Membe kuwania urais 2015...

Membe kuwania urais 2015...

naomba niendelee na nukuu:
'Ikulu ni mahala patakatifu,
Ikulu sio pango la walanguzi'
mwisho wa nukuu.
(Source:Kambarage wa Mwitongo)
 

Katika orodha ya wanaotajwa kuwania uteuzi wa ccm kwa nafasi ya urais wa JMT-2015, namba mbili (2) katika nisio shawishika nao ni Mh. Bernard Membe. Mh. Membe hanishawishi kuwa anastahili nafasi hiyo kwa sababu zifuatazo:


  1. 1. Historia halisi ya utendaji wake kama Mbunge na Waziri haina matokeo yanayosimama kumshuhudia Mh.Membe kama mtu wa kuleta mabadiliko chanya au maendeleo.

Asiyeweza katika dogo, ataweza katika makubwa? Mbele ya wapigakura wa Jimbo la Mtama, Mh. Membe anaonekana kama mtu aliyeshindwa kutimiza ahadi zake za muhula wa kwanza (2005-2010). Na walio wengi hawaoni umuhimu/mchango wa ukaribu wake na serikali katika kuwaletea mabadiliko. Ndo maana Mh. Membe alipata wakati mgumu sana kutoka kwa mgombea wa TLP, mtu ambaye hakuwa na jina, mali wala pesa bali support ya wananchi. Lakini kwa kutumia utaalamu aliojaaliwa, Mh. Membe aliweza “kumshughulikia” na kumdhibiti mpinzani huyu pekee na kuhakikisha wapiga kura wanakosa chaguo mbadala wakati wa uchaguzi. Ninashawishika kufikiri kuwa hata mpinzani mmoja angepenya na kusimama, matokeo ya Jimbo la Mtama yangekuwa sawa na ya Nyamagana.

Kuna jambo moja ambalo Mh. Membe ameshiriki na watu wasio na kumbukumbu nzuri au wafupi katika kuchambua mambo wanaweza kusema kalifanikisha. Ni suala la kurejeshwa kwa fedha za rada kupitia serikali badala ya NGOs kama wezi walivyotaka. Hii haiwezi kuhesabika kama jitihada ya Mh. Membe wala serikali ya Tanzania. Hili silielezi kwa ufasaha ili watu wajadili……………………..


  1. 2. Misingi ya mbinu anazotumia Mh. Membe katika kusaka kuungwa mkono na makundi yenye ushawishi mkubwa katika jamii haina maslahi kwa Taifa na inatengeneza viporo vya uporaji wa rasilimali za nchi na migogoro mikubwa ya kijamii hapo baadae.
Mathalani, katika suala la serikali kuanzisha na kuendesha Mahakama ya Kadhi na serikali ya JMT kujiunga na OIC, Mh. Membe akiwa mbele ya waandishi wa habari amekuwa akiwaondoa hofu wahusika kuwa haya mambo hayana shida na serikali iko katika hatua mbalimbali za kuyatekeleza. Mara tu upande wa pili wakianza kupaza sauti za kupinga, Mh. Membe hu-haha na hukimbia kimya kimya kwenda kwa viongozi wakuu wa upande wa pili “kutuliza mambo” kwa kificho. Katika hili, Mh. Membe anataka kuuma na kupuliza na ni ndumila kuwili. Ni vema, si kwa Mh. Membe tu, bali wanasiasa wote kuimarisha msingi wa msimamo ambao umekwishafikiwa na serikali katika suala hili nyeti.

Mh. Membe anasimama miongoni mwa viongozi wa Bara la Afrika waliosimama kidete kuomboleza kifo cha Shujaa wetu Mummar Gadaff. Lakini nyuma ya kilio na maombolezo ya msiba huu, kumefunikwa giza totoro la vitendawili juu ya nini haswa “majonzi” ya Mh. Membe? Wako wanaotoa nuru ili kutegua vitendawili kwa hadithi tofauti tofauti ambazo kwa ujumla wake ukizikusanya kwa ushambuzi makini unapata picha pana juu ya makubaliano/fadhila za utawala uliongushwa Libya kwa mgombea mtarajiwa. Watanzania tunapaswa kuwa tumejifunza madhara ya wagombea wetu kufadhiliwa na matajiri (nchi au mtu binafsi). Tutumie 2015 kuepuka kurudi chini ya utawala wa waliofadhili wagombea katika chaguzi kuu.

