Membe kuwania urais 2015...

Niko tayari kumpatia kura yangu ya ndiyo maiti kuliko kumpatia membe. huyu jamaa ni kibaraka mkubwa sana wa iran na katekwa sana na mataifa ya kiarabu. hajui nini atendalo wala nini tanzania inatakiwa kufanya ili kukuza maisha ya raia.


kakataa kufungua ofisi ya ubalozi nchini tel aviv na kisha kaenda kufungua kule oman! ubalozi wa uingereza ulichukizwa sana na tabia yake ya kuwaruhusu wamisri kuwatukana waingereza na hatuba zao za matusi kuandikwa katika gazeti la daily news wakati misri ilivyokuwa inaadhimisha miala 61 ya uhuru wake.

hajui kutumia busara wala akiri za kuzaliwa. yeye ni bora liende tuu.
 
Ni upuuzi kumlinganisha EL na Membe. EL mtendaji asiye na kifani
 
Wanaotaka kujenga kiwanda cha Cement Mtwara ni Dangote Cement, kampuni ya ki Nigeria inayomilikiwa na Mzee Dangote tajiri namba moja Africa. Pia akina TIOT wale wa mafuta wa Morogoro wasiojua cement ni nini pia wanataka kujenga.

Tatizo hapo ni TIOT ni Mudhiir na Dangote ni "Nyoka wa Mdimu". Malighafi ndo inagombaniwa maana kila mwekezaji lazima aangalia sustainability ya malighafi.

Ugomvi unaanzia hapo. Kila mmoja akitaka kiwanda kijengwe jimboni kwake.

Kwa urais ni Lowassa tu. Wengine tulieni.
 
Didi you mention the names Benard Membe for presidency 2015 thi mighty nation of Tanzania? Sorry, better re-organise your political cards a fresh on this wave-lenth please!

Internationally speaking, he has a lot of long-term personal re-packaging to make to fit the shoes of the much salivated seat just as much as, locally, he just can't shed-off the new-found anti-incubency bitterness at the backdrops of withered hopes for a new people constitution.

The sum total is that Membe broke loose into a chase after his dreams (of becoming a president) in the wilderness with a false step foward ever!!

Sijui atatoka vipi humo.
 


Hapo kwenye red naomba niseme natamani ningekuwa mwanasheria kitaaluma. Lakini kwa vile sina weledi wa sheria au kutabaharia katika fani hiyo, ninashindwa kutekeleza ombi lako.

Bila kumung'unya maneno na kufumba fumba, ukweli ni kwamba Lowassa amegundua kwamba in Membe he has a formidable challenger who can scuttle his bid to State House. Vita vilivyoanza na vitakavyoendelea kati ya sasa na miaka iliyobakia kuelekea 2015 ni ya kuhakikisha kwamba anamrarua membe kadri anavyoweza, kwa kutumia watu kama nyie ambao mnajifanya hamumuungi mkono Lowassa na wakati mwingine kujifanya hamtaki mgombea wa CCM kumbe ni mbinu yenu kwa vile mnajua mgombea anayeitwa Lowassa hakubaliki kamwe. Mnapojichanganya na kuacha traces ni pale mnapojifanya eti "Lowassa hatumtaki lakini kwa kulinganisha na Membe, basi bora Lowassa". Hizo pedestrian arguments na in the absence of a check list ya wagombea urais, utasemaje kwamba fulani hana sifa, lakini huelezi sifa ni zipi. At least tunajua kwamba uadilifu na kuwa na elimu nzuri, na uzoefu katika utumishi wa umma ni universal criteria na hizo Membe anazo. Tunajua pia kwamba Lowassa ana tatizo la kukosa uadilifu na hata vikao vya chama na bunge vinajua.

Come out clean boy. Turidhishe kwamba there is sense katika hoja zako!
 

Napenda uthubutu wako na kuonyesha wazi kwamba wewe Lowassa ndiyo chaguo lako, siyo wale wanafiki wengine wanaojifanya hawamuungi mkono, yet wako busy kushambulia perceived adversaries wa Lowassa.

Hata hivyo rejea makala ya Mzee Kisori.
 
Ni upuuzi kumlinganisha EL na Membe. EL mtendaji asiye na kifani

Nakubaliana na wewe babaa kwamba ni ujuha kulinganisha Shetani na Malaika! Shetani aliyejificha katika kichaka cha utendaji kazi hata siku moja haishiwi ushetani wake. Kwanza huo utendaji mbona hatuajuona? Halafu kwa kusema yeye ni mchapakazi, analinganishwa na nani na katika nafasi ipi? Ondoeni hii myopia.
 
mtu pekee ambae yuko ndani ya ccma ambae kidogo anaweza kugombea urais ndani ya ccm na wananchi wakawa na imani nae ni Dr.John Pombe Magufuli.This is the truth ingawa vigogo wa ccm hawamtaki kwasababu wanajua jamaa ni very strictly wanaofia wakimpa madaraka anaweza kuwasurubu kwa maovu yao.MAGUFULI IS THE ONLY ONE WHO CAN SELL CCM TO THE ORDINARY MWANANCHI!!!
 
