Mene Mene Tekeli Peresi ya Magufuli

Mene Mene Tekeli Peresi ya Magufuli

1954tanu

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
1,038
Reaction score
487
Siku mbili zilizopita vyombo vya habari vimeripoti kwamba NEMC imetangaza kwamba kuanzia sasa mirindimo yoyote na kelele zozote zinazohusiana na sherehe, matangazo, sauti kubwa kutoka majumba ya starehe, magari ya poromosheni, makanisani yatakuwa yanalipiwa shilingi milioni 5 hadi milioni 10. Na kwa yule atakayekiuka atatozwa shilingi milioni 50 ama kufungwa jela.

Kiuhalisia, hakuna kanisa ambalo litaweza kulipa shilingi milioni 5 kwa mkutano wa Injili ya Kristo kwa siku moja hata ingekuwa kwa mwezi. Kwa maana nyingine makanisa yamefungwa speed governor ya kutangaza Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni.

Chini ya utawala huu wa awamu ya tano, iwapo NEMC watatekeleza hiyo sheria yao, basi Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni zitaadimika kwa kiasi kikubwa.

Historia ya kanisa inaonesha kwamba yeyote aliyejaribu kuzuia makusudi ya Mungu wa mbinguni, mtu huyo aliondoshwa kabla kusudi hilo halijapotea. Mfano mzuri wa Biblia ni ule wa mfalme Herode ambaye tunasoma habari zake katika kitabu cha Mathayo sura ya pili.

ANGALIZO: Wote wenye mamlaka tufahamu kuwa mamlaka kuu ni ya Mungu wa Mbinguni; tuelewe kwamba hakuna atakayenyoosha kidole karibu na mboni ya jicho la Bwana akanusurika, mfalme Belshaza wa Ukaldayo; dola iliyokuwa ikitawala takribani dunia nzima; alijikinai akidhani ni mkuu mno mwenye kuweza kuchafua na kunajisi vyombo vya hekaluni kwa Mungu. Mungu alimfutia ufalme wake akaugawa kwa Waajemi na Wamedi. Daniel sura ya 6.
 
Siku mbili zilizopita vyombo vya habari vimeripoti kwamba NEMC imetangaza kwamba kuanzia sasa mirindimo yoyote na kelele zozote zinazohusiana na sherehe, matangazo, sauti kubwa kutoka majumba ya starehe, magari ya poromosheni, makanisani yatakuwa yanalipiwa shilingi milioni 5 hadi milioni 10. Na kwa yule atakayekiuka atatozwa shilingi milioni 50 ama kufungwa jela.

Kiuhalisia, hakuna kanisa ambalo litaweza kulipa shilingi milioni 5 kwa mkutano wa Injili ya Kristo kwa siku moja hata ingekuwa kwa mwezi. Kwa maana nyingine makanisa yamefungwa speed governor ya kutangaza Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni.

Chini ya utawala huu wa awamu ya tano, iwapo NEMC watatekeleza hiyo sheria yao, basi Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni zitaadimika kwa kiasi kikubwa.

Historia ya kanisa inaonesha kwamba yeyote aliyejaribu kuzuia makusudi ya Mungu wa mbinguni, mtu huyo aliondoshwa kabla kusudi hilo halijapotea. Mfano mzuri wa Biblia ni ule wa mfalme Herode ambaye tunasoma habari zake katika kitabu cha Mathayo sura ya pili.

ANGALIZO: Wote wenye mamlaka tufahamu kuwa mamlaka kuu ni ya Mungu wa Mbinguni; tuelewe kwamba hakuna atakayenyoosha kidole karibu na mboni ya jicho la Bwana akanusurika, mfalme Belshaza wa Ukaldayo; dola iliyokuwa ikitawala takribani dunia nzima; alijikinai akidhani ni mkuu mno mwenye kuweza kuchafua na kunajisi vyombo vya hekaluni kwa Mungu. Mungu alimfutia ufalme wake akaugawa kwa Waajemi na Wamedi. Daniel sura ya 6.
hapa kilicho fanyika ni kukumbusha sheria za Nchi zinasemaje kuhusu kujenga jamii iliyo fikia civilization ya aina kama yetu. kwani si unaweza ukajenga kanisa na ufanya mahubiri hukohuko kanisani? mbona ulaya na marekani wameweza? hakuna kitu kizuri kama kuwa na utaratibu kamili katika jamii.
 