Mh. Membe anapigania uraia wa nchi mbili. Kwa faida ya nani? Binafsi sioni kama hili jambo lina tija kwa Taifa lenye uchumi unaomilikiwa na asilimia mbili (2%) ya wananchi wake na ndio asilimia tisini na nane (98%) ya hao hao tayari wana uraia wa nchi zaidi ya mbili. Hapa Mh. Membe hasimami kutetea rasilimali watu za Watanzania walioko nje bali kutafuta kuongeza wigo wa kuungwa mkono na watu wasiokuwa na uchungu wa nchi hii. Hawa tunaowaita “Watanzania wenye asilia ya Kihindi” ambao ndo wanashawishi sana suala hili tayari wanao uraia Uswizi, Canada, Marekani na hapa kwetu kutokana na udhaifu wa idara zetu za uhamiaji wanaishi na kufanya wanalotaka kwa jeuri ya pesa yao.

Nahitaji kushawishiwa kwa historia na utendaji upi Mh. Membe anastahili kuomba ridhaa ya kubeba bendera ya ccm katika uchaguzi mkuu 2015. Michango yenu ikiwemo matusi na dhihaka vinakaribishwa. Na kuwa na hakika, nitavipokea vyote kama vilivyo. Kwa namna ya pekee nausubiri mchango wa MBOPO, mtu ambaye mara nyingi hujitahidi kujibu hoja na si kujadili mtoa hoja katika kumtetea Mh. Membe.


Nawatakia Mwaka Mpya Mwema na Wenye Mafanikio.

Omutwale kutoka Kanyigo.

Umenisaidia mkuu,mimi ndo naenda kuchukua jimbo la mtama,membe anapeleka watu hija kila kijiji,katika jimbo lake,alimnunua mgombea wa kafu mwaka jana ili apite bila kupingwa,unajua yule wa TLP alichelewa kuludishwa
 
Maskini Omutwale, chuki na kutumiwa kumekunyima fursa adhimu ya kufanya utafiti wa mambo ambayo ni very basic.

1. Membe amekuwa mbunge wa jimbo la Mtama kuanzia Novemba 2000 na muhula wake wa kwanza ulikwisha mwaka 2005. Katika historia ya jimbo la Mtama hakujawahi kutokea mbunge aliyetekeleza ahadi na kuanzisha miradi ya maendeleo Kama Membe. Kitakwimu, Membe ni kati ya wabunge wachache sana hapa nchini waliowekeza majimboni kwao, labda akitanguliwa na Mh. Nimrod Mkono. Ukiangalia miradi ya maji, afya, elimu na hata miundombinu na masuala ya kiimani utagundua kwamba ulichongea wewe hakina hata chembe ya ukweli kuhusu utendaji wa Membe jimboni kwake. Swali la kujiuliza ni je, ni mgombea yupi, akiwemo Slaa mwenye sifa ya utumishi bora jimboni unaomshinda Membe?

2. Msimamo kuhusu rada ulikuwa ni msimamo wa serikali na Membe Kama waziri mwenye dhamana ya mambo ya nje. Msimamo wa serikali ulikuwa ni kwamba chenji irejee serikalini, kosa lake Kama mtendaji na mtendaji na mtekelezaji wa maamuzi ya baraza la mawaziri ni nini? Mgombea makini angefanya tofauti na hivyo? Hiyo isingeitwa insubordination? Msimamo wa mgombea wako makini katika hili ni upi?

3. Hakuna siri kwamba Gadaffi alikuwa ni kiongozi wa nchi ambayo ilikuwa na uhusiano na Tanzania. Uhusiano huu haukuanza leo na wala haukuanza wakati wa uwaziri wa Membe. Leo hii hata ICC wameanzisha uchunguzi kuhusu kifo chake. Hii ni kwa vile kilikuwa cha kikatili na kisichostahili katika mazingira hayo. Msimamo wa serikali wakati wote ni kutatua mgogoro huu kwa amani. Ndiyo ulikuwa msimamo wa AU pia. Mtu anaweza asiupende msimamo huo lakini kwa kutokubaliana nao haumfanyi Membe kuwa mtu asiyefaa kuwa Rais japonica yeye mwenyewe hajawahi kutangaza nia.

