Men only (inahusu wanaume)

Men only (inahusu wanaume)

Professor of jungle

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2012
Posts
480
Reaction score
942
HESHIMA PESA, NDEVU HATA MBUZI ANAZO.

Sio nia yangu kuponda au kusolola mtu kumdogofisha au kufanya ajiskie mnyonge. Ila haya mambo tusipoyasikia toka kwenye vinywa vya watumishi wa Mungu haitaleta uzito.

Kuna wanaume wengi ambao sasa inabidi kusema bila kuficha kuwa wanatia aibu. Hakuna kitu kibaya duniani kama Mwanaume kukosa hela au nguvu ya kiuchumi.

Hata maandiko yanaweka wazi kuwa hekima ya maskini hudharaurika. Mwanaume kuwa na maneno mengi na mfuko tupu utaishia kukasirikia watu na kuweka vinyongo.

Wengi wanakwambia kazi hakuna, sijui ajira ngumu ila ukweli ni kwamba ni wavivu na wanachagua kazi.Unakuta mtu anamcheka muuza mkaa au muuza machungwa, anamdharau dereva wa bodaboda wakati yeye anakaa kwa shemeji hana mbele wala nyuma.

Dereva wa bodaboda anaingiza faida ya elfu hamsini kila siku 50000/= na hiyo ni kwa siku ambayo biashara haikuwa nzuri. Wako watu wanavibanda vya matunda wanaingiza mpaka laki moja T.Shs 100,000/= hakatwi TRA wala NSSF kwa siku. Wewe unaita hiyo kuwa ni kazi ya kijinga huwezi kufanya.

Umekalia kuzunguka maofisini na Bahasha ya kaki kutafuta ajira ambayo hata ukiajiriwa unalipwa Milion moja, ikikwanguliwa Makato unakuta kwa mwezi unapokea laki Saba au less.700,000/= ukipitia hesabu ya nauli kwenda na kurudi kazini, chakula na vocha unakuta mwezi mzima unafanya kazi shilingi laki moja 100,000/= ambayo mwenzako anaingiza kila siku. Usidharau kazi.

Usibweteke kama Mwanaume ukabaki kulaumu watu kuwa wamegoma kukusaidia. Mwanaume jiongeze. Kesho tu utakuwa Baba wa familia, kwani mkeo naye unategemea kaka zako watakusaidia kutunza?

Unawaza nini juu ya maisha ya kesho?Mwingine uko Chuo unalipwa Boom unanunua simu ya laki Saba na jeans, hata kusoma husomi kutwa uko Facebook, WhatsApp na Instagram unatupia picha tu.

Kesho simu halina hata vocha huwezi ku-access internet unabaki kucheza game. Wakati wenzako hilo Boom wanajinyima wanaanzisha miradi. Mpaka anamaliza Chuo tayari alishajitengenezea ajira.

Wakati wewe unahangaika na Bahasha kutafuta ajira mwenzako anaitwa Boss anaajiri. Hebu fungua fahamu zako, utakuwa tegemezi mpaka lini?Mwanaume ni chachu ya mabadiliko. Mwanaume ni kiongozi.

Najua unamaono makubwa na ndoto kubwa lakini kabla ndoto hazijatimia lazima kuwe na chakula mezani, kuwe na mavazi mwilini, na kuwe na nyumba ya kuishi (Kodi). Hayo hayatasubiri mpaka uwe Billionaire ni mahitaji ya kila siku.

Pata shughuli ya kufanya. Jiongeze. Usiwaze sijui watu watakudharau, sijui watu watakuonaje? Wakati njaa inakukong'ori utakuwa peke yako chumbani. Potezea watu, weka heshima pembeni, ingia mzigoni. Tengeneza PESA.

Namaliza na waimbaji mnaozunguka na CD makanisani mkitafuta nafasi za kuimba na mwisho mpewe "nauli" hakuna future ktk Hilo. Jipe shughuli itakayokuingizia PESA ili ufanye huduma kwa moyo na sio kwa kutazama pesa.

