Mengi VS Warioba

Status
Not open for further replies.

Spiderman

JF Admin
Jan 1, 1970
7,219
441

Source: MTANZANIA
 
Nafikiri wakati umefika sasa wa kuanza kuhoji issues badala ya watu. Sidhani kama ni kukomaa kumhusisha Mengi na habari zinazotolewa na vyombo vyake. Nafikiri hapa tuanze kuhoji nini magazeti yameandika badala ya kuanza kuhoji mahusiano ya watu wawili.
 
Mafuchila,
Nakuafiki. Lakini nadhani hapa kosa waliyofanya waandishi habari ni kutokuupa nafasi upande mwingine utoe maoni yake katika hili suala kabla ya makala hiyo kuchapishwa. Ndio maana Jaji Warioba ameamua kuwa"sue."
 
Mimi nakungana kusema Media Solution ishitakiwe na si Mengi kama yeye hili ni kosa na kumtisha Mengi maana huwa hatuko huko wanako andika habari hizi. Pia Warioba nadhani kuna kasoro mahala maana anahusika mno na watuhumiwa wa mambo mbali mbali kama Mahalu na sasa Mwananchi .Mwache aende huko wote ni wana CCM tutaujua ukweli mbele kwa mbele lakini afanye kweli si kusema na kukaa kimya .
 
Kwenye kesi za madai, unaweza kumdai hata mmiliki wa vyombo hivyo! siyo tu mwandishi au shirika..lenyewe!
 
Nimeshindwa kumuelewa Warioba, pamoja na udhoefu wake wa sheria anashindwa kutengeneza kesi, ukimshtaki Mengi eti amekukashfu ni rahisi sana kushindwa hiyo kesi udhibitisho wake utakuwa mgumu sana lazima uonyeshe kama Mengi alitumia madaraka yake kumshawishi Mhariri mkuu kuandika hiyo habari pia lazima mjue mengi hahusiki na kitu chochote na habari zinazotolewa kwenye magazeti yake kwa hiyo ni vigumu sana kumhusisha moja kwa moja hata kama kweli anahusika. Kesi kama hizi huwa ni ngumu sana kwani kuna jambo la kudhibitisha madhara uliyoyapata kwa hiyo habari. Ukimshtaki mwandishi ni kupoteza muda, wao siyo wanayoiweka habari kwenye gazeti. Mhariri mkuu ndiye anayepitisha habari zitoke. Katika mazingira ya namna hiyo inakuharibia sana kujenga kesi kwa kuwaingiza watu ambao hawahisi. Mazingira kama haya unatakiwa umshtaki Mhariri mkuu au gazeti kwa ujumla wao watajua ni nani anahusika. Ukimuiingiza mengi itakuwa rahisi sana kwakwe kuibadilisha anaweza akaifanya iwe na sura ya kisiasa kitu ambacho kitamuongezea Warioba ugumu kushinda hii kesi.
 
Sam,
Kushtakiwa kwa Mengi ni technical. Yeye kama owner wa gazeti kwa lugha nyingine anaitwa publisher. Yeye ndiye anayeshika mkoba wa IPP Media. Sasa ukimshtaki editor peke yake bila kumshirikisha tajiri wake umeachia nafasi kubwa kwa kampuni nzima kutowajibika. Nadhani Warioba kama mwanasheria analijua sana hilo. Unakumbuka kule Kenya kesi ya Biwott? Alishtaki duka lililouza kitabu, mwandishi na mchapishaji wa kitabu kilichoelezea kuwa alihusika katika mauaji ya Ouko.
 
Jasusi
nakubaliana na wewe na wala simlaumu Warioba kwa kufanya hivyo, lakini ukimwingiza Mengi kwenye kesi hiyo kesi, unaweza ukamshtaki lakini kushinda kesi ya namna hiyo itakuwa ngumu sana hasa ukiangalia yeye ni nani kwenye IPP Media. Mengi ni mkurugenzi mtendaji wa IPP Group na siyo IPP Media, IPP Media ni kampuni lililopo chini ya IPP Group na ina mkurugenzi wake. Ndiyo unaweza kumshtaki lakini itakuwa vigumu sana kumuhusisha na kushinda hiyo kesi. Kwenye IPP Group, mengi siyo publisher wa IPP Media. Ni sawa na kumshtaki Steve Ballmer ambaye ni CEO wa Microsoft ukitegemea utashinda kesi dhidi ya Microsoft au Bill kama founder au mtu mwenye hisa nyingi kwenye Microsoft. Sina nia ya kufananisha IPP Group na Microsoft lakini is the same type ya kesi.
 
Tunapotoka na kuacha mada yenyewe ama ni mimi napotoka ? Warioba ana hamaki kwamba yaliyosemwa ni uongo basi mwache aende Mahakamani yatajulikana huko.Ila najua kwamba This Day na kulikoni ni magazeti ya wana Mtandao Mengi katumika kama kivuli wacha waumane sisi tuone nani mwenye meno makali .Lakini sasa Warioba afanye kweli asiishie kusema ukweli uje nje hapa .Siasa hizi jamani duh!!!!!!!!
 