4. Suala la mahakama ya kadhi na suala la OIC ambayo ni moja ya kero za muungano lililo chini ya wizara ya nje yalikuwa ni sehemu ya ahadi za CCM kwa wana chi 2005 na walioitunga ilani hiyo wanafahamika na winging leo ndo wapiga debe wa baadhi ya wagombea wanaosifiwa sana. Yeye alijibu kwamba watu waache kuwatia wananchi hofu juu ya OIC na badala yake waachwe wajadili faida na hasara zake na baadae akaliarifu bunge juu ya kusitishwa kwa mchakato kuruhusu mageuzi ndani ya taasisi hiyo. Tatizo liko wapi?

5. Siri za baraza! Kichekesho Kikubwa! Ilibainika kwamba Membe hakuwepo kwenye kikao husika na isingewezekana avujishe siri ambazo alikuwa hazijui na Rais alipogundua kwamba hizo ni adolescent machinations za waliokata tamaa akazipuuza na watuhumu (those who were baying for Membe's blood) wakaaibika sana.

Ninachokiona katika thread hii ni woga na kuweweseka kwa mgombea mmoja ambaye kila mara amekuwa akijigamba kuwa na mtaji wa kimtandao lakini kila siku ushahidi wa kumiss kujiamini kwake kunadhihiri, kwa kupaka matope wenzie, kuwatisha na hata kudiriki kudhuru wenzie. Lakini si ni vyema tukahoji miaka zaidi ya 20 ya ubunge wa jimbo lake ana nini la kujivunia? Na ile ahadi ya ng'ombe kwa kila kaya chini ya "kopa ng'ombe lipa ng'ombe" ya mwaka 2003 kule mikoa ya kusini imeishia wapi?

Hoja yako haina mashiko na haina mnunuzi kwa sababu imekosa chembe chembe muhimu za kuipa sifa ya kujadiliwa kwa mapana. Ndo maana kuna kujihami kwingi. Mradi umeanza, basi utapata haki yako.

Niambie mwenzangu ulipigia kura kituo gani(jimbo la mtama)naona utakua unasimuliwa,mi nimepigia kura Madangwa,Mkono vs Membe=maendeleo katika jimbo mmmmh,hapo umeshemsha,Mkono anajenga shule zen anaipa serikali,Membe amefanya hayo mambo,nenda Nachunyu,mtegu,mnjonjo,ingawali,mnolela,mahumbika,kiwalala,shuka,londo,mtama vijijin,sisi tunataka maendeleo,jamaa ni mbunge wetu,ila hawez kua Rais,amemuangusha Abdul_aziz Lindi mjin(alimuunga mkono Balwany kupitia Cuf)nenda Lindi ukaulize,inaonyesha wewe ujui mambo ya Lindi.
 
Haya ndo mambo ambayo nayaona kama majibu kwa hoja yangu japo, ukizitaja hizo hospitali na shule itakuwa vizuri zaidi kama ushahidi.

Mwambie azitaje izo hospt na shule namsubiri nipo Madangwa
 
- Membe nafikiri ni best ever Foreign Minister we ever had, amepitia ngazi zote za Uongozi wa chini, amelitumikia Taifa kwa uaminifu bila wizi I understand kwamba njia iliyomfikisha hapo alipo haikuwa saafi sana so is Viongozi wetu karibu wote wa CCM na Upinzani, lakini in his case the end justifies the means, kutokana na kazi yake nzito ya kuleta stability huko juu na nidhamu pia, ana kura yangu akigombea!

Super Field Marshall Es!
 
