununuzi huo wa dhamana, Benki Kuu ilizibadilisha sehemu ya dhamana hizo kuwa dola za Marekani 118,396,460.36 ambazo zilipelekwa kwenye akaunti moja isiyojulikana ya Nedbank Ltd. ya Afrika Kusini, benki hiyo ikiwa imezipokea fedha hizo kupitia HSB Bank ya New York, Marekani zikitajwa kuwa malipo ya madeni ya kampuni mufilisi ya Meremeta Ltd.

Nyaraka ambazo Raia Mwema imeziona zinaonyesha kwamba sehemu nyingine ya fedha hizo zipatazo Dola za Marekani 13,736,628.73 zililipwa kwa kampuni ya TANGOLD kwenye akaunti ya kampuni hiyo iliyoko Benki ya NBC Corporate Branch, Dar es Salaam.

Mbali ya kamati ya madini na wakaguzi, kwa nyakati tofauti, kuhoji malipo hayo, bado usiri na juhudi kubwa za kufunika masuala hayo zimekuwa zikiendelea kufanywa.

Mwaka jana Mbunge wa Karatu Dk. Willibrod Slaa (CHADEMA), aliliingiza suala hilo katika hoja yake iliyokuja kugonga mwamba baadaye.

Katika hoja yake hiyo, Dk. Slaa alibainisha kwamba Meremeta Ltd. ni kampuni binafsi ya kigeni iliyoandikishwa Agosti 19, 1997 katika kisiwa cha Isle of Man nchini Uingereza na kupewa namba ya usajili 3424504, ikimilikiwa na TRIENNEX (PTY) LTD ya Afrika Kusini yenye asilimia 50 ya hisa za kawaida na Msajili wa Hazina (Treasury Registrar) akiwa na asilimia 50.

Kwa upande wa Tanzania, Dk. Slaa alisema Meremeta ilipewa Hati ya kutimiza masharti (Certificate of Compliance) Oktoba, 1997 lakini akasema kwamba Meremeta ilifilisiwa Uingereza Januari 2006.

Hata hivyo, Dk. Slaa ameeleza kwamba pamoja na kampuni hiyo kufilisiwa nchini Uingereza, hakuna ushahidi kuwa kwa upande wa Tanzania kampuni hiyo imefilisiwa au la kutokana na kutajwa katika marejeo mbalimbali kuwa moja ya makampuni yanayozalisha dhahabu.

“Taarifa na takwimu muhimu kuhusu Sekta za Nishati na Madini’, ya Julai, 2007, inaonyesha kuwa Meremeta bado inafanya kazi, na inazalisha tani 2.27 za dhahabu. Kama Serikali inasema Meremeta imefilisiwa na mali zake kuhamishiwa TANGOLD hali hii inaelezwa vipi? Taarifa hizi za utata zinaashiria nini?” alihoji Dk. Slaa.

Maelezo mengine yanayoibua utata zaidi na ambao Kamati ya Rais inayopitia mikataba ya madini itapata wakati mgumu kuitolea taarifa ni kuhusu Meremeta kudaiwa kuwa ni kampuni iliyoanzishwa kwa lengo la kusaidia JWTZ, Kikosi cha Nyumbu wakati ikiwa imeandikishwa nje ya nchi.

Taarifa ya awali ya wakaguzi waliokagua BoT, Juni 2006, iliibua sakata hilo la Meremeta pamoja na kashfa nyingine lakini haikuweza kufahamika ripoti hiyo ya wakaguzi ilivyoyeyuka na kutoanikwa hadharani kabla ya wakaguzi wengine wa nje kuibua suala la EPA pekee miongoni mwa uchafu mwingi ndani ya BoT na serikalini.

Taarifa hiyo ya wakaguzi ilibainisha kwamba Serikali ilitoa fedha hizo kiasi cha Sh. bilioni 155 kwa njia ya dhamana ya hazina ambayo inatakiwa kulipiwa riba ya asilimia 14.92 kila mwaka lakini hakukuwa na makubaliano yoyote rasmi kati ya Serikali na Meremeta hali inayoibua zaidi utata na kuonyesha hakuna njia yoyote ya kuweza kuzipata fedha hizo.