..naona siku hizi Membe yuko karibu sana na JK.

..tena hata ktk masuala yasiyohusiana na wizara ya mambo ya nje, kama mkutano na viongozi wa cdm, na ktk hotuba kwa wazee wa dsm.

..huenda anapewa "tuition" na kuwa groomed kwa nafasi ya Uraisi.

..kwa mtizamo wangu, come 2015 watu watataka Raisi mpya, siyo muendelezo wa Raisi anayeondoka.

..Membe anapaswa kujitofautisha na Kikwete.
 


- REspect Sana!

FMeS!
 
,
Mkuu Mbopo, ni ukweli yoye unayoyasema kumhusu Membe kuwa ndio kizingiti, now lets bet, nakuhakikishia katika vita hii ya kuingia ikulu, the real powers (hooks & crooks) lies with Lowassa!
 
WE MAY NOT KNOW WHO WILL BE THE NEXT PRESIDENT, BUT WE KNOW FOR SURE WHO WILL NOT BE. IT IS EDWARD NGOYAI LOWASSA!

Watch this space!
WE MAY NOT KNOW WHO WILL BE THE NEXT PRESIDENT, BUT WE KNOW FOR SURE WHO WILL NOT BE. IT IS BERNARD CAMILUS MEMBE!

We can bet, mimi niko tayari kudeposit agreed bid amount kwa Invisible!

Sababu why not Membe ni simple tuu, kwenye hili game la politics za kuelekea 2015, Membe ni boya tuu linaelea na kupeperushwa na upepo!. Zile enzi za yoyote atakayesimamishwa na CCM lazima atapita, are over now!, kumsimamisha Membe ni kuiweka CCM rehani kwenye game la sadakalawe! wait and see jinsi anatakavyo wekwa pembeni hata kabla ya 2015, mwakani EL anatinga tena ndani ya CC na Membe I doubt hata kama NEC atapita!,
 

You may be right but be sensible enough to identify the issue in contention. Hoja ya Mudavadi ilikuwa inajibu tuhuma kwamba Membe hakufanya chochote jimboni kwake. Kila mwenye akili timamu anajua kwamba kama utumishi wa jimbo ungekuwa ni kigezo cha kuwania kuteuliwa kugombea urais, basi mbunge wa Monduli asingethubutu hata kuulizia ofisi zinapotolewa fomu za kugombea urais.

Lakini Omutwale, wew ni nani mpaka udhani mapenzi yako ni kigezo cha kupatikana kwa kiongozi nchi hii?
 

So trivial and petty. Kwa taarifa yako urais hauwi determined na vitu vya kitoto kama hivyo. Mkapa anavaa cheni na alikuwa akifanya hivyo alipokuwa rais but he did well during his tenure. Suala la rangi ya magari inaonekana kuwaumiza sana, maana wewe unaakisi kile alichotumwa Lwanji pale bungeni last year. Mngejua taratibu za kidiplomasia msingeona kama hii ni big deal, lakini kwa vile watu ni maamuma wa eneo hili ndiyo maana makelele hayaishi. Kwa hiyo kwako wewe, cheni ni dosari kubwa kuliko wizi wa rasilimali na hazina ya nchi?
 
.......
Lakini Omutwale, wewe ni nani mpaka udhani mapenzi yako ni kigezo cha kupatikana kwa kiongozi nchi hii?

Ni Raia wa kawaida tu, mlipakodi na Mtanzania mpiga kura.

Labda Mbopo nikukumbushe, Husipoanza na moja huwezi kukusanya mia!
 
Halo hapo Madangwa umenigusa sana. Mimi namsubiri Mahumbika. Huyo anayemsifu Membe ni wa wapi? Membe hajafanya ya maana jimboni kwake.
Labda ataje na vijiji husika ambako hayo maendeleo yamefanyika!
Namsubiri nyumbani Mahumbika
 
Membe sio chaguo langu hata kidogo, labda niwe na psychological pronlems wakati wa kupiga kura. better kivuli kuliko membe. any way nimekumbulkia enzi za chama kimoja
 
Membe is not MY choice, kama ingalikuwa kipindi kile cha chama kimoja, basi bora nichague kivuli kuliko yeye. huku jimboni ni matatizo tu. infact he iz not elligible
 
Ni wapi alisema anagombea? Unatupa jiwe kichakani kuona nini kitatoka? umenoa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…