Siku mbili zilizopita vyombo vya habari vimeripoti kwamba NEMC imetangaza kwamba kuanzia sasa mirindimo yoyote na kelele zozote zinazohusiana na sherehe, matangazo, sauti kubwa kutoka majumba ya starehe, magari ya poromosheni, makanisani yatakuwa yanalipiwa shilingi milioni 5 hadi milioni 10. Na kwa yule atakayekiuka atatozwa shilingi milioni 50 ama kufungwa jela.

Kiuhalisia, hakuna kanisa ambalo litaweza kulipa shilingi milioni 5 kwa mkutano wa Injili ya Kristo kwa siku moja hata ingekuwa kwa mwezi. Kwa maana nyingine makanisa yamefungwa speed governor ya kutangaza Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni.

Chini ya utawala huu wa awamu ya tano, iwapo NEMC watatekeleza hiyo sheria yao, basi Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni zitaadimika kwa kiasi kikubwa.

Historia ya kanisa inaonesha kwamba yeyote aliyejaribu kuzuia makusudi ya Mungu wa mbinguni, mtu huyo aliondoshwa kabla kusudi hilo halijapotea. Mfano mzuri wa Biblia ni ule wa mfalme Herode ambaye tunasoma habari zake katika kitabu cha Mathayo sura ya pili.

ANGALIZO: Wote wenye mamlaka tufahamu kuwa mamlaka kuu ni ya Mungu wa Mbinguni; tuelewe kwamba hakuna atakayenyoosha kidole karibu na mboni ya jicho la Bwana akanusurika, mfalme Belshaza wa Ukaldayo; dola iliyokuwa ikitawala takribani dunia nzima; alijikinai akidhani ni mkuu mno mwenye kuweza kuchafua na kunajisi vyombo vya hekaluni kwa Mungu. Mungu alimfutia ufalme wake akaugawa kwa Waajemi na Wamedi. Daniel sura ya 6.
Mbona Kagame hajaondoshwa Rwanda?? tuache kuishi hovyo hovyo kwani neno la Mungu ukilifwata kanisani au msikitini hua halieleweki?? mpaka uende kwenye makazi ya watu usiku wa manane kuhubili,hata nyumbu huishi kwa mpangilio mbugani.
 
Jee hii inahusiana na ile adhana ya misikitini kabla ya sala za alfajiri na Ijumaa? Kama ndio basi tutegemee msuguano mkubwa utakao tokea
 
kwenye swala la ibada nawasihi wasiguse coz kila dini na madhehebu vina utaratibu wao wa kujiendesha utaratibu wao wa kujiendesha nashauri hao nemc wafanye kazi zingine watuache na mitindo yetu ya kuabudu
 
Wajenge Makanisa/Misikiti mziwekee sound proof.
Na kwa sherehe za harusi ni kuhakikisha waalikwa wanakuja na earphones.
Tu
 
Jee hii inahusiana na ile adhana ya misikitini kabla ya sala za alfajiri na Ijumaa? Kama ndio basi tutegemee msuguano mkubwa utakao tokea
Hapana...hao watalalamika na kuzua chaos, hivyo wao wataendelea kama kawaida. Ila hawa wengine si walalamikaji ni wazee wa kugeuza 'shavu lingine' hivyo ni rahisi kuwadhibiti.
 
Last edited:
WEWE NI MNAFIKI MKUBWA UNAYESIMAMA NA NGOZI YA UKRISTO. NINAKUKEMEA KTK JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETH USHINDWE. NA DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO ILIYOMWAGIKA MSALABANI KWA AJILI YA WENYE DHAMBI IKAFUTE LAANA ULIYOIACHILIA KWA RAIS WETU KIPENZI DR. JPM

UNAFIKI NI DHAMBI KUBWA SANA CHINI YA JUA!!!!!!

WEWE NI NANI HATA UMWAMBIE RAIS WETU UFALME WAKE UMEFIKA MWISHO!!!! UNA USAFI GANI HAPO ULIPO HATA UFIKIE KIWANGO CHA KIROHO CHA DANIEL. SITAKI KUYAWEKA MAMBO YAKO HUMU ILA NAKUONYA USIRUDIE TENA KUFANYA USHETANI HUU!!!