Ndani ya BoT bado kuna mianya mingi ambayo huenda ikaendelea kuibuka siku hadi siku hususan baada ya Bunge kuonyesha njia kwa kushughulikia sakata la umeme wa dharura uliokabidhiwa kwa kampuni ya Richmond Development LLC ya Marekani, sakata lililosababisha kuanguka kwa mawaziri watatu akiwamo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Wakati hayo yote yakiendelea, imefahamika kwamba Kamati ya Rais inayochunguza sekta ya madini, inatarajiwa kukabidhi ripoti yake wiki hii lakini Raia Mwema halikuweza kujua undani wa taarifa hiyo kutokana na usiri mkubwa wa yanayojiri ndani ya kamati hiyo.
 
Revealed: Meremeta Gold was an offshore company
By The Citizen Team

Meremeta Gold, the firm that was paid a whopping Sh155 billion by the Bank of Tanzania in unclear circumstances in mid last year, was an offshore company, registered in United Kingdom in 1997, The Citizen can reveal today.

That means that chances of recovering the taxpayers� money and the necessary taxes up to the date it closed shop are negligible.


A senior Cabinet minister told The Citizen in Dar es Salaam yesterday that �since it was registered as an offshore company� it would be difficult to recover the billions it had been paid.

Speaking on condition of anonymity, the minister said: �First of all, I am surprised that an offshore company was allowed to operate in this country�but the clear point is that any offshore company is untraceable.�

Legal experts concurred, saying that it would be difficult for the Government to recover the Sh155billion, due to the tough protection accorded to such business entities.


An offshore company does not conduct substantial business in its country of incorporation. Such firms are sometimes known as non-resident companies.

But the Companies Act 212, states clearly that offshore company can only be registered and given a certificate of compliance after fulfilling certain conditions, including renunciation of its original registration.

The Act prohibits offshore companies from operating in Tanzania unless they change and indicate that they will not be protected by offshore registration procedures.


Strangely, the Government registered Meremeta Gold. Asked why the State entered into partnership with an offshore company, the Minister for Energy and Minerals, Mr William Ngeleja, said: �The Government wasn�t aware until mid last year after the company went bankrupt.�

And fresh details show that the company wasn�t owned by Tanzania People�s Defence Forces (TPDF) and the South African Army, as was alleged in 1997, when its existence became public.

The firm started as an army project managed jointly by TPDF and the South African Army, to mine and export gold, before becoming a ghost company that looted about Sh155 billion from the public coffers.

Contacted yesterday, the Minister for Defence, Dr Hussein Mwinyi, said: �I am not familiar with the issue because I wasn�t in office during that period.�

He asked The Citizen to send him written questions by this morning.
The amount stashed away by the defunct company can build 500 kilometres of tarmac road or 7,500 classrooms at the cost of Sh20 million for each class.

Meremeta, the Kiswahili word for glitter, will not be glittering when the defunct gold company scandal is raised in Parliament.

After the controversial Richmond tender and External Payments Arrears (EPA) scandals, opposition and ruling party MPs believe that Meremeta poses a serious threat to the integrity of previous regime and the current administration.

Musoma Rural MP Nimrod Mkono of CCM plans to table a private�s member�s motion to establish who the real owner of Meremeta Gold is and why was the firm paid billions of shillings after going bankrupt.

The details, which are part of an investigation report sent to the donor community recently by the opposition parties led by Chadema�s Dr Willibrod Slaa, says that the defunct gold company was registered as an offshore company on August 19, 1997, and given a registration No. 3424504.

The reasons for the formation of offshore firms are privacy, asset protection, tax savings, lawsuit protection, flexible business laws and confidentiality
The opposition parties� report, which was made available to The Citizen, says that the company was then registered in Tanzania on October 3, 1997 as a branch of a foreign company and given a Certificate of Compliance No.32755.

On Sunday, our sister paper, Mwananchi Jumapili, quoted Mr Mkono as saying that the Government had been hesitating to reveal the real owners of the company that has cost taxpayers billions of shillings.

On Monday, speaking with The Citizen from the US: Mr Mkono said: �I have evidence that this ghost company pocketed a total of Sh181 billion and yet nobody wants to speak about it.�
This amount is more than what CAG revealed in the 2005/6 auditing report.


�If we are investigating EPA and Richmond why not Meremeta,� asked the Musoma Rural MP.

