Mende ni kero kwenye wodi za hospitali ya Benjamin Mkapa

IHOLOMELA

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,807
1,672
Kwa uongozi wa hospitali,

Nachukua fursa hii kutoa malalamiko yangu kuhusu suala la mende katika wodi za kulazwa wagonjwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa hapa Dodoma. Ingawa hospitali hii inatoa huduma nzuri kwa ujumla, suala la mende katika Wodi mbalimbali hospitalini hapo ni kero kubwa inayotia doa hospitali hii kubwa na yenye ubora hapa nchini.

Mende wamekuwa wakitambaa juu ya vitanda vya wagonjwa, vifaa vya tiba, na hata kwenye kuta za vyumba vya wodi. Hali hii ni hatari sana kwa afya na ustawi wa wagonjwa, na kwa kweli linakwenda kinyume na azma ya hospitali hii kutoa huduma bora na mazingira salama na safi.

Naomba uongozi wa hospitali hii kuweka mkazo kuhusu katika usafi na furmigation mara kwa mara na pia kuwa na utaratibu mzuri wa kusafisha na kutunza wodi. Pia ni muhimu kwa hospitali kuwa na ukaguzi wa mara kwa mara wa mazingira ili kubaini chanzo cha tatizo hili na kuweka mikakati sahihi ya kudhibiti mende kwa njia inayofaa.

Kwa sababu hiyo, tungependa kuona uongozi wa hospitali ukiangalia suala hili kwa umakini na kuchukua hatua za haraka kulimaliza tatizo hili la mende.

Tunatarajia kuona hatua za haraka zikichukuliwa kukabiliana na tatizo la mende katika wodi za kulazwa wagonjwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa. Tutafuatilia kwa karibu utekelezaji wa hatua hizo na tunatarajia kusikia kutoka kwa uongozi wa hospitali katika kipindi kifupi.
 
Kero kama hii nenda ofisi ya mganga mkuu mwambie / mchane . Ukiona ukanyamaza mwingine anaona na ananyamaza hivyo hivyo na hili ni tatizo kubwa
 
Hii ni chai aisee...Hospitali ya Benjamin Mkapa ni mojawapo ya Hospitali zinazojali usafi sana.Niliwahi kumuuguza mgonjwa pale kwa takribani wikinzima ni pasafi wanajitahidi sana .Mazingira yote ya hospitali ni pasafi labda mtoa mada utuambie hao mende wanaotambaa hadi kwenye vitanda vya wagonjwa wapo wodi ipi😀😀.

Changamoto pekee niliyo-inotice ni kule chini kama unaelekea COED UDOM kule kwenye uwanja wa mpira kuna harufu kali sana ya majitaka inayosambaa ambayo inaweza kuathiri wagonjwa.

Nadhani yale mashimo ya majitaka yalipaswa yajengwe mbali sana na eneo la Hospitali/Chuo.
 
Si wanasema Mende sijui wana Vitamini na Protini za kutosha,basi wawale tu wawapunguze kuliko kuingia gharama nyingine za Fumigation.
 
Na yale m
Hii ni chai aisee...Hospitali ya Benjamin Mkapa ni mojawapo ya Hospitali zinazojali usafi sana.Niliwahi kumuuguza mgonjwa pale kwa takribani wikinzima ni pasafi wanajitahidi sana .Mazingira yote ya hospitali ni pasafi labda mtoa mada utuambie hao mende wanaotambaa hadi kwenye vitanda vya wagonjwa wapo wodi ipi😀😀.

Changamoto pekee niliyo-inotice ni kule chini kama unaelekea COED UDOM kule kwenye uwanja wa mpira kuna harufu kali sana ya majitaka inayosambaa ambayo inaweza kuathiri wagonjwa.

Nadhani yale mashimo ya majitaka yalipaswa yajengwe mbali sana na eneo la Hospitali/Chuo.
NA YALE MAjitaka ni ya COED
 
Afadhali mende kuliko panya, kuna hospitali zingine mende wametamalaki wanasumbua wagonjwa hata mchana. Unakuta usiku wanawatambalia wagonjwa vitandani wakitafuta cha kutafunatafuna, mara wako kichwani wakidokoa nywele, mara kwenye viganja vya mikono na miguu, ni wasumbufu balaa
 
Na yale m

NA YALE MAjitaka ni ya COED
Ok sawa...kuna mwanachuo mmoja aliniambia pale chini bondeni ndio system ya kukusanya majitaka yote ya COED sasa sijajua kama ile system inakusanya pamoja na majitaka ya Hospital ya Benjamin Mkapa
 
"Tutafuatilia kwa karibu utekelezaji wa hatua hizo na tunatarajia kusikia kutoka kwa uongozi wa hospitali katika kipindi"


Sawa mkuu, uongozi husika utatekeleza agizo lako.
 