Niambie mwenzangu ulipigia kura kituo gani(jimbo la mtama)naona utakua unasimuliwa,mi nimepigia kura Madangwa,Mkono vs Membe=maendeleo katika jimbo mmmmh,hapo umeshemsha,Mkono anajenga shule zen anaipa serikali,Membe amefanya hayo mambo,nenda Nachunyu,mtegu,mnjonjo,ingawali,mnolela,mahumbika,kiwalala,shuka,londo,mtama vijijin,sisi tunataka maendeleo,jamaa ni mbunge wetu,ila hawez kua Rais,amemuangusha Abdul_aziz Lindi mjin(alimuunga mkono Balwany kupitia Cuf)nenda Lindi ukaulize,inaonyesha wewe ujui mambo ya Lindi.

Mimi nilipiga kura yangu Mahiwa. Katika historia yangu ya kupiga kura toka mwaka 1985 na kuchagua wabunge, jimbo la Mtama halijawahi kupata mbunge mwenye rekodi ya utendaji kama Membe. Tumeshuhudia mradi mkubwa wa Maji wa Chiuwe, wenye thamani ya shilingi milioni 800, mradi wa hospitali ya Rondo wa zaidi ya shilingi bilioni 1, mradi wa mahakama Rondo, mradi wa daraja la Nachui, miradi ya barabara. Ujenzi wa makanisa na misikiti na kupeleka mahujaji wa dini zote hija. Kusaidia vikundi vya wajasiri amali, miradi ya mashule na zahanati n.k. lakini kubwa na ambalo amejipambanua nalo ni kule kufanikisha kuvutia uwekezaji wa kiwanda kikubwa cha cement Lindi mjini ambacho kitatoa ajira za moja kwa moja za zaidi ya wafanyakazi 3,500.

Mohamed Abdul-Aziz amekuwa mbunge wa Lindi mjini toka 1995 na katika kipindi chote hicho hakuwahi hata kujenga tundu moja la choo. Katika chaguzi mbili mfululizo amekuwa akishinda kwa mbinde tena na wapinzani dhaifu na arobaini yake ilikuwa inasubiriwa na kila mwenye akili pale Lindi. Aliposhindwa hakuna aliyeshangaa, hata yeye mwenyewe alijua kwa sababu 'hakuwekeza' jimboni na hata kura za maoni alichakachua.

Take it or leave it, record ya membe jimboni ni ya kupigiwa mfano katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Whether hicho ni kigezo cha urais mimi sijui!
 
- Membe nafikiri ni best ever Foreign Minister we ever had, amepitia ngazi zote za Uongozi wa chini, amelitumikia Taifa kwa uaminifu bila wizi I understand kwamba njia iliyomfikisha hapo alipo haikuwa saafi sana so is Viongozi wetu karibu wote wa CCM na Upinzani, lakini in his case the end justifies the means, kutokana na kazi yake nzito ya kuleta stability huko juu na nidhamu pia, ana kura yangu akigombea!

Super Field Marshall Es!

Mheshimiwa huwezi sema tofauti na hili na hasa baada ya kujulikana Membe ni bosi wako.....kwanza declare interest kuwa wewe ni nani uko ubalozini.......we ever had.....ni bora kuliko JK na Mkapa kwahio....kwa lipi?siasa za miaka hio tz ikiheshimiwa kimataifa ni sawa na sasa.
 
- Membe nafikiri ni best ever Foreign Minister we ever had, amepitia ngazi zote za Uongozi wa chini, amelitumikia Taifa kwa uaminifu bila wizi I understand kwamba njia iliyomfikisha hapo alipo haikuwa saafi sana so is Viongozi wetu karibu wote wa CCM na Upinzani, lakini in his case the end justifies the means, kutokana na kazi yake nzito ya kuleta stability huko juu na nidhamu pia, ana kura yangu akigombea!

Super Field Marshall Es!
Mkuu Field Marshal!!! Ama kweli sasa mwaka tunaumaliza vizuri,umerudi Kamanda?ulipotelea wapi ?? Kuna siku memba Ashadii alifungua uzi wa vigogo wa jf walio dissapear,na wewe uliunganishwa katika orodha,ilionyesha watu walikumisssooo,karibu Mkuu!
RESPECT! (source:Field Marshall).
 