But the available details show that 50 per cent of the company�s shares were owned by the Registrar of Treasury, and 50 per cent by South Africa�s Trienex (PTY) Co Ltd.


Yesterday, Mr Ngeleja said: �The Government issued a statement on shareholders of Meremeta in June last year and clearly explained the profile of the company and why it had to be liquidated�I�m working on the issue and I will get back to you later in the day,�


According to CAG report, BoT paid Meremeta debts amounting to Sh155 billion for unknown reasons.

The CAG revealed that a total of $118,396,460.36 was transferred to an unknown account of Nedbank Ltd of South Africa through HSB of New York, in 2005/6. The balance of $13,736,628.73 was paid to Tangold account with NBC Corporate Branch Dar-Es-Salaam.

According to available details, Tangold Ltd is a foreign registered company that was registered again as an offshore company in Mauritus (No C 205006121) dated 8 April 2005 and subsequently registered in Tanzania as a branch of foreign company with Certificate of Compliance No 55661 dated 20th February 2006.

During last year�s budget session, former Energy and Minerals minister Nazir Karamagi defended the defunct company, saying it was a Government project, which was later replaced by Tangold Ltd.

While winding up his budget speech, Mr Karamagi told Parliament that Meremeta was jointly owned by the Government and South African firm called TRENEX PTY LTD.

The company was formed in order to buy gold from small scale miners in Lake zone regions, with a business plan of buying 300kg of gold a month. However, Mr Karamagi said it managed to buy only 40kgs.
 
Na mie niiliona hii kumbe tayari iko postes. Asante bubu. Nadhania kuna haja ya kuwawajibisha wote. Yaani watanzania walio wengi wanateseka na umaskini wakati huo huo mafisadi wanatesa. Hivi nyie mafisadi mnafikiri hizo fedha mtazikwa nazo? Manapata starehe gani kuwaona au kusikia wajawazito wakufa kwa kukosa huduma bora na kwa wakati muafaka kunakosababishwa na kutokuwa na hata dispensary maeneo yao ya jirani au ubovu wa miundombinu ya usafiri kuwawezesha kufika hospitali mapema. Shame on you Mkapa, afadhali hizo pesa ungejenga barabara, hospitali na shule nzuri kule kwenu Mtwara.
 
Mramba kawa bubu, Mkapa kawa bubu na wahusika wengine wote wameamua kuwa mabubu, lakini tutalala nao mbele mpaka kieleweke. Hawawezi kuendelea kuishi kwenye utajiri wa kukithiri kwa mapesa waliyoyapata kwa kuifisadi Tanzania.
 
Waungwana kuna shilingi bilioni 133 za EPA, halafu kuna shilingi bilioni 155 za Meremeta gold. Wahusika wote bado wanapeta mtaani. Ufisadi wa shilingi 155 bilioni wala hakuna anayeuchunguza, ndio bongo yetu hiyo ambayo inazidi kuangamia kila kukicha. Ufisadi wa bilioni 288 wahusika wote bado wako huru!

Revealed: Meremeta Gold was an offshore company
By The Citizen Team

Meremeta Gold, the firm that was paid a whopping Sh155 billion by the Bank of Tanzania in unclear circumstances in mid last year, was an offshore company, registered in United Kingdom in 1997, The Citizen can reveal today.

That means that chances of recovering the taxpayers' money and the necessary taxes up to the date it closed shop are negligible.

A senior Cabinet minister told The Citizen in Dar es Salaam yesterday that since it was registered as an offshore company it would be difficult to recover the billions it had been paid.

Speaking on condition of anonymity, the minister said: First of all, I am surprised that an offshore company was allowed to operate in this country but the clear point is that any offshore company is untraceable.

Legal experts concurred, saying that it would be difficult for the Government to recover the Sh155billion, due to the tough protection accorded to such business entities.

An offshore company does not conduct substantial business in its country of incorporation. Such firms are sometimes known as non-resident companies.

But the Companies Act 212, states clearly that offshore company can only be registered and given a certificate of compliance after fulfilling certain conditions, including renunciation of its original registration.

The Act prohibits offshore companies from operating in Tanzania unless they change and indicate that they will not be protected by offshore registration procedures.