Asenga ambaye ni katibu wa afya hapo hospitalini,ninaamini atalifanyia kazi hili suala,na kulimaliza kabisa.Huyu mtu ni makini sana, yawezekana wasaidizi wake hawajaripoti hilo suala,ofisini kwake.
Dr.Bush ajitahidi kumsaidia Asenga,kwenye masuala kama hayo na yote yale yanayoshabihiana na hilo.Wawavane hao kampuni ya usafi,iitwayo RIK,wafanye usafi wa kina.
 
Mleta mada mjasiriamali na ana kampuni ya fumigation, ukienda vyoo ni vyoo ni visafi, hao mende ameona alete chai ili baadaye Akaombe kazi
 
Kero kama hii nenda ofisi ya mganga mkuu mwambie / mchane . Ukiona ukanyamaza mwingine anaona na ananyamaza hivyo hivyo na hili ni tatizo kubwa
Hivi hospital panakuaje na mende!?..Tena hospital kubwa Kama hiyo,sisi waafrika tuna shida sana
 
Hii ni chai aisee...Hospitali ya Benjamin Mkapa ni mojawapo ya Hospitali zinazojali usafi sana.Niliwahi kumuuguza mgonjwa pale kwa takribani wikinzima ni pasafi wanajitahidi sana .Mazingira yote ya hospitali ni pasafi labda mtoa mada utuambie hao mende wanaotambaa hadi kwenye vitanda vya wagonjwa wapo wodi ipi😀😀.

Changamoto pekee niliyo-inotice ni kule chini kama unaelekea COED UDOM kule kwenye uwanja wa mpira kuna harufu kali sana ya majitaka inayosambaa ambayo inaweza kuathiri wagonjwa.

Nadhani yale mashimo ya majitaka yalipaswa yajengwe mbali sana na eneo la Hospitali/Chuo.
Ulimuuguza lini?
 
Hamna mdudu ambaye dah ananikera ndan kama mendi

X10 panya ILA sio mende
 
Mleta mada mjasiriamali na ana kampuni ya fumigation, ukienda vyoo ni vyoo ni visafi, hao mende ameona alete chai ili baadaye Akaombe kazi
Naongea kweli tupu, wodi tatu nimeingia kusalimia wagonjwa nimeshuhudia hao Mende!
 
Hii ni chai aisee...Hospitali ya Benjamin Mkapa ni mojawapo ya Hospitali zinazojali usafi sana.Niliwahi kumuuguza mgonjwa pale kwa takribani wikinzima ni pasafi wanajitahidi sana .Mazingira yote ya hospitali ni pasafi labda mtoa mada utuambie hao mende wanaotambaa hadi kwenye vitanda vya wagonjwa wapo wodi ipi.

Changamoto pekee niliyo-inotice ni kule chini kama unaelekea COED UDOM kule kwenye uwanja wa mpira kuna harufu kali sana ya majitaka inayosambaa ambayo inaweza kuathiri wagonjwa.

Nadhani yale mashimo ya majitaka yalipaswa yajengwe mbali sana na eneo la Hospitali/Chuo.
Hata asubuhi hii nimetoka kumuona mgonjwa wetu wodi ya wanaume waliofanyiwa surgery ghorofa ya kwanza, mende wapo wanapita pita. Ngoja nikienda nikapige picha japo wameweka bango la kuzuia kupiga picha
 
Kwa uongozi wa hospitali,

Nachukua fursa hii kutoa malalamiko yangu kuhusu suala la mende katika wodi za kulazwa wagonjwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa hapa Dodoma. Ingawa hospitali hii inatoa huduma nzuri kwa ujumla, suala la mende katika Wodi mbalimbali hospitalini hapo ni kero kubwa inayotia doa hospitali hii kubwa na yenye ubora hapa nchini.

Mende wamekuwa wakitambaa juu ya vitanda vya wagonjwa, vifaa vya tiba, na hata kwenye kuta za vyumba vya wodi. Hali hii ni hatari sana kwa afya na ustawi wa wagonjwa, na kwa kweli linakwenda kinyume na azma ya hospitali hii kutoa huduma bora na mazingira salama na safi.

Naomba uongozi wa hospitali hii kuweka mkazo kuhusu katika usafi na furmigation mara kwa mara na pia kuwa na utaratibu mzuri wa kusafisha na kutunza wodi. Pia ni muhimu kwa hospitali kuwa na ukaguzi wa mara kwa mara wa mazingira ili kubaini chanzo cha tatizo hili na kuweka mikakati sahihi ya kudhibiti mende kwa njia inayofaa.

Kwa sababu hiyo, tungependa kuona uongozi wa hospitali ukiangalia suala hili kwa umakini na kuchukua hatua za haraka kulimaliza tatizo hili la mende.

Tunatarajia kuona hatua za haraka zikichukuliwa kukabiliana na tatizo la mende katika wodi za kulazwa wagonjwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa. Tutafuatilia kwa karibu utekelezaji wa hatua hizo na tunatarajia kusikia kutoka kwa uongozi wa hospitali katika kipindi kifupi.
Hapo ukitoka hospitali,unaondoka na mende kwenye vitu vyako ulivyokuwa navyo hospital. Mwisho wa siku nyumbani kunakuwa na mende.
 
Back
Top Bottom