Mimi nilipiga kura yangu Mahiwa. Katika historia yangu ya kupiga kura toka mwaka 1985 na kuchagua wabunge, jimbo la Mtama halijawahi kupata mbunge mwenye rekodi ya utendaji kama Membe. Tumeshuhudia mradi mkubwa wa Maji wa Chiuwe, wenye thamani ya shilingi milioni 800, mradi wa hospitali ya Rondo wa zaidi ya shilingi bilioni 1, mradi wa mahakama Rondo, mradi wa daraja la Nachui, miradi ya barabara. Ujenzi wa makanisa na misikiti na kupeleka mahujaji wa dini zote hija. Kusaidia vikundi vya wajasiri amali, miradi ya mashule na zahanati n.k. lakini kubwa na ambalo amejipambanua nalo ni kule kufanikisha kuvutia uwekezaji wa kiwanda kikubwa cha cement Lindi mjini ambacho kitatoa ajira za moja kwa moja za zaidi ya wafanyakazi 3,500.

Mohamed Abdul-Aziz amekuwa mbunge wa Lindi mjini toka 1995 na katika kipindi chote hicho hakuwahi hata kujenga tundu moja la choo. Katika chaguzi mbili mfululizo amekuwa akishinda kwa mbinde tena na wapinzani dhaifu na arobaini yake ilikuwa inasubiriwa na kila mwenye akili pale Lindi. Aliposhindwa hakuna aliyeshangaa, hata yeye mwenyewe alijua kwa sababu 'hakuwekeza' jimboni na hata kura za maoni alichakachua.

Take it or leave it, record ya membe jimboni ni ya kupigiwa mfano katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Whether hicho ni kigezo cha urais mimi sijui!

Ubunge, uwaziri etc is one thing, na Urais is the other. Kuwa waziri mzuri au mbunge mzuri hakumaanishi kuwa utakuwa rais mzuri. I do not see Membe kuwa rais kwa kigezo cha perfomance yake bungeni.

JK was better MP kwa Chalinze, lakini angalia he is the worst Pressident Tanzania has ever seen
 
..rekodi ya Membe ni ipi?

..Mahakama ya Kadhi hajafanikisha.

..OIC hajafanikisha.

..Uraia pacha bado.

..ni kitu gani amekifanya mpaka astahili kugombea uraisi.

Kikwete alistahili vipi? Vigezo vya nani kafanya nini..kuna ambaye angemfikia Salim A. Salim kipindi kile?
 
Sioni tofauti kati ya wanaomuunga mkono na Benard Membe na waliokuwa wanamuunga mkono JK.
kwa sababy Wote wawili;

--wote Wanategemea ufadhiliwa toka nje kusaka urais - Benard na Libya na Jk Oman akisaidiwa na Rostam
-- wote Mawaziri wa wizara za mambo ya nje wasio leta tija
-- wote Hawana jambo jipya walilosimamia la kujitofautisha nalo ( Magufuli = barabara na Dr Slaa -kuondoa mafisadi)
-- wote Wanaunda mitandao ya ushindi ndani ya chama badala ya kujijenga kwa vitedo watu wakaona
-- wote wajumbe wazoefu wa mitandao. Walimwingiza JK mwenyewe madarakani kwa nguvu ya magazeti
-- wote wametoka pwani ( mkoa wa Lindi na mkoa wa pwani)
--wote Wanafanana kwa sura
-- wote wanapigania uraia wa nchi mbili kwa faida zao, siyo maskini watz. (Wakiharibu ikulu wapate pa kukimbilia)
-- wote waoga wa maamuzi magumu Ktk hili Membe =JK kwa 100%; Membe alikoroga OIC akaenda kwa Pengo kimya kimya
-- wote kwa hiyo baba yao ni mmoja? Nauliza tu
.

Hitimisho, Ubora wa urais wa JK = Urais wa Membe kwa 100%; Chaguo ni letu.