MKRISTO ALIYEJAZWA ROHO MTAKATIFU NGUVU YAKE IKO MAGOTINI. ULIMI WAKO UMEJAA LAANA BADALA YA BARAKA. HIZO LAANA ZIKURUDIE NA KUWA KAMA VAZI MAUNGONI MWAKO. WAKRISTO WENZIO WANAFUNGA NA KUOMBA KUMUOMBEA MHE. RAIS KTK MAENEO YOTE WEWE UNAACHILIA LAANA????? SHAME ON YOU!!!!!!! UMEISOMA VIZURI HIYO SHERIA NA KUIELEWA????

HIVI INJILI NI LAZIMA IHUBIRIWE KWA KUPAYUKA????? MIAKA ILE WAKATI TUNAOKOKA INJILI ILIKUWA MAN TO MAN. HUPANDI DALADALA AU BASI AU NDEGE NA KUFIKA UPANDE WA PILI BILA KUMSHUHUDIA MTU. WEWE LEO HATA JIRANI ZAKO NA UNAOFANYA KAZI NAO WANATILIA MASHAKA WOKOVU WAKO MAANA MATENDO YAKO HAYAFANANI NA NENO LA KRISTO!!!

INJILI YA LEO INA WAPIGA DEAL WANAFIKI WAKUBWA NA WAFANYABIASHARA. HIYO NI DALILI YA MAFARISAYO. UNGEKUWA UNA ROHO WA BWANA WEWE UNGEKAA MAGOTINI NA KUJUA TZ INAPITA KTK MAJIRA GANI YA KIROHO!!!!

UMENIUZI SANA KWA JINSI ULIVYOKOSA HEKIMA!!!!!! NA MANENO MABAYA ULIYOYATUMIA KWA RAIS WETU HALAFU UNAJIITA MKRISTO a.k.a FARISAYO

NAOMBA MLIONIELEWA MUMPUUZE HUYU FARISAYO NA MSIACHE KUMUOMBEA RAIS WETU. MAOMBI YAONGEZEKE BAADA YA KUMUONA ADUI WA NYUMBANI MWETU.

MUNGU AKULINDE RAIS WETU (Zakaria 4:5). UKAFANYIKE BARAKA KWA TAIFA LA TZ NA KWA WATANZANIA WOTE MUNGU ALIOWAWEKA MIKONONI MWAKO. HEKIMA KAMA ZA MFALME SULEIMAN ZIENDELEE KUTIRIRIKA KUANZIA KICHWANI MWAKO NA KUSHUKA KAMA MAFUTA NDEVUNI MWA HARUNI HADI KWA WATU WAKO. (ZABURI 41:1-2).

Queen Esther

Siku mbili zilizopita vyombo vya habari vimeripoti kwamba NEMC imetangaza kwamba kuanzia sasa mirindimo yoyote na kelele zozote zinazohusiana na sherehe, matangazo, sauti kubwa kutoka majumba ya starehe, magari ya poromosheni, makanisani yatakuwa yanalipiwa shilingi milioni 5 hadi milioni 10. Na kwa yule atakayekiuka atatozwa shilingi milioni 50 ama kufungwa jela.

Kiuhalisia, hakuna kanisa ambalo litaweza kulipa shilingi milioni 5 kwa mkutano wa Injili ya Kristo kwa siku moja hata ingekuwa kwa mwezi. Kwa maana nyingine makanisa yamefungwa speed governor ya kutangaza Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni.

Chini ya utawala huu wa awamu ya tano, iwapo NEMC watatekeleza hiyo sheria yao, basi Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni zitaadimika kwa kiasi kikubwa.

Historia ya kanisa inaonesha kwamba yeyote aliyejaribu kuzuia makusudi ya Mungu wa mbinguni, mtu huyo aliondoshwa kabla kusudi hilo halijapotea. Mfano mzuri wa Biblia ni ule wa mfalme Herode ambaye tunasoma habari zake katika kitabu cha Mathayo sura ya pili.

ANGALIZO: Wote wenye mamlaka tufahamu kuwa mamlaka kuu ni ya Mungu wa Mbinguni; tuelewe kwamba hakuna atakayenyoosha kidole karibu na mboni ya jicho la Bwana akanusurika, mfalme Belshaza wa Ukaldayo; dola iliyokuwa ikitawala takribani dunia nzima; alijikinai akidhani ni mkuu mno mwenye kuweza kuchafua na kunajisi vyombo vya hekaluni kwa Mungu. Mungu alimfutia ufalme wake akaugawa kwa Waajemi na Wamedi. Daniel sura ya 6.
 
