Membe unajua jengo la ubalozi haliguswi, linalindwa na kuheshimiwa kama sehemu ya nchi husika. Sasa wenzetu wana ubalozi wao huko nyumbani na balozi wao Dk Bilal ni high kamishna maana hata gari lake nasikia mmemwekea ngao ya taifa, tena ana msafara tofauti na mabalozi wengine. Huyu ikitokea vurugu hatasita kuwapa hifadhi ndugu zake katika jengo la ubalozi wao. Katika songombingo za huku na maboti kujaa abiria, tulishindwa pa kukimbilia. Tusingeweza wote kukimbilia makanisani kwa sababu wengine sio waumini halafu walisema wangeyachoma makanisa yenyewe. Hatuna balozi wa kututetea. Membe mwambie JK anunue jengo la ubalozi kisha mteueni nani yule sijui.....aje awe balozi wetu huku, tupate kinga ya kidiplomasia wenzetu wanapopandisha mori.
Asante sana
Asante sana