Wote ni wanafiki na wasio amini wanaokisema!
 
hoja dhaifu kutoka kwa mtu makini.mleta mada wanatakiwa wakae karibu na aweda wajikosoe kabla hawaleta blaa blaa zao hapa.
 
omutwale, una hisa na mgombea yeyote ambaye unadhani Membe ni threat kwake? kwani lini Membe katangaza nia? au umekurupuka tu? Isitoshe robo tatu 3/4 ya posts za hii thread ni zako,, unalala humu kulinda hii thread? Unajiabisha mkuu
 

Katika orodha ya wanaotajwa kuwania uteuzi wa ccm kwa nafasi ya urais wa JMT-2015, namba mbili (2) katika nisio shawishika nao ni Mh. Bernard Membe. Mh. Membe hanishawishi kuwa anastahili nafasi hiyo kwa sababu zifuatazo:


  1. 1. Historia halisi ya utendaji wake kama Mbunge na Waziri haina matokeo yanayosimama kumshuhudia Mh.Membe kama mtu wa kuleta mabadiliko chanya au maendeleo.

Asiyeweza katika dogo, ataweza katika makubwa? Mbele ya wapigakura wa Jimbo la Mtama, Mh. Membe anaonekana kama mtu aliyeshindwa kutimiza ahadi zake za muhula wa kwanza (2005-2010). Na walio wengi hawaoni umuhimu/mchango wa ukaribu wake na serikali katika kuwaletea mabadiliko. Ndo maana Mh. Membe alipata wakati mgumu sana kutoka kwa mgombea wa TLP, mtu ambaye hakuwa na jina, mali wala pesa bali support ya wananchi. Lakini kwa kutumia utaalamu aliojaaliwa, Mh. Membe aliweza “kumshughulikia” na kumdhibiti mpinzani huyu pekee na kuhakikisha wapiga kura wanakosa chaguo mbadala wakati wa uchaguzi. Ninashawishika kufikiri kuwa hata mpinzani mmoja angepenya na kusimama, matokeo ya Jimbo la Mtama yangekuwa sawa na ya Nyamagana.

Kuna jambo moja ambalo Mh. Membe ameshiriki na watu wasio na kumbukumbu nzuri au wafupi katika kuchambua mambo wanaweza kusema kalifanikisha. Ni suala la kurejeshwa kwa fedha za rada kupitia serikali badala ya NGOs kama wezi walivyotaka. Hii haiwezi kuhesabika kama jitihada ya Mh. Membe wala serikali ya Tanzania. Hili silielezi kwa ufasaha ili watu wajadili……………………..


  1. 2. Misingi ya mbinu anazotumia Mh. Membe katika kusaka kuungwa mkono na makundi yenye ushawishi mkubwa katika jamii haina maslahi kwa Taifa na inatengeneza viporo vya uporaji wa rasilimali za nchi na migogoro mikubwa ya kijamii hapo baadae.
Mathalani, katika suala la serikali kuanzisha na kuendesha Mahakama ya Kadhi na serikali ya JMT kujiunga na OIC, Mh. Membe akiwa mbele ya waandishi wa habari amekuwa akiwaondoa hofu wahusika kuwa haya mambo hayana shida na serikali iko katika hatua mbalimbali za kuyatekeleza. Mara tu upande wa pili wakianza kupaza sauti za kupinga, Mh. Membe hu-haha na hukimbia kimya kimya kwenda kwa viongozi wakuu wa upande wa pili “kutuliza mambo” kwa kificho. Katika hili, Mh. Membe anataka kuuma na kupuliza na ni ndumila kuwili. Ni vema, si kwa Mh. Membe tu, bali wanasiasa wote kuimarisha msingi wa msimamo ambao umekwishafikiwa na serikali katika suala hili nyeti.

Mh. Membe anasimama miongoni mwa viongozi wa Bara la Afrika waliosimama kidete kuomboleza kifo cha Shujaa wetu Mummar Gadaff. Lakini nyuma ya kilio na maombolezo ya msiba huu, kumefunikwa giza totoro la vitendawili juu ya nini haswa “majonzi” ya Mh. Membe? Wako wanaotoa nuru ili kutegua vitendawili kwa hadithi tofauti tofauti ambazo kwa ujumla wake ukizikusanya kwa ushambuzi makini unapata picha pana juu ya makubaliano/fadhila za utawala uliongushwa Libya kwa mgombea mtarajiwa. Watanzania tunapaswa kuwa tumejifunza madhara ya wagombea wetu kufadhiliwa na matajiri (nchi au mtu binafsi). Tutumie 2015 kuepuka kurudi chini ya utawala wa waliofadhili wagombea katika chaguzi kuu.