Ndio maana mkialikwa makanisa madogo hamuendi kwasababu mnajua hakuna hela huko. Mnaishia kununuliwa na kuendeshwa. Kipaji bila hela ni mzigo tu. Angalia Muhindi hajui kuimba wala hajui kiswahili vizuri lakini wasanii wanampigia magoti.

Pesa ni jawabu. Pambana upate pesa na ni mpango wa Mungu utajirike. Sukuma toroli la maji cha msingi unaingiza pesa. Acha upedeshee na nguo za kuazima. Loh! Mwanaume hasifiwi usafi wala uzuri wa uso, mwanaume anasifiwa uchapakazi.

Kukaa kanisani masaa 24 unaomba bila kujishughulisha hiyo ni kazi ya wajane waliovuka miaka 60, wewe toka nje pambana ulete sadaka na fungu la kumi.

KUMBUKA HESHIMA PESA, NDEVU HATA MBUZI ANAZO.Hii nayo ni habari njema. (2Wathesalonike 3:10)
 
Inawezekana ni mada nzuri ila haivutii kusoma, haina aya, inachosha na inakatisha tamaa kusoma.
 
kwani wewe ni bilionea gani ?
au le billionea le mutuz
 
HESHIMA PESA, NDEVU HATA MBUZI ANAZO.
Sio nia yangu kuponda au kusolola mtu kumdogofisha au kufanya ajiskie mnyonge. Ila haya mambo tusipoyasikia toka kwenye vinywa vya watumishi wa Mungu haitaleta uzito. Kuna wanaume wengi ambao sasa inabidi kusema bila kuficha kuwa wanatia aibu. Hakuna kitu kibaya duniani kama Mwanaume kukosa hela au nguvu ya kiuchumi. Hata maandiko yanaweka wazi kuwa hekima ya maskini hudharaurika. Mwanaume kuwa na maneno mengi na mfuko tupu utaishia kukasirikia watu na kuweka vinyongo.
Wengi wanakwambia kazi hakuna, sijui ajira ngumu ila ukweli ni kwamba ni wavivu na wanachagua kazi.
Unakuta mtu anamcheka muuza mkaa au muuza machungwa, anamdharau dereva wa bodaboda wakati yeye anakaa kwa shemeji hana mbele wala nyuma. Dereva wa bodaboda anaingiza faida ya elfu hamsini kila siku 50000/= na hiyo ni kwa siku ambayo biashara haikuwa nzuri. Wako watu wanavibanda vya matunda wanaingiza mpaka laki moja T.Shs 100,000/= hakatwi TRA wala NSSF kwa siku. Wewe unaita hiyo kuwa ni kazi ya kijinga huwezi kufanya.
Umekalia kuzunguka maofisini na Bahasha ya kaki kutafuta ajira ambayo hata ukiajiriwa unalipwa Milion moja, ikikwanguliwa Makato unakuta kwa mwezi unapokea laki Saba au less. 700,000/= ukipitia hesabu ya nauli kwenda na kurudi kazini, chakula na vocha unakuta mwezi mzima unafanya kazi shilingi laki moja 100,000/= ambayo mwenzako anaingiza kila siku. Usidharau kazi. Usibweteke kama Mwanaume ukabaki kulaumu watu kuwa wamegoma kukusaidia. Mwanaume jiongeze. Kesho tu utakuwa Baba wa familia, kwani mkeo naye unategemea kaka zako watakusaidia kutunza?
Unawaza nini juu ya maisha ya kesho?
Mwingine uko Chuo unalipwa Boom unanunua simu ya laki Saba na jeans, hata kusoma husomi kutwa uko Facebook, WhatsApp na Instagram unatupia picha tu. Kesho simu halina hata vocha huwezi ku-access internet unabaki kucheza game. Wakati wenzako hilo Boom wanajinyima wanaanzisha miradi. Mpaka anamaliza Chuo tayari alishajitengenezea ajira. Wakati wewe unahangaika na Bahasha kutafuta ajira mwenzako anaitwa Boss anaajiri. Hebu fungua fahamu zako, utakuwa tegemezi mpaka lini?
Mwanaume ni chachu ya mabadiliko. Mwanaume ni kiongozi.
Najua unamaono makubwa na ndoto kubwa lakini kabla ndoto hazijatimia lazima kuwe na chakula mezani, kuwe na mavazi mwilini, na kuwe na nyumba ya kuishi (Kodi). Hayo hayatasubiri mpaka uwe Billionaire ni mahitaji ya kila siku. Pata shughuli ya kufanya. Jiongeze. Usiwaze sijui watu watakudharau, sijui watu watakuonaje? Wakati njaa inakukong'ori utakuwa peke yako chumbani. Potezea watu, weka heshima pembeni, ingia mzigoni. Tengeneza PESA.
Namaliza na waimbaji mnaozunguka na CD makanisani mkitafuta nafasi za kuimba na mwisho mpewe "nauli" hakuna future ktk Hilo. Jipe shughuli itakayokuingizia PESA ili ufanye huduma kwa moyo na sio kwa kutazama pesa. Ndio maana mkialikwa makanisa madogo hamuendi kwasababu mnajua hakuna hela huko. Mnaishia kununuliwa na kuendeshwa. Kipaji bila hela ni mzigo tu. Angalia Muhindi hajui kuimba wala hajui kiswahili vizuri lakini wasanii wanampigia magoti. Pesa ni jawabu. Pambana upate pesa na ni mpango wa Mungu utajirike. Sukuma toroli la maji cha msingi unaingiza pesa. Acha upedeshee na nguo za kuazima. Loh! Mwanaume hasifiwi usafi wala uzuri wa uso, mwanaume anasifiwa uchapakazi. Kukaa kanisani masaa 24 unaomba bila kujishughulisha hiyo ni kazi ya wajane waliovuka miaka 60, wewe toka nje pambana ulete sadaka na fungu la kumi. KUMBUKA HESHIMA PESA, NDEVU HATA MBUZI ANAZO.
Hii nayo ni habari njema. (2Wathesalonike 3:10)

