Mengi VS Warioba

Status
Not open for further replies.
Kuna mjumbe mmoja mpya wa kamati ya bunge ambayo zamani ilikuwa ujenzi, na sasa ni Miundombinu, anasema kuwa huko kuna ushahidi wa kutosha kuwafunga maisha mzee Mkapa pamoja na Magufuli, kwa hiyo pole pole utaona vitu vinatolewa mapaka atoke!

Mkulu FMES,

Mzee Mkapa alikukosea nini?kila muda lazima umuandike??au ndiyo hasira za Mzee Butiku na wewe zimekutawala?
 
Kwa vile FMES ni shabiki mkubwa wa JSM (na AKM?) shutuma zake dhidi ya Jaji Waryoba hazishangazi sana. Labda nisaidiwe tu, Waryoba na Malecela walipishana wapi?

- Sina ushabiki na kiongozi yoyote mwenye harufu za ufisadi, huwezi linganisha jm na Warioba, maana records ziko very clear, wewe unajua wazi kwamba kitendo cha waziri mkuu wa zamani kushirikiana na fisadi Mahalu kuanzisha shirika la sheria la binafsi ingekua majuu Warioba angekua kwenye matata makubwa sana, lakini kwa vile ni bongo na yeye eti bado ana ubavu kupigia kelele rushwa na mafisadi, wakati yeye pia ni mshirika na fisadi!

- Mkuu kwenye ufisadi sina ukabila wala aibu na kiongozi yoyote yule fisadi kama unayajua ya ufisadi wa Malecela uyaweke hapa, halafu pia Warioba aulizwe ile ripoti yake ya rushwa iko wapi? Ile ripoti iliyodai kwamba toka tupate uhuru, Tanzania viongozi waliokula rushwa ni Kiula, Mlingwa na Ngasongwa tu! What a joke?

Fisadi ni fisadi tu, Warioba atueleze ya Mwananchi Gold yalikoanzia na kuishia, alisema atamshitaki Mengi, sasa vipi hiyo kesi iko wapi?
 
FMES,
Jaji Waryoba na Balozi Mahalu walianzisha lini ile firm yao ya UWAKILI?
 
Mkulu FMES,

Mzee Mkapa alikukosea nini?kila muda lazima umuandike??au ndiyo hasira za Mzee Butiku na wewe zimekutawala?

- Wow! wow! now wait a minute wewe Mkulu wangu Gembe, kweli unaona furaha masikini kina Mramba, Yona, na Mgonja wakisota rumande huku Mkapa aliyekua akiwatuma anatesa tu nje kama sio yeye na kujficha nyuma ya immunity ambayo kwanza haipo anyways!

- Sasa unasema na mimi nilikuwa ninatafuta mlo kwa Mkapa kama Butiku? Is that so? Dr. Slaa naye alikuwa anatafuta mlo kwa Mkapa? Mbunge Kimaro naye alikuwa anatafuta mlo kwa Mkapa? Pinda aliyesema Mkapa haogopwi na serikali yake naye alikuwa anatafuta mlo kwa Mkapa?

Mkulu Gembe, hivi vita vya ufisadi naona vinaanza kuku-wear out, wewe tuachie sisi wengine tutaendelea navyo mpaka kieleweke, huwezi ongelea kusafisha mafisadi bila kukamata Mkapa na kumburuza Kisutu, lakini milango iko wazi kama kuna mafisadi tuliowasahau muwataje hapa tule nao sahani moja!
 
FMES,
Jaji Waryoba na Balozi Mahalu walianzisha lini ile firm yao ya UWAKILI?