Mh. Membe anapigania uraia wa nchi mbili. Kwa faida ya nani? Binafsi sioni kama hili jambo lina tija kwa Taifa lenye uchumi unaomilikiwa na asilimia mbili (2%) ya wananchi wake na ndio asilimia tisini na nane (98%) ya hao hao tayari wana uraia wa nchi zaidi ya mbili. Hapa Mh. Membe hasimami kutetea rasilimali watu za Watanzania walioko nje bali kutafuta kuongeza wigo wa kuungwa mkono na watu wasiokuwa na uchungu wa nchi hii. Hawa tunaowaita “Watanzania wenye asilia ya Kihindi” ambao ndo wanashawishi sana suala hili tayari wanao uraia Uswizi, Canada, Marekani na hapa kwetu kutokana na udhaifu wa idara zetu za uhamiaji wanaishi na kufanya wanalotaka kwa jeuri ya pesa yao.

Nahitaji kushawishiwa kwa historia na utendaji upi Mh. Membe anastahili kuomba ridhaa ya kubeba bendera ya ccm katika uchaguzi mkuu 2015. Michango yenu ikiwemo matusi na dhihaka vinakaribishwa. Na kuwa na hakika, nitavipokea vyote kama vilivyo. Kwa namna ya pekee nausubiri mchango wa MBOPO, mtu ambaye mara nyingi hujitahidi kujibu hoja na si kujadili mtoa hoja katika kumtetea Mh. Membe.


Nawatakia Mwaka Mpya Mwema na Wenye Mafanikio.

Omutwale kutoka Kanyigo.
...........kaka umenena, maumivu tunayopata kutoka kwa jk ndio tutayapata kutoka kwa membe, tena even worse, hatuhitaji rais aina ya jk, rais anayetumia taili ya bendera kuongoza, yaani upepo unakoelekea na yeye kule kule.........
 
Ina maana Membe nae anataka kugombea urais? du hivi hawezi pima upepo? ameshupalia chenji ya rada mbona hatumsikii akisisitiza kukamatwa kwa waliotufikisha hapo na kuhujumu uchumi wa nchi maskini kama Tanzania? kwa ushauri tu kwa chama cha magamba,msimamisheni Membe 2015 ili mkione cha mtema kuni! yaani itakuwa ni ukombozi kwa watanzania.
 
omutwale, una hisa na mgombea yeyote ambaye unadhani Membe ni threat kwake?

Hapana. Sina. Na tena akinishawishi yeye LABDA anaweza kuwa chaguao langu

kwani lini Membe katangaza nia?

Sijasema waliotangaza nia. Nimesema

Omutwale
Katika orodha ya wanaotajwa kuwania uteuzi wa ccm kwa nafasi ya urais wa JMT-2015

..Isitoshe robo tatu 3/4 ya posts za hii thread ni zako,, unalala humu kulinda hii thread? Unajiabisha mkuu

Jibu lake ni rahisi sana. Mimi ndiye nimeanzisha mada. Kuna wanaoiunga mkono na kuna wanaiopinga. Wanaoipinga wanahitaji maelezo zaidi nami nahitaji melezo toka kwao. Kwa hiyo ulitaka nisiwajibu ili waseme nimewakimbia? Hata kwenye filamu kinara (steering) lazima haonekane zaidi!
 
hoja dhaifu kutoka kwa mtu makini.mleta mada wanatakiwa wakae karibu na aweda wajikosoe kabla hawaleta blaa blaa zao hapa.

Onyesha basi huo udhaifu wa hoja. Tuachane na kauli za kijumla jumla. Ebu tuje na mifano itakayotusaidia kuidhoofisha au kuiua kabisa hoja.
 
Mi sijasikia kitu cha maana, nakumbuka alivyomnyong'onyeza Mudhihir, mpaka akampa joka la mdimu, zaidi najua lazima V8 lake liwe jeusi, akiletewa jeupe anaenda kubadilisha liwe jeusi, na benzi moja naona analitumia nalo ni jeusi, najua anavaa cheni kubwa na anafungua kifungo ili ionekana, ki ufupi na namuona kama sharobaro, sina la zaidi ninalo lijua
 
Back
Top Bottom