Gamba la Nyoka
JF-Expert Member
- May 1, 2007
- 7,038
- 9,350
Ni taathira ya mambo
Si bishara za tambo
Kwani toka kitambo
Twalisema hili jambo
Likilia la mgambo
Jua hapo kuna jambo
Kinazama hiki chombo
Wenye mpini wa mambo
Wasema hatuna nyimbo
Haki inachapwa fimbo.
Kama watoto wa kambo
Tunaachiwa makombo
Uchumi wavushwa ng'ambo
Na: Gamba la Nyoka, a.k.a(Kombeo la Daudi)
Jeshi hili ni la nani, mimi nauliza nini,
La nini tena kwanini, mwenye kujibu ni nani
Nauliza kwa makini, mtanipa jibu gani,
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwanini?
Meremeta ni ya nani, Mkuu tuelezeni,
Twataka mtangazeni, tujue wazi kwanini,
Mnachotuficha nini, mnamuogopa nani,
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwanini?
Mnatuzuga kwanini, kwa majibu yalo duni, (mbadala- "ya kihuni")
"Tusiseme hadharani", mwatung'akia Bungeni,
Hivi nyinyi kina nani, mnatuona wageni,
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwa nini?
Ati wabunge "nyamazeni, serikali ni makini,
Mambo haya ya sirini, hatutawajulisheni,
Mengine yajadilini, Meremeta iacheni,"
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwa nini?
Si kura tuliwapeni, mtuwakilishe Bungeni,
Kimya chenu ni cha nini, mnaburuzwa na nani,
Mbona mwagwaya kwanini, vigugumizi vya nini,
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwa nini?
Mwamunyange ndiye nani, Jeshi lake ndiyo gani,
Sumari yeye ni nani, Jeshi ni la nchi gani,
Walipa kodi ni nani, Jeshi linaitwa nini,
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwa nini?
Walioiba kina nani, wakijificha jeshini,
Ni usalama wa nani, mbona hatuambiani,
Na usalama wa nini, nawauliza semeni,
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwanini?
Nasema nyinyi kubalini, Meremeta ni uhuni,
Uchafu umilikini, na bora jisafisheni,
Mtatuficha mpaka lini, hamtaweza jamani,
Siri hizi ni za nini, zanani, tena kwanini?
Kagoda nayo ninini, Dipu girini magirini,
Mwanchi goldi ya nani, Tanigolidi ya nini,
Haya yote mpaka lini, nauliza kijiweni,
Siri hizi ni za nini, zanani, tena kwa nini?
Mtakula mpaka lini, mtavimbiwa jamani,
Kula huku kula gani, ni njaa namna gani,
Bila kunawa watani, hadi ndotoni kwanini,
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwanini?
Watoto waje kula nini, na mnakomba chunguni,
vidole mwavilambani, njaa haiwaisheni,
Uraiani na jeshini, mwamega na kumegani,
Siri hizi ni za nini, za nani, tena kwanini?
Jembe ninaweka chini, wamenikera mtimani,
Dharau yao ya nini, mipasho nayo ya nini,
Watapeta mpaka lini, atawazuia nani,
Siri hizi ni zanini, za nani, tena kwa nini?
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Meremeta siri ya jeshi la mafisadi!!
Dear Sita na Pinda!
kuna vitu sita anavyovichukia Bwana,
naam, viko saba vilivyo chukizo kwake
macho ya kiburi, ulimi wa uwongo,
na mikono imwagayo damu isiyo na hatia
moyo uwazao mawazo mabaya
miguu iliyomyepesi kukimbilia maovu;
Shahidi wa uwongo asemaye uongo;
naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu
Kazi kwenu!
Mara ya mwisho niliposoma jina la Jeshi letu lilikuwa linasomeka "JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA" - na kwa kimombo "Tanzania People's Defence Force"
Sasa najiuliza:
a. Ni lini jeshi letu liliacha kuwa la Wananchi wa Tanzania na kuwa Jeshi la Serikali ya Tanzania?
Mwenye contact za Mwamunyange au au msemaji wa Jeshi hilo naomba mnipatie. Tafadhali.
Mwenye contact za Mwamunyange au au msemaji wa Jeshi hilo naomba mnipatie. Tafadhali.
Mara ya mwisho niliposoma jina la Jeshi letu lilikuwa linasomeka "JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA" - na kwa kimombo "Tanzania People's Defence Force"
Sasa najiuliza:
a. Ni lini jeshi letu liliacha kuwa la Wananchi wa Tanzania na kuwa Jeshi la Serikali ya Tanzania?
Mwenye contact za Mwamunyange au au msemaji wa Jeshi hilo naomba mnipatie. Tafadhali.
Machozi yamenitoka kwa kusoma tunzi zenu. Kwa kweli naomba utume kopi hii kwenye magazeti mbalimbali.
Hiyo kwa tafasiri ya kiswahili ana Maana
Mungu awasaidie nyinyi.Na kila mtakalofanya lifanikiwe!
Mara ya mwisho niliposoma jina la Jeshi letu lilikuwa linasomeka "JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA" - na kwa kimombo "Tanzania People's Defence Force"
Sasa najiuliza:
a. Ni lini jeshi letu liliacha kuwa la Wananchi wa Tanzania na kuwa Jeshi la Serikali ya Tanzania?
It is rather ridiculous!! mtu anaulizwa ametumiaje hela ya Wananchi, jibu analotupa ati ni siri,lakini kinachoulizwa ni legitimacy ya kutumia hela na inaonekana kuna ujanja/wizi umefanyika sasa kama bunge haliwezi kuambiwa matumizi yetu yakoje ni nani mwingine anayewakilisha interest za watanzania?
Mimi naomba Spika atoe kibali bunge liende kwenye closed session kwamba sisi wengine tusijue wabunge wamekula kiapo hivi waelezwe kwa undani na umakini alafu wao watapima kama ni usalama wa nchi ulikuwa at stake or wa CCM or wa Ikulu peke yake kwa maana watu walikwiba ili ipatikane hela ya Campaign au ni wizi tu kama wa EPA lakini kusema ati tusizungumze wala kuuliza kwa sababu Pinda alisema hawezi kusema!!
Ni kutetea wizi nami siamini kama bunge zima liko pale kulinda wizi wa watu wachache.
Mungu Ibariki Tz watu wafunguke macho na haki itendeke.