habari ya hapa
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 12,789
- 8,752
Heko heko Comrade Membe, kwa sasa wewe mwanga kwa maccm wenzio,
Tabia ya mtu hujitokeza hasa anapokosa anachokitaka.huu ni unafiki mbaya sana.siku zote mbona hakuwahi kukosoa utawala was ccm? Ajitokeze kwenye vyombo vya habari atangaze kupinga utawala was magufuliKwani kuna kipi cha ajabu hapa,Membe hakuongelea suala la uchaguzi Zanzibar?
Sasa kama aliweza kuongelea suala zito kama lile hili atashindwa vipi?
Aliyekuwa waziri wa mashauri ya nje, Ndg.Membe amewajibu wanaotaka akae kimya kuwa hawezi kunyamaza na anatumia haki yake kikatiba bila kuvunja sheria. Membe amewataka wajibu kwa hoja badala ya kumziba mdogo. Membe ameongeza kuwa baadhi ya wana CCM wamekuwa wanafiki wa kutupwa na hawataki Magufuli akosolewe. Atakuwa mstari wa mbele kutoa maoni huru kwa mambo yanayoendelea bila kuvunja sheria.Amesisitiza kuwa rais Kikwete atakumbukwa sana kwa kuwapa watu uhuru wa kutoa maoni yao
Kweli mkuu vita ya panzi, harafu wataropoka mengi tu hali inavyoonesha maana huyu kiongozi anashambulia balaaNahisi kuna mgogoro mkubwa ndani ya CCM,mpaka Membe anajitokeza hadharani kusema haya basi amini nawaambieni kuna kundi kubwa nyuma yake linalompa ujasiri huu.
Hata hivyo wanazidi kuturahisishia kazi 2020 sio mbali.
Kwa hiyo Membe ana ile roho ya kwa nini afanye yeye. ?Ni wazi kabisa kuwa team Jk hawafurahishwi na mengi yanayofanywa na Magufuli kwakuwa
1.halikuwa chaguo Lao tangu mwanzo
2.anagusa maslahi yao
3.anagusa maslahi ya 'watu' wao
4.anawavua nguo peupe kwa timua timua ya watendaji walioteuliwa kipindi chao na kuibua kila aina ya uozo
5.ongezeko la mapato ya TRA linawaumbua kuwa hawakuwa makini
Orodha ni ndefu na kwakweli watafanya kila juhudi kumkwamisha ili aonekane hafai
Time will tell. ...!!!
Subiri uone huko mbeleni watakavyotibuanaKwa hiyo Membe ana ile roho ya kwa nini afanye yeye. ?
Walitegemea Magufuli atachemsha ili tuukumbuke utawala wa Msoga bahati ndio anawaumbua kila kitu kiko wazi.
CCM tunao watu wapumbavu sana... Yaani hawataki Magufuli akosolewe... Ni ujinga... Magufuli sio malaika, hivyo lazima akosoleweHaki yake kuongea msitake kumfanya magufuli ni malaika nadhani yupo sahihi jibuni hoja cyo vijembe kwan hoja hujibiwa na hoja
Kikwete ndio rais bora kuliko wote waliopita hivi sasa kiongozi wa umma huna uhakika kesho kama utarudi kazini ni presha tuMwambieni basi amtaje mtanzania hata mmoja atakayemkumbuka rais mstaafu! Ninachokiona hapa, hili nalo limeiva tena dokta kalichelewesha mno.