Siku mbili zilizopita vyombo vya habari vimeripoti kwamba NEMC imetangaza kwamba kuanzia sasa mirindimo yoyote na kelele zozote zinazohusiana na sherehe, matangazo, sauti kubwa kutoka majumba ya starehe, magari ya poromosheni, makanisani yatakuwa yanalipiwa shilingi milioni 5 hadi milioni 10. Na kwa yule atakayekiuka atatozwa shilingi milioni 50 ama kufungwa jela.

Kiuhalisia, hakuna kanisa ambalo litaweza kulipa shilingi milioni 5 kwa mkutano wa Injili ya Kristo kwa siku moja hata ingekuwa kwa mwezi. Kwa maana nyingine makanisa yamefungwa speed governor ya kutangaza Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni.

Chini ya utawala huu wa awamu ya tano, iwapo NEMC watatekeleza hiyo sheria yao, basi Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni zitaadimika kwa kiasi kikubwa.

Historia ya kanisa inaonesha kwamba yeyote aliyejaribu kuzuia makusudi ya Mungu wa mbinguni, mtu huyo aliondoshwa kabla kusudi hilo halijapotea. Mfano mzuri wa Biblia ni ule wa mfalme Herode ambaye tunasoma habari zake katika kitabu cha Mathayo sura ya pili.

ANGALIZO: Wote wenye mamlaka tufahamu kuwa mamlaka kuu ni ya Mungu wa Mbinguni; tuelewe kwamba hakuna atakayenyoosha kidole karibu na mboni ya jicho la Bwana akanusurika, mfalme Belshaza wa Ukaldayo; dola iliyokuwa ikitawala takribani dunia nzima; alijikinai akidhani ni mkuu mno mwenye kuweza kuchafua na kunajisi vyombo vya hekaluni kwa Mungu. Mungu alimfutia ufalme wake akaugawa kwa Waajemi na Wamedi. Daniel sura ya 6.


Mkuu unakosea sana! Nyumba za ibada zinafungwa speaker kwa ajili ya waumini waliopo ndani tu! Sasa kufunga maspika ya nje ni ili iweje!? Kila mtu ana iman yake, kuwaambia watu wengine iman yako eti kisa unahubiri, sidhan kama ni sahihi sana.

Nafikiri hiyo sheria haina haja ya kumnyima mtu asipate neno la Mungu bali ni kupunguza bugudha kwa watu wengine! Kwa mfano unaweza ukawa upo mahali, unapita mgari wa matangazo, kila kitu kinakuwa hovyo, kama unaongea na simu inabidi uikate maana hata huyo unayeongea nae haelewi kitu!

Kwenye nyumba za ibada hasa misikiti nahisi kutaleta kuzunguzungu, maana sijawi kuona msikiti ambao hauna loud speaker kwa nje!

Ni hayo tu!

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Siku mbili zilizopita vyombo vya habari vimeripoti kwamba NEMC imetangaza kwamba kuanzia sasa mirindimo yoyote na kelele zozote zinazohusiana na sherehe, matangazo, sauti kubwa kutoka majumba ya starehe, magari ya poromosheni, makanisani yatakuwa yanalipiwa shilingi milioni 5 hadi milioni 10. Na kwa yule atakayekiuka atatozwa shilingi milioni 50 ama kufungwa jela.

Kiuhalisia, hakuna kanisa ambalo litaweza kulipa shilingi milioni 5 kwa mkutano wa Injili ya Kristo kwa siku moja hata ingekuwa kwa mwezi. Kwa maana nyingine makanisa yamefungwa speed governor ya kutangaza Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni.

Chini ya utawala huu wa awamu ya tano, iwapo NEMC watatekeleza hiyo sheria yao, basi Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni zitaadimika kwa kiasi kikubwa.

Historia ya kanisa inaonesha kwamba yeyote aliyejaribu kuzuia makusudi ya Mungu wa mbinguni, mtu huyo aliondoshwa kabla kusudi hilo halijapotea. Mfano mzuri wa Biblia ni ule wa mfalme Herode ambaye tunasoma habari zake katika kitabu cha Mathayo sura ya pili.

ANGALIZO: Wote wenye mamlaka tufahamu kuwa mamlaka kuu ni ya Mungu wa Mbinguni; tuelewe kwamba hakuna atakayenyoosha kidole karibu na mboni ya jicho la Bwana akanusurika, mfalme Belshaza wa Ukaldayo; dola iliyokuwa ikitawala takribani dunia nzima; alijikinai akidhani ni mkuu mno mwenye kuweza kuchafua na kunajisi vyombo vya hekaluni kwa Mungu. Mungu alimfutia ufalme wake akaugawa kwa Waajemi na Wamedi. Daniel sura ya 6.
 