Strangely, the Government registered Meremeta Gold. Asked why the State entered into partnership with an offshore company, the Minister for Energy and Minerals, Mr William Ngeleja, said: The Government was n't aware until mid last year after the company went bankrupt.

And fresh details show that the company was n't owned by Tanzania People's Defence Forces (TPDF) and the South African Army, as was alleged in 1997, when its existence became public.
The firm started as an army project managed jointly by TPDF and the South African Army, to mine and export gold, before becoming a ghost company that looted about Sh155 billion from the public coffers.

Contacted yesterday, the Minister for Defence, Dr Hussein Mwinyi, said: I am not familiar with the issue because I wasn�t in office during that period.

He asked The Citizen to send him written questions by this morning. The amount stashed away by the defunct company can build 500 kilometres of tarmac road or 7,500 classrooms at the cost of Sh20 million for each class.

Meremeta, the Kiswahili word for glitter, will not be glittering when the defunct gold company scandal is raised in Parliament.

After the controversial Richmond tender and External Payments Arrears (EPA) scandals, opposition and ruling party MPs believe that Meremeta poses a serious threat to the integrity of previous regime and the current administration.

Musoma Rural MP Nimrod Mkono of CCM plans to table a private's member's motion to establish who the real owner of Meremeta Gold is and why was the firm paid billions of shillings after going bankrupt.

The details, which are part of an investigation report sent to the donor community recently by the opposition parties led by Chadema's Dr Willibrod Slaa, says that the defunct gold company was registered as an offshore company on August 19, 1997, and given a registration No. 3424504.

The reasons for the formation of offshore firms are privacy, asset protection, tax savings, lawsuit protection, flexible business laws and confidentiality
The opposition parties' report, which was made available to The Citizen, says that the company was then registered in Tanzania on October 3, 1997 as a branch of a foreign company and given a Certificate of Compliance No.32755.

On Sunday, our sister paper, Mwananchi Jumapili, quoted Mr Mkono as saying that the Government had been hesitating to reveal the real owners of the company that has cost taxpayers billions of shillings.

On Monday, speaking with The Citizen from the US: Mr Mkono said: I have evidence that this ghost company pocketed a total of Sh181 billion and yet nobody wants to speak about it.
This amount is more than what CAG revealed in the 2005/6 auditing report.

If we are investigating EPA and Richmond why not Meremeta, asked the Musoma Rural MP.

But the available details show that 50 per cent of the company's shares were owned by the Registrar of Treasury, and 50 per cent by South Africa's Trienex (PTY) Co Ltd.

Yesterday, Mr Ngeleja said: The Government issued a statement on shareholders of Meremeta in June last year and clearly explained the profile of the company and why it had to be liquidated I am working on the issue and I will get back to you later in the day,

According to CAG report, BoT paid Meremeta debts amounting to Sh155 billion for unknown reasons.

The CAG revealed that a total of $118,396,460.36 was transferred to an unknown account of Nedbank Ltd of South Africa through HSB of New York, in 2005/6. The balance of $13,736,628.73 was paid to Tangold account with NBC Corporate Branch Dar-Es-Salaam.

According to available details, Tangold Ltd is a foreign registered company that was registered again as an offshore company in Mauritus (No C 205006121) dated 8 April 2005 and subsequently registered in Tanzania as a branch of foreign company with Certificate of Compliance No 55661 dated 20th February 2006.

During last year�s budget session, former Energy and Minerals minister Nazir Karamagi defended the defunct company, saying it was a Government project, which was later replaced by Tangold Ltd.

While winding up his budget speech, Mr Karamagi told Parliament that Meremeta was jointly owned by the Government and South African firm called TRENEX PTY LTD.

The company was formed in order to buy gold from small scale miners in Lake zone regions, with a business plan of buying 300kg of gold a month. However, Mr Karamagi said it managed to buy only 40kgs.
 
Asked why the State entered into partnership with an offshore company, the Minister for Energy and Minerals, Mr William Ngeleja, said: The Government was n't aware until mid last year after the company went bankrupt.


...this guy is total idiot!
 
TanGold ndio ilikuwa inaongozwa na Chenge, Anna Muganda na Daudi Balali?
 
DR SLAA said it kuwa hawa ni kampuni binafsi tena lililosajiliwa huko Uingereza sasa hapa kuna haja ya kujua kuwa source alikuwa slaa.
 
Back
Top Bottom