Tulisema siku nyingi kuwa huyu Warioba, ni mnafiki na ni corrupt kama wengine anaowapigia kelele, ndio maana hakwenda Elimu na sayansi kwa Mahalu, baadaye akawa patner naye kwenye Law Firm!

Sasa mambo yanaanza kutoka pole pole, tena sio peke yake na moto umeanza huo, kuna mzee Maguifuli ambaye mtandao sasa wamepania kumuondoa, stay tuned more yanakuja...............!
 
Mzee ES,

Magufuli wanataka kumuondoa ? safi sana huyu mtu ni mbaya sana kazi yake ni kutunyanyasa sisi wanyonge anatunyanganya viwanja vyetu pale mbezi , Hati ya kujenga kwa miaka mingi wamekuwa wakitunyima sasa wameamua kutunyanganya tuu!
 
Kwa jinsi This Day na Kulikoni walivyoandika ile habari nivigumu kuamini kwamba ni uongo. Hawa bwana inaonekana wana credible sources of information. Huyu Warioba anajikosha tu na anatujua fika hamna kesi ya yeye kushinda pale. Tunashukuru tumeanza kupata rangi halisi za Warioba, amejificha kwa muda mrefu kwenye ngozi isiyoyake. Hatimaye sasa tunaanza kumjua. He is has no intergrity as he has always tried to portray himself.
 
Mzee Rufiji,

Huyo mzee Magufuli, wabongo pole pole wameanza kumshitukia kama nilivyosema siku nyingi zilizopita kuwa hana tofauti na Keenja, kazi ya Billioni moja wao wataifanya kwa billioni Tano na kuwadanganya wananchi na viongozi wenzao wasiojua kitu kuwa ni wachapakazi hodari,

Mtu wa kwanza kunishitua kuhusu Keenja na Magufuli, alikuwa mzee Mkama, aliyechukua nafasi ya Keenja kule Halmashauri ndiye aliyenushitua kuwa hawa wawili ni magirini hawa, tena akanionyesha mpaka mahesabu ya Keenja, ambayo baadaye yalipelekwa kwa Mkapa, lakini hakuna hatua iliyochukuliwa maana Keenja ameoa nyumba moja na rafiki mkubwa wa Mkapa, mzee Sumaye!

Kuna mjumbe mmoja mpya wa kamati ya bunge ambayo zamani ilikuwa ujenzi, na sasa ni Miundombinu, anasema kuwa huko kuna ushahidi wa kutosha kuwafunga maisha mzee Mkapa pamoja na Magufuli, kwa hiyo pole pole utaona vitu vinatolewa mapaka atoke!
 
Polepole vitu vitatolea hadi atoke je nini nafasi ya CCM baadaye kwenye kampeni ama watasema wanasafisha Nchi kwa kuwaondoa wala rushwa maana najua JK na CCM yake ikifikia kwenye maslahi ya CCM wanakuwa macho zaidi maslahi ya Taifa .Sijaona wala kusikia PhD feki ziko wapi ? Zimeishia ? Au bado DCI anafanay uchunguzi ? Au ni kiini macho sasa ???
 
Editorial Comment: Mwananchi Gold: The truth shall set you free

 
PROF mahalu pia ,nafikiri na warioba walinunua kiwanda cha UBUNGO GARMENTS kikibwa tu kwa 120mil,tena wanalipa kidogo kidogo Hadi leo hakijaanza kazi na wala hakitegemei kuanza ,hii ni kunyima fursa ya wawekezaji serious ambao wangekua wameshafungua kiwanda na kuleta ajira .tatizo wanasiasa walitumia sera ya ubinafsishaji kujilimbikizia mali.

zainnadunin adamjee na wenzake walitumia fursa ya ubunge wa kawe kununua kiwanda maarufu cha nyama tena kilichotoa mchango mkubwa hadi kufilisika kipindi cha vita ,ambapo walikuwa wakipeleka beef mstari wa mbele kwa ajili ya vijana ,kilikuwa kimeajiri moja kwa moja watu 1,500 leo muwekezaji amenunua amebadilisha matumizi ya awali na anataka kujenga apartments ,hapa tunapata madhara ya kukosesha watu ajira na vilevile masoko ya ngombe wetu yaliyotegemea kiwanda hichi yanaathiriwa ....

hawa wanasiasa waliojilimbikizia viwanda bila hata kuwa na mitaji wanyanganywe!!!!!
 
IPP ni Limited company. Ingawa sijui sawaswa sheria yetu ya makampuni has limited companies. Ila ninategema kuwa makosa yote yatokananyo na biashara za kampuni hayahusishwi na wamilikaji wake unless ikithibitika kuwa wamilikaji hao walichangia kwa makusudi kufanya kampuni itende makosa hayo.
 
Let say Warioba & Co go to court and loose then what...??

Let say THISDAY is 100% right..then what??


The system is corrupt, JK & Co knows that...kwa wananchi wa Tz this is a perfect LOOSE - LOOSE situation. NOBODY will be punished for this....just another Billions wachache wameamua kujichukulia.

Mzee ES

You are...right on the money bro, somebody naughty must be behind ThisDay. May be wana-Mtandao...but bro what is their motive??? Just to embarrass Warioba???!!! That's not good enough. Any ideas???
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…