Hapo kwenye Red nikweli kabisa mkuu;90% ya university students tuko hivyo!
 
Riziki anatoa mungu lkn inabidi kufanya kz kwa bidii,c vyema kwa mwanaume kukaa bure bila shughuli na shughuli zinatafutwa na ni vema mtu ukawa mbunifu wa miradi mbalimbali na kuwa mbunifu pia wa kutafuta mtaji,hakika ndg yng koromeo umenena vyema sana,bg up ndg
 
Thanx broo, mimi naanza mazoezi ya kuondoa aibu ili nianzishe biashara ya kuuza makopo.
 
Koromeo ubarikiwe,Thread yako ina maana sana.
Hivi leo mabinti wengi wanakaribia kutupita
sisi wanaume,kwa kujitoa muhanga kujishughulisha
wakati wanaume wanaona soo,eti watachekwa.

Binafsi naona ni heri uchekwe ukitumia nguvu zako
kutafuta kipato,kuliko kuchekwa unapoenda mahali kuombafedha.
Wengi wanaishia kugombana na mashemeji zao
eti kaka kaoa mke bahiri,toka ameoa pesa hatupewi.
Huu usemi hautakiwi kotoka kinywani
mwa mwanaume anayejitambua.
 
Last edited by a moderator:
Elimu ya bongo kabla ya kuwaongezea ujasiri na kutokuwa na aibu kwenye kutafuta hela badala yake inageuza mchapakazi kuwa mvivu, bishoo, na kuwa selective wa kufanya baadhi ya kazi.Mi nimekuelewa mtoa mada huu ujumbe uanzie na kwako
 
huu uzi wanaume wengi wataukandia ila mtoa mada umeongea kwel tupu..........mwanaume kuwa omba omba na kutegemea ndugu haifai.............vijana siku izi wanajisifia idad ya madem na uzur wa nguo/simu badala ya kujisifia kunona account bank etc.......aibu sana
 
Kwakweli huu ujumbe umetulia sana..kazi ni kwenye kutekeleza
 
big up kaka kwa ujumbe wako maana vijana wanashinda kwenye vijiwe kazi yao ni kugongea tu,,
 
ukipita kuwapa hi mda huo umetoka mzigo umechoka kinyama utasikia bro huna hata jero la karibu hapa? nimeuawa mwanangu.
 
Back
Top Bottom