Kwani kuhubiri ni lazima kupiga kelele kila sehemu hata sehemu za makazi?
 
Balaa lipo huku tunakoishi wanakokuita sinza Kwa wajanja, kuna ndugu wawili watani wa jadi mmoja anaungurumisha kengele zake na mwengine anavurumisha adhana alaf usishangae kusikia nghara(camera flash sound) ekotite, ekotite, siunajua kumejaa club za kufa mtu. Lkn raha ilioje ni jirani yangu mlokole akianza vile vipindi vyetu vya kunena kwa lugha uwa nasuuzika na roho yangu. Hapo bado yale magar ya promotion mziki haujaisha anapandishia mwingine mara sijui anasugua vinini saut za ajab ajab tu zinatoka.
Sasa ukichanganya sauti zote hizo unapata mziki wenye radha na maadhi ya aina yake.
Anyway tunahitaji kuishi kama binadam wacha nemc wa-impose hizo sheria.
 
WEWE NI MNAFIKI MKUBWA UNAYESIMAMA NA NGOZI YA UKRISTO. NINAKUKEMEA KTK JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETH USHINDWE. NA DAMU TAKATIFU YA YESU KRISTO ILIYOMWAGIKA MSALABANI KWA AJILI YA WENYE DHAMBI IKAFUTE LAANA ULIYOIACHILIA KWA RAIS WETU KIPENZI DR. JPM

UNAFIKI NI DHAMBI KUBWA SANA CHINI YA JUA!!!!!!

WEWE NI NANI HATA UMWAMBIE RAIS WETU UFALME WAKE UMEFIKA MWISHO!!!! UNA USAFI GANI HAPO ULIPO HATA UFIKIE KIWANGO CHA KIROHO CHA DANIEL. SITAKI KUYAWEKA MAMBO YAKO HUMU ILA NAKUONYA USIRUDIE TENA KUFANYA USHETANI HUU!!!

MKRISTO ALIYEJAZWA ROHO MTAKATIFU NGUVU YAKE IKO MAGOTINI. ULIMI WAKO UMEJAA LAANA BADALA YA BARAKA. HIZO LAANA ZIKURUDIE NA KUWA KAMA VAZI MAUNGONI MWAKO. WAKRISTO WENZIO WANAFUNGA NA KUOMBA KUMUOMBEA MHE. RAIS KTK MAENEO YOTE WEWE UNAACHILIA LAANA????? SHAME ON YOU!!!!!!! UMEISOMA VIZURI HIYO SHERIA NA KUIELEWA????

HIVI INJILI NI LAZIMA IHUBIRIWE KWA KUPAYUKA????? MIAKA ILE WAKATI TUNAOKOKA INJILI ILIKUWA MAN TO MAN. HUPANDI DALADALA AU BASI AU NDEGE NA KUFIKA UPANDE WA PILI BILA KUMSHUHUDIA MTU. WEWE LEO HATA JIRANI ZAKO NA UNAOFANYA KAZI NAO WANATILIA MASHAKA WOKOVU WAKO MAANA MATENDO YAKO HAYAFANANI NA NENO LA KRISTO!!!

INJILI YA LEO INA WAPIGA DEAL WANAFIKI WAKUBWA NA WAFANYABIASHARA. HIYO NI DALILI YA MAFARISAYO. UNGEKUWA UNA ROHO WA BWANA WEWE UNGEKAA MAGOTINI NA KUJUA TZ INAPITA KTK MAJIRA GANI YA KIROHO!!!!

UMENIUZI SANA KWA JINSI ULIVYOKOSA HEKIMA!!!!!! NA MANENO MABAYA ULIYOYATUMIA KWA RAIS WETU HALAFU UNAJIITA MKRISTO a.k.a FARISAYO

NAOMBA MLIONIELEWA MUMPUUZE HUYU FARISAYO NA MSIACHE KUMUOMBEA RAIS WETU. MAOMBI YAONGEZEKE BAADA YA KUMUONA ADUI WA NYUMBANI MWETU.

MUNGU AKULINDE RAIS WETU (Zakaria 4:5). UKAFANYIKE BARAKA KWA TAIFA LA TZ NA KWA WATANZANIA WOTE MUNGU ALIOWAWEKA MIKONONI MWAKO. HEKIMA KAMA ZA MFALME SULEIMAN ZIENDELEE KUTIRIRIKA KUANZIA KICHWANI MWAKO NA KUSHUKA KAMA MAFUTA NDEVUNI MWA HARUNI HADI KWA WATU WAKO. (ZABURI 41:1-2).