- Mkuu Wildcard, kweli inajalisha ni lini Warioba ameanzisha ushirika na fisadi tena a proven one kama Mahalu? Huyu Mahalu mkuu wangu niliwahi kumuona kwa macho yangu somewhere huko majuu, akiwa mkurugenzi wa elimu ya juu, alikwenda kuwarudisha wanafunzi waliokuwa huko kwa scholarship za serikali akidai kuwa serikali haiwezi tena kujihusisha na malipo ya hizo elimu zao, lakini guess what hapo hapo alikua ameleta mtoto wake na shemeji yake yaani mdogo wa mkewe na kuwachomeka kwenye hizo hizo scholarship uchwara alizowatoa watoto wa wananchi masikini na walalahoi,

Sasa wewe mkuu wangu unauliza timeline za ufisadi? hawa mafisadi walianza siku nyingi sana tena ukifuatilia utakuta madudu mengi sana ambayo hatuyajui, lakini record zipo walianza ufisadi longtime ago!
 
FMES,
Jaji Waryoba si mmoja wa mafisadi wa NCHI hii. Kama ni urafiki na mafisadi hilo kila mtu kwa wakati fulani kalifanya maana ni vigumu mno kuwajua mafisadi, wezi, wabadhirifu hasa hawa wenye nafasi kubwa katika jamii yetu. Jiulize tu kidogo, kwa nini Malecela mara zote mbili hakufika angalau kwenye tano bora.
 
FMES,
Jaji Waryoba si mmoja wa mafisadi wa NCHI hii. Kama ni urafiki na mafisadi hilo kila mtu kwa wakati fulani kalifanya maana ni vigumu mno kuwajua mafisadi, wezi, wabadhirifu hasa hawa wenye nafasi kubwa katika jamii yetu. Jiulize tu kidogo, kwa nini Malecela mara zote mbili hakufika angalau kwenye tano bora.

- Mkuu Wildcard labda ufungue topic ya Malecela na kugombea urais hii ni topic ya Mengi VS Warioba, au?

- Mimi hapa nitaendelea na Warioba tu na Mengi, sasa naomba kukuuliza swali vipi hii kesi vipi Warioba mbona hajaifungua dhidi ya Mengi aliyedai amemuharibia jina na yeye sio fisadi?
 
FMES,
Jaji Waryoba si mmoja wa mafisadi wa NCHI hii. Kama ni urafiki na mafisadi hilo kila mtu kwa wakati fulani kalifanya maana ni vigumu mno kuwajua mafisadi, wezi, wabadhirifu hasa hawa wenye nafasi kubwa katika jamii yetu. Jiulize tu kidogo, kwa nini Malecela mara zote mbili hakufika angalau kwenye tano bora.

WildCat nakubaliana na wewe! Waryoba alikuwa na nadhani bado ni mtu safi na kiongozi ambaye aliweka maslahi ya nchi mbele kuliko utajiri binafsi. Kujiunga na Mahalu siyo tatizo maana Mahalu hakuwa fisadi kabla ya kwenda ubalozini Italy ambapo alifundishwa na wenzake kula!
 
- Wow! wow! now wait a minute wewe Mkulu wangu Gembe, kweli unaona furaha masikini kina Mramba, Yona, na Mgonja wakisota rumande huku Mkapa aliyekua akiwatuma anatesa tu nje kama sio yeye na kujficha nyuma ya immunity ambayo kwanza haipo anyways!

- Sasa unasema na mimi nilikuwa ninatafuta mlo kwa Mkapa kama Butiku? Is that so? Dr. Slaa naye alikuwa anatafuta mlo kwa Mkapa? Mbunge Kimaro naye alikuwa anatafuta mlo kwa Mkapa? Pinda aliyesema Mkapa haogopwi na serikali yake naye alikuwa anatafuta mlo kwa Mkapa?

Mkulu Gembe, hivi vita vya ufisadi naona vinaanza kuku-wear out, wewe tuachie sisi wengine tutaendelea navyo mpaka kieleweke, huwezi ongelea kusafisha mafisadi bila kukamata Mkapa na kumburuza Kisutu, lakini milango iko wazi kama kuna mafisadi tuliowasahau muwataje hapa tule nao sahani moja!
Mkulu FMES,
Kiundani kabisa kina mramba na yona ndiyo walimleta Mkapa mambo haya ya klina stewart na Mkulu hakuwa na muda wa kyapitia vizuri.

Ni kama suala la RDC,EL alimpelekea Muungwana bila Muungwana kujua dili nzima na mwishoni Muungwana kuja kugundua walikuwa wanamuuingiza kingi akawaruka na kuamua kuwakaanga.

