Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,053
Jamani naweza nisiwe na hoja ........
Ni vema umejitambua na kujihukumu mapema na kwa haki.
......Katika swala la Pesa za radar, jambo moja ambalo niliona Membe ana kifua kipana ni pale alipotamuka kwamba pesa lazima zirudi .......
Sasa wacha tukusaidie ili ukirudi uwe na hoja.
Ndo maana nilisema kwenye hoja yangu ya msingi kwamba hili jambo naliacha ili watu walichokonoe na kulijadili kwa upana zaidi. Mh. Membe alidandia tukio ambalo lilikuwa lazima litokee katika mkondo na staili lilivyotokea. Naamisha fedha kurudishwa Tanzania tena kupitia serikalini ilikuwa si jitihada za Kamati ya Mh. Membe wala hisani bali lazima kutokana na amri ya mahakama-Uingereza na msukumo wa serikali ukichagizwa na wabunge. Matamko ya serikali za wenzetu yanaogopwa kama baa la njaa, na amri pamoja na hukumu za mahakama zao zinaheshimiwa. Sio kama Serikali ya Tanzania inatunishiwa kifua na Meneja wa Kampuni kama BP kisha inanywea.
Baada ya hukumu ya BAE iliyofuatiwa na kauli za serikali ya UK zikishagizwa na wabunge wakitaka BAE watekeleze hukuma kama walivyoagizwa, Mh. Membe akapata fursa ya kuokota mpira nyavuni wasiojua wakashangilia wakidhani Mtanganyika Mh. Membe ndiye kafunga goli!
BAE na kampuni yoyote ile haina jinsi yoyote ambayo inawawezesha kudharau au kutotii hukumu na amri za mahakama na zikabaki salama kibiashara katika nchi za wenzetu. Ndo maana walikubali haraka kulipa fine kwa baadhi ya vifungu vya kesi yao hata bila kusikilizwa. Mh. Membe analijua hili ndo maana akaandaa timu ya Wabunge na kuwatengenezea nafasi ya kula posho za ziara za kikazi nje ya nchi kwa shughuli isiyokuwepo. Vyombo vya habari vya ndani vikalishwa na kulisha watu kasa kuonyesha ukinzani usiokuwepo katika kulipa serikali fidia.
Hivi nikuulize swali; wafanyakzai wa BOT waliopokea hela za KAGODA zilizorejeshwa na Manji nao ni majasiri?