Queen Esther

Ameen.
 
Hii sheria mbona ipo siku zote? Je, si kwamba utekelezaji wake tu ndio ulikuwa tatizo?

Kwa maoni umetia chumvi nyingi sana juu ya agizo hili ambalo kiuhalisia NEMC wanakumbusha watu kuzingatia sheria za mazingira ktk kila wanalolifanya.

Sina hakika kama hili linahusu na sauti za vipaza sauti zinazotoka ktk misikiti au matangazo ya mikutano ya dini au hata matangazo ya serikali ambapo gari maalumu hupita mitaani na kutangaza juu ya jambo flani labda kinamama kupeleka watoto ktk chanzo nk

Hii inahusu mfano kumbi za disco zisizokidhi viwango na zinazopiga muziki usiku kucha katikati ya makazi ya watu, watu wenye sherehe za harusi kupiga muziki usiku kucha nje ya nyumba zao kiasi ambacho inaleta usumbufu mkubwa kwa watu hata wasiohusika hata kushindwa kulala!!

Hapa mtaani kwetu kuna baa moja yaani inatuletea usumbufu wa hali ya juu kwa kupiga muziki mkubwa karibu mchana kutwa hadi usiku.

Hii sheria inawahusu watu kama hawa wasiojali haki za watu wengine
 
Ona mnakimbilia miavuli wkti kila siku tunasikia magari ucku yana pita yakitangaza disco toto na matamasha makubwa
 
Tumechoka Na Makelele ya KWAYA kila siku.
Bora yakomeshwe.

Walokole Nuksi
 
Siku mbili zilizopita vyombo vya habari vimeripoti kwamba NEMC imetangaza kwamba kuanzia sasa mirindimo yoyote na kelele zozote zinazohusiana na sherehe, matangazo, sauti kubwa kutoka majumba ya starehe, magari ya poromosheni, makanisani yatakuwa yanalipiwa shilingi milioni 5 hadi milioni 10. Na kwa yule atakayekiuka atatozwa shilingi milioni 50 ama kufungwa jela.

Kiuhalisia, hakuna kanisa ambalo litaweza kulipa shilingi milioni 5 kwa mkutano wa Injili ya Kristo kwa siku moja hata ingekuwa kwa mwezi. Kwa maana nyingine makanisa yamefungwa speed governor ya kutangaza Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni.

Chini ya utawala huu wa awamu ya tano, iwapo NEMC watatekeleza hiyo sheria yao, basi Habari Njema za Ufalme wa Mbinguni zitaadimika kwa kiasi kikubwa.

Historia ya kanisa inaonesha kwamba yeyote aliyejaribu kuzuia makusudi ya Mungu wa mbinguni, mtu huyo aliondoshwa kabla kusudi hilo halijapotea. Mfano mzuri wa Biblia ni ule wa mfalme Herode ambaye tunasoma habari zake katika kitabu cha Mathayo sura ya pili.

ANGALIZO: Wote wenye mamlaka tufahamu kuwa mamlaka kuu ni ya Mungu wa Mbinguni; tuelewe kwamba hakuna atakayenyoosha kidole karibu na mboni ya jicho la Bwana akanusurika, mfalme Belshaza wa Ukaldayo; dola iliyokuwa ikitawala takribani dunia nzima; alijikinai akidhani ni mkuu mno mwenye kuweza kuchafua na kunajisi vyombo vya hekaluni kwa Mungu. Mungu alimfutia ufalme wake akaugawa kwa Waajemi na Wamedi. Daniel sura ya 6.
Mbona ukifika airport watu wamejaa saa kumi za usiku bila kuamshwa wala kupigiwa kelele? Mbona maelfu ya wanafunzi wanafanya mitihani yao? Mbona mnapotoa michango ya harusi hamkumbushwi kwa magari ya matangazo? Acheni kujificha katika dini ili kufanya upuuzi usiomithilika, kama huamini huamini tu, nani kawatangazia mkusanyika kunywa pombe na kupiga kelele mkesha wa mwaka mpya, usisingizie watu kama huna utashi huna tu
 
Wasitupigie kelele bwana Dini gani hiyo ya vurugu????
 
Back
Top Bottom