Mara zote dili hizi huwa zinaanzia wizarani na baadaye baada ya kuonekana zina dili basi utafutwa mtu na kutumw aikulu kumueleezea Mkulu nini wanataka.

Wazaee kama Kingunge ndiyo watu wa kuanzwa kuwekwa ndani sababu hawa ndiyo huwa wanaongoza kutetea dili kwa kuonekana wako karibu na Rais.(hawa ni swa na wshenga).Kipindi cha Mkapa walikuwa wakimtumia sana Ruhinda ambaye alijidai kama Nyerere after Mwalimu kufariki.

Mkapa hana Hatia,Kosa lake alikurupuka kujiunga na watu wezi!Vita dhidi ya Mafisadi nipo na wewe mkuu mzee wa sauti ya Umeme mpaka kieleweke!

I would be pleased watu kama Kingunge na Mzee Ruhinda kwenda Gerezani kwanza
 
- Mkuu Wildcard labda ufungue topic ya Malecela na kugombea urais hii ni topic ya Mengi VS Warioba, au?

- Mimi hapa nitaendelea na Warioba tu na Mengi, sasa naomba kukuuliza swali vipi hii kesi vipi Warioba mbona hajaifungua dhidi ya Mengi aliyedai amemuharibia jina na yeye sio fisadi?

Naomba nisiwe msemaji wa Jaji Waryoba. Namfahamu tu kama kiongozi mstaafu wa nchi yetu.
 
Mkapa hana Hatia,Kosa lake alikurupuka kujiunga na watu wezi!Vita dhidi ya Mafisadi nipo na wewe mkuu mzee wa sauti ya Umeme mpaka kieleweke!

- Mkuu Gembe, bongo huwa tunasema hivi huwezi ua nyoka bila kupiga kichwa, sasa huyu nyoka wa ufisadi si unajua kichwa chake haswa sasa bila kukipiga hicho kichwa tutaua vipi huyu nyoka?
 
- Mkuu Kigoma, kwa kawaida huwa ninakuaminia sana, ila kwenye hili inaonekana huna uhakika na unachokisema, maana ungekua na uhakika ungekua unajua kua Warioba ni mbia na Fisadi Mahalu, kwenye law firm, halafu ungekuwa unajua kua kwenye uchunguzi wa kamati yake ya rushwa hakuenda kumchunguza Mahalu kule Elimu na Sayansi,

- Mkuu wangu hivi umeyasikia ya Mwananchi Gold na Warioba au unakurupuka tu ndugu yangu? Hivi unafikiri ni kwa nini mtoto wake wa kike aliyekua akisoma majuu alirudi ghafla bila kumaliza shule?

Pole pole ndugu yangu kama huyajui ni kuuliza, hivi umesikia aliyoyafanya baada ya Yona na Mramba kutinga Kisutu, akihofia na yeye kutinga huko? Hana lolote mgombea wake Salim aliposhindwa urais akatukana sana kuwa rushwa imezidi, lakini Dr. Slaa alipotoa ile list ya aibu akasema ni kuligawa taifa, hana lolote huyu filimbi nyingi lakini na yeye Warioba ni fisadi aliyeshitukia wakati hana nafasi!

Mkuu heshima kwako. Nimesoma ulichoandika hapo juu, ila napata tabu kuelewa. Mbona maneno yako hayatoshi?

Unazungumzia Kamati ya rushwa kutomhusu Mahalu. Kwani ilimhusu kila mtu? Mahalu hakuwa kwenye watu walioshukiwa wakati ule. Labda uelezee zaidi. Pia umezungumzia kurudi kwa mtoto wa Warioba kutoka Ulaya bila kumaliza shule. Ila hujaeleza sababu unazozijua wewe. Umeacha ikielea tu. Sema tuelewe Mkuu, sababu ni zipi? Tatu umezungmzia kwa kufupi kabisa kuhusu aliyoyafanya baada ya Yona na Mramba kutinga Kisutu. Nini alichofanya?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom